Manufaa ya Kusilimu (sehemu ya 1 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Maswali yako yote yamejibiwa.

  • Na Aisha Stacey (© 2011 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 09 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 27 Apr 2022
  • Ilichapishwa: 2
  • Imetazamwa: 5,178 (wastani wa kila siku: 6)
  • Ukadiriaji: 2.3 kati ya 5
  • Imekadiriwa na: 9
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

BenefitsOfConvertingPart1.jpgMakala nyingi katika wavuti huu zinafafanua jinsi ilivyo rahisi kwa mtu kusilimu. Kadhalika, kuna makala na video zinazojadili vizuizi vinavyoweza kusababisha mtu kutoukubali Uislamu. Waliosilimu kihakika husimulia hadithi zao, na tunaweza kuelezea na kusambaza furaha zao na misisimko yao. Hata kuna makala inayoelezea jinsi ya kuwa Muislamu. Kujiunga na Uislamu kumeshughulikiwa katika sehemu mbalimbali na msururu wa makala hii unajadili manufaa yanayotokana na kusilimu.

Kuna manufaa mengi yanayopatikana mtu anaposilimu, iliyowazi zaidi ni hali ya utulivu na uzima anayoipata mtu yeyote baada ya kugundua ukweli wa kimsingi wa maisha. Kuimarisha uhusiano na Mwenyezi Mungu katika njia halisi na rahisi hukuacha huru na kukusisimua, na matokeo yake huwa ni utulivu wa moyo. Hata hivyo, haya siyo manufaa ya pekee ya kusilimu, kuna manufaa mengine ambayo mtu huweza kuyapata na tutayajadili hapa, moja moja.

1.Kusilimu humkomboa mtu kutoka utumwa, mifumo ya kiubinadamu pamoja na mitindo ya kimaisha.

Uislamu huikomboa akili kutoka kwa ushirikina na mambo yasiyo na uhakika; huikomboa nafsi kutoka kwa dhambi na ufisadi na huiweka huru dhamira kutoka kwa uonevu na woga. Kujisalimisha kwa Mungu, hakuzuii uhuru, bali, huleta uhuru mwingi sana kwa kuikomboa akili kutoka ushirikina na kuijaza ukweli pamoja na elimu.

Pindi tu mtu anapoukubali Uislamu, hujinasua kutoka utumwa wa fasheni, ama ulaji, na hujikomboa kutoka utumwa wa mfumo wa kifedha unaolenga kuwadhalilisha watu. Katika kiwango kidogo lakini kilicho na umuhimu mkubwa, Uislamu humuweka mtu huru kutokana na ushirikina unaoyatawala maisha ya wale ambao hawajajisalimisha kwa Mwenyezi Mungu. Muumini hujua kwamba hakuna bahati nzuri na mbaya. Vipengele vyote vya uzuri na ubaya wa maisha yetu hutoka kwa Mwenyezi Mungu kama alivyofafanua Mtume Muhammad, rehema na amani zimshukie yeye, kuwa mambo yote ya muumini ni mazuri, "Anapofanyiwa wepesi, hushukuru, na hali hii ni nzuri kwake. Na anapozongwa na ugumu wa maisha, huvumilia, na hali hii ni nzuri kwake".[1]

Baada ya mtu kukombolewa kutoka mifumo ya kiubinadamu na mitindo ya kimaisha, huwa huru kumuabudu Mwenyezi Mungu kwa njia inayofaa. Muumini huweza kumwamini Mungu na kuwa na matarajio mazuri kwa Mungu na hutafuta kwa dhati Rehema zake.

2.Kusilimu humpa mtu nafasi kuyapata mapenzi ya dhati ya Mwenyezi Mungu.

Mtu huyapata mapenzi ya Mungu anapojiunga na Uislamu kwa kufuata mwongozo wa Allah katika maisha yake - ambao ni Kurani, na mafundisho sahihi na mwenendo wa Mtume Muhammad. Wakati Mungu alipoumba ulimwengu, hakuuacha ulimwengu uyumbe na kukosa ulinzi kamili. Alituma kamba (hablu au dini), thabiti na imara, na kwa kushikilia kamba hiyo vyema, binadamu asiyethaminiwa anaweza kufikia daraja la ukuu na kupata amani ya kudumu. Katika maneno ya Kurani, Mwenyezi Mungu anayaweka waziwazi matakwa yake, hata hivyo, wanadamu wana hiari ya kumfurahisha au kumkasirisha Mwenyezi Mungu.

Sema (Ewe Muhammad): "Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu." (Kurani 3:31)

Na anayetafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasiri (kupata hasara). (Kurani 3:85)

Hapana kulazimisha katika dini. Kwani Uongofu umekwishapambanuka na upotofu. Basi anayemkataa Taghut[2] na akamuamini Mwenyezi Mungu bila ya shaka amekamata kishikio madhubuti, kisichovunjika. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua. (Kurani 2:256)

3.Manufaa ya kujiunga na Uislamu ni kwamba Mwenyezi Mungu anamuahidi Pepo aliyeamini.

Pepo, kama ilivyoelezewa kwenye aya nyingi za Kurani, ni sehemu ya furaha ya kudumu na imeahidiwa kwa waumini. Mwenyezi Mungu anaonyesha rehema yake kwa waumini kwa kuwazawidi Pepo. Yeyote yule anayemkana Mwenyezi Mungu ama kuabudu kitu kingine, au badala ya Allah, ama kudai kwamba Mwenyezi Mungu ana mtoto wa kiume ama wa kike au mshirika, ataangamia Akhera ndani ya Jehanamu. Kusilimu kutamwokoa mtu na adhabu ya kaburi, mateso ya Siku ya Hukumu na Jehanamu ya milele.

"Na ambao wameamini na wakatenda mema, bila ya shaka tutawaweka katika maghorofa ya Peponi yenye kupitiwa chini yake mito, wakidumu humo. Ni neema ya malipo ya watendao." (Kurani 29:58)

4.Furaha, utulivu na amani ya dhati huweza kupatikana kwa kujiunga na Uislamu.

Uislamu pekee unahusishwa moja kwa moja na amani ya dhati na utulivu. Maneno Uislamu, Muislamu na salaam (amani) yote hutokana na shina la neno "Sa - la – ma" yakimaanisha amani, ulinzi na usalama. Mtu anaponyenyekea kwa Mungu atapata usalama na amani.

Furaha halisi hupatikana Peponi pekee. Huko, tutapata amani kamili, utulivu na ulinzi na kuwa huru na woga, wasiwasi na maumivu, hali ambazo ni sehemu ya maisha ya binadamu. Hata hivyo, mwongozo uliotolewa na Uislamu unaturuhusu, sisi wanadamu wenye mapungufu, kutafuta furaha katika ulimwengu huu. Njia bora ya kuwa na furaha katika ulimwengu huu na kesho Akhera ni kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu, na kumuabudu, bila ya kumshirikisha na chochote.

Katika makala ifuatayo tutaendelea na majadiliano yetu kuhusu manufaa ya kusilimu kwa kutaja msamaha na huruma, pamoja na majaribio na masaibu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Saheeh Muslim

[2] Taghut – Ni neno la Kiarabu lenye maana nyingi. Kimsingi, ni kitu chochote kinachoabudiwa bila ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu mmoja wa Kweli, wakiwemo shetani, mapepo, masanamu, mawe, nyota, jua, mwezi, malaika, wanadamu, makaburi ya mawalii au watakatifu, watawala na viongozi.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.