Sam, Mwagnosti wa Zamani, Uingereza

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi tabia njema za Waislamu na hekima katika mafundisho ya Uislamu zilimvutia Sam kwa Uislamu.

  • Na Sam
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,015 (wastani wa kila siku: 1)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Nadhani nilikuwa na ufahamu wa Uislamu kwa mara ya kwanza baada ya kutazama filamu ya Spike Lee ya Malcolm X. Ingawa Taifa la Uislamu la Amerika ni harakati ya kisiasa, Malcolm X alibadilisha dini yake na kuingia katika Uislamu wa Kiorthodoksi baada ya kwenda Hajj. Nilivutiwa hata wakati huo nilipokuwa na umri wa miaka 15, jinsi mhuni wa mtaa anaweza kuibadilisha kabisa malezi na silika yake na kuwa balozi wa uhuru na masuala ya kiroho. Ingawa wakati huo, nilikuwa najishughulisha zaidi na shughuli za kidunia; Kulewa, matumizi ya madawa ya kulevya na wanawake ndivyo vilikuwa vipaumbele vyangu vya kwanza, na vilionekana kuwa ni vipaumbele vya kila mtu mwingine pia. Ingawa wazazi wangu walinilea vizuri, sikuweza kupinga ushawishi ulionizunguka, na kama kijana wa familia maskini, nilianza kuiba ili kutimiza mambo haya. Nilijikosea heshima mwenyewe, na kuwakosea marafiki zangu wa kike na wazazi wangu wote. Ilikuwa njia ya ubinafsi na yenye uharibifu. Nilibadilika kuwa mtu bora wakati nilisuhubiana na familia ya Kiislamu walionialika kuishi nao. Mke na mama wa familia alinifundisha mambo mengi ya Uislamu, na kwamba niheshimu wazazi wangu na nijiheshimu mimi mwenyewe, na nikule chakula cha halali na nisiingize sumu mwilini. Walinifundisha kuwa na upendo, wema na hisani na pia kuwa mnyenyekevu. Niliona hekima katika hili na kupata furaha kwa muda mfupi nilipofuata mfano wake. Wakati huo , nilikuwa na umri wa miaka 19. Kwa bahati mbaya, mume wa mwanamke huyu mzuri hakuwa Muislamu mzuri, na alikuwa mwizi na muuzaji wa madawa ya kulevya, na nikaanza kufuata mfano wake vilevile, jambo ambalo lilikinzana na mabadiliko yangu ya awali.

Tulipotengana, nilikuwa mtu bora mwenye maadili bora zaidi. Nilimwamini Mungu sasa, nikawa nala halal tu, na nilikuwa nikiwaheshimu wazazi wangu, nikatoa sadaka na kuwa mnyenyekevu, na sikuiba, lakini bado sikuwa Muislamu. Kwa kuwa nilikuwa mtu wa kukesha sana, nilifikiri haiwezekani kwangu kuswali sala ya Fajr. Pia sikuamini ningeweza kusema dua za Kiarabu na kujitolea kuachana na pombe na wanawake. Pia sikuwa na uhakika kuhusu dini gani ilikuwa sahihi kwani nilikuwa na marafiki wengi wazuri wahindu pia. Lakini ilikuwa ni mwanzo.

Kwa miaka 16 iliyofuata, nilifanya kazi, na nilisoma na hatua kwa hatua nilijiinua mwenyewe hadi nikafika cheo cha heshima katika jamii, nilipata shahada nzuri katika uhuishaji na nikawa mchoraji mzuri. Nilimuoa mwanamke mzuri na kuzaa msichana na mvulana (pamoja na msichana kutoka ndoa ya awali ya mke wangu). Nilikuwa nimekutana na Waislamu wengi wa Uingereza, na nilihisi mshikamano nao na kuheshimu njia zao, daima nikiwatetea katika majadiliano na kuwaheshimu. Tulitembelea Uturuki mwaka wa 2010 na ilinifungulia macho kuona jinsi Waislamu wa Kituruki walivyoongozwa na familia, walivyokuwa na urafiki na wasio na pupa. Kisha mnamo Agosti 2011, katika mwezi wa Ramadhani, tulitembelea kama familia mji wa Luxor nchini Misri wakati wa likizo. Mimi na mke wangu tulishangazwa na ukarimu wa waislamu wa Misri , ingawa walikuwa maskini sana. Ukweli kwamba wangeweza kufunga kwa masaa 15 kwa siku katika joto kali na bado kuwa na wema na upendo, hasa kwa watoto wetu. Hapa palikuwa na watu walioweka mbele upendo na undugu kabla ya utajiri na mali. Familia yetu ilikaribishwa katika familia ya mwendeshaji farasi maskini ambaye alitupeleka nyumbani kwake ndogo na kutupatia vyakula vizuri. Mwishoni mwa kila siku tungealikwa kula kwa upande wa barabara na wageni tusiowajua katika sherehe ya kuvunja swaumu.

Nilianza kutazama kwa kina uzuri wa Uislamu, mafundisho ya Uislamu, na maisha ya Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake. Nilianza kutazama misingi yote ya imani ya Kiislamu na kustaajabia kila mmoja. Jinsi Waislamu walivyoomba na kujinyenyekeza mbele ya Mwenyezi Mungu mara 5 kwa siku, ilikuwa kama ukumbusho wa mara kwa mara kwamba walikuwa wafu na walifuata nguvu ya juu. Kufunga kulikuwa kama ukumbusho kwamba mtu anafaa kuwasaidia mafukara na kumshukuru Mungu kwa baraka zake. Jinsi Waislamu walivyofuata mfano wa Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, hakika ilikuwa kitu cha kushangaza.

Mambo ambayo awali yalikuwa yamenifanya niepukane na dini kupitia “jicho la kimagharibi” sasa yalikuwa na maana kamili kwangu. Tuliporudi kutoka Misri sikuweza kupata amani. Nilitaka kujiunga na Uislamu lakini sikutaka kufanya hivyo iwapo mke wangu mpendwa hakufanya hivyo. Nilisoma kuhusu utafiti wa kisayansi uliofanywa kuhusu Qurani kutoka duniani kote, kama vile maelezo ya hatua zinazoendelea za mtoto mchanga akiwa tumboni, na kwamba mtu aliyeishi miaka 1500 iliyopita hakuweza kujua mambo kama hayo, na kwamba ilikuwa ni ushahidi kwamba Qurani ilikuwa neno la Mungu , na hii ilikuwa kichocheo kwangu. Hapa palikuwa na ushahidi wa kisayansi kwa kitu kilichoonekana vinginevyo kama jambo la imani pekee. Niliamua kuingia uislamu na kuomba kwamba mke wangu angenifuata baada ya kuona mabadiliko yaliyoletwa na uislamu kwangu. Nilikuwa na wasiwasi kuhusu kujifunza dua za Kiarabu, lakini ndani ya muda wa mwezi mmoja tu nilikuwa nimezihifadhi kwa urahisi hadi kiwango cha juu. Sasa niko katika amani kabisa na nafsi yangu na Mwenyezi Mungu. Ingawa mke wangu bado hajaongoka, anamwamini Mungu na ni mtu mwema, na anaunga mkono sana uchaguzi wangu na anawalea watoto wetu wawili kama Waislamu.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa