Anselm Turmeda, Kasisi na Mwanazuoni Mkristo, Hispania

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mwanafunzi mwaminifu wa mwanazuoni mashuhuri wa Kikristo huko Andalusia ya zamani anasikia mazungumzo kuhusu Paraclete, nabii ajaye anayetajwa katika Biblia.

  • Na Anselm Tormeeda
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,267 (wastani wa kila siku: 1)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Idadi kubwa ya Wakristo walisilimu wakati na mara baada ya ushindi wa Kiislamu baada ya kifo cha Mtume. Hawakuwahi kulazimishwa, bali ilikuwa ni utambuzi wa kile ambacho walikuwa wakikitarajia. Anselm Tormeeda[1], kasisi na msomi wa Kikristo, alikuwa mmoja wa watu kama hao ambaye historia yake inafaa kuhusishwa. Aliandika kitabu maarufu kinachoitwa “The Gift to the Intelligent for Refuting the Arguments of the Christians”[2]. kwa utangulizi [3] wa kazi hii anahusishwa na historia yake:

“Ifahamike kwenu nyote kwamba asili yangu ni kutoka katika jiji la Majorca, ambalo ni jiji kubwa la baharini kati ya milima miwili inayogawanywa na bonde dogo. Ni jiji la kibiashara, lenye bandari mbili za ajabu. Meli kubwa za wafanyabiashara huja na kutia nanga bandarini na bidhaa tofauti. Jiji liko kwenye kisiwa ambacho kina jina moja - Majorca, na sehemu kubwa ya ardhi yake ina miti ya mtini na mizeituni. Baba yangu alikuwa mtu aliyeheshimika sana mjini. Nilikuwa mtoto wa pekee.

Nilipokuwa na umri wa miaka sita, alinipeleka kwa kasisi ambaye alinifundisha kusoma Injili na mantiki, ambayo nilimaliza baada ya miaka sita. Baada ya hapo, niliondoka Majorca na kusafiri hadi jiji la Larda, katika eneo la Castillion, ambalo lilikuwa kitovu cha elimu kwa Wakristo katika eneo hilo. Wanafunzi wa Kikristo elfu moja hadi elfu moja na nusu walikusanyika hapo. Wote walikuwa chini ya usimamizi wa kasisi aliyewafunza. Nilijifunza Injili na lugha yake kwa miaka mingine minne. Baada ya hapo, niliondoka kwenda Bologne katika eneo la Anbardia. Bologne ni jiji kubwa sana, likiwa kitovu cha kujifunza kwa watu wote wa eneo hilo. Kila mwaka, zaidi ya wanafunzi elfu mbili hukusanyika kwa pamoja kutoka sehemu tofauti. Wanajifunika nguo wanazoziita “Rangi ya Mungu.” Wote, awe mwana wa mfanya kazi au mwana wa mtawala, huvaa shuka hii, ili kuwatofautisha wanafunzi na wengine.

Kuhani pekee ndiye anayewafundisha, kuwadhibiti, na kuwaelekeza. Niliishi kanisani pamoja na kasisi mzee. Aliheshimiwa sana na watu kwa sababu ya ujuzi wake na dini na kujinyima mambo, ambapo kulimtofautisha na mapadre wengine wa Kikristo. Maswali na maombi ya ushauri yalikuja kutoka kila mahali, kutoka kwa Wafalme na watawala, pamoja na zawadi. Walitumaini kwamba angekubali zawadi zao na kuwapa baraka zake. Kasisi huyu alinifundisha kanuni za Ukristo na hukumu zake. Nikawa karibu naye sana kwa kumhudumia na kumsaidia majukumu yake mpaka nikawa mmoja wa wasaidizi wake wa kutegemewa, akaniamini kwa funguo za makazi yake kanisani na za maduka ya vyakula na vinywaji. Alibaki na ufunguo tu wa chumba kidogo alichokuwa akilala. Nafikiri, na Mungu anajua vyema zaidi, kwamba aliweka kasha lake la hazina mle ndani. Nilikuwa mwanafunzi na mtumishi kwa kipindi cha miaka kumi, kisha akaugua na kushindwa kuhudhuria mikutano ya mapadre wenzake.

Pindi alipokuwa hayupo, makasisi walijadili baadhi ya mambo ya kidini, mpaka wakafikia yale yaliyosemwa na Mwenyezi Mungu kupitia nabii wake Yesu katika Injili: “Baada yake atakuja Nabii anayeitwa Paracleti. Walibishana sana kuhusu Mtume huyu na kuhusu yeye ni nani miongoni mwa Mitume. Kila mtu alitoa maoni yake kulingana na ujuzi wake na ufahamu wake; na walimaliza bila kupata faida yoyote katika suala hilo. Nilienda kwa kasisi wangu, na kama kawaida yake akaniuliza kuhusu yale yaliyozungumziwa katika mkutano siku hiyo. Nilimtajia maoni tofauti ya makasisi kuhusu jina Paraclete, na jinsi walivyomaliza mkutano bila kufafanua maana yake. Aliniuliza: “Jibu lako lilikuwa nini?” Nilitoa maoni yangu ambayo yalichukuliwa kutoka kwenye tafsiri ya ufafanuzi unaojulikana sana. Alisema kwamba karibu nilikuwa sahihi kama makasisi fulani, na makasisi wengine walikuwa na makosa. “Lakini ukweli ni tofauti na hayo yote. Hii ni kwa sababu tafsiri ya jina hilo tukufu inajulikana na idadi ndogo tu ya wanazuoni waliobobea. Na tuna ujuzi mdogo tu.” Nikaanguka chini na kubusu miguu yake, nikisema: “Bwana, unajua kwamba nilisafiri na kuja kwako kutoka nchi ya mbali, nimekutumikia sasa kwa zaidi ya miaka kumi; na kupata elimu zaidi ya makadirio, basi tafadhali nineemeshe na uniambie ukweli kuhusu jina hili.” Kisha kasisi huyo alilia na kusema: “Mwanangu, hakika, ninakupenda sana kwa kunitumikia na kujitolea kunitunza. Jua ukweli kuhusu jina hili, na kuna faida kubwa, lakini pia kuna hatari kubwa. Na ninachelea kwamba mtakapojua ukweli huu, na Wakristo wakagundua hilo, mtauawa mara moja.” Nikasema: “hakika, kwa Injili na Aliyetumwa pamoja nayo, sitasema neno lolote kuhusu yale utakayoniambia, nitayaweka moyoni mwangu.” Akasema: “Mwanangu, ulipokuja hapa kutoka katika nchi yako, nilikuuliza ikiwa upo karibu na Waislamu, na kama wanakufanyia shambulizi na ikiwa mnawafanyia mashambulizi. Hii ilikuwa ni kupima chuki yako kwa Uislamu. Jua, mwanangu, kwamba Paraclete ni jina la Mtume wao Muhammad, ambaye aliteremshiwa kitabu cha nne kama ilivyotajwa na Danieli. Njia yake ndiyo njia iliyo ya wazi iliyotajwa katika Injili.” Nikasema: “Basi bwana, unasemaje kuhusu dini ya Wakristo hawa?” Akasema: “Mwanangu, lau Wakristo hawa wangebakia katika dini ya asili ya Yesu, basi wangekuwa katika dini ya Mwenyezi Mungu, kwa sababu dini ya Isa na Mitume wengine wote ni dini ya kweli ya Mwenyezi Mungu. Lakini waliibadilisha na wakawa wasio amini.” Nilimuuliza: “Basi, bwana, ni nini wokovu kutoka kwenye hili?” Akasema: Ewe mwanangu, kusilimu. Nikamuuliza: “Je, yule anayesilimu ataokolewa?” Akajibu: Ndio, katika dunia hii na ijayo. Nilisema: “Mwenye busara huchagua mwenyewe; kama unajua, bwana ubora wa Uislamu, basi ni nini kinakuepusha nayo?” Akajibu: “Mwanangu, Mwenyezi Mungu hakunidhihirishia ukweli wa Uislamu na Mtume wa Uislamu mpaka baada ya kuwa mzee na mwili wangu kudhoofika. Ndiyo, hakuna udhuru kwa ajili yetu katika hili, kinyume chake, uthibitisho wa Mungu umethibitishwa dhidi yetu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeniongoza kwa haya nilipokuwa katika umri wenu, ningeliacha kila kitu na kushika dini ya haki. Kuipenda dunia hii ndiyo kiini cha kila dhambi, na tazama jinsi ninavyoheshimiwa, kutukuzwa na kuheshimiwa na Wakristo, na jinsi ninavyoishi katika ukwasi na faraja! Kwa upande wangu, kama nikionyesha mwelekeo mdogo kuelekea Uislamu wataniua mara moja. Tuseme nimeokoka kutoka kwao na nikafaulu kutorokea kwa Waislamu, wangesema usiuone Uislamu wako kuwa ni fadhila juu yetu, bali umejinufaisha kwa kuingia katika Dini ya Haki, Dini itakayokuepusha na adhabu ya Mungu! Kwa hiyo ningeishi kama mzee maskini wa zaidi ya miaka tisini, bila kujua lugha yao, na ningekufa kwa njaa. Mimi, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, juu ya Dini ya ukristo na aliyokuja nayo, na Mwenyezi Mungu anajua kutoka kwangu.” Kwa hiyo nikamuuliza: “Je, unanishauri niende katika nchi ya Waislamu na kuchukua dini yao?” Akaniambia: “Ikiwa una hekima na una matumaini ya kujiokoa, basi kimbia kwenye yale ambayo yatafikia maisha ya dunia na akhera. Lakini mwanangu, hakuna hata mmoja aliyepo pamoja nasi katika jambo hili; ni kati yako na mimi tu. Jitahidi na uifanye kuwa siri. Kama ikifichuka na watu wanajua kuhusu hilo watakuua mara moja. Sitakuwa na faida kwako dhidi yao. Wala haitakuwa na manufaa kwako ikiwa utawaambia yale uliyoyasikia kutoka kwangu kuhusu Uislamu, au kwamba nilikuhimiza kuwa Muislamu, kwa maana mimi nitakanusha. Wanaamini ushuhuda wangu dhidi yako. Basi usiseme neno lolote litakalotokea.” Nilimuahidi kutofanya hivyo.

