Mazungumzo katika Pepo na Jahannamu (sehemu ya 3 kati ya 3): Na sitawahi wakasirikia tena.

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mazungumzo na familia, majadiliano ya ndani na jinsi Mwenyezi Mungu anavyo itika kwa watu wa Akhera.

  • Na Aisha Stacey (© 2012 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 11 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 16 Jan 2023
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,866 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Majadiliano ya ndani

conversationinParadise3.jpg Itakapo hukumiwa jambo, na watu wa Jahannamu wakaondoka, na watu wa Peponi wakaingia Bustani, kila kundi la watu litaongea kati yao. Maisha yao duniani hayajasahauliwa na makundi yote mawili yana wakati usioisha wa kuangalia nyuma na kuchambua kwa nini - kwa nini ninateseka, au kwa nini nina haki ya kufurahia anasa hii? Hukumu imeshaamuliwa, muda mfupi uliotumika katika maisha ya dunia umekwisha na uzima wa milele umeanza.

Atawauliza Mungu:"Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka? Watasema: "Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu." Atasema Mungu: "Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua." (Kurani 23:112-114)

Tunajua ya kwamba watu wa Peponi na Jahannamu wataulizana, lakini wataambiana nini, watahisi vipi, unyonge na upweke? Mungu anatuambia kwamba watashusha pumzi, kwa hofu, kwa kuchanganyikiwa. Ni vigumu kwetu kufikiria hilo lakini tunajua kwamba wanaonekana kukata tamaa.

“ Ama wale wa mashakani hao watakuwamo Motoni wakiyayayatika na kukoroma." (Kurani 11:106)

“… Hakika Mwenyezi Mungu amewalaani makafiri na amewaandalia Moto unao waka kwa nguvu. Watadumu humo milele na hawampati mlinzi wala wa kuwanusuru. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungeli mt'ii Mwenyezi Mungu, na tungeli mt'ii Mtume." (Kurani 33:64-66)

Na watu wa Jahannamu wanapotafakari kwa nini wale waliowafuata katika dunia hii hawawezi kuwasaidia katika mateso yao, basi ndani yake kuna somo la kujifunza. Katika Kurani na hadeeth ya Mtume Muhammad tunaweza kusoma na kuona kwa jicho la akili yetu jinsi hali yetu inaweza kuwa.

Kwa upande mwingine, furaha ilioje kwa walio ingia Peponi. Watapata radhi ya kumwona Mwenyezi Mungu. Hayo ni ya kunyimwa kwa watu wa Jahannamu. "Hakika watakuwa wamefunikwa na kumwona Mola wao siku hiyo." (Kurani 83:15)

Watu wa Peponi na watu wa Jahannamu wakizungumza na familia zao

Hakuna aya nyingi za Kurani au hadeeth kutoka kwa Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, ambazo zinatuonyesha mazungumzo yanayojiri kati ya watu na familia zao katika makao yao ya milele . Hata hivyo kuna ushahidi wa kuonyesha kwamba watakumbuka maisha yao katika ulimwengu huu na kufikiri juu ya familia zao.

“ Wataelekeana wakiulizana. Watasema: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa, basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto. Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu." (Kurani 52:25-28)

Mazungumzo baina ya Mwenyezi Mungu na watu wa Motoni

Mazungumzo tunayoyakuta baina ya Mwenyezi Mungu na watu wa Jahannamu si mengi. Tunaziona Aya za Kurani, ambapo watu wa Jahannamu wanajadiliana baina yao, au pamoja na Malaika wanaolinda milango ya Jahannamu. Hata hivyo kuna mazungumzo ambayo ni ya kushangaza na yanapaswa kuwa wazi katika akili zetu, ili tujilinde tusiwahi kuyasikia maneno haya ya kutisha. Watasema watu wa Motoni:

“ Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu."

Atasema Mwenyezi Mungu: "Tokomeeni humo, wala msinisemeze." (Kurani 23:107-108)

Mazungumzo baina ya Mwenyezi Mungu na watu wa Peponi

Katika hadeeth ya Mtume Muhammad tunapata mazungumzo yenye kupendeza sana kati ya Mungu na mtu wa mwisho kutoka katika adhabu ya Jahannamu kwa rehema ya Mungu. Mtu huyo anaalikwa kuingia Peponi na hivyo ataenda huko na kudhani kuwa Pepo imejaa. Anarudi kwa Mwenyezi Mungu na kusema: "Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimeona Pepo imejaa." Na Mwenyezi Mungu atasema: "Nenda ukaingie Peponi hakika unayo mle yaliyo bora mara kumi kuliko dunia na yote yaliyomo ndani yake." Akasema Mtume Muhammad: "Huyo ndiye mwenye hadhi ya chini kabisa kati ya watu wa Peponi." [1]

Na mtu mwingine ataulizwa na Mwenyezi Mungu kama ana kila anachotaka, naye atamjibu Mola wake Mlezi akisema: "Naam, lakini napenda kupanda mbegu." Hivyo atakwenda na kupanda mbegu zake, na kwa muda wa kupepesa kwa macho zitakua, kuiva, kuvunwa na kupangwa kama milima.[2]

Tutamalizia msururu wetu wa sehemu tatu kwa msemo mzuri sana kwa matumaini ya kwamba kila mmoja anayesoma au kusikia mazungumzo haya mazuri, atashiriki mazungumzo haya mwisho wa maisha yake duniani na mwanzo wa maisha yake ya Akhera.

Mwenyezi Mungu atawaambia watu wa Peponi: "Enyi Watu wa Peponi! Watajibu: "Sisi tuko hapa Mola wetu Mlezi, na kheri zote ziko mikononi mwako." Mwenyezi Mungu atasema: "Je, mumeridhika?" Watasema: "Kwa nini tusitosheke, na hali umetupa usiyowapa viumbe vyako?" Atasema: "Je! Nisiwape kilicho bora kuliko hicho? Watasema: "Ewe Mola wetu Mlezi! Nini inaweza kuwa bora kuliko hiyo? Mwenyezi Mungu atasema: "Nawapa radhi Zangu, wala sitawakasirikia tena."[3]



Vielezi-chini:

[1] Saheeh Al-Bukhari

[2] Saheeh Al-Bukhari

[3] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.