Safari ya Kuelekea Akhera (sehemu ya 1 kati ya 8): Utangulizi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Utangulizi wa dhana ya kuwepo maisha baada ya kifo katika Uislamu, na jinsi inavyofanya maisha yetu kuwa na maana; kwa kusudi.

  • Na Imam Mufti (co-author Abdurrahman Mahdi)
  • Iliyochapishwa mnamo 12 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 13 Mar 2023
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,614
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Utangulizi

The_Journey_into_the_Hereafter_(part_1_of_8)_001.jpgMuhammad, Mtume wa Uislamu aliyefariki mwaka 632, alisimulia:

"Jibril alikuja kwangu na kuniambia, ‘Ewe Muhammad, ishi upendavyo, kwani mwishowe utakufa. Mpende unayemtaka, kwani hatimaye utaondoka. Fanya upendavyo, kwani utalipwa. Jua kuwa sala ya usiku[1]ni heshima ya Muumini, na fahari yake ni kuwa huru bila kuwategemea wengine.’" (Silsilah al-Saheehah)

Kuna jambo moja tu la uhakika kuhusu maisha, nalo ni kuwa yana mwisho. Kauli hii ya ukweli huzua swali la kiada ambalo huwashughulisha watu wengi angalau mara moja katika umri wao: Kuna nini kinaendelea baada ya kifo?

Katika kiwango cha fiziolojia (sayansi ya mwili wa viumbe unavyofanya kazi), safari ambayo marehemu hupitia hushuhudia waziwazi na wote. Sehemu za mwili kitabia zikiachwa zijiendeshe peke yake,[2] moyo utaacha kupiga, mapafu yataacha kupumua, na seli za mwili zitakuwa na njaa ya damu na oksijeni. Kukomesha mtiririko wa damu kupitia seli hizo na kusambaa mwili mzima hivi karibuni huzifanya kupauka rangi. Oksijeni ikiwa imekatwa, seli zitapumua kama anerobi (viumbe vyenye kuishi bila oksijeni) kwa muda, na kutoa asidi ya maziwa yaliyochachuka inayosababisha ukakamaaji wa misuli - kukausha misuli ya maiti. Kisha, seli zinapoanza kuoza, ukakamavu hupungua, ulimi hujitokeza nje, halijoto huteremka, ngozi hubadilika rangi, nyama huoza, na vimelea huwa na karamu yao - mpaka kinachobaki ni jino na mifupa iliyokauka.

Kuhusu safari ya roho baada ya kufa, basi hili si jambo linaloweza kushuhudiwa, wala haliwezi kupimwa kwa uchunguzi wa kisayansi. Hata katika mwili ulio hai, fahamu, au roho, ya mtu haiwezi kufanyiwa majaribio ya kiuchunguzi. Ni nje ya udhibiti wa binadamu. Kuhusu hili, dhana ya Akhera - maisha baada ya kifo, ufufuo, na Siku ya Hesabu; bila kusahau kutaja uwepo wa Mwenyezi Mungu, Muumba Muweza wa yote, malaika Wake, majaaliwa, na kadhalika - huwekwa chini ya mada ya imani ya mambo ya ghaibu. Njia pekee ambayo mwanadamu anaweza kujua lolote la ulimwengu usioonekana ni kupitia wahyi wa kiungu.

"Na ziko kwake funguo za ghaibu; hakuna azijuaye ila Yeye tu. Na Yeye anajua kilioko nchi kavu na baharini. Na halidondoki jani ila analijua. Wala punje katika giza la ardhi, wala kinyevu, wala kikavu ila kimo katika Kitabu kinachobainisha." (Kurani 6:59)

Ingawa yale yaliyotufikia kutoka Taurati, Zaburi, Injili - maandiko yaliyoteremshwa kwa mitume wa mwanzo - yote yanazungumzia Akhera, ni kupitia Wahyi wa Mwisho wa Mwenyezi Mungu kwa wanadamu, Kurani Tukufu, kama ilivyoteremshwa kwa Mtume Wake wa Mwisho, Muhammad, kwamba tunajifunza mambo zaidi kuhusu maisha ya baada ya kifo. Na kama vile Kurani ilivyo, na itabakia daima, imehifadhiwa na bila kuvurugwa na mikono ya wanadamu, ubainifu unaotupa katika ulimwengu wa ghaibu, kwa Muumini, ni ukweli, halisi na uhakika kama vile kitu chochote kinachoweza kufunzwa kupitia jitihada yoyote ya kisayansi (na bila athari yoyote katika matokeo!).

"…Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote. Kisha kwa Mola wao Mlezi watakusanywa." (Kurani 6:38)

Sambamba na swali la kile kinachotokea baada ya kufa, ni swali jingine: Kwa nini tuko hapa? Kwani ikiwa kwa hakika hakuna kusudi kubwa zaidi la kuishi (yaani, kubwa zaidi ya kuishi maisha yenyewe), swali la kile kinachotokea baada ya kifo huwa la kitaaluma, ama lisiwe na maana yoyote. Ni kama tu mtu akikubali kwanza kuwa usanifu wetu wa akili, uumbaji wetu, unahitaji yule mwenye akili na ruwaza zaidi nyuma yake, na ni Muumba ambaye atatuhukumu kwa yale tunayofanya katika uhai huu wa duniani, ndipo maisha huwa na maana muhimu.

"Je, mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa? Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa Arshi Tukufu." (Kurani 23:115-116)

Ikiwa sivyo, mtu mwenye utambuzi atalazimika kukata kauli kwamba maisha duniani yamejaa ukosefu wa haki, ukatili na uonevu; kwamba sheria ya msituni, kuishi kwa walio na nguvu zaidi, ndio muhimu zaidi; kwamba ikiwa mtu hawezi kupata furaha katika maisha haya, iwe ni kutokana na kutokuwepo vitu vya kupumbaza, mapenzi ya kimwili, au kufurahia starehe nyingine, basi maisha hayo mtu hafai kuyaishi. Kwa hakika, mtu hukata tamaa na maisha ya hapa duniani akiwa na imani ndogo, au hana imani kabisa, au ana imani isiyo kamilifu kuhusu maisha ya baada ya kifo, ndipo anaweza kujiua. Baada ya yote, ni nini kingine kinachofanya wasio na furaha, wasiopendwa na wasiohitajika; waliovunjika moyo (waliokata tamaa), wenye kuhuzunika na waliokosa matumaini, kupoteza wakikosa budi?![3]

"Akasema: Na nani anayekata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale waliopotea?" (Kurani 15:56)

Kwa hivyo, je, twaweza kukubali ya kwamba kifo chetu kinategemea kusitishwa tu kifiziolojia, au kuwa uhai ni tokeo tu la nadharia ya mageuko ya upofu na ya kibinafsi? Hakika, kuna mambo zaidi tusiyoyajua kuhusu kifo, na vivyo hivyo uhai, kuliko hili.



Rejeleo la maelezo:

[1] Hii ni sala (salati)ambayo ni ya hiari na inasaliwa usiku baada ya sala ya mwisho (isha) na kabla ya kwanza (fajr), ambazo ni miongoni mwa sala tano rasmi za kila siku. Wakati mzuri wa kusali sala ya tahajjud ni katika theluthi ya mwisho ya usiku.

[2]Ingawa moyo unaweza kudumishwa kuendelea kupiga kupitia mashine, na damu kusukumwa kwa msaada wa mashine, iwapo ubongo umekufa, ndivyo kiumbe kwa ujumla.

[3]Kulingana na ripoti ya Umoja wa Mataifa inayoadhimisha 'Siku ya Kuzuia Kujiua Ulimwenguni', "Watu wengi hujiua kila mwaka kuliko wanaokufa kutokana na vita na mauaji kwa pamoja ... Kati ya milioni 20 hadi 60 hujaribu kujiua kila mwaka, lakini karibu milioni moja tu ya watu wanaojiua. hufanikiwa." (Reuters, Septemba 8, 2006)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa