您所请求的文章/视频尚不存在。
The article/video you have requested doesn't exist yet.
あなたが要求した記事/ビデオはまだ存在していません。
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
您所请求的文章/视频尚不存在。
The article/video you have requested doesn't exist yet.
あなたが要求した記事/ビデオはまだ存在していません。
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Itakapo hukumiwa jambo, na watu wa Jahannamu wakaondoka, na watu wa Peponi wakaingia Bustani, kila kundi la watu litaongea kati yao. Maisha yao duniani hayajasahauliwa na makundi yote mawili yana wakati usioisha wa kuangalia nyuma na kuchambua kwa nini - kwa nini ninateseka, au kwa nini nina haki ya kufurahia anasa hii? Hukumu imeshaamuliwa, muda mfupi uliotumika katika maisha ya dunia umekwisha na uzima wa milele umeanza.
Atawauliza Mungu:"Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka? Watasema: "Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu." Atasema Mungu: "Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua." (Kurani 23:112-114)
Tunajua ya kwamba watu wa Peponi na Jahannamu wataulizana, lakini wataambiana nini, watahisi vipi, unyonge na upweke? Mungu anatuambia kwamba watashusha pumzi, kwa hofu, kwa kuchanganyikiwa. Ni vigumu kwetu kufikiria hilo lakini tunajua kwamba wanaonekana kukata tamaa.
“ Ama wale wa mashakani hao watakuwamo Motoni wakiyayayatika na kukoroma." (Kurani 11:106)
“… Hakika Mwenyezi Mungu amewalaani makafiri na amewaandalia Moto unao waka kwa nguvu. Watadumu humo milele na hawampati mlinzi wala wa kuwanusuru. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungeli mt'ii Mwenyezi Mungu, na tungeli mt'ii Mtume." (Kurani 33:64-66)
Na watu wa Jahannamu wanapotafakari kwa nini wale waliowafuata katika dunia hii hawawezi kuwasaidia katika mateso yao, basi ndani yake kuna somo la kujifunza. Katika Kurani na hadeeth ya Mtume Muhammad tunaweza kusoma na kuona kwa jicho la akili yetu jinsi hali yetu inaweza kuwa.
Kwa upande mwingine, furaha ilioje kwa walio ingia Peponi. Watapata radhi ya kumwona Mwenyezi Mungu. Hayo ni ya kunyimwa kwa watu wa Jahannamu. "Hakika watakuwa wamefunikwa na kumwona Mola wao siku hiyo." (Kurani 83:15)
Hakuna aya nyingi za Kurani au hadeeth kutoka kwa Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, ambazo zinatuonyesha mazungumzo yanayojiri kati ya watu na familia zao katika makao yao ya milele . Hata hivyo kuna ushahidi wa kuonyesha kwamba watakumbuka maisha yao katika ulimwengu huu na kufikiri juu ya familia zao.
“ Wataelekeana wakiulizana. Watasema: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa, basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto. Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu." (Kurani 52:25-28)
Mazungumzo tunayoyakuta baina ya Mwenyezi Mungu na watu wa Jahannamu si mengi. Tunaziona Aya za Kurani, ambapo watu wa Jahannamu wanajadiliana baina yao, au pamoja na Malaika wanaolinda milango ya Jahannamu. Hata hivyo kuna mazungumzo ambayo ni ya kushangaza na yanapaswa kuwa wazi katika akili zetu, ili tujilinde tusiwahi kuyasikia maneno haya ya kutisha. Watasema watu wa Motoni:
“ Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu."
Atasema Mwenyezi Mungu: "Tokomeeni humo, wala msinisemeze." (Kurani 23:107-108)
Katika hadeeth ya Mtume Muhammad tunapata mazungumzo yenye kupendeza sana kati ya Mungu na mtu wa mwisho kutoka katika adhabu ya Jahannamu kwa rehema ya Mungu. Mtu huyo anaalikwa kuingia Peponi na hivyo ataenda huko na kudhani kuwa Pepo imejaa. Anarudi kwa Mwenyezi Mungu na kusema: "Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimeona Pepo imejaa." Na Mwenyezi Mungu atasema: "Nenda ukaingie Peponi hakika unayo mle yaliyo bora mara kumi kuliko dunia na yote yaliyomo ndani yake." Akasema Mtume Muhammad: "Huyo ndiye mwenye hadhi ya chini kabisa kati ya watu wa Peponi." [1]
Na mtu mwingine ataulizwa na Mwenyezi Mungu kama ana kila anachotaka, naye atamjibu Mola wake Mlezi akisema: "Naam, lakini napenda kupanda mbegu." Hivyo atakwenda na kupanda mbegu zake, na kwa muda wa kupepesa kwa macho zitakua, kuiva, kuvunwa na kupangwa kama milima.[2]
Tutamalizia msururu wetu wa sehemu tatu kwa msemo mzuri sana kwa matumaini ya kwamba kila mmoja anayesoma au kusikia mazungumzo haya mazuri, atashiriki mazungumzo haya mwisho wa maisha yake duniani na mwanzo wa maisha yake ya Akhera.
Mwenyezi Mungu atawaambia watu wa Peponi: "Enyi Watu wa Peponi! Watajibu: "Sisi tuko hapa Mola wetu Mlezi, na kheri zote ziko mikononi mwako." Mwenyezi Mungu atasema: "Je, mumeridhika?" Watasema: "Kwa nini tusitosheke, na hali umetupa usiyowapa viumbe vyako?" Atasema: "Je! Nisiwape kilicho bora kuliko hicho? Watasema: "Ewe Mola wetu Mlezi! Nini inaweza kuwa bora kuliko hiyo? Mwenyezi Mungu atasema: "Nawapa radhi Zangu, wala sitawakasirikia tena."[3]
[1] Saheeh Al-Bukhari
[2] Saheeh Al-Bukhari
[3] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim
Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.
Orodha yako ya historia ipo tupu.
Kwa nini kujiandikisha? Tovuti hii ina miundo kadhaa uliyoundwa mahsusi kwa ajili yako, kama vile: vipendwa vyako, historia yako, kutia alama makala ambazo umezitazama awali, kuorodhesha makala zilizochapishwa tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho, kubadilisha ukubwa wa herufi, na zaidi. Vipengele hivi vinatokana na vidakuzi na vitafanya kazi ipasavyo tu unapotumia kompyuta ile ile. Ili kuwezesha vipengele hivi kutoka kwa kompyuta yoyote, unapaswa kuingia wakati katika tovuti hii.
Tafadhali ingiza Jina lako la mtumiaji na anwani ya barua pepe kisha ubofye kitufe cha Tuma neno la siri. Utapokea neno la siri jipya hivi karibuni. Tumia neno la siri hili jipya kufikia tovuti.
Ongeza maoni