Mashahidi wa Yehova ni nani? (sehemu ya 2 kati ya 3): Siku za Mwisho

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mashahidi wa Yehova wanatabiri tukio ambalo Mungu alitangaza kulijua Yeye pekee.

  • Na Aisha Stacey (© 2012 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 19 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,614 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Jehovahs-Witnesses2.jpgMashahidi wa Yehova (JW) ni dini ya kimataifa yenye wanachama katika nchi zaidi ya 200. Ni dhehebu la Kikristo, lakini Wakristo wengi wa kawaida hupinga vikali imani za JW. Kulingana na Kanisa la Kipresbiteri la Othodoksi, “Mashahidi wa Yehova wana dini bandia ya Kikristo. Hiyo ina maana kwamba inajifanya kuwa Ukristo, Hata hivyo, si kweli. Mafundisho yao na matendo yao hayalingani na Maandiko”.[1]

Katika sehemu ya 1 tulijifunza kidogo juu ya historia ya dini ya JW na kugundua kwamba ilikuwa ni dini mpya, iliyoanzishwa mnamo mwaka 1870. Tulitaja kwa ufupi imani yao na mtazamo wao wa nadharia za Siku za Mwisho na sasa katika sehemu ya 2, tutachimba kwa undani zaidi tabiri nyingi za siku za mwisho ambazo hazijatokea.

Utafiti wa Siku za Mwisho, unaoitwa kwa usahihi zaidi eskatologia, ni msingi wa imani ya JW. Chimbuko lake linaonekana kutokana na imani zilizopendekezwa na Nelson Horatio Barbour, mwandishi na mchapishaji wa Kiadventista mashuhuri, anayejulikana sana kwa kushirikiana , na baadaye kumpinga, Charles Taze Russell. Yafuatayo ni maelezo mafupi ya imani ya awali ya eskatologia ya JW kama ilivyofafanuliwa kwenye tovuti yao.

“Waadventista wa Pili walioshirikiana na Nelson H. Barbour walitazamia kurudi kwa Kristo kwa kuonekana na kwa kushangaza katika mwaka wa 1873, na baadaye katika mwaka wa 1874. Walikubaliana na vikundi vingine vya Waadventista kwamba “wakati wa mwisho” (unaoitwa pia “siku za mwisho”) ulikuwa umeanza. katika mwaka wa 1799. Muda mfupi baada ya kukatishwa tamaa mwaka wa1874, Barbour alikubali wazo la kwamba Kristo alikuwa amerudi duniani katika mwaka wa 1874, lakini bila kuonekana. 1874 ilizingatiwa kuwa mwisho wa miaka 6,000 ya historia ya mwanadamu na mwanzo wa hukumu ya Kristo. Charles Taze Russell na kikundi ambacho baadaye kilijulikana kuwa Wanafunzi wa Biblia walikubali maoni hayo kutoka kwa Barbour.”[2]

“Har–Magedoni ingetokea mwaka wa 1914. Kuanzia 1925–1933, Watchtower Society ilibadili imani yake kwa kiasi kikubwa baada ya kutofaulu kwa matazamio ya Har–Magedoni katika miaka ya 1914, 1915, 1918, 1920, na 1925. Mnamo 1925, Mnara wa Mlinzi lilieleza badiliko kubwa ambalo Kristo alikuwa amelifanya. sasa ametawazwa kuwa Mfalme mbinguni katika mwaka wa 1914 badala ya 1878. Kufikia 1933, ilifundishwa waziwazi kwamba Kristo alikuwa amerudi bila kuonekana katika mwaka wa 1914 na “siku za mwisho” pia zilikuwa zimeanza kwa wakati huo.[3]

Maoni haya yanatofautiana sana na yale ya mwenzi wa JW's leo na cha kushangaza, wanaonekana kuwa hawana shida na mabadiliko makubwa na muhimu kwa mfumo wao wa imani. 1914 labda ndiyo tarehe muhimu zaidi katika eskatologia ya JW's. Ilikuwa tarehe ya kwanza iliyotabiriwa ya Russell ya Har–Magedoni[4], lakini hilo liliposhindwa kutokea lilirekebishwa ili “kwamba watu walio hai katika mwaka wa 1914 wangekuwa bado hai wakati wa Har–Magedoni”; hata hivyo kufikia 1975 watu hawa sasa walikuwa wazee.

“Wakati wa miaka ya 1960 na mwanzo wa miaka ya 1970, Mashahidi wengi walichochewa na makala katika fasihi zao na kutiwa moyo zaidi na wasemaji kwenye mikutano yao kabla ya mwaka 1975, kuamini kwamba Har–Magedoni na utawala wa Kristo wa miaka elfu moja wa milenia ungeanza kufikia mwaka 1975. Ingawa maoni ya Har–Magedoni na Milenia ya Kristo ilianza mwaka wa 1975 haikuungwa mkono kikamili au waziwazi na Watch Tower Society, wengi katika idara ya uandishi ya mashirika, pamoja na Mashahidi kadhaa wakuu, Wazee, na waangalizi-wasimamizi , walidokeza kuwa utawala wa milenia wa Kristo juu ya dunia. utaanza mwaka 1975.”

