Nataka kuwa Muislamu lakini... Uongo Bunifu kuhusu kusilimu (sehemu ya 2 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mengi kuhusu uongo bunifu unaomzuia mtu kusilimu.

  • Na Aisha Stacey (© 2011 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 09 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 19
  • Imetazamwa: 4,047 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

IwantToBeMuslimPart2.jpgHapana mungu ila Mwenyezi Mungu. Ni kauli rahisi inayofanya kusilimu kuwa rahisi. Kuna Mungu Mmoja tu, na vilevile dini moja, hakuna kitu kinachoweza kuwa rahisi zaidi. Hata hivyo, kama tulivyojadili katika makala iliyopita, wakati wowote mtu anapotambua ukweli na anataka kuwa Muislamu, Shetani humjulisha neno lakini. Nataka kuwa Muislamu...LAKINI. Lakini bado siko tayari. Lakini sizungumzi Kiarabu, au lakini sitaki kubadilisha jina langu. Leo tutajadili uongo bunifu zaidi ambao unawazuia watu kusilimu.

3.Nataka kuwa Muislamu lakini sitaki kutahiriwa.

Mtume Muhammad alisema kuwa kila mtoto alizaliwa katika hali ya fitra, na ufahamu sahihi wa Mungu.[1] na hadithi za Mtume Muhammad zinatuambia kwamba hali zinazohusiana na fitra (hali ya asili ya kuwa) ni tano.

“Vitu vitano ni sehemu ya maumbile: kunyoa mavuzi, kutahiriwa, kupunguza masharubu, kung'oa au kukwanyua nywele za makwapani, na kukata kucha”.[2] Hii inaaminika kuwa ada ya kale, ni njia ya asili, iliyofanywa na Mitume wote, na wakawaamrisha waumini wao waitekeleze kulingana na sheria walizoleta.[3]

Wanazuoni wengi wa Kiislamu wanakubali ya kwamba kutahiriwa ni lazima kwa wanaume mradi wasiwe na hofu ya kwamba inaweza kuwaletea madhara. Wakati wa kukadiria kiwango cha madhara ni lazima mtu atumie mafundisho sahihi ya Kurani pamoja na mwongozo sahihi wa hadithi za Mtume Muhammad. Iwapo mwanamume hana uwezo wa kutahiriwa kwa sababu ya woga wa kupata jeraha au kwa sababu nyingine yoyote halali ambayo inaweza kufanya maisha yake yawe ya taabu basi wajibu huu umeondolewa kwake. Hairuhusiwi suala hilo kuwa kizuizi ambacho kitamzuia mtu kuukubali Uislamu[4]. Kwa maneno mengine, hii sio sharti ya kuwa Muislamu. Pia, haimzuii mtu kuongoza sala.[5]

Hakuna sharti la kupashwa tohara kwa mwanamake katika Uislamu.

4.Nataka kuwa Muislamu lakini asili yangu ni ya rangi nyeupe.

Uislamu ni dini ambayo iliteremshwa kwa watu wote, katika kila mahali, kwa wakati wote. Haikupelekwa kwa ajili ya watu wa asili fulani au kabila maalumu. Ni njia kamili ya maisha inayoambatana na mafundisho yanayopatikana katika Kurani na hadithi sahihi zenye kuelezea mwenendo wa Mtume Muhammad. Ingawa Kurani iliteremshwa kwa lugha ya Kiarabu na Mtume Muhammad alikuwa Mwarabu, itakuwa makosa kudhani kuwa Waislamu wote ni Waarabu, au vivyo hivyo, kuwa Waarabu wote ni Waislamu. Kwa kweli idadi kubwa ya Waislamu bilioni 1.4 ulimwenguni sio Waarabu.

Hakuna mahitaji ya rangi ya uasili au ukabila kwa mtu kuwa Muislamu. Katika hotuba yake ya mwisho Mtume Muhammad alisisitiza ukweli huu kwa maneno machache ya wazi.

“Wanadamu wote nasaba yao inatokana na Adamu na Hawa, Mwarabu hana ubora juu ya asiye Mwarabu na asiye Mwarabu hana ubora juu ya Mwarabu; mwenye uasili wa weupe hana ubora juu ya mwenye uasili wa weusi wala mwenye uasili wa weusi hana ubora juu ya mwenye uasili wa weupe, isipokuwa kwa uchaji Mungu na matendo mema. Jueni kuwa kila Muislamu ni ndugu wa kila Muislamu na kwamba Waislamu ni ndugu moja.”[6]

“Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane…” (Kurani 49:13)

5.Nataka kuwa Muislamu lakini sijui chochote kuhusu Uislamu.

Hakuna haja ya kujua mengi kuhusu Uislamu ili kuwa Muislamu. Inatosha kujua maana ya shahada na nguzo sita za imani. Pindi tu mtu atakapoukubali Uislamu, kuna muda wa yeye kujifunza kuhusu dini yake. Hakuna haja ya kukimbilia mambo kwa pupa kisha ukazidiwa. Nenda polepole, lakini usonge mbele kwa kasi yako mwenyewe. Kuna muda wa kufahamu uzuri wa ushawishi wa Uislamu na wepesi wake, na pia kujifunza kuhusu mitume wote na wajumbe wa Uislamu akiwemo mtume wa mwisho, Muhammad. Muislamu haachi kujifunza; ni mchakato ambao utaendelea hadi kifo.

Mtume Muhammad alisema, "Muumini hatatosheka kusikiliza mambo ya kheri (kutafuta elimu) hadi atakapofikia Peponi.”[7]

6.Nataka kuwa Muislamu lakini nimefanya madhambi mengi.

Mtu anapotamka shahada, ninakiri ya kwamba hapana mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu na nakiri ya kwamba Muhammad ni mjumbe Wake, anakuwa kama mtoto mchanga aliyezaliwa. Madhambi yake yote yaliyopita, hayajalishi ni makubwa au madogo, hufutwa yote. Rekodi huwa safi, haina dhambi lolote, hung'ara na nyeupe; huu ni mwanzo mpya.

“Waambie wale waliokufuru kuwa wakikoma, watasamehewa yaliyokwisha pita…” (Kurani 8:38)

Hakuna kulazimishwa kwa mtu yeyote kuukubali ukweli wa Uislamu. Hata hivyo, ikiwa moyo wako unakuambia kuna Mungu mmoja tu, usisite.

“Hapana kulazimisha katika Dini. Kwani Uongofu umekwishapambanuka na upotofu. Basi anayemkataa Shetani na akamuamini Mwenyezi Mungu bila ya shaka amekamata kishikio madhubuti, kisichovunjika. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.” (Kurani 2:256)



Rejeleo la maelezo:

[1] Saheeh Muslim

[2] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim

[3] AS-Shawkaani, Nayl al-Awtaar, Baab Sunan al-Fitrah

[4] Fataawa al-Lajnah al-Daa’imah, 5/115, Al-Ijaabaat ‘ala As’ilah al-Jaaliyaaat, 1/3,4

[6] Matini ya Hotuba ya Mwisho yanaweza kupatikana katika Saheeh Al-Bukhari na Saheeh Muslim, na kwenye vitabu vya Tirmidhi na Imam Ahmad.

[7] At Tirmidhi

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa