Maria Luisa “Maryam” Bernabe, Mkatoliki wa Zamani, Ufilipino (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Sisi sote tumezaliwa na mwelekeo wa kiasili wa kumwabudu Mungu na jitihada zangu kwa ajili Yake zilianza nikiwa na umri mdogo sana.

  • Na Maria Luisa “Maryam” Bernabe
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,113 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

MariaLuisa1.jpgMachi 11, 2011 ndio siku nilipojisalimisha kikamilifu kwa Mungu. Nilifanya shahaadah yangu baada ya miezi ya utambuzi. Hali zilizonipeleka kwa Uislamu hazikuwa rahisi. Lakini Alhamdulillah (Sifa zote an Shukrani ziwe kwa Mungu), kwa sasa, hatimye nimekuwa Muslimah (mwanamake Muislamu).

Ningependa kuwaeleza kuhusu safari yangu ya kufikia kwa Uislamu.

Nilikuwa mkatoliki tangu kuzaliwa kwangu. Mama yangu alikuwa mtawa kwa miaka kadhaa kabla ya kuacha konventi, na alitulea katika maisha ya maombi na sala kwa Mungu. Tangu nikiwa na miaka saba, alinifunza tabia ya kujisalimisha kwa Mungu na kukiona kila kitu kinachotendeka kama taratibu za Mungu za kunitayarisha kwa mazuri yanayokuja.

Kwa kuwa nilijijengea uhusiano wa kibinafsi na Mungu, nilikuwa nimejihusisha sana na kazi za kitume. Nilifundisha hata katekisimu na nilipewa tuzo ya Katekista wa Mwaka nilipohitimu Shule ya Upili. Baada ya hapo, maisha yangu yalikuwa safari ya kudumu ya imani.

Katika hatua muhimu sana katika maisha yangu, nilifanya kazi kwa shirika la kibinadamu lililokusudiwa kuelekeza miradi iliyotazamiwa kuunganisha Wafilipino kwa maombi bila kujali dini. Shirika lilikuwa na imani kwamba sisi sote ni ndugu na dada chini ya utunzaji wa Mungu. Hata kabla sijajihusisha na shirika hilo, maisha yangu ya sala yalikuwa yakieleka kwa Mungu Mmoja Mwenye Uwezo. Hata hivyo, bila shaka, baada ya kulelewa kikatoliki nyumbani na shuleni, nilikuwa na mnyenyekeo fulani kwa watakatifu fulani wa kanisa, nikiwatambua sio kama miungu wadogo, lakini kama marafiki katika sala kwa nia yangu. Kulikuwa na wakati ningejiuliza ni nani kati ya watakatifu ndiye mwenye uwezo zaidi katika kuleta baraka. Na hivyo, ningeishia kuomba tena moja kwa moja kwa Mungu - Mlezi Mmoja Mkuu, Mwenye Nguvu, nikijua Yeye ndiye chanzo kikuu cha baraka.

Wakati mama yangu alipopataa lukemia na katika nyakati za mwisho za ugonjwa wake, kilikuwa kipindi cha mapambano tupu. Wakati mmoja, niliamka nikimwomba Mungu aniweke mimi kwa nafasi yake ili nipate kuugua badala yake. Ilikuwa jitihada isiyo na mwisho ya kutafuta rasilimali kwa matumaini ya kupata matibabu ya kisasa ya kumponya mama yangu. Mpaka kasisi wetu wa parokia ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa familia alisema - JISALIMISHE... JISALIMISHE KWA MUNGU. Kisha, nilikumbuka tena kujisalimisha, hasa wakati mwili wa mama yangu ulikuwa tayari umeshakataa matibabu ya kemotherapi.

Kifo cha mama yangu kilikuwa hatua muhimu katika maisha yangu. Tangu wakati huo, maisha yangu yamekuwa vita vya kudumu vya kujisalimisha kwa Mungu. Ubinafsi ungenifanya niegemee zaidi kwa mipango yangu - nikipambana kwa ajili ya kuyatimiza na kutafuta kwa ukaidi vile nilivyovitaka mimi licha ya ishara nyingi kutoka kwa Mungu. Katika nyakati hizi, ningepata amani tu nilipojisalimisha. Lakini kwa sababu ya ubinadamu wangu, siku zote ningerudi kuanguka katika mtego wa kutaka mambo yafanyike kwa njia yangu mwenyewe.

Baada ya kifo cha mama yangu, niliitwa kazi huko Qatar. Ilikuwa mwaka wa 2003. Pengine, sikuwa tayari wakati huo. Nilichukua kazi nyingine nchini Ufilipino kwani hakukuwa na haja ya kutafuta kazi nje ya nchi kwa sababu mama yangu alikuwa amekwisha kufa. Je, kuna haja gani ya kupata mapato niliyoyataka kupata wakati alipokuwa hai ili niweze kuendeleza matibabu yake na pia kumpeleka mahali tofauti tofauti? Hakuna.

Kisha mwaka wa 2006, wito wa mahojiano ya kikazi nisioutarajia ulikuja kutoka kwa mwajiri wa Ujerumani mwenye mradi mkubwa huko Qatar. Qatar mara nyingine tena iliniita na ilibidi niyahudhurie mahojiano kwa ushauri wa baba yangu aliyeniambia niyajaribu. Sikutarajia kupata kazi lakini ishara wakati wa taratibu za mahojiano zilinifanya niamini kazi hiyo ilikuwa iwe yangu. Nilienda Qatar baada ya mwezi mmoja. Nilidhani Qatar ilikuwa inipe fursa ya kupata mapato ya zaidi, ila cha kushangaza ni kuwa ilinipa zaidi ya hayo.

Katika malezi yangu ya Kikatoliki, iliingizwa katika vichwa vyetu kwamba kusudi la maisha ni KUMJUA, KUMPENDA na KUMTUMIKIA MUNGU. Hakika, ni hulka ya kiasili ya mwanadamu kuendelea kutafuta maana ya maisha. Utafutaji usio na mwisho wa chemchemi ya ujana umejikita mizizi katika hamu ya mwanadamu ya kuelewa maana na kusudi la kuwepo kwake. Mwanadamu hawezi kamwe kuacha utafiti wake isipokuwa pale atakapopata anachokitafuta. Kwa hivyo, hawezi kusimama kwa ajili ya kitu chochote na kununua angalau muda na afya ili aendelee na kampeni yake. Mamilioni ya wasomaji waliokifanya kitabu cha “Maisha Yanayoongozwa na Lengo” kiwe kati ya vitabu vilivyouzwa sana duniani, ni ushuhuda tosha wa jinsi watu wengi wanatafuta mwelekeo na lengo.

Nilipokuwa na umri wa miaka 8 au 9, nilimuuliza mama yangu - “Mungu alikuwa wapi kabla ya Uumbaji?” Nilimwambia ningetumia muda mrefu nikiwa nimefunga macho yangu na kulowa jasho kutokana na umakini wangu nikiwaza tu kuhusu zifuatazo kwa utaratibu — nafasi yangu na mahali nipo, mawingu, anga ya samawati, mwezi, sayari tisa, nje ya Kundi la nyota la Kilimia, kisha napata kuna nafasi kubwa ya anga ya nje. Licha ya upana na ukubwa wa nafasi hii, Mungu bado yuko juu yake... ”Wakati hapakuwa na kitu alikuwa wapi?” Niliendelea kuuliza. Na mama yangu alitabasamu na kunikumbatia — “Tayari unafikiria mambo hayo?” aliuliza. Kisha akasema, “Hivyo, mpendwa wangu, ndivyo Mungu wetu alivyo mkubwa na Asiye na mwisho. Yeye ni mkubwa kuliko ufahamu wetu, lakini niamini, Yupo mahali yupo.

Tamaa na hamu ya Mwanadamu- vijana na wazee, si kwa ajili ya mambo ya kimwili, wala anasa za kihisia na za kimwili... ni haya yote na zaidi. Sisi sote tangu kuzaliwa kwetu tunamtafuta Mungu. Tumeumbwa ili kumjua, kumpenda, kumtumikia na sasa, kwa kuwa mimi ni Muslimah, wacha niongeze moja zaidi — kumwabudu Mungu kwa Umoja Wake.

Katika safari yangu ya kumtafuta Mungu katika maisha yangu yote, namtukuza kwa kuniongoza kwenye Njia ya Uislamu.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.