Kuanzia mwaka 1975 JW's waliuza nyumba zao, waliacha kazi zao, walitumia akiba zao bila mpangilio, au wakongeza deni la maelfu ya dola. Ila, 1975 ilipita kwa bahati mbaya. Baada ya kutokuwepo kwa tukio hili, watu wengi waliacha JW na ilichukua, kulingana na vyanzo vyao wenyewe, hadi 1979 kabla ya idadi kurudi na kuongezeka tena. Mashahidi walishikilia rasmi kwamba Har–Magedoni ingefika huku kizazi kilichoona 1914 kikibaki hai. Kufikia 1995, kwa sababu ya kupungua kwa kasi kwa idadi ya wanachama walio hai katika mwaka wa 1914, JW's walilazimika kuacha rasmi moja ya sifa zao kuu.

Leo Mashahidi wanadai kuwa 1914 ni mwaka wa maana sana, unaotia alama ya mwanzo wa “siku za mwisho.” Lakini hawatoi tena ratiba yoyote ya matukio kwa tamati ya “siku za mwisho,” wakipendelea kusema kuwa kizazi chochote ambacho kimeishi tangu 1914 kinaweza kuwa ndicho kitakachoona Har–Magedoni. Inaeleweka kuwa Har–Magedoni itahusika na kuharibiwa kwa serikali zote za kidunia na Mungu, na baada ya Har–Magedoni, Mungu atapanua ufalme wake wa mbinguni kkuuweka duniani.[5]

JW's wanaamini kwamba wafu watafufuliwa hatua kwa hatua hadi kwenye “siku ya hukumu” itakayodumu kwa miaka elfu moja na kuwa hukumu hii itategemea matendo yao baada ya ufufuo, wala si matendo ya wakati uliopita. Mwisho mwa ile miaka elfu moja, jaribu la mwisho litatokea Shetani atakaporudishwa ili kuwapotosha wanadamu wakamilifu na matokeo yatakuwa jamii ya wanadamu iliyojaribiwa kikamilifu na kutukuzwa.[6]

Je, tafsiri hii ya “siku za mwisho” inalingana vipi na Uislamu? Tofauti kubwa na iliyo dhahiri ni kwamba Uislamu hautabiri tarehe ambayo siku za mwisho zitaanza wala hautabiri tarehe ya Siku ya Kiyama, ni Mwenyezi Mungu pekee ndiye anayejua itatokea lini.

Watu wanakuuliza khabari ya Saa (ya Kiyama). Sema: Ujuzi wake uko kwa Mwenyezi Mungu. (Kurani 33:63)

Hakika Saa itakuja bila ya shaka. Nimekaribia kuificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyo yafanya. (Kurani 20:15)

"Sema: Hapana katika mbingu na ardhi ajuaye ya ghaibu isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Wala wao hawajui lini watafufuliwa. "(Kurani 27:65)

Tofauti nyingine kubwa ni dhana ya Siku ya Mwisho, wakati Wakristo na Wakristo bandia wanaamini katika vita vya mwisho kati ya wema na uovu, inayojulikana kama Har-Magedoni, hakuna kitu kama hicho katika Uislamu. Uislamu unafundisha kwamba ulimwengu huu wa sasa uliumbwa ukiwa na mwanzo mahususi na utakuwa na mwisho mahususi wenye alama za matukio ya eskatolojia. Matukio haya ni pamoja na kurudi kwa Yesu. Wakati wa kihistoria utafikia mwisho na utafuatiwa na ufufuo kwa wanadamu wote na hukumu ya mwisho.

Katika sehemu ya 3 tutajadili imani nyingine zinazoonekana kuwa sawa na Uislamu lakini hazina dhana ya msingi inayokubalika kwa Waislamu. Pia tutachunguza kwa ufupi kwa nini baadhi ya imani hizo zimesababisha madhehebu kadhaa ya Kikristo kukataa madai ya Mashahidi wa Yehova kuwa kikundi cha Kikristo.



Rejeleo la maelezo:

[1] (http://www.opc.org/qa.html?question_id=176)

[2] (http://www.watchtowerinformationservice.org/doctrine-changes/jehovahs-witnesses/#8p1)

[3] Ibid.

[4] Vita vya mwisho kati ya wema na uovu vinavyotetewa na madhehebu mengi ya Kikristo.

[5]Mnara wa Mlinzi, matoleo mbalimbali, ikiwemo Mei 2005, Mei 2006 na Agosti 2006.

[6] Ibid.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa