Huruma ya Mungu (sehemu ya 3 kati ya 3): Mwenye Dhambi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi Huruma ya Mungu inavyowazunguka wale wanaoanguka katika dhambi.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,937 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Divine_Mercy_of_God_(part_3_of_3)_001.jpgHuruma ya Mungu iko karibu sana na kila mmoja wetu, inatusubiri kuipata tunapokuwa tayari. Uislamu unatambua mwelekeo wa mwanadamu kufanya dhambi, kwani Mungu amemuumba mwanadamu dhaifu. Mtume amesema:

"Watoto wote wa Adamu hukosea kila mara ..."

Wakati huo huo, Mungu hutujulisha kuwa anasamehe dhambi. Tukiendeleza Hadithi hiyo hiyo:

"...lakini walio bora zaidi kwa wanao wanaokosea daima ni wale wanaotubu daima." (Al-Tirmidhiy, Ibn Majah, Ahmad, Hakim)

Mungu anasema:

"Anasema: ‘Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.’" (Kurani 39:53)

Muhammad, Mtume mwenye Rehema, alipewa jukumu la kufikisha habari njema kwa watu wote:

"Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu." (Kurani 15:49)

Toba huvutia Rehema ya Kimungu:

"…Kwa nini mnauhimiza uwovu kabla ya wema? Kwa nini hamuombi msamaha kwa Mwenyezi Mungu ili mrehemewe?" (Kurani 27:46)

"…Hakika rehema ya Mwenyzi Mungu iko karibu na wanao fanya mema.!" (Kurani 7:56)

Tangu nyakati za kale, rehema ya Mungu ya kuokoa imewaokoa waaminifu kutokana na maangamizi yanayo wasubiri:

"Ilipo fika amri yetu, tulimwokoa Huud na walio amini pamoja naye, kwa rehema itokayo kwetu…." (Kurani 11:58)

"Na ilipo fika amri yetu, tulimwokoa Shua'ibu na wale walio amini pamoja naye kwa rehema yetu…." (Kurani 11:94)

Ukamilifu wa huruma ya Mungu kwa mwenye dhambi unaweza kuonekana katika yafuatayo:

1. Mungu Anakubali Toba

"Na Mwenyezi Mungu anataka kukurejezeni kwenye ut'iifu wake, na wanao taka kufuata matamanio wanataka mkengeuke makengeuko makubwa." (Kurani 4:27)

"Je! Hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaka, na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu." (Kurani 9:104)

2. Mungu Anampenda Mwenye Dhambi Anayetubu

"…Kwa maana Mungu huwapenda wale wanaomgeukia daima…." (Kurani 2:22)

Mtume akasema:

"Kama wanadamu hawakuwa wakifanya madhambi, Mwenyezi Mungu angeumba viumbe wengine wanaofanya madhambi, kisha angewasamehe, kwani Yeye ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu." (Al-Tirmidhi, Ibn Majah, Musnad Ahmed)

3. Mungu Hufurahi Mwenye Dhambi Anapotubu Maana Anatambua Anaye Bwana Anayesamehe Dhambi!

Mtume akasema:

“Mwenyezi Mungu hufurahishwa sana na toba ya mja wake anapotubia kuliko yeyote miongoni mwenu ikiwa (angemkuta) ngamia wake ambaye alikuwa amempanda katika jangwa lisilo na maji baada ya kumtoroka akiwa amebeba chakula chake na kinywaji chake. Baada ya kukata tamaa akauendea mti na akajilaza katika kivuli chake, kisha alipokuwa katika kukata tamaa kwake, akaja ngamia na kusimama ubavuni mwake, akazishika hatamu zake na akapiga kelele kwa furaha: Ewe Mola. Wewe ni mja wangu, na mimi ni Bwana wako’ – kufanya kosa hili (kwa maneno) kutokana na furaha yake iliyopitiliza.” (Saheeh Muslim)

4. Lango la Toba liko wazi Mchana na Usiku

Huruma ya Mwenyezi Mungu inatoa msamaha kila siku na kila usiku kwa mwaka. Mtume akasema:

“Mwenyezi Mungu hunyoosha mkono wake usiku ili kupokea toba ya aliye fanya dhambi mchana, na hunyoosha mkono wake mchana ili kupokea toba ya aliye fanya dhambi usiku mpaka [siku itakapofika] jua kutoka Magharibi (moja ya alama kuu za Siku ya Kiyama). (Saheeh Muslim)

5. Mungu Anakubali Toba Hata Dhambi Zikirudiwa

Mara kwa mara Mungu huonyesha huruma yake kwa mwenye dhambi. Fadhili za upendo za Mungu kwa Wana wa Israeli zinaweza kuonekana kabla ya dhambi ya ndama wa dhahabu kufanywa, Mungu alishughulika na Israeli kulingana na huruma yake, hata baada ya kutenda dhambi, aliwatendea kwa rehema. Ar-Rahman anasema:

"…Na tulipo muahidi Musa masiku arubaini, kisha mkachukua ndama (mkamuabudu) baada yake, na mkawa wenye kudhulumu: Kisha tukakusameheni baada ya hayo, ili mpate kushukuru." (Kurani 2:51-52)

Mtume anasema:

“Mtu mmoja alifanya dhambi, kisha akasema, ‘Ewe Mola wangu nisamehe dhambi yangu,’ Mwenyezi Mungu akasema, ‘Mja wangu ametenda dhambi, kisha akatambua kwamba ana Mola anayeweza kusamehe dhambi na anaweza kumuadhibu kwa hilo. Kisha yule mtu akairudia dhambi hiyo, kisha akasema: ‘Ewe Mola wangu, nisamehe dhambi yangu. Yule mtu akarudia dhambi hiyo (mara ya tatu), kisha akasema, ‘Ewe Mola wangu nisamehe dhambi yangu,’ na Mwenyezi Mungu akasema, ‘Mja wangu ametenda dhambi, kisha akatambua kwamba ana Mola awezaye kusamehe dhambi na anayeweza kuadhibu. Fanya upendavyo, kwani mimi nimekusamehe." (Saheeh Muslim).

6. Kuingia Uislamu Hufuta Dhambi Zote Zilizotangulia

Mtume ameeleza kwamba kuukubali Uislamu kunafuta dhambi zote za awali za Muislamu mpya, bila kujali jinsi zilivyokuwa kubwa kwa sharti moja: Muislamu mpya anaukubali Uislamu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu. Baadhi ya watu walimuuliza Mtume wa Mungu, ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je, tutawajibishwa kwa yale tuliyoyafanya wakati wa siku za ujinga kabla ya kusilimu?’ Akajibu:

"Yeyote anayeukubali Uislamu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu hatahesabiwa, lakini mwenye kufanya hivyo kwa sababu nyingine atawajibika kwa muda kabla ya Uislamu na baada yake." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)

Ingawa rehema ya Mungu inatosha kufunika dhambi yoyote, haimwachii mwanadamu kutoka kwenye wajibu wake wa kutenda ifaavyo. Nidhamu na bidii inahitajika katika njia ya wokovu. Sheria ya Wokovu katika Uislamu inatilia maanani imani na kushika Sheria, si imani tu katika Mungu. Sisi si wakamilifu na ni dhaifu na Mungu alituumba hivi. Tunapokosa kushika Sheria takatifu, Mungu Mwenye Upendo yuko tayari kusamehe. Msamaha unapokelewa kwa urahisi kupitia kuungama dhambi kwa Mungu peke yake na kuomba rehema zake, akiwa na nia thabiti ya kutofanya tena. Lakini mtu anapaswa kukumbuka daima kwamba Pepo haipatikani kwa matendo ya mtu pekee, bali hutolewa kwa rehema ya Mwenyezi Mungu. Mtume wa Rehema aliweka wazi ukweli huu:

“Hataingia Peponi hata mmoja wenu kwa vitendo vyake peke yake.’ Wakauliza, ‘Hata wewe ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?’ Akasema, ‘Hata mimi, isipokuwa Mwenyezi Mungu amenifunika kwa fadhila na rehema zake." (Saheeh Muslim)

Imani katika Mungu, kushika Sheria Yake, na matendo mema, yanazingatiwa kuwa kama sababu, sio njia ya kuingia Peponi.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.