Vyanzo vya Uislam: Kurani na Sunnah (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Dini ya Uislamu imejengwa na Kurani (Neno la Mungu) na Sunnah (mafundisho na sifa za Mtume Muhammad). sehemu ya 1: Kurani: Chanzo cha kwanza cha Uislam.

  • Na islaam.net
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,431
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Islamic-Sources-Part-1.jpgUfunua wa mwisho wa neema ya Mungu kwa mwanadamu, hekima ya mwisho, na uzuri wa mwisho wa wazo: kwa kifupi, neno la Mungu. Hivi ndivyo Msomi wa Kijerumani, Muhammad Asad, pindi alipoielezea Kurani. Iwapo mtu angelimuuliza Muislam yoyote kuifafanua, kuna uwezani mkubwa wakusema maneno sawa. Quran, kwa Muislam, ni takatifu, neno la Mungu lisilo na mfano. Ilifunuliwa na Mungu Mtukufu, kwa kupitia njia ya Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake. Mtume mwenyewe hakuwa na jukumu la kuiandika Kurani, alikuwa ni Mjumbe tu, akirudia maono ya Mtukufu Muumba:

“Wala hatamki kwa matamanio.Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa; .” (Kurani 53:3-4)

Kurani ilifunuliwa kwa Kiarabu, kwa Mtume Muhammad, katika kipindi cha miaka ishirini na tatu. Imeundwa katika mdindo wa kipekee, kwamba haiwezi kuchukuliwa kama shairi au nathari, ila kwa jinsi flani ni mchanganyiko wa vyote. Kurani haina mfananisho wake; haiwezi kuigwa wala kunakiliwa, na Mungu Mtukufu ametoa mtihani kwa binadamu kujaribu kama wanahisi wanaweza:

“ Ama wanasema ameizua? Sema: Hebu leteni sura moja mfano wake na muwaite (kukusaidieni) muwawezao, isipo kuwa Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.” (Kurani 10:38)

Lugha ya Kurani hakika ni ya mafumbo, usomaji wake unavutia, kama mmoja ya msomi asiye Muislam alivyo elezea, “kilikuwa kitulizo cha mapigo yangu ya moyo”. Juu ya mtindo wa kipekee wa lugha, Kurani siyo tu inasomeka sana, ila pia ni rahisi kukumbukwa. Katika hali hii ya mwisho imekuwa na jukumu kubwa siyo tu katika uhifadhi wa Kurani,buli hata katika maisha ya kiroho kwa Waislam pia. Mungu mwenyewe amesema,

“Na kwa hakika, Sisi tumeisahilisha Kurani ifahamike (upesi), lakini je, yupo anayekumbuka?” (Kurani 54:17)

Moja ya sifa muhimu ya Kurani ni kwamba imebaki hadi leo, kitabu pekee cha dini ambacho hakijabadilika; kimebaki huru kutoka kwenye uchafuzi wowote. Bwana William Muir ameeleza, “Inawezekana ikawa kitabu pekee duniani kilichokaa karne (kumi na nne) kikiwa na maandishi safi.”The Kurani was written down during the lifetime and under the supervision of the Prophet, who himself was unlettered. Thus its authenticity is unblemished, and is its preservation is seen as the fulfillment of God’s promise:

“Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutakaoilinda.” (Kurani 15:9)

Kurani ni kitabu ambacho kinampa mwanadamu lishe ya kiroho na kiakili anayotamani. Mada yake kuu ikiwemo Mungu kuwa Mmoja, kusudi la uwepo wa mwanadamu, imani na utambuzi wa Mungu, Maisha ya baadae na umuhimu wake. Kurani pia inaweka umuhimu mkubwa wa sababu na uelewa. Ndani ya duara hili la uelewa wa mwanadamu, Kurani inakwenda zaidi katika kuiridhisha akili ya mwanadamu; inasababisha mtu kujitafakari. Tofauti na maandiko mengine, Kuna maswali ya Kurani na utabiri. imejaa ukweli ambao umekuja kutambulika hivi karibuni; Sehemu moja ya kufurahisha ambayo imegunduliwa hivi karibuni ni kuwa na taarifa nyingi za kisayansi katika Kurani, ikiwemo tukio la bigibengi, taarifa za embryolojiko, na taarifa nyingine zinazohusu unajimu baioloji, nk., hakuna taarifa hata moja ambayo haijathibitishwa na vumbuzi za kisasa. Kwa kifupi, Kurani inakamilisha moyo, roho, na akili. Labda wasifu bora wa Kurani ulitolewa na Ali, mpwa wa Mtume Muhammad alipokuwa akifafanua kuwa,

“Ni Kitabu cha Mungu. Ndani yake kuna nakala ya yaliyopita, hukumu ya kile kilichopo kati yenu, na ubashiri wa nini kitakuja baada yenu. ni maamuzi, siyo swala la utani. Yoyote aliye dhalimu na kuipuuza Kurani ataangamizwa na Mungu. yoyote mwenye kutafuta mwongozo kwa wengine bila Mungu atapotezwa. Kurani ni fundo lisilovunjika la muunganiko na Mungu; ni ukumbusho wa hekima na njia iliyo nyooka. Kurani haiwezi kuja kupotoshwa na ndimi; wala haiwezi kubadilika kwa upotovu. Haikinaishi kutokana na utafiti unaorudiwa; Wasomi mara zote wataitaka zaidi. Maajabu ya Kurani hayawezi kuisha. Yeyote mwenye kuongea nayo ataongea ukweli, yoyote atakaye tawala nayo atakuwa muadilifu, na yoyote atakaye ishikaataongozwa katika njia iliyo nyooka.” (Al-Tirmidhi)

Mbaya Nzuri zaidi

Vyanzo vya Uislam: Kurani na Sunnah (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Dini ya Uislamu imejengwa na Kurani (Neno la Mungu) na Sunnah (mafundisho na sifa za Mtume Muhammad). sehemu ya 2: Sunnah: Chanzo cha Pili cha Uislamu

  • Na islaam.net
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,157
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Sunnah

Neno Sunnah linatokana na neno sanna, likimaanisha kuweka nafasi au kufanya njia ipitike kirahisi, hivyo ikaja njia ya kufuatwa na kila mtu baadae. Hivyo Sunnah inaweza kutumika kuelezea mtaa au barabara au njia ambayo watu, wanyama, na magari yanasafiri. Cha kuongezea, inaweza kutumika kwa njia ya kinabii, mf. sheria ambayo waliileta kama ufafanuzi au maelezo zaidi ya kitabu kilichofunuliwa na Mungu. Kwa kawaida, njia ya kinabii inahusisha marejeo ya aliyosema, vitendo, sifa za kimwili na tabia.

Kutoka katika mtazamo wa Kiislam, Sunnah inamaanisha kitu chochote kilichosemwa au kumuhusu Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, inafuatiliwa kwa kuthibitisha kwake ikihusisha mafunzo yake, vitendo, sifa, na idhini ya kimya kimya.

Kila simulizi imeundwa na sehemu mbili: isnad na matn. Isnad inahusisha mlolongo wa watu ambao wamesimulia kisa flani. Matn ni maandishi halisi ya kisa. Isnad lazima iwe na watu waadilifu na wakweli ambao uadilifu wao hauna shaka.

Maneno ya Mtume Muhammad

Maneno ya Mtume Muhammad yanachukuliwa kama misemo yake. Kwa mfano, alisema:

“Vitendo uhukumiwa kutokana na makusudio; kila mtu hutunzwa kulingana na makusudio yake. Hivyo mtu yoyote mwenye kuhama kwaajili ya Mungu na Mtume Wake basi uhamaji wake utanakiliwa kwasababu ya Mungu na Mtume Wake. kinyume chake, mtu akihama kwaajili ya sababu ya kidunia au kuoa, basi kuhama kwake kutakuwa na thamani ya alichokusudia.” (Saheeh Al-Bukhari)

Mtume pia amesema:

“Mtu yoyote mwenye kumuamini Mungu na Siku ya Mwisho, anatakiwa aseme kitu kizuri au akae kimya.”

Simulizi hizi mbili za juu zinaonyesha wazi kuwa Mtume ameongea maneno hayo. Kwa hivyo, hizi zinajulikana kama simulizi zake.

Vitendo vya Mtume Muhammad

Matendo yake yanamaana chochote alichokifanya, kama ilivyo thibitishwa na Sahabah (Maswahaba). Kwa mfano, Hudhayfah ameeleza kuwa Kila mtume akiamka usiku, alikuwa akisafisha meno yake na mswaki. Pia Aishah ameeleza kuwa Mtume anapenda kufanya kila kitu katika upande wake wa kulia - kuvaa viatu, kutembea, kujisafisha, na mambo yake yote kiujumla.

