Ukanaji Mungu (Sehemu 1 kati ya 2): Kukataa Kisichokatalika

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Ingawa mtu anaweza kukataa kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, lakini ndani ya moyo wake, ni ukweli ambao hawezi kuukanusha.

  • Na Laurence B. Brown, MD
  • Iliyochapishwa mnamo 29 Nov 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 31 Jan 2024
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,274
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Janga kubwa la maisha ni kumpoteza Mungu na kutotamani kurudi kwake.”

--F.W. Norwood

Atheism_(part_1_of_2)_001.jpgWakanaji Mungu wanaweza kudai kwamba hawakubali kuwepo kwa Mungu, lakini mtazamo wa baadhi ya Wakristo na Waislamu wote ni kwamba kwa kiwango fulani hata yule mkanaji sugu anakubali uwepo wa Mungu. Ufahamu wa ndani uliopuuzwa wa uwepo wa Mungu kawaida hujitokeza tu katika akili za Wakanaji kwenye nyakati za dhiki nyingi, na mfano bora ni dondoo hili la Vita vya Pili vya Dunia “Hakuna Wakanaji Mungu kwenye mashimo ya vita.”[1]

Bila shaka kuna nyakati - iwe siku za uchungu wa ugonjwa usioisha, au nyakati za udhalilishaji usioisha, au sekunde chache kabla ya ajali ya gari - ambapo wanadamu wote wanatambua ukweli wa udhaifu wa mwanadamu na kuwa hana udhibiti juu ya hatima na majaliwa. Mtu humwomba nani msaada katika hali kama hizo isipokuwa Muumba? Nyakati hizo za kukatatisha tamaa zinapaswa kumkumbusha kila mtu, awe ni msomi wa dini au Mkanaji sugu, kuhusu utegemezi wa wanadamu kwa Kitu kikubwa zaidi kuliko maisha yetu wenyewe ndogo. Kitu kikubwa zaidi kwa ujuzi, nguvu, dhati, adhama na utukufu.

Katika nyakati hizo za dhiki, wakati jitihada zote za binadamu zimeambulia patupu na hakuna kitu kingine duniani kinaweza kuwa na uwezo wa kuleta faraja, Nani mwingine wa kuombwa? Katika nyakati hizo za majaribio, ni dua ngapi, zinazosababishwa na matatizo, zinaombwa kwa Mungu, zikiwa na ahadi za kuwa wanyenyekevu baada ya hapo? Hata hivyo, ni ahadi zipi chache hutimizwa?

Bila shaka siku ya dhiki kubwa kabisa itakuwa Siku ya Kiyama. Na mtu atakuwa ni mwenye bahati mbaya iwapo atamwamini Mungu kwa mara ya kwanza kwa siku hiyo. Mshairi wa Kiingereza, Elizabeth Barrett Browning, alikejeli kilio cha mwanadamu akiwa kwenye masaibu katika kilio cha Binadamu:

“Na midomo inasema “Mungu nionee huruma,”

Na ni nani ambaye hayajawahi kusema, “Mwenyezi Mungu atukuzwe”

Anayemkana Mwenyezi Mungu mwenye tafakuri zake, akiwa na shaka kubwa lakini anaogopa uwezekano wa kuwepo kwa Mungu na Siku ya Hukumu, anaweza kukubali 'dua ya wasio na hakika, 'kama ifuatavyo:

“Ewe Mola--ikiwa kuna Mola,

Okoa roho yangu--ikiwa nina roho.”[2]

Mbele ya shaka inayozuia imani, mtu anawezaje kupotea akiwa na dua iliyopo hapo juu? Ikiwa wakanaji watabaki kwa ukufuru wao, hawatakuwa wamepoteza chochote. Ikiwa Imani itafuata dua hiyo, Thomas Jefferson anasema yafuatayo:

“Ikiwa unapata sababu ya kuamini kuwa kuna Mungu, ufahamu kwamba upo chini ya ulinzi wake, na kwamba Anakukubali, itakuwa uhimizi mkubwa zaidi; ikiwa kutakuwa na hali ya baadaye, matumaini ya kuwepo kwa furaha inayoongeza hamu ya kuistahili...”[3]

Pendekezo linaweza kufanywa kwamba ikiwa mtu haoni ushahidi wa kuwepo kwa Mungu katika ukubwa wa uumbaji wake, wangeshauriwa kutazama mara nyingine. Kama Francis Bacon anavyoeleza kwa maoni yake, “Afadhali niamini hurafa zote za kale , na Talmud, na alkoran (yaani Kurani), kuliko kuamini kwamba ulimwengu huu hauna muumba.” [4] Aliendelea kutoa maoni, “Mungu hakuleta miujiza kuwashawishi Wakanaji Mungu, kwa sababu kazi zake za kawaida zina ushawishi wa kutosha.” [5] Jambo linalostahili kufikiriwa ni kwamba hata viumbe vidogo kabisa vya Mungu, ingawa uumbaji wake ni wa kawaida kwake, ni miujiza kwetu. Chukua mfano wa mnyama mdogo kama buibui. Je, kuna mtu yeyote anayeamini kwamba kiumbe hicho cha ajabu kilitokana na supu ya asili (Primordial soup)? Mmoja tu kati ya viumbe hivi vya miujiza anaweza kuzalisha hadi aina saba tofauti za hariri, ambapo baadhi ni nyembamba kama lukoka ya mwanga unaoonekana, lakini imara kuliko chuma. Hariri mbalimbali hutofautiana, kuanzia kwa zile nyumbufu nata za kutumika kwa mnaso, hadi kwa yasiyo ya wambiso na fremu ya nyuzi , pamoja na hariri za kufunikia mawindo, na kutengeneza kifuko yai, nk. Buibui anaweza pia, kulingana na mahitaji, kutengeneza hariri zozote kati ya aina hizo saba, na pia kuzifyonza tena, kuvunja na kutengeneza tena,ujirejelezaji-binafsi, kwa kutumia vipengele vya mwanzo. Na hii ni sehemu moja tu ndogo ya muujiza wa buibui.

Hata hivyo, wanadamu hujiinua kwa kiburi. Mtazamo wa kina unapaswa kuelekeza mioyo ya wanadamu kwa unyenyekevu. Akiangalia jengo mtu anafikiria mchoraji, akitazama uchongaji hufikiria msanii . Lakini kuchunguza utata wa kifahari wa maumbile, kutoka kwa utata na usawa wa fizikia ya nyuklia ya chembe hadi kwa ukubwa wa anga, na mtu hafikirii chochote? Tukizungukwa na ulimwengu wenye utata wa kihandisi, sisi kama wanadamu hatuwezi hata kutengeneza ubawa wa mbu. Na bado dunia nzima na Ulimwengu wote ambao uko katika hali ya usawa kamili ulitokana na ajali za hapa na pale tu ambazo zimepanga msukosuko wa ulimwengu na kuufanya uwe na ukamilifu na uwiano? Baadhi watasema ni ajali tu, na wengine uumbaji.



Rejeleo ya maelezo:

[1] N.Y. Times. 13 Apr 1944. Cummings: Mahubiri ya Bataan, Ufilipino.

[2] Renan, Joseph E. Sala ya Mwenye Mashaka.

[3] Parke, David B. uk. 67.

[4] Bacon, Francis. Atheism p. 16.

[5] Bacon, Francis. Atheism. p. 16.

Mbaya Nzuri zaidi

Ukanaji Mungu (Sehemu 2 kati ya 2): Suala la Ufahamu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kushindwa kuelewa baadhi ya kazi za Mungu sio sababu ya kupuuza kuwepo kwake.

  • Na Laurence B. Brown, MD
  • Iliyochapishwa mnamo 29 Nov 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,668
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Hoja nyingi za Wakanaji Mungu zinaongelea kuhusu uhusiano kati ya Mungu mwenye upendo na dhuluma zinazoonekana maishani. Wenye dini huona kuwa hoja kama hizi zinaonyesha kiburi kwa upande wa mwanadamu — kuwa na dhana kwamba sisi kama wanadamu, ambao sisi wenyewe ni kipengele cha uumbaji, tunajua mengi kuliko Mungu na jinsi uumbaji wake unapaswa kuendelezwa- pamoja na kushindwa kufahamu muundo mkubwa zaidi.

Ukweli kwamba wanadamu wengi wanashindwa kuelewa mambo fulani ya maisha haya haupaswi kuzuia imani kwa Mungu. Wajibu wa mwanadamu si kuhoji au kukataa sifa au uwepo wa Mungu, na si kuwa na kiburi kwa kudai kuwa na uwezo wa kufanya kazi bora zaidi, bali kukubali cheo cha binadamu katika maisha haya na kufanya vizuri iwezekanavyo na kile tulichopewa. Kwa kulinganisha, ukweli kwamba mtu hapendi jinsi bosi wake anavyofanya kazi, na anashindwa kuelewa maamuzi anayofanya, haipuuzi kuwepo kwake. Badala yake, wajibu wa kila mtu ni kutimiza malengo ya kazi yake ili kulipwa na kupewa cheo. Vilevile, kushindwa kufahamu au kuridhishwa na jinsi Mungu anavyoendeleza uumbaji wake haupuuzi kuwepo kwake. Badala yake, wanadamu wanapaswa kutambua kwa unyenyekevu kwamba, tofauti na bosi wa kazini, ambaye anaweza kukosea, Mungu ni wa ukamilifu kabisa, daima mwenye kufanya haki na kamwe hakosei. Binadamu anapaswa kuinama kwake kwa kujisalimisha nakutambua kwamba kushindwa kuelewa muundo wake kwa upande wetu hakumaanishi kuna makosa kwa upande wake. Badala yake, Yeye ni Bwana na Muumba wa Ulimwengu na sio sisi, Yeye anajua yote na sisi hatujui, Anaamuru mambo yote kulingana na sifa zake kamili, na sisi tunabaki tu viumbe vyake, tukiendelea tu kwa ajili ya safari ya maisha yetu.

Mioyo iliyochanganyikiwa na mizito inayoona ugumu katika kupatanisha kuwepo kwa Mungu na aghlabu maisha magumu yenye uchungu mwingi yanahitaji huruma na maelezo ya kina. Ikiwa mtu anakubali ukweli kwamba Mungu anajua anachofanya na sisi hatujui, anapaswa kutulia na kufahamu kwamba mambo yanaweza kuwa tofauti na yale yanayoonekana mwanzoni. Labda waovu miongoni mwa wanadamu wanastahili mateso yao maishani kwa sababu zisizojulikana na wanadamu, na pengine wanakabiliwa na mateso kwa muda mfupi tu wa kidunia ili wapokee thawabu ya milele katika maisha ya Ahera. Asije mtu akasahau, Mwenyezi Mungu aliwapatia viumbe vyake alivyovipenda (k.v. Mitume), zawadi kubwa zaidi duniani, ambayo ni uongofu na ufunuo; ila waliteseka sana kwa mujibu wa kidunia. Kwa kweli, majaribio na dhiki ya watu wengi huwa madogo kwa kulinganisha na yale ya manabii. Hivyo ingawa watu wengi wanateseka sana, ujumbe wa matumaini ni kwamba vielelezo vya Wapenzi wa Mungu, yaani manabii, walikuwa wamenyimwa raha ya dunia hii na badala yake kupewa malipo ya Akhera. Mtu anaweza kutarajia thawabu inayofanana na ya wale wanaovumilia majaribu na shida za maisha haya, huku wakisimama wima kwa imani ya kweli.

Vilevile mtu hawezi kulaumiwa kwa kutazamia madhaalimu makafiri kupata kheri zote za duniani, ila wasipate za Akhera. Baadhi ya wakazi wanaojulikana wa Jahannamu huja akilini. Farao, kwa mfano, aliishi maisha ya raha mustarehe hadi kwamba alijitangaza kuwa mungu mkuu. Kivyovyote, mtu anaweza kutarajia kuwa farao kwa sasa haridhiki akikumbuka kuwa makao yake ya raha, na kumbukumbu ya mazulia yake maridadi, na vyakula anuwai na wasichana wenye harufu nzuri, kwa sasa hawampi raha na faraja tena kutokana na joto la jahanamu .

Watu wengi wamepitia hisia za kumaliza siku nzuri kwa hali mbaya kutokana na tukio baya lililotokea mwisho wa siku hiyo. Hakuna mtu anayethamini chakula kizuri kinachomalizika kwa talaka, au kujamiana kunakoleta UKIMWI, au usiku wa raha unaoisha kwa kuibiwa kikatili au ajali mbaya ya gari . Jinsi gani ingekuwa nzuri? Vile vile, hakuna furaha katika maisha haya, bila kujali ni furaha kiasi gani au wa muda gani, ambao haufutwi hapo hapo kwa asilimia 100 kutoka kwa kumbukumbu baada ya kuchomwa mwili mzima kikamilifu. Upande mmoja wa mkono mmoja unawakilisha asilimia 1% ya jumla ya mwili wa mwanadamu, na kuchomeka jikoni kwa sehemu ya kidole ina wakilisha chini ya asilimia 0.1 ya mwili. Hata hivyo, ni nani asiyesahau kabisa kila jambo ndogo, kila jambo kubwa, kila kitu katika sekunde hiyo ya mateso na maumivu ya moto? Maumivu ya kuchomwa kwa mwili mzima, hasa kama hakuna misaada -- hakuna kuruka nyuma, hakuna kuuvuta mwili mbali -- ni zaidi ya uwezo wa mawazo ya kibinadamu. Wachache ambao wamepona baada ya kuchomeka watakubaliana. Mateso ya kuchomeka mwili mzima hauzidi tu mipaka ya mawazo ya kibinadamu, bali pia uchungu wake unapita mipaka ya kuelezwa kwa lugha yoyote. Hofu haiwezi kuelezwa kwa ukamilifu na waliokuwa na bahati mbaya ya kuipitia, wala kueleweka kikamilifu na wale wenye bahati nzuri ya kuiepuka. Hakika uchomwaji mmoja mreeeeeeefu, wa milele, wa mwili mzima katika moto inaweza kutarajiwa kufuta kumbukumbu zozote nzuri ya zamani, jambo ambalo linaafikiana na hitimisho kwamba

