Safari ya Kuelekea Akhera (sehemu ya 2 kati ya 8): Muumini ndani ya Kaburi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Maelezo ya maisha ndani ya kaburi kuanzia kifo hadi Siku ya Hukumu kwa waumini waaminifu.

  • Na Imam Mufti (co-author Abdurrahman Mahdi)
  • Iliyochapishwa mnamo 12 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,805 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Ulimwengu wa Kaburini

Sasa tutaangalia kwa ufupi safari ya roho baada ya kifo. Kwa kweli hii ni hadithi ya kushangaza, hususan kwa sababu ni ya kweli na ambayo sote lazima tutaipitia. Elimu tuliyonayo kuhusu safari hii, usahihi wake na undani wake, ni dalili ya wazi kwamba Muhammad alikuwa kweli Mtume wa Mwisho wa Mwenyezi Mungu kwa wanadamu. Wahyi alioupokea kisha akatufikishia kutoka kwa Mola Wake Mlezi hauna utata katika maelezo yake ya maisha ya Akhera kwa sababu ni pana. Unapoitazama elimu hii kijuujuu utaanza na ugunduzi mfupi wa safari ya roho ya muumini kutoka muda wa kifo hadi mahali pake pa kupumzika Peponi.

Muumini anapokaribia kuondoka duniani, malaika wenye nyuso nyeupe hushuka kutoka mbinguni na kusema:

"Ewe nafsi iliyotulia, toka mwilini upate msamaha wa Mwenyezi Mungu na radhi zake." (Hakim na wengine)

Muumini atatarajia kukutana na Muumba wake, kama alivyoeleza Mtume, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu zimshukie:

"…wakati wa kifo cha Muumini unapokaribia, anapokea habari njema ya radhi za Mungu pamoja na baraka Zake juu yake, na hivyo wakati huo hakuna kitu chenye thamani zaidi kwake kuliko kile kilicho mbele yake. Kwa hivyo anapenda kukutana na Mungu, na Mungu anapenda kukutana naye." (Saheeh Al-Bukhari)

Roho hutoka mwilini kwa amani kama tone la maji litokalo kwenye kiriba, na malaika huishikilia:

Malaika huitoa kwa upole, wakiwaambia:

"…Msiogope wala msihuzunike; nanyi furahini kwa Pepo mliyokuwa mkiahidiwa. Sisi ni vipenzi vyenu katika maisha ya dunia na katika Akhera, na humo mtapata kinachotamaniwa na nafsi zenu, na humo mtapata mtakavyovitaka. Ni takrima itokayo kwa Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu." (Kurani 41:30-32)

Mara baada ya kutolewa kutoka kwenye mwili, malaika huifunika roho katika sanda yenye harufu ya miski na kupaa nayo juu mbinguni. Malango ya Mbinguni yanapofunguka kwa ajili ya roho hiyo, malaika huisalimu:

"Roho njema imekuja kutoka duniani, Mungu akubariki na mwili uliokuwa ukiishi ndani yake."

…itatambulishwa kwa majina bora ambayo iliitwa nayo katika maisha haya ya duniani. Mungu anaamuru "kitabu" chake kirekodiwe, na roho inarudishwa tena duniani.

Roho itabakia kuzimuni ndani ya kaburi lake, iitwayo Barzakhi, ikingojea Siku ya Hukumu. Malaika wawili wa kutisha, wanaoitwa Munkar na Nakir huitembelea roho ili kuiuliza kuhusu dini yake, Mungu, na mtume. Roho ya muumini hukaa wima katika kaburi lake huku Mwenyezi Mungu akiipa nguvu ya kuwajibu malaika hao kwa imani kamili na yakini.[1]

Munkar na Nakir: "Dini yako ni ipi?"

Roho ya Muumini: "Uislamu."

Munkar na Nakir: "Nani Mola wako?"

Roho ya Muumini: "Allah."

Munkar na Nakir: "Nani Mtume wako?" (au "Unasemaje kuhusu mwanamume huyu?")

Roho ya Muumini: "Muhammad."

Munkar na Nakir: "Ulijuaje mambo haya?"

Roho ya Muumini: "Nilisoma Kitabu cha Mwenyezi Mungu (yaani Kurani) na nikaamini."

Na roho ikishapita mtihani, sauti kutoka mbinguni itaita:

"Mja wangu amesema kweli, mpeni vyombo vya Peponi, mvisheni mavazi ya Peponi, na mfungulieni lango moja la Peponi."

Kaburi la muumini hupanuliwa nafasi na kufanywa pana na kujazwa nuru. Huonyeshwa yale yangekuwa makazi yake katika Jehanamu – lau angekuwa mwovu mtenda dhambi – hayo yatatendeka kabla ya mlango kufunguliwa kwa ajili yake kila asubuhi na jioni ukimuonyesha makazi yake halisi Peponi. Kwa msisimko na matarajio ya furaha, muumini ataendelea kuuliza: ‘Saa (ya Ufufuo) itakuja lini?! Lini Saa itafika?!’ mpaka aambiwe atulie.[2]



Rejeleo la maelezo:

[1] Musnad Ahmad

[2] Al-Tirmidhi

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.