Aliridhika na ahadi yangu. Nilianza kujiandaa na safari yangu na kumuaga. Aliniombea na kunipa dinari hamsini za dhahabu[4]. Kisha nikachukua meli hadi jiji langu la Majorca ambako nilikaa na wazazi wangu kwa miezi sita. Kisha nikasafiri hadi Sicily na kukaa huko kwa muda wa miezi mitano, nikingojea meli iliyokuwa ikisafiri kwenda nchi ya Waislamu. Hatimaye meli iliwasili ikielekea Tunis. Tuliondoka kabla ya jua kutua na tukafika bandari ya Tunis saa sita mchana siku ya pili. Niliposhuka kwenye meli, wasomi wa Kikristo waliosikia kuwasili kwangu walikuja kunisalimia na nilikaa nao kwa muda wa miezi minne kwa raha na furaha. Baada ya hapo, niliwauliza ikiwa kuna mtafsiri. Sultani katika siku hizo alikuwa Abu al-Abbas Ahmed. Walisema kulikuwa na mtu mwema, daktari wa Sultani, ambaye alikuwa mmoja wa washauri wake wa karibu. Jina lake lilikuwa Yusuf al-Tabiyb. Nilifurahi sana kusikia hivyo, na nikaulizia anaishi wapi. Walinipeleka huko kukutana naye. Nilimwambia kuhusu hadithi yangu na sababu ya kuja kwangu huko; ambayo ilikuwa ni kusilimu. Alifurahi sana kwa sababu jambo hili lingekamilika kwa msaada wake. Tulipanda hadi Ikulu ya Sultani. Alikutana na Sultani na kumweleza kuhusu hadithi yangu na akaomba ruhusa yake ili nionane naye.

Sultani alikubali, na nikajiwasilisha mbele yake. Swali la kwanza alilouliza Sultani lilikuwa kuhusu umri wangu. Nilimwambia kwamba nilikuwa na umri wa miaka thelathini na tano. Kisha akaniuliza kuhusu masomo yangu na sayansi ambayo nilikuwa nimesoma. Baada ya kumwambia alisema. “Ujio wako ni ujio wa wema. Uwe Muislamu kwa baraka za Mwenyezi Mungu.” Kisha nikamwambia daktari, “Mwambie mheshimiwa Sultani kwamba kila mara hutokea kwamba mtu yeyote akibadili dini yake watu wake wanamkashifu na kumsema vibaya. Kwa hiyo, natamani kwa ukarimu wake kama ataagiza kuletwa kwa makasisi wa Kikristo na wafanyabiashara wa jiji hili ili kuwauliza kuhusu mimi na kusikia wanachosema. Kisha kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu nitaukubali Uislamu.” Akaniambia kupitia kwa mfasiri, “Umeuliza kile Abdullah bin Salaam aliuliza kutoka kwa Mtume alipokuja Abdullah kutangaza Uislamu wake. Kisha akaagiza waitwe makasisi na wafanyabiashara fulani wa kikristo na kuniruhusu niketi katika chumba kilichokuwa karibu na wasiweze kuniona. “Mnasemaje kuhusu huyu kasisi mpya aliyewasili kwa meli?” Aliuliza. Wakasema: “Ni mwanachuoni mkubwa katika dini yetu. Maaskofu wetu wanasema yeye ndiye msomi zaidi na hakuna aliye bora kuliko yeye katika elimu yetu ya kidini.” Baada ya kusikia yale ambayo Wakristo waliyasema, Sultani aliniita, na nikajihudhurisha mbele yao. Nilitangaza shahidi mbili kwamba hakuna apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na kwamba Muhammad, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ni Mtume wake, na Wakristo waliposikia hivyo wakajikataa na kusema: “Hakuna lolote lililomchochea kufanya hivyo isipokuwa tamaa yake ya kutaka kuoa, kwa sababu makasisi katika dini yetu hawawezi kuoa.” Kisha wakaondoka kwa dhiki na huzuni.

Sultani aliniwekea robo ya dinari kila siku kutoka kwenye hazina na kuniruhusu nimuoe binti ya Al-Hajj Muhammed al-Saffar. Nilipoamua kufunga ndoa, alinipa dinari mia moja za dhahabu na lundo la nguo bora. Kisha nikafunga ndoa na Mungu akanijaalia mtoto ambaye nilimpa jina la Muhammad kama baraka kutoka kwa jina la Mtume.[5]



Rejeleo la maelezo:

[1] Baada ya kuukubali uislam, alijulikana kwa jina la Abu Muhammad bin Abdullah Al-Tarjuman. Aliitwa Al-Tarjuman (Mfasiri), kwa sababu katika muda usiozidi miezi mitano baada ya kusilimu kwake, Sultani alimteua kuwa mkuu wa Utawala wa Majini ambako alijifunza lugha ya Kiarabu na akawa mfasiri stadi katika majadiliano kati ya Waislamu na Wakristo. Baada ya mwaka mmoja tu, alifaulu katika lugha ya Kiarabu na akateuliwa kuwa mkuu wa Masuala ya Tafsiri. Alijulikana sana na watu wa kawaida, ambao walimpa majina ya kupendeza; maarufu zaidi lilikuwa Sidi Tohfah, ambalo lina maana ya "Zawadi ya Mwalimu Wangu", akimaanisha kitabu chake maarufu.

[2] Tuhfat al-arib fi al-radd ‘ala Ahl al-Salib kwa Kiarabu. Kitabu hiki kilikuwa pigo kubwa kwa muundo wa imani ya Kikristo kwa sababu kiliandikwa na mmoja wa wasomi wakuu wa Kikristo wa zama hizo.

[3] Kufuatia utangulizi huo, aliandika kuhusu baadhi ya matukio yanayohusu Jimbo la Hafsah. Alifuata sura tisa ikiwa ni pamoja na moja inayoonyesha kwamba injili nne hazikuandikwa na wanafunzi wa Yesu ambazo kwa kawaida zinahusishwa nao. Pia alijadili mada zingine zikiwemo Ubatizo, Utatu, Dhambi ya Asili, Chakula cha Bwana, Kujinyima, Sheria ya Imani. Alikanusha mafundisho haya yote yaliyotegemea maandiko ya Injili na hoja zenye mantiki. Alithibitisha pia asili ya ubinadamu wa Kristo na kukanusha madai yake ya Uungu. Kisha akafichua migongano katika maandiko ya Bibilia. Vile vile alizungumzia mambo ambayo Wakristo waliwakosoa Waislamu nayo, kama vile kuruhusiwa kwa ndoa kwa wanachuoni wa kidini na wanaume wachamungu, tohara na starehe ya kimwili Peponi. Alihitimisha kitabu chake kwa kuthibitisha ukweli wa Utume wa Muhammad kwa kutumia maandiko kutoka katika Biblia.

[4] Sarafu za fedha

[5] Imetolewa kutoka kwenye Nyenzo juu ya Usahihi wa Kurani: Uthibitisho wa kuwa ni Ufunuo kutoka kwa Mwenyezi Mungu na Abdur-Raheem Greene.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.