“…Na uhai wa dunia kwa kulingana na Akhera si kitu ila ni starehe ndogo.” (Kurani 13:26)

Kuhusiana na suala la kiambatisho cha sasa [1], mambo mawili ya kuongoza ufahamu yanastahili kuzingatiwa, ya kwanza ni kuwa ndani ya mioyo yao watu wote wana elimu ya asili ya kuwepo kwa Muumba. Binadamu wanaweza kutupilia mbali elimu na ufahamu huu katika pilkapilka za kutafuta urahisi na raha za dunia hii, lakini ndani kwa mioyo yao, wanadamu wote wanajua ukweli huu. Zaidi ya hayo, Mungu anajua kwamba tunajua hili, na Yeye peke yake ndiye anayeweza kuhesabu kiwango cha uasi wa mtu binafsi na/au ujisalimishaji wake.

Kipengele cha pili cha ufahamu wa kiroho ni kuelewa tu kwamba hakuna kitu cha bure maishani. Ni nadra sana kupata kitu bila ya kupeana kingine. Iwapo mtu anafanya kazi kwa bwana ambaye hamuelewi au ambaye hakubaliana naye, hatimaye bado anahitaji kufanya kazi yake ili alipwe. Hakuna mtu anayeenda kufanya kazi (kwa muda mrefu) na asifanye chochote zaidi ya kusema, “Ninafanya kazi,” akitarajia alipwe kwa kuhudhuria tu bila kufanya chochote. Vilevile, mwanadamu lazima atimize wajibu wa utumwa na kumuabudu Mungu ikiwa anatarajia kupokea thawabu yake. Kwani hili si lengo la maisha tu, bali ndio maelezo ya kazi na majukumu yetu. Kwa jambo hilo, Waislamu wanaamini kuwa hayo ndiyo maelezo ya kazi kwa wanadamu na majini (wingi, umoja ni 'Jinn'ee, ambayo ndio asili ya neno la Kimagharibi' genie '), kwani Mungu anaeleza katika Kurani Tukufu:

“Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.” (Kurani 51:56)

Watu wengi wanajiuliza malengo ya maisha, lakini msimamo wa waaminifu wa dini nyingi ni hasa ule uliotajwa hapo juu - wanadamu hawapo kwa sababu nyingine isipokuwa ya kumtumikia na kumwabudu Mungu. Pendekezo ni kwamba kila kipengele cha maumbile kinafanya kazi ya kuwaunga mkono au kuwajaribu wanadamu katika kutimiza wajibu huo. Tofauti na ajira ya kidunia, mtu anaweza kupuuza majukumu yake na bado akapewa kipindi cha kutosha. Hata hivyo, mwishoni mwa kipindi hiki cha majaribio kinachoitwa maisha, akaunti lazima zilipwe, na huo si wakati mzuri wa kupata akaunti ya mtu ina alama 'nyekundu. '

Francis Bacon alitoa hitimisho ya ajabu kwa mada ya kiambatisho hiki, akisema, “Wale wanaomkataa Mungu huharibu utukufu wa mwanadamu; kwa hakika mwanadamu ni wa jamaa moja na wanyama kwa mwili wake; na, kama yeye si wa jamaa moja na Mungu kwa roho yake, yeye ni kiumbe cha msingi kisicho na faida.” [2] Iwapo mtu anaamini kwamba baada ya miaka milioni kitu kinacholingana na nyama choma kitaibuka kutoka kwa povu ya Stanley Miller na Harold Urey ya supu asili, binadamu bado anafaa kueleza kile ambacho sisi wote husikia ndani ya mioyo yetu- yaani roho au nafsi. Kila mwanadamu ana moja, na huu ndio mpaka wa kimetafizikia unaomtenganisha mtu kutoka kwa wanyama.

Pia, wale ambao wana shaka kuhusu yale ambayo hayawezi kuhisika moja kwa moja wanaweza kupata udhuru ya kukataa roho, lakini watakuwa na uwezekano mkubwa wa kujikuta kuwa na elimu chache. Zaidi ya hayo, majadiliano kisha huenda kwa ya asili ya ukweli, maarifa, na ushahidi, ambayo huruka kimantiki kwa sehemu inayofuata, uagnosti.



Rejeleo la maelezo:

[1] Makala hii ni kiambatisho kwa kitabu “The First and Final Commandment” cha mwandishi huyo.

[2] Bacon, Francis. Atheism. uk. 16.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.