Maria Luisa “Maryam” Bernabe, Mkatoliki wa Zamani, Ufilipino (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Hatua zangu ndogo ndogo kuelekea kwa Mwenyezi Mungu na kuingia kwangu katika Uislamu

  • Na Maria Luisa “Maryam” Bernabe
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,370 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Mwenyezi Mungu amenileta hapa Qatar kwa lengo hili, ili nimalize jitihada zangu na kutumia siku zilizobaki za maisha yangu kumwabudu Yeye kwa njia za Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Njia za Mwenyezi Mungu sio njia zetu, kwani Yeye ndiye anayejua zaidi. Hakika, kuhusiana na matukio yaliyotokea katika maisha yangu hapa Qatar, ninatazama nyuma na kuona jinsi alivyonitengenezea njia ambayo imeniongoza kwake.

Mwaka wa 2009, kampuni iliyonileta Qatar ilikuwa imekutana na matatizo na kuanza kuwafuta watu kazi na kuwapa hiari ya kutafuta kazi nyingine. Jinsi nilivyokuja kufanya kazi katika kampuni ambayo nipo kwa sasa pia ni mojawapo ya maajabu mazuri aliyoniwekea Mwenyezi Mungu. Jinsi nilivyobadilisha kazi kutoka kampuni yangu ya awali hadi hii yangu ya sasa ilikuwa njia nyepesi sana. Taasisi ambayo ninafanya kazi ni taasisi ya Kiislamu inayoongozwa na sharia (sheria ya Kiislamu) na idara ninayofanya kazi kwa sasa imenipa fursa ya kutua katika kazi yangu ya ndotoni - mawasiliano ya kikampuni. Kwa kuwa nimezama katika utayarishaji wa majarida na matangazo ya kibiashara, ilibidi nijue vizuri maadili ya ushirika yaliyo katika mwongozo wa Sharia, ambayo imenipelekea kusoma zaidi kuhusu Uislamu. Katika hatua hiyo, Nilijikuta nikifurahia kile nilichokuwa nikifanya na ningesoma chochote nilichoweza kupata.

Mnamo mwaka wa 2010, nilikutana na Muislamu wa Kifilipino. Hakukuwa na mazungumzo yoyote kuhusu dini yetu. Alijua jinsi nilivyokuwa na maombi na sala nyingi kwa sababu ya Rozari yangu na vijitabu vya Novena. Aliniambia kuwa katika familia yake, kuna Waislamu na Wakristo pia. Alinihakikishia kwamba sikuwa na haja ya kuwa na wasiwasi wowote kuhusu hilo kabisa. Nilipata kwake sifa ambazo nimekuwa nikizitafuta. Maoni yake kuhusu uhusiano ni sawa na yangu. Kwa hivyo, dini haikuwa suala na sisi sote tuliheshimu imani zetu.

Wakati mmoja, nilikwenda kwa Fanar (kituo cha utamaduni wa Kiislamu cha Qatar) na bosi wangu wakati wa maonyesho ya sanaa za kaligrafia ili kununua vitu kadhaa kwa ajili ya kampuni yetu. Nilipata nakala ya kitabu cha MUSLIMAH BORA na kuanza kuisoma miezi mitatu baada ya kukipata kitabu huku mchumba wangu hakuwepo Qatar wakati huo. Nilihisi aya za Qur'an zinazungumza nami moja kwa moja. Niliposoma sifa za Muslimah Bora (mwanamke wa Kiislamu), nilitambua kwamba njia yangu ya maisha ilikuwa kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu. Kisha, nilipata nakala ya Qur'an katika lugha ya Tagalog na ningehisi aina fulani ya amani kubwa moyoni mwangu ambayo ingenifanya nitokwe na machozi. Nilijiambia mwenyewe itabidi niifuatilie. Nilitafuta mwongozo kutoka idara ya Shari'a na kutoka kwa wenzangu wenye nia nzuri kuhusu vitabu vipi vya kusoma. Ningeingia mtandaoni na kusoma kila kitu nilichopata. Mpaka siku moja, nilipoamua kuacha. Niliacha kutafuta maarifa kwa sababu sikutaka kutekeleza kitu chochote nikiwa bado nina uhusiano na mchumba wangu ambaye alikuwa amefika kutoka Ufilipino wakati huo. Ingawa hakuzungumzia kuhusu suala la dini yangu, nilijiambia, ilibidi niangalie kwa makini kama nilikuwa ninaathiriwa na uwepo wake maishani mwangu au kama kukumbatia kwangu kwa Uislamu kunatokana na chaguo langu mwenyewe... kutoka kwa kina cha ndani kabisa cha moyo wangu na roho yangu.

