Familia katika Uislamu (sehemu ya 1 kati ya 3): Hukumu ya Maisha ya Familia ya Kiislam

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Watu wa matabaka mablimbali ya maisha wanazungumza kuhusu maoni yao juu ya maisha ya familia katika Uislamu.

  • Na AbdurRahman Mahdi (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 06 Feb 2023
  • Ilichapishwa: 2
  • Imetazamwa: 4,751 (wastani wa kila siku: 6)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Family_in_Islam_(part_1_of_3)_001.jpgKatika Uislamu, katika kuzingatia ustawi wa yule "mwingine" badala ya "nafsi" tu ni fadhila iliyojikita katika dini hiyo kuwa ya uwazi hata kwa wale walio nje yake. Wakili wa Uingereza wa haki za kibinadamu na haki za raia, Clive Stafford-Smith, ambaye sio Muislamu, alisema: "Ninachopenda juu ya Uislamu ni kulenga kwake kikundi, ambapo ni kinyume na mtazamo wa Magharibi juu ya moja moja."[1]

Watu wanajumuisha jamii yoyote inayojifunga pamoja kwa vifungo vya kundi linalohusiana. Vifungo vyenye nguvu zaidi ni vile vya familia. Na ingawa inaweza kusemwa kwa haki kuwa msingi wa familia ni msingi wa jamii yoyote ya wanadamu, hii inashikilia ukweli kwa Waislamu. Hakika, hadhi kubwa ambayo Uislamu unatoa katika mfumo wa familia ndio kitu ambacho mara nyingi huvutia waliosilimu wengi, haswa wanawake.

"Pamoja na sheria kuwepo karibu katika kila nyanja ya maisha, Uislamu unawakilisha utaratibu wa kiimani ambao wanawake wanaweza kuuona kama muhimu katika kuunda familia na jamii zenye afya, na kurekebisha uharibifu uliofanywa na uwanadamu wa kidunia wa miaka thelathini au zaidi iliyopita, wataalam kadhaa wanasema. Kwa kuongezea, wanawake kutoka kwenye nyumba zilizovunjika wanaweza kuvutiwa na dini hiyo kwa sababu ya thamani inayokewa familia, alisema Marcia Hermansen, profesa wa masomo ya Kiislamu katika Chuo Kikuu cha Loyola huko Chicago na Mmarekani ambaye pia alisilimu. "[2]

Hakuna mahali ambapo mwelekeo huu wa watu wanaothamini maadili ya jadi ya kifamilia wanapokubali Uislamu umeenea zaidi katika jamii ya Kilatino ya Amerika ya Kaskazini au jamii ya Wahispania. Kama mmoja wa Waislamu wa Florida alivyoona: "Nimeona kuongezeka kwa kiwango cha Wahispania wakisilimu na kuwa Waislamu. Nadhani utamaduni wa Wahispania yenyewe unathamini sana familia, na hilo ni jambo ambalo linajulikana sana katika dini ya Uislamu. "

Sasa, yepi maadili au tabia fulani ya maisha ya familia ya Kiislamu ambayo wengi wanayaona ya kupendeza sana?

Katika hafla ya Kiislamu ya Chuo Kikuu cha Columbia, Hernan Guadalupe, Mmarekani-wa Ecuado: “alizungumzia kufanana kwa kitamaduni na maadili ya kifamilia yaliyo kwa Wahispania na Waislamu. Kwa kawaida, kaya za Wahispania zina uhusiano thabiti na zinajitolea, na watoto hulelewa katika mazingira thabiti- tabia ambazo zinaonekana katika familia za Waislamu.”[3]

Na katika ripoti nyingine ya hivi karibuni ya gazeti, ilionekana pia jinsi: "Maadili ya kifamilia yana jukumu muhimu katika malezi ya jamii ya Waislamu. Kwa sababu ya maadili hayo ya kifamilia, kuna kanuni zingine nyingi ambazozipo sawa kati ya jamii ya Wahispania na Uislamu; kwa mfano, kuheshimu wazee, maisha ya ndoa, na kulea watoto, hizi ni mila za Wahispania zinazofanana na Uislamu. ”[4]

Baadhi ya Wamarekani wa kawaida waliosilimu pia wamekuwa na maoni juu ya uzoefu wa maisha halisi, na baadhi yao hukusanywa katika kitabu cha mama wa huyo aliyesilimu; Daughters of Another Path na Carol L. Anway.. Mwanamke mmoja, aliyenukuliwa katika kitabu hicho[5], alizungumzia juu ya mabadiliko yake ya mtazamo juu ya ndoa na maisha ya familia baada ya kusilimu. “Nilikuwa msafi zaidi na mtulivu kadiri nilivyoendelea kuingia katika dini. Niliwa na nidhamu ya hali ya juu. Sikukusudia kuolewa kabla ya kuwa Muislamu, lakini haraka nikawa mke na baadaye mama. Uislamu umetoa mfumo ambao umeniruhusu kuelezea imani, kama vile upole, fadhila, na upendo, ambayo nilikuwa nayo tayari. Imeniongoza pia kupata furaha kupitia ndoa na kuzaa watoto wawili. Kabla ya Uislamu, sikuwa na hamu ya kuwa na familia yangu mwenyewe kwani nilichukia (wazo la kuwa na) watoto. ”

Mwanamke mwingine anazungumzia juu ya kukubalika kwake katika familia kubwa katika kitabu hicho hicho. "Tulikutana katika uwanja wa ndege na familia yake kubwa, na ilikuwa wakati uliogusa sana, ambao sitaisahau. Mama (mama mkwewe) ni kama malaika… Nimetumia muda mwingi kulia, kwa sababu ya kile ninachokiona hapa. Mfumo wa familia ni wa kipekee kabisa na ukaribu ambao ni zaidi ya maneno.”[6]

Katika Kiambatisho C cha kitabu hicho, Mmarekani aliye badili dini mwenye umri wa miaka 35, wakati huo akiwa na miaka 14 akiwa Muislamu, aliandika juu ya familia ya mumewe na maadili yao kulingana na maadili yake ya Kimarekani. "Nimekutana na watu wote wa familia ya karibu ya mume wangu na watu wengine wa familia yake kubwa… nimejifunza mengi kutoka kwa wakwe zangu. Wana njia nzuri za kushirikiana na watoto wao, njia ambayo inaleta heshima kwa wengine na ujithamini. Inafurahisha kuona jinsi utamaduni na dini unavyofanya kazi kwa watoto. Mashemeji zangu, kwa sababu ya kuwa tofauti na utamaduni wa Kimarekani, imenifanya mwenye kushukuru katika vitu kadhaa vya tamaduni yangu ya Marekani… nimeona kuwa Uislamu ni wa kweli kwa kusema kuwa ni njia sahihi. ”[7]

Kutoka kwenye nukuu hizi, moja kutoka kwa msomi asiye Muislamu, wengine kutoka kwa walioingia kwenye Uislamu na waandishi wa habari, na wengine wanawake wa kawaida wa Marekani ambao walisilimu, tunaweza kuona kwamba maadili ya kifamilia katika Uislamu ni moja wapo ya vivutio vyake vikubwa. Maadili haya yanatokana na Mungu na mwongozo Wake, kupitia Quran na mfano na mafundisho ya Mtume Wake, Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, ambaye anaonyesha familia ni kama moja ya misingi ya dini na Uislamu ni njia ya maisha. Umuhimu wa kuunda familia umesisitizwa na msemo wa Mtume mwenyewe Mtukufu, ambaye alisema:

“Mtu akioa, ametimiza nusu ya dini yake, kwa hivyo amwogope Mungu juu ya nusu iliyobaki.”[8] (al-Baihaqi)

Vifungu viwili vifuatavyo vitajadili familia katika Uislamu kulingana na Quran na mafundisho ya Unabii. Kupitia uchunguzi wa Uislam juu ya mada za maisha ya ndoa, heshima kwa wazazi na wazee, na kulea watoto, tunaweza kuanza kushukuru faida za familia katika Uislamu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Emel Magazine, Issue 6 - Juni/Julai 2004.

[2] “Islam’s Female Converts”; Priya Malhotra, February 16, 2002. (angalia http://thetruereligion.org/modules/xfsection/article.php?articleid=167).

[3] “Some Latinos convert to Islam”; Marcela Rojas, The Journal News (http://www.thejournalnews.com/apps/pbcs.dll/article?AID=/20051030/NEWS02/510300319/1028/NEWS12)

[4] “Islam Gains Hispanic Converts”; Lisa Bolivar, Special Correspondent, September 30, 2005 (http://thetruereligion.org/modules/xfsection/article.php?articleid=405)

[5] Daughters of Another Path, chapisho la 4, Al-Attique Publishers, uk.81.

[6] Daughters of Another Path, uk.126.

[7] Daughters of Another Path, uk.191.

[8] A hadithi kutoka kwa Mtume, na Anas b. Malik, mtumishi wake binafsi; zilizokusanywa na kutolewa maoni na Imam al-Baihaqi katika al-Baihaqi ndani ya Shu’ab al-Iman (Branches of Faith).

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.