Nataka kuwa Mwislamu lakini... Uongo Bunifu kuhusu kusilimu (sehemu ya 1 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mungu hufanya kitendo cha kusilimu kuwa rahisi, sio kigumu.

  • Na Aisha Stacey (© 2011 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 09 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 14 Aug 2022
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,749
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

IwantToBeMuslimPart1.jpgImani kuu ya msingi katika dini ya Uislamu ni kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu. Yeye, ni Peke Yake, wa Kwanza na wa Mwisho, hana washirika, watoto wa kiume, mabinti au wasta. Yuko Peke Yake katika Miliki Yake na Kudura Yake. Ni dhana rahisi sana, ni ukweli mtupu. Walakini, wakati mwingine imani halisi ya Mwenyezi Mungu inaweza kuwazidia au kuwashinda watu. Mara kwa mara tunashangaa tunapomwomba Mwenyezi Mungu na Anatujibu papo hapo.

Dini ya Uislamu inahusisha dhana hiyo rahisi - kwamba Mwenyezi Mungu ni Mmoja na imejumuishwa kwenye neno kujisalimisha. Uislamu unamaanisha, kujisalimisha kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu. Mzizi wa neno Uislamu (sa-la-ma) ni lile lile linaloshirikisha neno la Kiarabu lenye maana ya amani na usalama. Kimsingi, amani na usalama hupatikana kwa kuishi maisha kulingana na matakwa ya Mwenyezi Mungu. Daima, kama mzunguko wa maisha huanzia na kuishia mahali pamoja - hapana mungu ila Mwenyezi Mungu. Tunapojisalimisha kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu, tunakuwa ni Waislamu na ili kudhihirisha uaminifu wetu tunakiri kuwa sisi ni Waislamu kwa kutamka, peke yetu au katika makundi ya Waislamu wengine, Laa ilah illa Allah, Muhammad rasoolu Allah. Hapana mungu wa kweli isipokuwa Mwenyezi Mungu na Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ni mtume Wake.

Wakati wowote mwanadamu yeyote anapopata uzoefu wa na kuelewa huruma ya Mungu, Shetani hujaribu kila awezalo kumdhuru mtu huyo. Shetani hataki tufarijike wala kupata huruma; anataka tuwe na wasiwasi na huzuni. Anataka tufanye makosa na kutenda madhambi. Shetani daima hukata tamaa kupendwa na Mungu, kwa hivyo hutaka kuwapotosha wanadamu wengi kadri ya uwezo wake.

(Shetani akasema) “…Kwa kuwa umenihukumia upotofu, basi nitawavizia katika Njia yako Iliyonyooka. Kisha nitawazukia mbele yao na nyuma yao na kuliani kwao na kushotoni kwao. Wala hutawakuta wengi wao wenye shukrani.” (Kurani 7:16-17)

Wakati wowote mtu anapotambua ukweli na kutaka kuwa Mwislamu, Shetani humjulisha neno 'lakini'. Nataka kuwa Mwislamu...LAKINI! Lakini bado siko tayari. Lakini sizungumzi Kiarabu. Lakini mimi ni mweupe (nina ngozi nyeupe). Lakini sijui chochote kuhusu Uislamu. Kwa hakika Mwenyezi Mungu alituonya dhidi ya Shetani na hila zake.

“Enyi wanadamu! Asije Shetani kukufitinini…” (Kurani 7:27)

“Hakika Shetani ni adui yenu, basi mfanyeni kuwa ni adui…” (Kurani 35:6)

Minong'ono ya Shetani hujaribu kutuzuia kusilimu. Mawazo haya hayapaswi kuwa kizuizi baina ya mtu mwenye mafungamano na Mungu, au anayejiunga tena na Mungu Mwingi wa Rehema. Katika mfululizo huu au makala hizi tutajadili baadhi ya mambo maarufu zaidi ya uongo yaliyobuniwa (tutayaita Uongo Bunifu), tutayaweka wazi kwa kuyakagua na kuthibitisha kwamba Mungu ni Mwingi wa Rehema. Yeye husababisha tendo la kusilimu kuwa rahisi, wala sio gumu. Hakuna lakini wala hatihati!

1.Nataka kuwa Mwislamu lakini sitaki kubadilisha jina langu.

Mtu anayeingia katika Uislamu sio lazima abadilishe jina lake. Mtume Muhammad, rehema na amani za Mungu zimshukie yeye, alisema kwamba kila mtu ana haki ya kuwa na jina zuri, jina ambalo lenye maana na linaambatana na sifa. Hii sio shida kwa idadi kubwa ya watu, japo ikiwa utagundua kuwa maana ya jina lako ni baya au limehusishwa na watenda madhambi au madhalimu ni vyema kulibadilisha liwe jina linalokubalika. Ikiwa jina la mtu huyo ni jina la sanamu au linaashiria utumwa wa kitu au mtu mwingine asiyekuwa Mungu, basi lazima libadilishwe. Kumbuka kuwa Uislamu ni rahisi. Iwapo kubadilisha jina lako kirasmi kungesababisha dhiki, wasiwasi au madhara, inatosha kulibadilisha na lijulikane miongoni mwa marafiki na jamaa.

2.Nataka kuwa Muislamu lakini sijui chochote kuhusu Kiarabu.

Dini ya Uislamu iliteremshwa kwa watu wote, katika kila mahali, kwa wakati wote. Hii sio dini maalumu ya Waarabu au wasemaji wa Kiarabu. Kwa kweli, idadi kubwa ya Waislamu bilioni 1.4 ulimwenguni hawana asili ya Uarabu. Mtu anaweza kuwa Mwislamu bila kujua neno moja la Kiarabu; haiathiri uwezo wake wa kuukubali Uislamu. Hata hivyo, lugha ya Kurani ni ya Kiarabu na sala za kila siku zinatekelezwa kupitia Kiarabu, basi ingawa sio lazima kujifunza lugha nzima, baada ya kusilimu itakuwa muhimu kujifunza maneno kadhaa ya Kiarabu kwa ajili ya ibada.

Iwapo mtu hawezi kujifunza Kiarabu cha kutosha kwa lengo la kutekeleza sala zake kwa sababu ya kasoro ya kuongea au pia hawezi kutamka Kiarabu, itabidi ajaribu kadri ya uwezo wake. Na Ikiwa pia kujifunza Kiarabu kwa uchache haiwezekani, basi huondolewa jukumu hili, kwa sababu Mungu habebeshi watu dhiki zaidi ya uwezo wao. Walakini Mungu pia anasema ya kwamba amerahisisha kujifunza Kurani, kwa hivyo ni vyema mtu kujaribu awezalo.

“Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya iwezavyo…” (Kurani 2:286)

“Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Kurani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anayekumbuka?” (Kurani 54:17)

Mtu alienda kwa Mtume akasema: "Ee Mjumbe wa Mungu, nifundishe kitu katika Kurani ambacho kitanitosha, kwa maana siwezi kusoma." Akamwambia, "Sema: Subhaan-Allaah wa’l-hamdu Lillaah wa laa ilaaha ill-Allaah wa Allaahu akbar wa laa hawla wa laa quwwata illa Billaah (Ametakasika Mwenyezi Mungu na kila upungufu, na shukrani na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni mkubwa kuliko chochote, na hakuna uwezo wala nguvu ila za Mwenyezi Mungu).”[1]

Kuingia kwenye pote la Uislamu ni rahisi. Ni njia rahisi, isiyo na shida. Katika sehemu ya 2 tutajadili upashaji tohara, ukweli kwamba Uislamu hauna pingamizi za ukabila au uasili na kuwa Mwislamu bila kujua sana juu ya Uislamu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Abu Dawood, An Nasai.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa