Salman Mwajemi, Uzoroastria, Uajemi (sehemu ya 2 kwa 2): Kutoka Ukristo hadi Uislalm.

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Utafutaji mrefu hatimaye unamalizika kwa Salman kukutana na Mtume aliyeahidiwa, na kupata uhuru wake na kuwa mmoja wa masahaba wake wa karibu.

  • Na Salman the Persian
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,393 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Mtu huyo alikufa, na Salman akabaki Amuria. Siku moja, “Wafanyabiashara fulani kutoka kabila la Kalb[1] walinipita,” Salman akasema, “Nikawaambia, ‘Nipelekeni Uarabuni nami nitawapa ng’ombe wangu na kondoo pekee nilio nao.’” Wakasema, “Sawa.” Salman aliwapa kile alichotoa, na wakamchukua pamoja nao. Walipofika Waadi al-Quraa [karibu na Madina], walimuuza kama mtumwa kwa mwanamume Myahudi. Salman alikaa na yule Myahudi, na aliiona Mitende [kama sahaba wake wa awali alivyokuwa amemweleza].

"Ninatumaini kuwa hapa pangekuwa ndipo mahali pale pale palipoelezwa na swahaba wangu."

Siku moja, mtu ambaye alikuwa binamu wa kwanza wa bwana wa Salman kutoka kabila la Kiyahudi la Bani Quraizhah huko Madina alikuja akiwatembelea. Alimnunua Salman kutoka kwa bwana wake Myahudi.

“Alinichukua na kwenda naye Madina. Hakika! Nilipoiona, nilijua ni sehemu ambayo swahaba alieleza.

Kisha Mwenyezi Mungu akatuma[2] Mtume Wake [yaani, Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake]. Alikaa Makka muda mrefu kama alivyokaa.[3] Sikusikia chochote kuhusu yeye kwa sababu nilikuwa na kazi nyingi sana za utumwa, kisha akahamia Madina.

[Siku moja,] Nilikuwa juu ya mtende juu ya mojawapo ya nguzo zake za tende nikifanya kazi fulani kwa ajili ya bwana wangu. Akaja binamu yake wa kwanza na kusimama mbele yake [bwana wake alikuwa ameketi] na akasema: “Ole wao Bani Qeelah [watu wa kabila la Qeelah] wamekusanyika Qibaa”[4] kumzunguka mtu aliyekuja leo kutoka Makka akijidai kuwa ni Mtume!

Nilitetemeka sana nilipomsikia hata niliogopa kwamba ningemwangukia bwana wangu. Nikashuka na kusema, ‘Unasemaje!? Unasema nini!?'

Bwana wangu alikasirika na kunipiga ngumi kali akisema, “Una biashara gani katika [jambo] hili? Nenda ukafanye mambo yako."

Nikasema, “Hakuna kitu! Nilitaka tu kuwa na uhakika wa kile anachosema.”

Jioni hiyo, nilikwenda kumuona Mtume wa Mwenyezi Mungu alipokuwa Qibaa. Nilichukua kitu ambacho nilikuwa nimekihifadhi. Niliingia ndani na kusema, “Niliambiwa kwamba wewe ni mtu mwadilifu na kwamba kundi lako [ambalo] ni wageni [hapa] wana uhitaji. Ninataka kukupa kitu nilichohifadhi kama sadaka. Nimeona kwamba unastahili zaidi kuliko mtu mwingine yeyote.”

Nilimtolea; akawaambia masahaba wake, “Kuleni,” lakini yeye mwenyewe akauzuia mkono wake [yaani, asile]. Nikajiambia: “Hii ni moja ya alama za Utume wake.

Kufuatia kukutana huku na Mtume, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, Salman aliondoka kujiandaa kwa mtihani mwingine! Safari hii alileta zawadi kwa Mtume pale Madina.

“"Niliona kuwa haukula sadaka iliyotolewa, kwa hivyo hapa kuna zawadi ambayo ninataka kukupa." Mtume akala na akawaamuru masahaba wake wafanye hivyo hivyo. Nikajiambia, “Sasa zipo mbili [yaani, dalili mbili za Utume]."

