Rehema ya Mungu (sehemu ya 1 kati ya 3): Mungu mwingi wa Rehema, Mgawaji wa Rehema.

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Ufafanuzi wa vitendo wa majina mawili ya Mwenyezi Mungu yanayorudiwa mara kwa mara: ar-Rahman na ar-Raheem, na asili ya Rehema yote ya Mwenyezi Mungu.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 03 Jan 2022
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 5,251
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Divine_Mercy_of_God_(part_1_of_3)_001.jpgIkiwa mtu angeuliza, ‘Ni nani Mungu wako?’ Jibu la Muislamu lingekuwa, ‘Mwingi wa Rehema, Mgawaji wa Rehema.’ Kulingana na vyanzo vya Kiislamu, manabii, huku wakikazia hukumu ya Mungu, pia walitangaza rehema Yake. Katika maandiko ya Kiislamu, Mwenyezi Mungu anajitambulisha kama:

“Yeye ndiye Mwenyezi Mungu, ambaye hapana mungu isipo kuwa Yeye tu. Mwenye kuyajua yaliyo fichikana na yanayo onekana. Yeye ndiye Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.” (Kurani 59:22).

Katika msamiati wa Kiislamu ar-Rahman na ar-Raheem ni majina binafsi ya Mungu Aliye Hai. Yote yamechukuliwa kutoka kwa nomino rahmah, ambayo inaashiria "rehema", "huruma", na "huruma ya upendo". Ar-Rahman inaelezea asili ya Mwenyezi Mungu ya kuwa Mwenye kurehemu, wakati ar-Raheem inaelezea matendo Yake ya rehema yaliyotolewa kwa viumbe Vyake, utofauti iliofichika, lakini ambao unaonesha rehema zake zote.

"Sema, ‘Mwombeni Allah (Mwenyezi Mungu), au mwombeni (Rahman) Mwingi wa Rehema, kwa jina lolote mnalo mwita – Kwani Yeye ana majina mazuri....’" (Kurani 17:110)

Majina haya mawili ni baadhi ya Majina ya Mwenyezi Mungu yanayotumika sana katika Quran: ar-Rahman imetumika mara hamsini na saba, wakati ar-Raheem imetumika mara mbili zaidi (mia na kumi na nne).[1] Moja huwasilisha hisia kubwa ya ukarimu na upendo, Mtume alisema:

"Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkarimu, na anapenda ukarimu. hutoa kwa upole asiyetoa kwa ukali." (Saheeh Muslim)

Zote pia ni sifa za kimungu zinazoashiria uhusiano wa Mungu na uumbaji.

"Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote; Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu." (Kurani 1:2-3)

Katika sala ambayo Waislamu huisoma angalau mara kumi na saba kwa siku, huanza kwa kusema:

"Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu. Sifa njema zote ni za Mwenyeezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote; Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu.." (Kurani 1:1-3)

Maneno haya yenye nguvu yanaibua jibu la Mungu:

"Mja anaposema: ‘Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote’ Mimi (Mwenyezi Mungu) husema: ‘Mja wangu amenisifu.’ Anaposema: ‘Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu.,’ Mimi (Mwenyezi Mungu) husema: ‘Mja wangu amenitukuza.’" (Saheeh Muslim)

Majina haya mara kwa mara yanamkumbusha Muislamu kuhusu rehema ya Mwenyezi Mungu inayomzunguka. Sura zote isipokuwa moja tu za Maandiko ya Kiislamu zinaanza kwa maneno, ‘Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu.’ Waislamu huanza kwa Jina la Mungu kuonyesha utegemezi wao wa mwisho juu Yake na kujikumbusha juu ya rehema ya Mungu kila wakati wanapokula, kunywa, kuandika barua, au kufanya jambo lolote la maana. Roho huchanua katika ulimwengu. Dua mwanzoni mwa kila tendo la ki ulimwengu huifanya kuwa la muhimu, ikiita baraka ya Mungu juu ya tendo hilo na kulitakasa. Kanuni hii ni mapambo maarufu katika maandishi na mapambo ya usanifu.

The_Divine_Mercy_of_God_(part_1_of_3)_002.jpg

"Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu." Maandishi ya Yousef, msanii wa Uholanzi.