Idhini ya Kimya Kimya ya Mtume Muhammad

Idhini yake ya kimya kimya inamaana hapingi au kujali alichokiona, kusikia au kujua vitendo au misemo ya maswahaba zake. katika kipindi kimoja, kwa mfano, Mtume alijifunza vitendo vya baadhi ya maswahaba kutoka kwa maswahaba wengine. Mara baada ya vita ya Khandaq, Mtume Muhammad aliwaamuru maswahaba wake kwenda haraka kwenye kabila la Banu Quraydah, aliwahimiza kuharakisha ili angalau waswali Asr (swala ya jioni) kule. Baadhi ya maswahaba waliitikia haraka na kuondoka bila kuswali Asr. Walifika jioni, wakaweka kambi na kuswali Asr- baada ya jua kuzama. Muda huo huo, kundi lingine la maswahaba walitengeneza shauri lao kitofauti. Walifikiri Mtume aliwahimiza wafike haraka tu uko wanakokwenda, badala ya kuchelewesha Asr mpaka jua kuzama. Hivyo, waliamua wakae Madinah mpaka wawe wameswali Asr. Maramoja baada ya hapo walielekea kwenye kabila la Banu Quraydhah. Pindi Mtume alipoambiwa jinsi kila kundi lilivyoitikia tofauti maelekezo yake, aliyakubali mawazo ya wote.

Tabia za Kimwili na Kimaadili za Mtume Muhammad

Kila kitu kilichothibitishwa kinachosimuliwa kumuhusu Mtume kufanya na sifa zingine za mwili pia zinahusika katika maana ya Sunnah. Umm Ma’bad anasimulia aliona nini kwa Mtume. Anasema:

“Nilimuona mwanaume, uso wake uling'aa na mwanga mkali, sio mwembamba wala mnene, msafi na mtanashati. Macho yake yalikuwa na kiini cheusi yakiwa na kope ndefu. Sauti yake ilikuwa ya kupendeza na shingo yake ilikuwa ndefu. Alikuwa na ndevu nyingi. Nyusi zake ndefu zilikuwa zimepinda vizuri na zimeungana. kwa ukimya, alibaki kuwa na adabu, kuamrisha kwa hofu na kwa heshima. Kama akiongea, mazungumzo yake yalikuwa mazuri. kwa watu wote alikuwa ni mtanashati na msafi, hata akija kwa mbali. Ana kwa ana, alikuwa wa kipekee na kupendeza. haiba ya ufasaha, maongezi yake yalikuwa mazuri. Hoja zake zilikuwa zina mantiki kama zilikuwa safu za vito. Hakuwa mrefu wala mfupi, bali wa katikati. Katika watatu, anaonekana kwenye kun'gaa na imara. alikuwa na maswahaba ambao walimuheshimu. Alipokuwa akiongea, walikuwa wakimsikiliza kwa umakini mkubwa. Pindi akitoa amri, walikuwa kwa haraka wanatekeleza. Walijikusanya kwake wakimlinda. Hakuwahi kukunja uso wala kuongea upuuzi.” (Hakim)

Pamoja na wasifu wake, Masahaba zake wanasimulia tabia zake na tabia zake kwa watu. Anas anasimulia:

“Nimemtumikia Mtume wa Allah, amani iwe juu yake, kwa miaka kumi. kipindi iko chote, hajawahi kuongea sana zaidi ya ‘Oof’kama nikifanya kitu kibaya. Hajawahi kuniuliza, kama nimeshindwa kufanya kitu, ‘Kwanini haujafanya?,’ na hajawahi kuniambia, kama nimefanya kitu kibaya, ‘Kwanini umefanya?’”

Kutoka juu tumeona vizuri kuwa neno Sunnah linapoonekana katika muktadha wa jumla humuhusisha Mtume Muhammad hii inajumuisha chochote kinachosimuliwa kuhusu Mtume na kimethibitishwa kuwa kinatoka kwake. Pindi Muislamu anapojifunza uthibitishwaji wa simulizi zozote anawajibu wa kuufuata. Utiifu huu ni walazima kwa Mungu kama Alivyoeleza:

“... Mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, wala msijiepushe naye, nanyi mnasikia.” (Kurani 8:20)

Wakati mwingine,baadhi ya Waislamu wanashangaa watu wanaposema Sunnah ni kitu kilichopendekezwa tu na siyo cha lazima. Hivyo wanahitimisha kuwa tunatakiwa kufuata Kurani na siyo Sunnah. Hoja kama hiyo inaleta kutokuelewana Wasomi wa Kiislamu wa sheria hutumia neno Sunnah kuonyesha yepi yamethibitishwa kuanzishwa na Mtume Muhammad aidha ambayo hayakufanywa ya lazima na Mungu.

Wanazidi kushikilia kuwa hii inajumuisha misemo yoyote ya Mtume Muhammad ambapo aliwahimiza kufanya jambo flani na kuwapongeza wale ambao wamedumisha sifa hiyo. Hivyo kwao, neno Sunnah linahusisha nini kilicho “pendekezwa” na siyo cha lazima (fard au wajib).

Kutoka juu, tunaweza kuona vizuri kuwa neno Sunnah linachukua maana tofauti tofauti pindi linapotumiwa katika nidhamu za Uislamu.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.