Raphael Narbaez, Md, Waziri wa Mashahidi wa Yehova, Marekani (sehemu ya 2 kwa 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Makutano yake ya kwanza na Waislamu na imani, na hatimaye kuukubali Uislamu.

  • Na Raphael Narbaez, Jr.
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,220 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Tunafanya kazi kwenye hili duka kuu. Ni msimu wa likizo, na wanaweka vibanda hivi vya ziada kwenye barabara za ukumbi. Kulikuwa na msichana mmoja, na ilibidi tupite mbele yake. Nilisema, “Habari za asubuhi, hujambo?” Ikiwa atasema chochote, ilikuwa ni "Sijambo." Na ilikuwa hivyo.

Hatimaye, nikasema, “binti, husemi chochote. Nilitaka tu kuomba msamaha ikiwa kuna kitu nilikisema kibaya."

Akasema, “Hapana, unaona, mimi ni Muislamu.”

“Wewe ni nani?”

“Mimi ni Muislamu, na wanawake wa Kiislamu, hatuongei na wanaume isipokuwa tuwe na jambo maalum la kuzungumza; vinginevyo hatuna uhusiano wowote na wanaume."

“Ohhhhh. Muislamu.”

Akasema, “Ndiyo, tunafuata dini ya Kiislamu.”

"Uislamu - unaisemaje hiyo?"

“U-i-s-l-a-m-u.”

Wakati huo, nilijua kwamba Waislamu wote walikuwa magaidi. Hana hata ndevu. Je, angewezaje kuwa Muislamu?

“Dini yako ilianzaje?”

“Kulikuwa na mtume”

“Mtume?”

“Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake”

Nilianza utafiti. Lakini nilitoka kwenye dini moja tu. Sikuwa na nia ya kuwa Muislamu.

Likizo zimeisha. Kibanda kikasonga. msichana akaondoka.

Niliendelea kuomba na kuuliza kwa nini maombi yangu hayajajibiwa. Mnamo Novemba 1991, lilikuwa naenda kumleta mjomba wangu Rockie nyumbani kutoka hospitalini. Nilianza kufungua droo zake ili kuviweka vitu vyake, kulikuwa na Biblia ya Gideon. Nikasema, Mungu amejibu maombi yangu. Hii ni Biblia ya Gideoni. (Bila shaka, waliiweka katika kila chumba cha hoteli.) Hii ni ishara kutoka kwa Mungu kwamba yuko tayari kunifundisha. Kwa hiyo niliiba Biblia.

Nilienda nyumbani na nikaanza kuomba: Ee Mungu, nifundishe kuwa Mkristo. Usinifundishe njia ya Mashahidi wa Yehova. Usinifundishe njia ya Kikatoliki. Nifundishe njia yako! Usingefanya Biblia hii kuwa ngumu sana kwamba watu wa kawaida walio waaminifu katika sala wasingeweza kuielewa.

Nilipitia Agano Jipya. Nilianza Agano la Kale. Basi , hatimaye kuna sehemu katika Biblia kuhusu manabii.

Puu!

Nikasema, Ngoja kidogo, yule mwanamke wa Kiislamu alisema walikuwa na nabii. Vipi hayupo humu?

Nilianza kufikiri, Waislamu - bilioni moja duniani. Jamani, mtu mmoja kati ya kila watu watano mitaani kinadharia anaweza kuwa Muislamu. Na nikafikiria: Watu bilioni moja! Haya sasa, Shetani ni mzuri . Lakini yeye sio mzuri sana.

Hivyo basi nikasema, nitasoma kitabu chao, Quran, na nitaona ni aina gani ya uwongo wa kitu hiki. Pengine ina kielelezo cha jinsi ya kutenganisha AK-47. Kwa hiyo nilienda kwenye duka la vitabu vya Kiarabu.

Wakauliza, “Nikusaidie nini?”

“Natafauta Quran.”

“Sawa, tunavyo hapa.”

Walikuwa na nzuri sana - dola thelathini, dola arobaini."

"Ona, nataka kuisoma tu, sitaki kuwa mmoja wao, sawa?"

"Sawa, tuna toleo hili dogo la dola tano."

Nilikwenda nyumbani na nikaanza kuisoma Quran yangu tangu mwanzo, Al-Fatihah. Na sikuweza kuyatoa macho yangu kutoka kwake.

Jamani, angalia hii. Inazungumza juu ya Nuhu hapa. Tuna Nuhu katika Biblia yetu pia. Jamani, inazungumza juu ya Loti na Ibrahimu. Siwezi kuamini. Sikuwahi kujua jina la Shetani ni Iblees. Jamani, vipi kuhusu hilo.

Unapopata picha hiyo kwenye runinga yako na ina chenga kidogo na ukabonyeza kitufe hicho [klop] - kuona vizuri. Hivyo ndivyo ilivyotokea Kwa Quran.

Nilipitia kote. Kwa hiyo nikasema, Sawa, nimefanya hivi, sasa ni jambo gani linalofuata unalopaswa kufanya? Kweli, lazima uende sehemu yao ya makutano. Niliangalia katika kurasa za njano, na hatimaye nikapata: Kituo cha Kiislamu cha Kusini mwa California, huko Vermont. Nilipiga simu na wakasema, "Njoo Ijumaa."

Sasa ninaanza kuwa na woga, `kwa sababu sasa najua itabidi nikabiliane na Habib na AK-47 yake.

Nataka watu waelewe inakuwaje kwa Mkristo wa Marekani anayeingia katika Uislamu. Ninatania kuhusu AK-47, lakini sijui kama watu hawa wana majambia ndani ya makoti yao, unajua. Basi nikaenda mbele, na kwa hakika, kuna ndugu huyu wa futi sita, pauni 240, ana ndevu na kila kitu, na nikiwa na msangao mkubwa.

Nilikwenda na kusema, “Samahani, bwana.”

[Lafudhi ya Kiarabu:] “Nenda nyuma!”

Alinidhania mimi ni ndugu yake tayari.

Nikasema, “sawa, sawa” [kwa upole].

Sikujua ninakwenda nyuma kwa nini, lakini hata hivyo nilikwenda. Walikuwa na hema na mazulia nje. Nikiwa nimesimama pale, kwa namna fulani ya haya, na watu wakiwa wameketi chini wakisikiliza hotuba. Na watu wakisema, Nenda mbele, ndugu, keti. Na nikaenda, Hapana, asante, hapana, asante, ninatembelea tu.

Basi mwisho hotuba ikaisha. Wote wakajipanga kwa ajili ya sala na wanakwenda kwenye sajdah. Kwa kweli nilipigwa na butwaa.

Ilianza kuwa na maana kiakili, katika misuli yangu, katika mifupa yangu, moyoni mwangu, na katika nafsi yangu.

basi maombi yakaisha. Nikasema, jamani, ni nani atanitambua? Kwa hivyo nikaanza kujichanganya kama mmoja wa ndugu, na nikaingia msikitini na kaka anasema, "Assalaamu Alaikum." Na nikawaza, Je, alisema “chumvi na nyama ya nguruwe”?

“Assalaamu Alaikum.”

Kuna mtu mwingine ambaye aliniambia "chumvi na nyama ya nguruwe".

Sikujua walikuwa wanasema nini, lakini wote walitabasamu.

Kabla mmoja wa watu hawa hajagundua kuwa sikupaswa kuwa pale na kunipeleka kwenye chumba cha mateso, au kunikata kichwa, nilitaka kuona kadri niwezavyo. Kwa hiyo hatimaye nilienda kwenye maktaba, na kulikuwa na kijana mdogo Mmisri; jina lake lilikuwa Omar. Mungu alimtuma kwangu.

Omar alikuja kwangu, na akasema , “Samahani. Hii ni mara yako ya kwanza hapa?" Ana lafudhi kali sana.

Na niakasema, Ndio.

“Oh, vizuri sana. Wewe ni Muislamu?”

“Hapana,Ninasoma tu kidogo.”

“Oh, Unasoma? Hii ni mara yako ya kwanza kuutembelea msikiti?”

“Ndio.”

"Njoo, nikuonyeshe." Na huku akinishika mkono, na nikitembea na mtu mwingine - nikishikana mikono. Nilisema Waislamu hawa ni marafiki.

Basi akanitembeza

“Kwanza kabisa, hii ni jumba yetu ya maombi, na unavua viatu vyako hapa.”

“Hivi ni vitu gani?”

“Hivi ni visanduku vidogo. Hapo ndipo unapoweka viatu vyako."

“kwanini?”

“Vizuri, kwa sababu unakaribia eneo la maombi, na ni takatifu sana. Huingii huko na viatu vyako; kumehifadhiwa kwa usafi sana."

Akanipeleka kwenye chumba cha wanaume.

"Na hapa ndipo tunafanya wudhu."

"Voodoo! Sikusoma chochote kuhusu Voodoo!”

“Hapana, siyo voodoo. Wudhu!”

"Sawa, kwa sababu niliona vitu hivyo na madoli na pini, na bado siko tayari kwa ahadi kama hiyo."

Akasema, "Hapana, Wudhu, ni wakati tunapojisafisha."

“Kwanini mnafanya hivyo?”

"Vizuri, unapoomba kwa Mungu, lazima uwe msafi, kwa hiyo tunanawa mikono na miguu yetu."

Kwa hiyo nilijifunza mambo haya yote. Akaniacha, na kusema, “Rudi tena.”

Nilirudi na kumwomba msimamizi wa maktaba kijitabu kuhusu maombi, na nilienda nyumbani na kufanya mazoezi. Nilihisi kwamba ikiwa ningejaribu kufanya hivyo kwa njia ifaayo, Mungu angekubali. Niliendelea tu kusoma na kusoma na kutembelea msikiti.

Nilikuwa na ahadi ya kwenda kwenye ziara ya Kati Magharibi kwenye vichekesho. Basi, nilichukua zulia la maombi. Nilijua kuwa nilitakiwa kusali nyakati fulani, lakini kuna sehemu ambazo hutakiwi kusali, moja wapo ni bafuni. Niliingia kwenye chumba cha wanaume kwenye kituo cha watalii na nikaweka kapeti yangu na nikaanza kufanya maombi yangu.

Nilirudi, na Ramadhani ilipoisha, nilianza kupigiwa simu kutoka sehemu mbalimbali za nchi ili niende kuhutubia kama waziri Shahidi wa Yehova aliyekubali Uislamu. Watu wananiona kama kitu kipya.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.