Kutoa rehema kunahitaji mtu ambaye ameonyeshwa rehema. Anayeonyeshwa rehema lazima awe mhitaji. Rehema kamilifu ni kuwajali wale wanaohitaji, ambapo rehema isiyo na kikomo inaenea kwa wale wanaohitaji au wasio na uhitaji, inaenea kutoka kwa ulimwengu huu hadi maisha ya kushangaza baada ya kifo.

Katika mafundisho ya Kiislamu, wanadamu wanafurahia uhusiano binafsi na Mungu Mwenye Upendo, Mwenye Rehema, aliye tayari kusamehe dhambi na kuitikia maombi, lakini Yeye si mwenye huruma wa kibinadamu wa kuhisi huzuni na huruma kwa mtu aliye katika dhiki. Mungu haji kuwa mwanadamu ili kuelewa mateso. Badala yake, rehema ya Mungu ni sifa inayolingana na utakatifu Wake, inaleta usaidizi wa kimungu na upendeleo.

Rehema za Mungu ni nyingi sana:

"Sema: Mola Mlezi wenu ni Mwenye rehema iliyo enea.….’" (Kurani 6:147)

Kuenea kwa uwepo wote:

"…na rehema yangu imeenea kila kitu…." (Kurani 7:156)

Uumbaji wenyewe ni kielelezo cha upendeleo wa kimungu, rehema na upendo. Mungu anatualika kutazama athari za rehema yake karibu nasi:

"Basi ziangalie athari za rehema ya Mwenyezi Mungu, jinsi anavyo ihuisha ardhi baada ya kufa kwake!..." (Kurani 30:50)

Mungu Anawapenda wenye Huruma

Mungu anapenda huruma. Waislamu wanauona Uislamu kuwa ni dini ya rehema. Kwao, Mtume wao ni rehema ya Mwenyezi Mungu kwa watu wote.

"Na hatukukutuma, (ewe Nabii), ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote" (Kurani 21:107)

Kama vile wanavyoamini kuwa Yesu alikuwa rehema ya Mungu kwa watu:

"Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu, na Rehema itokayo kwetu." (Kurani 19:21)

Mmoja wa mabinti wa Mtume Muhammad rehma na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alimpelekea habari za mtoto wake aliyekuwa mgonjwa. Akamkumbusha kuwa Mwenyezi Mungu ndiye anaye toa, ndiye anaye twaa, na kila mtu ana muda maalumu. Akamkumbusha kuwa mvumilivu. Habari za kifo cha mwanawe zilipomfikia, machozi ya huruma yalitiririka machoni pake. Wenzake walishangaa. Mtume wa Rehema alisema:

"Hii ni huruma Mungu ameiweka ndani ya mioyo ya waja wake. Katika waja wake wote, Mungu huwahurumia tu wenye huruma." (Saheeh Al-Bukhari)

Wamebarikiwa wenye kurehemu, kwani watahurumiwa, kama Mtume Muhammad alivyosema:

"Mungu hatamrehemu mtu asiye na huruma kwa watu." (Saheeh Al-Bukhari)

Pia alisema:

"Mwingi wa rehema huwaonea huruma wenye kurehemu. Warehemu waliomo ardhini, na Yeye aliye juu ya mbingu atakurehemu." (At-Tirmidhi)



Rejeleo la maelezo:

[1] Badala yake, ‘Mwenye Rehema’ halionekani kuwa jina la kimungu katika Biblia. (Kitabu cha kiyahudi, ‘Majina ya Mungu,’ uk. 163)

Mbaya Nzuri zaidi

Huruma ya Mungu (sehemu ya 2 kati ya 3): Kumbatio lake la Joto

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Rehema, kama inavyodhihirika katika maisha ya dunia na Akhera.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,985
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Rehema ya kimungu inafunika uwepo wote katika zizi lake, lenye kudumu milele. Mola Mlezi wa watu ni mwenye kuwarehemu, mwenye huruma. Jina la Mwenyezi Mungu, Ar-Rahman, linapendekeza rehema Yake ya upendo ni kipengele kinachobainisha nafsi Yake; utimilifu wa huruma zake hauna kikomo; bahari isiyo na mwisho isiyo na ufukwe. Ar-Razi, mmoja wa wasomi wa kiislamu wa kitambo aliandika, ‘Haiwezekani kwa viumbe kuwa na rehema zaidi kuliko Mwenyezi Mungu!’ Hakika Uislamu unafundisha kwamba Mungu ni mwenye huruma zaidi kwa mwanadamu kuliko mama yake mwenyewe.

Katika rehema nyingi za Mungu, Huteremsha mvua ili kuzalisha matunda kutoka kwenye bustani ili kuupa mwili wa mwanadamu. Nafsi pia inahitaji lishe nzuri ya kiroho kama vile mwili unavyohitaji chakula. Katika rehema zake nyingi, Mungu alituma manabii na wajumbe kwa wanadamu na kuwafunulia maandiko ili kutendeleza roho ya mwanadamu. Rehema ya Mwenyezi Mungu imejidhihirisha katika Torati ya Musa:

"…Na katika maandiko yake mna uwongofu na rehema kwa wanao mwogopa Mola wao Mlezi." (Kurani 7:154)

Na ufunuo wa Kurani:

"…Hii (Kurani) ni hoja zinazo toka kwa Mola wenu Mlezi, na uwongofu na rehema kwa watu wanao amini." (Kurani 7:203)

Rehema haitolewi kwa sifa fulani za mababu. Huruma ya Kimungu inatolewa kwa kutenda kulingana na Neno la Mungu na kusikiliza kisomo chake:

"Na hichi ni Kitabu tulicho kiteremsha, kilicho barikiwa. Basi kifuateni, na mchenimngu, ili mrehemewe." (Kurani 6:155)

"Na isomwapo Kurani isikilizeni na mnyamaze ili mpate kurehemewa." (Kurani 7:204)

Rehema ni matokeo ya utiifu:

"Na shikeni Swala, na toeni Zaka, na mt'iini Mtume, ili mpate kurehemewa." (Kurani 24:56)

Rehema ya Mungu ni tumaini la mwanadamu. Kwa hiyo waumini wanamwomba Mwenyezi Mungu rehema yake.

"Mimi yamenipata madhara. Na Wewe ndiye unaye rehemu kuliko wote wanao rehemu!" (Kurani 21:83)

Wanaomba rehema ya Mungu kwa uaminifu:

"Mola wetu Mlezi! Usizipotoe nyoyo zetu baada ya kwisha tuongoa, na utupe rehema itokayo kwako. Hakika Wewe ndiye Mpaji." (Kurani 3:8)

Na wanawaombea rehema ya Mwenyezi Mungu wazazi wao:

"…Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni.!" (Kurani 17:24)

Ugawaji wa Rehema za Mungu

Huruma ya kimungu inawafunga mikononi waaminifu na wasio na imani, watiifu na waasi, lakini katika maisha yajayo itawekwa akiba kwa ajili ya waaminifu. Ar-Rahman ni mwenye huruma kwa viumbe vyote duniani, lakini rehema yake imehifadhiwa kwa waaminifu katika maisha yajayo. Ar-Raheem atasambaza rehema zake kwa waumini siku ya kiama:

"…Adhabu yangu nitamsibu nayo nimtakaye. Na rehema yangu imeenea kila kitu. Lakini nitawaandikia khasa wanao mchamngu, na wanao toa Zaka, na wale ambao wanaziamini Ishara zetu- Ambao kwamba wanamfuata huyo Mtume, Nabii, asiye soma wala kuandika, wanaye mkuta kaandikwa kwao katika Taurati na Injili…." (Kurani 7:156-157)

Ugawaji wa rehema za Mwenyezi Mungu umeelezewa na Mtume wa Uislamu:

"Mwenyezi Mungu ameumba sehemu mia za rehema. Akaweka sehemu moja kati ya viumbe vyake kwa ajili ya kuhurumiana wao kwa wao. Mwenyezi Mungu amehifadhi sehemu tisini na tisa zilizosalia kwa ajili ya Siku ya Hukumu ili kuwafadhilisha waja Wake." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim, Al-Tirmidhi, na wengineo.)

Sehemu ndogo tu ya rehema ya Mwenyezi Mungu inajaza mbingu na ardhi, wanadamu wanapendana, wanyama na ndege wanakunywa maji.

Pia, rehema ya Mungu ambayo itadhihirika Siku ya Hukumu ni kubwa kuliko yale tunayoyaona katika maisha haya, kama vile adhabu ya Mungu itakuwa kali zaidi kuliko ile tunayoipata hapa. Mtume wa Uislamu alielezea jinsi hizi sifa mbili tukufu zilivyokithiri:

"Iwapo Muumini angejua ni adhabu gani aliyoiweka Mwenyezi Mungu, basi atakata tamaa na hakuna hata mmoja atakayetazamia kuingia Peponi. Kama kafiri angejua rehema nyingi za Mwenyezi Mungu, hakuna hata mmoja atakayekata tamaa kuifikia Pepo." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim, Al-Tirmidhi)

Hata hivyo, katika mafundisho ya Kiislamu, rehema ya Mungu inapita hasira ya Mungu:

"Hakika rehema yangu imepita adhabu yangu." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)

Mbaya Nzuri zaidi

Huruma ya Mungu (sehemu ya 3 kati ya 3): Mwenye Dhambi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi Huruma ya Mungu inavyowazunguka wale wanaoanguka katika dhambi.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,979
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Divine_Mercy_of_God_(part_3_of_3)_001.jpgHuruma ya Mungu iko karibu sana na kila mmoja wetu, inatusubiri kuipata tunapokuwa tayari. Uislamu unatambua mwelekeo wa mwanadamu kufanya dhambi, kwani Mungu amemuumba mwanadamu dhaifu. Mtume amesema:

"Watoto wote wa Adamu hukosea kila mara ..."

Wakati huo huo, Mungu hutujulisha kuwa anasamehe dhambi. Tukiendeleza Hadithi hiyo hiyo:

"...lakini walio bora zaidi kwa wanao wanaokosea daima ni wale wanaotubu daima." (Al-Tirmidhiy, Ibn Majah, Ahmad, Hakim)

Mungu anasema:

"Anasema: ‘Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.’" (Kurani 39:53)

Muhammad, Mtume mwenye Rehema, alipewa jukumu la kufikisha habari njema kwa watu wote:

"Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu." (Kurani 15:49)

Toba huvutia Rehema ya Kimungu:

"…Kwa nini mnauhimiza uwovu kabla ya wema? Kwa nini hamuombi msamaha kwa Mwenyezi Mungu ili mrehemewe?" (Kurani 27:46)

"…Hakika rehema ya Mwenyzi Mungu iko karibu na wanao fanya mema.!" (Kurani 7:56)

Tangu nyakati za kale, rehema ya Mungu ya kuokoa imewaokoa waaminifu kutokana na maangamizi yanayo wasubiri:

"Ilipo fika amri yetu, tulimwokoa Huud na walio amini pamoja naye, kwa rehema itokayo kwetu…." (Kurani 11:58)

"Na ilipo fika amri yetu, tulimwokoa Shua'ibu na wale walio amini pamoja naye kwa rehema yetu…." (Kurani 11:94)

Ukamilifu wa huruma ya Mungu kwa mwenye dhambi unaweza kuonekana katika yafuatayo:

1. Mungu Anakubali Toba

"Na Mwenyezi Mungu anataka kukurejezeni kwenye ut'iifu wake, na wanao taka kufuata matamanio wanataka mkengeuke makengeuko makubwa." (Kurani 4:27)

"Je! Hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaka, na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu." (Kurani 9:104)

2. Mungu Anampenda Mwenye Dhambi Anayetubu

"…Kwa maana Mungu huwapenda wale wanaomgeukia daima…." (Kurani 2:22)

Mtume akasema:

"Kama wanadamu hawakuwa wakifanya madhambi, Mwenyezi Mungu angeumba viumbe wengine wanaofanya madhambi, kisha angewasamehe, kwani Yeye ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu." (Al-Tirmidhi, Ibn Majah, Musnad Ahmed)

3. Mungu Hufurahi Mwenye Dhambi Anapotubu Maana Anatambua Anaye Bwana Anayesamehe Dhambi!

Mtume akasema:

“Mwenyezi Mungu hufurahishwa sana na toba ya mja wake anapotubia kuliko yeyote miongoni mwenu ikiwa (angemkuta) ngamia wake ambaye alikuwa amempanda katika jangwa lisilo na maji baada ya kumtoroka akiwa amebeba chakula chake na kinywaji chake. Baada ya kukata tamaa akauendea mti na akajilaza katika kivuli chake, kisha alipokuwa katika kukata tamaa kwake, akaja ngamia na kusimama ubavuni mwake, akazishika hatamu zake na akapiga kelele kwa furaha: Ewe Mola. Wewe ni mja wangu, na mimi ni Bwana wako’ – kufanya kosa hili (kwa maneno) kutokana na furaha yake iliyopitiliza.” (Saheeh Muslim)

4. Lango la Toba liko wazi Mchana na Usiku

Huruma ya Mwenyezi Mungu inatoa msamaha kila siku na kila usiku kwa mwaka. Mtume akasema:

“Mwenyezi Mungu hunyoosha mkono wake usiku ili kupokea toba ya aliye fanya dhambi mchana, na hunyoosha mkono wake mchana ili kupokea toba ya aliye fanya dhambi usiku mpaka [siku itakapofika] jua kutoka Magharibi (moja ya alama kuu za Siku ya Kiyama). (Saheeh Muslim)

5. Mungu Anakubali Toba Hata Dhambi Zikirudiwa

Mara kwa mara Mungu huonyesha huruma yake kwa mwenye dhambi. Fadhili za upendo za Mungu kwa Wana wa Israeli zinaweza kuonekana kabla ya dhambi ya ndama wa dhahabu kufanywa, Mungu alishughulika na Israeli kulingana na huruma yake, hata baada ya kutenda dhambi, aliwatendea kwa rehema. Ar-Rahman anasema:

"…Na tulipo muahidi Musa masiku arubaini, kisha mkachukua ndama (mkamuabudu) baada yake, na mkawa wenye kudhulumu: Kisha tukakusameheni baada ya hayo, ili mpate kushukuru." (Kurani 2:51-52)

Mtume anasema:

“Mtu mmoja alifanya dhambi, kisha akasema, ‘Ewe Mola wangu nisamehe dhambi yangu,’ Mwenyezi Mungu akasema, ‘Mja wangu ametenda dhambi, kisha akatambua kwamba ana Mola anayeweza kusamehe dhambi na anaweza kumuadhibu kwa hilo. Kisha yule mtu akairudia dhambi hiyo, kisha akasema: ‘Ewe Mola wangu, nisamehe dhambi yangu. Yule mtu akarudia dhambi hiyo (mara ya tatu), kisha akasema, ‘Ewe Mola wangu nisamehe dhambi yangu,’ na Mwenyezi Mungu akasema, ‘Mja wangu ametenda dhambi, kisha akatambua kwamba ana Mola awezaye kusamehe dhambi na anayeweza kuadhibu. Fanya upendavyo, kwani mimi nimekusamehe." (Saheeh Muslim).

6. Kuingia Uislamu Hufuta Dhambi Zote Zilizotangulia

Mtume ameeleza kwamba kuukubali Uislamu kunafuta dhambi zote za awali za Muislamu mpya, bila kujali jinsi zilivyokuwa kubwa kwa sharti moja: Muislamu mpya anaukubali Uislamu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu. Baadhi ya watu walimuuliza Mtume wa Mungu, ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je, tutawajibishwa kwa yale tuliyoyafanya wakati wa siku za ujinga kabla ya kusilimu?’ Akajibu:

"Yeyote anayeukubali Uislamu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu hatahesabiwa, lakini mwenye kufanya hivyo kwa sababu nyingine atawajibika kwa muda kabla ya Uislamu na baada yake." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)

Ingawa rehema ya Mungu inatosha kufunika dhambi yoyote, haimwachii mwanadamu kutoka kwenye wajibu wake wa kutenda ifaavyo. Nidhamu na bidii inahitajika katika njia ya wokovu. Sheria ya Wokovu katika Uislamu inatilia maanani imani na kushika Sheria, si imani tu katika Mungu. Sisi si wakamilifu na ni dhaifu na Mungu alituumba hivi. Tunapokosa kushika Sheria takatifu, Mungu Mwenye Upendo yuko tayari kusamehe. Msamaha unapokelewa kwa urahisi kupitia kuungama dhambi kwa Mungu peke yake na kuomba rehema zake, akiwa na nia thabiti ya kutofanya tena. Lakini mtu anapaswa kukumbuka daima kwamba Pepo haipatikani kwa matendo ya mtu pekee, bali hutolewa kwa rehema ya Mwenyezi Mungu. Mtume wa Rehema aliweka wazi ukweli huu:

“Hataingia Peponi hata mmoja wenu kwa vitendo vyake peke yake.’ Wakauliza, ‘Hata wewe ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?’ Akasema, ‘Hata mimi, isipokuwa Mwenyezi Mungu amenifunika kwa fadhila na rehema zake." (Saheeh Muslim)

Imani katika Mungu, kushika Sheria Yake, na matendo mema, yanazingatiwa kuwa kama sababu, sio njia ya kuingia Peponi.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.