L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Moja ya sababu ambazo familia ya Kiislamu inafanya kazi ni kwa sababu ya muundo wake uliofafanuliwa kwa uwazi, ambapo kila mwanakaya anajua jukumu lake. Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alisema:
“Kila mmoja wenu ni mchungaji, na nyote mnawajibika kwa mlichokichunga.” (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)
Baba ndiye mchungaji wa familia yake, anawalinda, anawapatia mahitaji yao, na anajitahidi kuwa mfano wao wa kuigwa na kuongoza kwa uwezo wake kama mkuu wa kaya. Mama ndiye mchungaji wa juu katika nyumba, akiilinda na kuyaingiza ndani, yale mazuri, yenye upendo ambayo ni ya umuhimu kwa maisha ya familia yenye furaha na afya. Yeye pia ndiye anayehusika na mwongozo wa watoto na elimu. Isingekuwa mgawanyo wa majukumu mmoja wa wazazi angechukua jukumu la uongozi, basi bila shaka kutakuwa na mabishano na mapigano ya kila wakati, na kusababisha kuvunjika kwa familia - kama vile kungekuwa na shirika lolote ambalo lisingekuwa na mamlaka yoyote ya kihierarkia.
“Mwenyezi Mungu amepiga mfano wa mtu mwenye mabwana washirika wanao gombana, na wa mtu mwengine aliye khusika na bwana mmoja tu. Je! Wako sawa katika hali zao? Alhamdulillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu! Lakini wengi wao hawajui.” (Kurani 39:29)
Ni jambo la busara kuwa yule ambaye kwa asili ana nguvu ya mwili na hisia katika wazazi hao wawili hufanywa mkuu wa kaya: mwanaume.
“…wanawake wanayo haki kwa Sharia kama ile haki iliyo juu yao. Na wanaume wana daraja zaidi kuliko wao…” (Kurani 2:228)
Na kwa watoto, ni matunda ya upendo ya mzazi wao, Uislamu unaweka maadili kamili yanayoamuru uwajibikaji wa wazazi na jukumu linarudi kwa mtoto kwa wazazi wao.
“na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni.’” (Kurani 17:23-24)
Ni wazi, ikiwa wazazi wanashindwa kuweka hofu ya Mungu ndani ya watoto wao tangu utotoni kwa sababu wao wenyewe hawajali, basi hawawezi kutarajia kuona shukrani ya haki ikirudishwa kwao. Kwa hivyo, onyo kali la Mungu katika Kitabu Chake:
“Enyi mlio amini! Jilindeni nafsi zenu na ahali zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe.” (Kurani 66:6)
Ikiwa wazazi kweli watajitahidi kulea watoto wao katika haki, basi, kama vile Mtume alisema:
“Pindi mwana wa adamu anapokufa, vitendo vyake vyote vimekoma isipokuwa [vitatu, sadaka inayoendelea, maarifa yenye faida, na] mtoto mwadilifu ambaye huwaombea wazazi wake.” (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)
Haijalishi jinsi gani wazazi wamemlea mtoto wao, na bila kujali dini yao (au ukosefu wao), utii na heshima ambayo mwana wa Kiislamu au binti anahitajika kuwaonyesha ni ya pili kwa utii ukilinganisha na kwa Muumba Mwenyewe. Kwa hivyo Ukumbusho Wake:
“Na tulipo funga agano na Wana wa Israili: Hamtamuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu; na muwafanyie wema wazazi na jamaa na mayatima na masikini, na semeni na watu kwa wema, na shikeni Swala, na toeni Zaka.’” (Kurani 2:83)
Hakika, ni kawaida kusikia wazee wasio Waislamu kusilimu kwa sababu ya kuongezeka kwa matunzo na uadilifu ambao watoto wao huwapatia kufuatia wao (yaani watoto) kuwa Waislamu.
“Sema: Njooni nikusomeeni aliyo kuharimishieni Mola wenu Mlezi. Nayo ni kuwa, msimshirikishe Yeye na chochote. Na wazazi wenu wafanyieni wema. Wala msiwauwe watoto wenu kwa sababu ya umasikini. Sisi tunakuruzukuni nyinyi na wao…’” (Kurani 6:151)
Wakati mtoto analazimika kuonyesha utii kwa wazazi wote wawili, Uislamu unamchagua mama kuwa ndiye anayestahili kwa sehemu kubwa ya shukrani ya upendo na fadhila. Mtume Muhammad alipoulizwa, “Ewe Mjumbe wa Mungu! Ni nani kati ya wanadamu anayeidhinishwa nimfanyie wema?” alijibu:“Mama Yako” mtu huyo akauliza:“kisha nani?” Mtume akamjibu: “Mama yako.” Mtu huyo akauliza: “Kisha nani?” Mtume akarudia tena: “Mama yako.” Mtu yule akauliza tena: ‘Kisha nani?’ Mwisho mtume akamjibu “(Kisha) baba yako.”[1]
“Na tumemuusia mwanaadamu awatendee wema wazazi wake wawili. Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu, na akamzaa kwa taabu. Na kuchukua mimba kwake hata kumwachisha ziwa ni miezi thalathini. Hata anapo fika utu uzima wake, na akafikilia miaka arubaini, husema: Mola wangu Mlezi! Niwezeshe nishukuru neema zako ulizo nineemesha mimi na wazazi wangu, na nitende mema unayo yapenda. Na unitengenezee dhuriya zangu. Hakika mimi nimetubu kwako, na mimi ni miongoni mwa Waislamu. ’” (Kurani 46:15)
Katika Uislamu kunakanuni ya jumla inayosema kwamba kile kinachomfaa mtu ni kizuri kwa mwingine. Au, kwa maneno ya Mtume:
“Hatoamini mmoja wenu kweli mpaka ampendelee ndugu yake (aliyeamini) kile anachokipenda mwenyewe.” (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)
Kama inavyotarajiwa, kanuni hii inadhihirika zaidi katika familia ya Kiislamu, kiini cha jamii ya Kiislamu. Ila, jukumu la mtoto kwa wazazi wake, hakika, linaelekezwa hata kwa wazee wote wa jamii. Rehema na wasiwasi walio nao wazazi kwa watoto wao ndivyo iwepo kwa watoto wote. Hakika, sio kwamba Muislamu ana chaguo katika mambo kama haya. Baada ya yote, Mtume alisema:
“Yeye asiyeonyesha huruma kwa vijana wetu, wala kuwaheshimu wazee wetu, hatoki kwetu.” (Abu Dawood, Al-Tirmidhi)
Je! Ni jambo la kushangaza, kwamba watu wengi, waliolelewa kama wasio Waislamu, hupata kile ambacho wamekuwa wakikitafuta, kile ambacho wamekuwa wakikiamini kila wakati kuwa kizuri na cha kweli, katika dini ya Uislamu? Dini ambayo inawakaribisha haraka na kwa uchangamfu kama mshiriki wa familia moja yenye upendo.
“Sio wema kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi. Bali wema ni wa anaye muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, na anawapa mali, kwa kupenda kwake, jamaa na mayatima na masikini na wasafiri, na waombao, na katika ugombozi, na akawa anashika Swala, na akatoa Zaka, na wanao timiza ahadi yao wanapo ahidi, na wanao vumilia katika shida na dhara na wakati wa vita; hao ndio walio sadikisha, na hao ndio wajilindao. ” (Kurani 2:177)
[1] Imeelezewa ndani ya Saheeh al-Bukhari and Saheeh Muslim.
Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.
Orodha yako ya historia ipo tupu.
Kwa nini kujiandikisha? Tovuti hii ina miundo kadhaa uliyoundwa mahsusi kwa ajili yako, kama vile: vipendwa vyako, historia yako, kutia alama makala ambazo umezitazama awali, kuorodhesha makala zilizochapishwa tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho, kubadilisha ukubwa wa herufi, na zaidi. Vipengele hivi vinatokana na vidakuzi na vitafanya kazi ipasavyo tu unapotumia kompyuta ile ile. Ili kuwezesha vipengele hivi kutoka kwa kompyuta yoyote, unapaswa kuingia wakati katika tovuti hii.
Tafadhali ingiza Jina lako la mtumiaji na anwani ya barua pepe kisha ubofye kitufe cha Tuma neno la siri. Utapokea neno la siri jipya hivi karibuni. Tumia neno la siri hili jipya kufikia tovuti.
Ongeza maoni