Usimfuate Herakyulasi (sehemu ya 2 kati ya 2): Masuala ya kisasa na shinikizo za nje

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Iwapo mtu anaamini Uislamu ni ukweli, basi anapaswa kusilimu bila kuchelewa.

  • Na Aisha Stacey (© 2012 NewMuslims.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 09 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,922 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

DoNotFollowHeraclius2.jpgAmi mpendwa wa Mtume Muhammad Abu Talib, na Herakyulasi, Mfalme wa Dola ya Baizantina, wote walichagua kutokubali Uislamu. Katika visa vyote viwili tunaweza kuwa na hakika kuwa ulikuwa uamuzi ambao hawakuuchukulia kijuujuu, hata hivyo wote wawili walichagua kutii shinikizo za nje. Badala ya kumcha Mungu pekee walijikuta wakiogopa yale ambayo wengine watafikiria, watasema au watafanya. Leo, zaidi ya milenia baadaye, watu wengi hujikuta katika hali hiyo hiyo. Wanajua au wanahisi kuwa Uislamu ni dini sahihi au ya kweli lakini wanaikataa zawadi ambayo Mungu amewapa.

Kuna shinikizo nyingi katika jamii ya kisasa ambazo hufanya kusilimu kuwa jambo la kukatisha tamaa. Shinikizo za nje zinaweza kuwaweka watu wa kisasa katika nafasi ile ile kama ya kina Abu Talib and Mfalme Herakyulasi. Hata hivyo, Mungu hamwiti mtu katika Uislamu halafu akamwacha. Ikiwa mtu anajua bila shaka kuwa Uislamu ni dini sahihi anaweza pia kuwa na hakika, bila shaka, kwamba Mungu ana mamlaka na nguvu ya kuendelea kuwaongoza na kurahisisha safari yao. Wakati mwingine mlima ulio mbele unaweza kuonekana kuwa mkubwa na wa kutisha lakini mlima ni nini isipokuwa sehemu ya mahuluku vinavyonyenyekea moja kwa moja kwa mapenzi ya Mungu?

“Je, huoni kwamba vinamsujudia Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi, na jua, na mwezi, na nyota, na milima, na miti, na wanyama, na wengi miongoni mwa watu…” (Kurani 22:18)

Mwenyezi Mungu hufanya kuingia katika Uislamu kuwa rahisi lakini sisi, watu, wanadamu, tuna njia isiyo ya kawaida ya kufanya maisha yetu kuwa ngumu na iliyojaa vizuizi ambavyo kwa ukweli havipo.

“…Hapendi Mwenyezi Mungu kukutieni katika taabu…” (Kurani 5:6)

“…Na anayemtegemea Mwenyezi Mungu, basi Yeye humtosha…” (Kurani 65:3)

Kauli hii ya Kurani kuhusu utegemezi ni rahisi kusema na kueleweka hata hivyo linapokuja suala la utekelezaji wa utegemezi kamili, huwa sio rahisi kila wakati. Hii ni kwa sababu mbili. Kwa kweli, mtu anapokaribia kuukubali Uislamu, Shetani humshambulia kwa hila na udanganyifu ulioundwa kumwelekeza mtu huyo mbali na njia ya Mungu iliyonyooka. Na pili, watu ambao hawaelewi kabisa asili ya Mungu huelekea kuogopa jinsi familia zao, marafiki zao au wenzao watakavyowachukulia. Abu Talib aliogopa kufikiriwa kama mtu asiyeheshimika angekataa dini ya mababu zake, na Herakyulasi alidhani atapoteza nafasi yake, nguvu zake au maisha yake. Mambo haya hayana faida yoyote yakilinganishwa na neema ya milele au laana, hata hivyo wanadamu hupigana vita kila uchao ili kujitenga na ulimwengu huu wa hadaa.

Mtu anaposilimu mabadiliko kadhaa makubwa hutokea. Mabadiliko ya kuingia katika Uislamu huibua hisia mbalimbali. Kila mtu huanza kujisikia kama mtu aliyebadilika na kwa hivyo huanza kutenda mambo kwa njia tofauti. Maswali, mawazo na matukio hujaza akili zetu, na Shetani hachoki kufanya kazi ya ziada. Pengine Abu Talib aliweza kuyashughulikia maswala hayo hayo, naye Herakyulasi aliajabia maisha yake yangekuwa hatarini ikiwa angesisitiza jambo hilo au kudhihirisha nia yake ya kufuata mafundisho ya Muhammad.

Siku hizi tunajiuliza mfululizo mwingine wa maswali lakini vivyo hivyo huvuruga utulivu wetu. Je, napaswa kuvaa tofauti? Je, niwaambie familia yangu? Je, bado naruhusiwa kwenda nje, kunywa pombe, kupanga miadi ya kukutana na msichana au mwanamke? Yapo mamia ya maswali, lakini ukweli ni kwamba maswali haya hayana uhusiano wowote na mtu kutaka kusilimu au la. Iwapo mtu anaamini Uislamu ni ukweli, basi hana budi kusilimu bila kukawia. Maelezo zaidi yatafuata mtu atakapoanzisha uhusiano na Mungu, atakapoelewa asili ya Muumba wetu.

Kila mtu ana muda wa kuishi uliokadiriwa zamani. Hatujui ni lini tutakufa na dakika inayofuata inaweza kuwa ndiyo ya mwisho wetu katika dunia hii. Kwa sababu hii peke yake mtu lazima asijifananishe na Herakyulasi au Abu Talib. Wanaume wote wawili waliyafuata mapenzi yao ya ulimwengu huu wa hadaa uongoze Akhera yao. Kusilimu kunapaswa kufanyika na kumtegemea Mungu kunapaswa kumwongoza Muislamu mpya kuwa na uhusiano wa maisha pamoja na Mungu.

Kudhihirisha kuwa wewe ni Muislamu sio sharti la kukubali Uislamu. Wakati huo huo, hata hivyo, ni lazima tuyatilie maanani mabadiliko ambayo Uislamu unahitaji kutoka kwetu na kumwomba Mungu aturahisishie njia. Tabia za zamani lazima ziachwe polepole lakini kwa yakini ya kuyamaliza, na vilevile kujifunza juu ya asili ya Mungu na sheria zake kutampa fursa kila mtu abadilike awe aina ya mtu anayependwa na Mungu. Ingawa kusilimu ni tukio la papo kwa hapo, kuwa Muislamu bora kunahitaji juhudi nzuri na endelevu kwa kila mmoja wetu.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.