Wakati huo nilipoacha kutafuta maarifa zaidi, nilikuwa napitia mgogoro pia. Matatizo yaliendelea kuongezeka na nilichanganyikiwa kuhusu jinsi ya kusali. Nifanye maombi ya Rozari au nifanye swalaah (maombi ya Waislamu) ambayo sikujua chochote kuhusu jinsi ya kuifanya? Kwa miezi kadhaa, nilikuwa na utata, mpaka usiku mmoja nilipoamka na nikamwomba Mungu na kusema - “Mungu wangu, nimechanganyikiwa. Sijui tena jinsi ya kuomba. Angalia moyo wangu. Ninajisilimu kwako!“ Baada ya hapo, nilihisi amani fulani.

Rehema za Mungu zikaanza. Mchumba wangu alikwenda nyumbani kwa Ufilipino mapema kabla ya wakati aliopanga kuenda. Mungu alinipa muda niliohitaji kwa utambuzi wangu.

Sikutarajia kwamba siku ambayo tsunami kubwa ingepiga Japani ingekuwa siku nitakayofanya Shahaadah yangu (ushuhuda wa imani unaotamkwa ili kuingia kwa Uislamu). Nilihisi tu moyo wangu ulikuwa kimya sana. Nilikwenda kwa Fanar nikiwa na nia ya kuhudhuria madarasa ya kimsingi ya Uislamu. Nilichukua hatua hii nilipokuwa na uwezo hatimaye wa kujibu maswali ya kimsingi niliyokuwa nayo. Kwanza, iwapo mchumba wangu na mimi tusingeweza kuishia pamoja, ningeweza kuendelea kuwa Muislamu? Nitakapokufa, familia yangu ingesitiri vipi mabaki yangu? Na kisha, niliona akilini mwangu wenzangu wa kiislamu wa kike na nilihisi utangamano fulani wa kijamii. Kisha nilijiambia , kuna uwezekano wa kupoteza mtu mmoja, lakini ningepata wengi zaidi. Pili, kwa nini wanaume wa Kiislamu wanaruhusiwa kuoa hadi wake wanne? Je! Hawajui ni uchungu kwa mwanamke ikiwa mwanamke mwingine anapendwa zaidi kuliko yeye? Swali hili lilibaki bila majibu kwa miezi kadhaa mpaka siku hiyo nilipokuwa nikijiandaa kwenda Fanar. Kwa kweli, swali hili daima lingenizuia kukubali masomo niliyoyapata kuhusu Uislamu na nilikuwa na matumaini ya kupata jibu mara nilipopewa fursa ya kuhudhuria masomo katika Fanar. Hatimaye, asubuhi hiyo nilipokuwa nikijiandaa kuenda Fanar, nilijiuliza maswali mengine kwa akili yangu - je, hisia ya wivu ndio itakuwa ya kunivuta nyuma kutoka kwa Mwenyezi Mungu? Je! Kwani kitu cha kidunia kama hicho kitanizuia nimjue Mwenyezi Mungu? Sikujijibu mwenyewe. Badala yake, nilikimbilia kujiandaa kuondoka. Hatua hiyo peke yake ilikuwa jibu.

Baada ya kufika Fanar, nilikuwa na fursa ya kuwa na mazungumzo ya moja kwa moja na washauri wao wawili - Dada Zarah na Dada Maryam. Hamu ya moyo wangu ilianza kujifunua. Dada Maryam alisema kuwa ninaonekana niko tayari. Aliponiuliza kama ningependa kufanya shahaadah, nilijibu tu kwa kusema - JE, KUNA MTU YEYOTE AMBAYE ANGEWEZA KUNIONGOZA KUIFANYA? Tena, hisia hiyo ya uhakika - sio kuhusu NDIO au HAPANA, ni kuhusu upatikanaji wa mtu ambaye angeweza kuniongoza kuifanya shahadah.

Baada ya kusema Shahadah, machozi yalianza kutirirka. Dada Maryam aliponikumbatia na kuniambia tayari nimeshakuwa Muislamu, Nilimshukuru kwa machozi. Familia yangu ya karibu ilinikaribisha kama Muslimah na namshukuru Allah kwa hilo. Ingawa wanabaki kuwa Wakatoliki, kukubali kwao, msaada na upendo wao unanisaidia sana. Kwa upande wa mchumba wangu, alishangaa kupokea ujumbe kutoka kwangu dakika chache baada ya mimi kuingia kwa Uislamu. Hakutarajia kupokea habari kama hizo kutoka kwangu.

Kuingia kwangu kwa Uislamu kulisisitizwa na tsunami kubwa. Ninaiangalia kama ishara ya kuwa Mwenyezi Mungu ameniosha kabisa na kunitakasa kutoka kwa dhambi zangu. Ningekuwa nini leo kama nisingelijisalimisha kwake? Ningekuwa wapi?

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.