Kuamini maisha baada ya kifo

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Umuhimu wa imani katika maisha ya baadaye, na pia mtazamo wa nini kinamsubiri mtu kaburini, Siku ya Hukumu, na Mwisho Mkuu.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 09 Jul 2023
  • Ilichapishwa: 2
  • Imetazamwa: 3,613 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Belief_in_Life_after_Death_001.jpgKilamtu anaogopa kufa na ni sawa kuwa hivyo. Kutokuwa na uhakika wa kile kilicho mbele kunatisha. Inaweza kuwa dini zote, Uislamu, hutoa maelezo zaidi ya kile kinachokuja baada ya kifo na kilichopo mbele. Uislamu unatazama kifo kuwa kiwango asili cha kutuelekeza katika hatua inayofuata ya kuishi.

Mafundisho ya Uislamu yanashikilia kwamba uwepo wa mwanadamu unaendelea baada ya kifo cha mwili wa mwanadamu kwa njia ya ufufuo wa kiroho na wa mwili. Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya mwenendo hapa duniani na maisha ya baadaye. Maisha ya baadae yatakuwa ya zawadi na adhabu ambayo inaambatana na mwenendo wa kidunia. Siku itakuja ambapo Mungu atafufua na kukusanya wa kwanza na wa mwisho wa uumbaji wake na kuhukumu kila mtu kwa haki. Watu wataingia kwenye makao yao ya mwisho, Jehanamu au Peponi. Imani ya maisha baada ya kifo inatuhimiza kutenda mema na kukaa mbali na dhambi. Katika maisha haya wakati mwingine tunaona wacha Mungu wanateseka na wasio wacha Mungu wanafurahi. Wote watahukumiwa siku moja na haki itatendeka.

Imani ya maisha baada ya kifo ni moja ya msingi wa imani zinazohitajika kwa Muislamu ili kukamilisha imani yake. Kulikataa hili kunafanya imani zingine zote ziwe hazina maana. Fikiria juu ya mtoto ambaye hautii mkono wake kwenye moto. Hafanyi hivyo kwa sababu ana hakika utaungua. Linapokuja suala la kufanya kazi ya shule, mtoto huyo huyo anaweza kuhisi uvivu kwa sababu haelewi kabisa elimu bora itamfanyia nini katika maisha yake ya baadaye. Sasa, fikiria mtu ambaye haamini Siku ya Hukumu. Je! angefikiria kumwamini Mungu na maisha yanayoongozwa kutokana na kumwamini Mungu kuwa ina matokeo yoyote? Kwake yeye, utii wa Mungu hauna maana, wala kutotii hakuna madhara. Je! Anawezaje kuishi maisha ya kumjali Mungu? Je! Ni motisha gani itakayomlazimu kuteseka na majaribu ya maisha kwa uvumilivu na kuepuka kujifurahisha kupita kiasi katika raha za ulimwengu? Na ikiwa mtu hafuati njia ya Mungu, basi imani yake katika Mungu ina faida gani, ikiwa anayo? Kukubali au kukataa maisha baada ya kifo labda ndio jambo kubwa zaidi katika kuamua mwendo wa maisha ya mtu.

Wafu wanaendelea kuishi na kuwepo katika aina flani kaburini. Waislamu wanaamini kuwa, baada ya kufa, mtu huingia katika hatua ya kati ya maisha kati ya kifo na ufufuo. Matukio mengi hufanyika katika "ulimwengu" huu mpya, kama vile "hukumu" ya kaburi, ambapo kila mtu ataulizwa na malaika juu ya dini yao, nabii, na Mola. Kaburi ni bustani ya peponi au shimo la Motoni; malaika wa rehema hutembelea roho za waumini na malaika wa adhabu huja kwa makafiri.

Ufufuo utaanza baada ya mwisho wa ulimwengu. Mungu ataamuru malaika mkubwa kupuliza Tarumbeta. Mpulizo wa kwanza, wakaazi wote wa mbingu na dunia wataanguka kwa kupoteza fahamu, isipokuwa wale waliookolewa na Mungu. Ardhi itawekwa sawa, milima itageuzwa kuwa vumbi, mbingu zitapasuka, sayari zitatawanywa, na makaburi yatapindukaliwa.

Watu watafufuliwa katika miili yao ya asili kutoka kwenye makaburi yao, na hivyo kuingia katika awamu ya tatu na ya mwisho ya maisha. Tarumbeta litapulizwa tena ambapo watu watainuka kutoka kwenye makaburi yao, wakiwa wamefufuliwa!

Mungu atakusanya wanadamu wote, waumini na wasio waaminifu, majini, mapepo, hata wanyama wa porini. Utakuwa mkutano wa ulimwengu wote. Malaika watawafukuza wanadamu wote wakiwa uchi, wasiotahiriwa, na peku kwenye Uwanda Mkubwa wa Mkusanyiko. Watu watangojea hukumu na wanadamu watatoa jasho kwa uchungu. Wenye haki watalindwa chini ya kivuli cha Kiti cha Enzi cha Mungu.

Pindi hali hiyo itakapokuwa haiwezi kuvumilika, watu watawaomba mitume na wajumbe kuwaombea kwa Mungu kwa niaba yao ili kuwaokoa kutoka kwenye shida.

Mizani itawekwa na matendo ya wanadamu yatapimwa. Ufunuo wa taarifa za matendo yaliyofanywa katika maisha haya utafuata. Yule atakayepokea rekodi zake katika mkono wake wa kulia atakuwa na hesabu rahisi. Atarudi kwa furaha kwa familia yake. Ila, mtu ambaye atapokea taarifa yake kwa mkono wake wa kushoto angeona kufa ni bora kwani atatupiliwa motoni. Atajuta sana na atatamani kuwa asingekabidhiwa taarifa zake au kutokujua.

Ndipo Mungu atahukumu uumbaji wake. Watakumbushwa na kutaarifiwa matendo yao mema na dhambi zao. Waaminifu watatambua makosa yao na watasamehewa. Makafiri hawatakuwa na matendo mema ya kutangaza kwa sababu kafiri anapewa zawadi yake katika maisha haya. Wasomi wengine wana maoni kwamba adhabu ya kafiri inaweza kupunguzwa badala ya matendo yake mema, isipokuwa adhabu ya dhambi kubwa ya ukafiri.

Siraat ni daraja ambalo litaanzishwa juu ya moto linaloelekea hadi Peponi. Mtu yeyote ambaye yuko thabiti juu ya dini ya Mungu katika maisha haya atapata urahisi kupita.

Peponi na Motoni yatakuwa makao ya mwisho kwa waaminifu na waliolaaniwa baada ya Hukumu ya Mwisho. Ni vya kweli na vya milele. Furaha ya watu wa Peponi haitaisha kamwe na adhabu ya makafiri waliohukumiwa Jehanamu haitaisha kamwe. Tofauti na mfumo wa kufaulu katika mifumo mingine ya imani, mtazamo wa Kiislamu ni wa hali juu zaidi na unaonyesha kiwango cha juu cha haki ya kimungu. Hii inaweza kuonekana kwa njia mbili. Moja, waumini wengine wanaweza kuteseka kuzimu kwa dhambi ambazo hazitubiki, zambi kubwa. Pili, Pepo na Jahannamu ina viwango.

Pepo ni bustani ya milele ya raha za mwili na furaha ya kiroho. Mateso hayatakuwepo na tamaa za mwili zitatoshelezwa. Matakwa yote yatatimizwa. Majumba, watumishi, utajiri, mito ya divai, maziwa na asali, harufu nzuri, sauti za kutuliza, washirika wema kwa ajili ya urafiki; mtu hatachoka kamwe au kukinai!

Furaha kubwa, ingawa, itakuwa sura ya Mola wao ambayo makafiri watanyimwa kumuona.

Motoni ni mahali penye moto wa adhabu kwa wasioamini na utakaso kwa waumini wenye dhambi. Mateso na adhabu ya mwili na roho, kuchomwa na moto, maji ya kunywa yanayochemka, chakula kilichoteketezwa, minyororo, na nguzo za moto. Makafiri watahukumiwa milele, ila waumini wenye dhambi baadae watatolewa motoni na kuingizwa Peponi.

Peponi ni kwa ajili ya wale waliomwabudu Mungu peke yake, waliamini na kumfuata nabii wao, na kuishi maisha ya maadili kulingana na mafundisho ya maandiko.

Jehanamu ndio makao ya mwisho ya wale waliomkana Mungu, waliabudu viumbe vingine badala ya Mungu, walikataa mwito wa manabii, na wakaishi maisha ya dhambi, bila kutubu.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.