Katika kutano la mara ya tatu, Salman alikuja Baqee-ul-Gharqad [makaburi ya Madina] ambapo Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikuwa akihudhuria mazishi ya mmoja wa masahaba zake. Salman alisema:

“Nilimsalimia [kwa salamu ya Uislamu: ‘Amani iwe juu yako], kisha nikasogea kuelekea mgongoni mwake nikijaribu kuona muhuri [wa Utume] ambao nilielezewa na sahaba wangu. Aliponiona [nikifanya hivyo], alijua kwamba nilikuwa nikijaribu kuthibitisha jambo lililoelezewa kwangu. Alitoa vazi mgongoni mwake na mimi nikautazama muhuri. Niliitambua. Nilianguka juu yake, nikimbusu na kulia. Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, aliniambia nizunguke [yaani, kuzungumza naye]. Nilimsimulia kisa changu kama nilivyofanya kwako, Ibn ‘Abbaas [kumbuka kwamba Salman anasimulia kisa chake kwa Ibn ‘Abbaas]. Yeye [Mtume] alikipenda sana akataka niwasimulie kisa changu maswahaba zake.

Bado alikuwa mtumwa anayemilikiwa na bwana wake. Mtukufu Mtume akamwambia, “Fanya mkataba [na bwana wako] kwa ajili ya uhuru wako, ewe Salman.” Salman alitii na akafanya mkataba [na bwana wake] kwa ajili ya uhuru wake. Alifikia makubaliano na bwana wake ambapo atamlipa wakia arobaini za dhahabu na angepanda na kufanikiwa kukuza mitende mipya mia tatu. Kisha Mtume akawaambia masahaba zake, “Msaidieni ndugu yenu.”

Walimsaidia kwa miti na wakamkusanyia kiasi kilichoainishwa. Mtukufu Mtume alimuamuru Salman kuchimba mashimo sahihi ya kupanda miche hiyo, na kisha akaipanda kila moja kwa mikono yake mwenyewe. Salman alisema, “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu iko mikononi Mwake [yaani, Mungu], hakuna mti hata mmoja uliokufa.”

Salman alimpa bwana wake miti hiyo. Mtukufu Mtume alimpa Salman kipande cha dhahabu ambacho kilikuwa na ukubwa wa yai la kuku na akasema, “Chukua hiki, Ewe Salman, na umlipe [yaani, bwana wako] kile unachodaiwa.”

Salman alisema, “Hii ni kiasi gani kuhusiana na deni langu!”

Mtume akasema, “Ichukue! Mwenyezi Mungu ataifanya sawa na deni lako.”[5]

Nilichukua na nikapima kipande chake na kilikuwa wakia arobaini. Salman alimpa bwana wake dhahabu. Alitimiza makubaliano na akaachiliwa.

Kuanzia hapo, Salman akawa mmoja wa masahaba wa karibu sana na Mtume.

Kutafuta Ukweli

Mmoja wa masahaba wakubwa wa Mtume kwa jina la Abu Hurairah ameeleza:

“Tulikuwa tumekaa pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu ilipoteremshwa Sura al-Jumuah (Sura ya 62). Alikariri maneno haya:

“Na kwa wengine ambao bado hawajaungana nao…” (Quran 62:3)

Akasema mtu miongoni mwao: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je, ni akina nani ambao hawajajiunga nasi?’

Mtume wa Mwenyezi Mungu hakujibu. Salman Mwajemi alikuwa miongoni mwetu. Mtume wa Allah akaweka mkono wake juu ya Salman kisha akasema, ‘Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake, hata kama imani ingekuwa karibu na Pleiades (nyota saba), watu miongoni mwa hawa [yaani. Watu wa Salman] bila shaka wataipata.” (At-Tirmidhi)

Wengi katika ulimwengu huu ni kama Salman, wanatafuta ukweli kuhusu Mungu wa Kweli na wa Pekee. Hadithi hii ya Salman ni sawa na hadithi za watu katika zama zetu hizi. Utafutaji wa baadhi ya watu uliwachukua kutoka kanisa moja hadi lingine, kutoka kanisani hadi Ubuddha au Passivenesi, kutoka Uyahudi hadi 'Kutoegemea upande wowote', kutoka dini hadi kutafakari hadi unyanyasaji wa kiakili. Wapo waliohama kutoka kwenye wazo moja kwenda jingine, lakini hawafikirii hata kutaka kujua kitu kuhusu Uislamu! Hata hivyo, walipokutana na baadhi ya Waislamu, walifungua akili zao. Hadithi ya Salman ni ile ya utafutaji wa muda mrefu. Unaweza kufanya utafutaji wako wa ukweli kuwa mfupi na kufaidika kutoka kwake.



Rejeleo la maelezo:

[1] Kabila la Kiarabu.

[2] Salman amefika Madina kabla ya Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, hajafanywa kuwa mtume.

[3] Miaka kumi na tatu baada ya kupokea ufunuo kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

[4] Viunga vya Madina.

[5] Muujiza wa Mwenyezi Mungu

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.