Uislam ni nini? (sehemu ya 2 kati ya 4): Asili ya Uislamu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jukumu la Uislamu katika didi zingine za ulimwenguni, Hususani katika uhusiano na Mila ya Ukristo wa Kiyahudi.

  • Na M. Abdulsalam (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 12
  • Imetazamwa: 6,582 (wastani wa kila siku: 8)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Ila wapi ujumbe wa Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, unakaa kwenye jumbe zilizofunuliwa mwanzo na Mungu? Historia fupi ya mitume itaonyesha hili.

Mwanadamu wa kwanza, Adamu, aliufuata Uislamu, katika hilo alielekezwa kumuabudia Mungu peke yake na siyo mwingine na kutii amri zake. Ila baada ya muda kupita na kutawanyika kwa watu duniani kote, watu walitoka katika ujumbe huu na kuanza kuwaabudia wengine badala ya au pamoja na Yeye. Baadhi waliamua kuwaabudia wachamungu waliokufa katika wao, na wengine waliamua kuabudia roho na nguvu za asili. Hapo ndipo Mungu alipoanza kutuma wajumbe kwa wanadamu ili kuwarudisha katika kumuabudu Mungu Pekee, kulingana na asili yao, na kuwaonya na matokeo mabaya ya kuwaabudia wengine badala ya Yeye.

Miongoni mwa Wajumbe wa awali hawa alikuwa Nuhu, ambaye alitumwa kuhubiri ujumbe huu wa Uislamu kwa watu wake, baada ya kuwaabudia wachamungu wa wazee wao na Mungu. Nuhu aliwaita watu wake kuacha kuabudia masanamu, na kuwaamuru kurudi kumwabudia Mungu Pekee. Baadhi walifuata mafundisho ya Nuhu, wakati wengine wengi hawakumuamini. Wale waliomfuata Nuhu walikuwa wafuasi wa Uislamu, au Waislamu, na wale ambao hawakufuata, walibaki kwenye kutokuamini na walipotezwa kwa adhabu kwa kufanya hivyo.

Baada ya Nuhu, Mungu alituma wajumbe katika kila Nchi ambao walipotea kutoka kwenye ukweli, ili kuwarudisha. Ukweli huu ulikuwa katika muda wote: kukataa vitu vyote vya kuabudu na kumuabudia bila shaka Mungu na siyo yoyote, Muumbaji na Mola wa wote, na kutii sheria Zake. Ila kama tulivyosema kabla, sababu kila nchi ipo tofauti na jinsi wanavyoishi, lugha, na tamaduni, wajumbe mahususi walitumwa katika nchi mahususi katika kipindi cha wakati mahususi.

Mungu ametuma wajumbe katika mataifa yote, na katika utawala wa Babiloni alimtuma Ibrahimu – mmoja wa mitume ya mwanzo na wakubwa – ambaye aliwaita watu wake kukataa kuwaabudia masanamu ambayo walijitoa kwao. Aliwaita kwenye Uislamu, ila wakamkataa na hata wakataka kumuua. Mungu alimjaribu Ibrahimu kwa majaribu mengi, na akaishinda yote. Kwa kafara zake nyingi, Mungu akatangaza kuinua taifa kubwa katika kizazi chake na kutoa manabii. Kila mara watu kutoka katika kizazi chake walipoanza kupotea kutoka kwenye Ukweli, ambao ulikuwa kumuabudia Mungu peke yake na kufuata sheria zake, Mungu aliwatumia mjumbe mwingine kuwarudisha kwenye njia.

Hivyo, tunaona wajumbe wengi walitumwa katika kizazi cha Ibrahim, kama vile watoto wake wawili Iskhaka na Ismaili, pamoja na Yakobo (Israeli), Yusufu, Daudi, Sulemani, Musa, na bila shaka, Yesu, kwa kutaja wachache, amani na baraka za Mungu ziwe juu yao. Kila mtume alitumwa kwa wama wa Israeli (Wayahudi) walipotoka katika dini ya Mungu, na walikuwa na jukumu la kufuata ujumbe ambao uliletwa kwao na kutii sheria zake. Wajumbe wote walikuja na ujumbe sawa sawa, kukataa kuabudu viumbe vyote ila Mungu pekee na kutii Sheria Zake. Baadhi walikuwa hawawamini mitume, wakati wengine waliwaamini. Wale walio waamini walikuwa wafuasi wa Uislamu, au Waislamu.

Miongoni mwa wajumbe alikuwa Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, kutoka katika kizazi cha Ismaili, mtoto wa Ibrahim, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, ambaye alituma mjumbe katika mfululizo na Yesu. Muhammad alihubiri ujumbe ule ule wa Uislamu kama mitume na wajumbe – Kupeleka ibada zote kwa Mungu na siyo mwingine na kutii sheria Zake – ambapo wafuasi wa mitume iliyopita walipotea.

Hivyo kama tulivyoona, Mtume Muhammad hakuwa muanzilishi wa dini mpya, kama watu wengi wanavyokosea kufikiria, ila alitumwa kama Mtume wa mwisho wa Islam. kwa ufunuo wa mwisho kwa Muhammad, ambao ni wa milele na, wa kilimwengu kwa wanadamu, Hatimae Mungu alitimiza agano lake aliloliweka kwa Ibrahim.

Kama ilivyokuwa juu ya wale walio hai kufuata ujumbe wa mwisho wa Mitume uliotumwa kwao, Imekuwa wajibu kwa wanadamu wote kuufuata ujumbe wa Muhammad. Mungu ameahidi kuwa ujumbe huu utabaki bila kubadilika na kuweza kukidhi kwa muda wote na sehemu yoyote. Inatosha kusema Uislamu ni njia ile ile ya Ibrahim, kwa sababu vyote Biblia na Kurani vinamwelezea Ibrahimu kuwa mfano mzuri kama mtu aliyejisalimisha kikamilifu kwa Mungu na kumuabudia Mungu pekee na sio mwingine, bila waombezi wengine. Hili likieleweka, itajulikana kuwa Uislamu una ujumbe unaoendelea na, wa kilimwengu ukilinganisha na dini nyingine, kwa sababu mitume yote na wajumbe walikuwa “Waislamu”, mf. wale wanaojisalimisha kwa mapenzi ya Mungu, na walihubiri“Uislamu”, mf. kujisalimisha katika mapenzi ya Mungu mtukufu kwa kumuabudu Yeye Peke na kutii Sheria zake.

Hivyo tumeona wale wanao jiita Waislamu leo hawafuati dini mpya; bali wanafuata dini na ujumbe wa manabii na wajumbe ambao ulitumwa kwa wanadamu kwa amri ya Mungu, pia inajulikana kama Uislamu. Neno “Islam” ni neno la Kiarabu ambalo linamaana ya “kujisalimisha kwa Mungu”, na Waislamu ni wale kwa ridhaa zao hujisalimisha na, kwa bidii humtii mungu, huishi kulingana na ujumbe Wake.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.