Wokovu katika Uislamu (sehemu ya 2 kati ya 3): Ibada na Umtii wa Mungu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: monotheazimu ni njia ya wokovu katika Uislamu.

  • Na Aisha Stacey (© 2010 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,835 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Salvation_in_Islam_(part_2_of_3)_001.jpg Katika sehemu ya 1 ya mfululizo huu wa 'Wokovu katika Uislamu', tulijifunza kuwa wokovu unapatikana kwa kumwabudu Mungu Mmoja. Tunamwabudu yeye peke yake na tunafuata amri zake. Tulijifunza pia Uislamu hautambui dhana ya dhambi ya asili, kwa hivyo Waislamu wanaamini kuwa watu wote huzaliwa bila dhambi. Katika nakala ifuatayo tutajadili dhana ya Kikristo ya kafara, ambayo, Yesu kufa kwa dhambi za wanadamu, na tutagundua kuwa dhana hii imekataliwa kabisa na Uislamu. Wokovu katika Uislamu ni kupitia tawheed, monotheazimu .

Tawheed ni neno la Kiarabu ambalo linamaanisha umoja, na tunapozungumza juu ya tawheed kuhusiana na Mungu inamaanisha kutambua na kuthibitisha umoja wa Mungu. Ni imani ya kuwa Mungu ni Mmoja, bila mshirika au jamaa. Hakuna mungu anayestahiki kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu, na huu ndio msingi wa Uislamu. Kukiri imani kama hiyo pamoja na imani ya kuwa Muhammad ni mjumbe wake ndiyo inayomfanya mtu kuwa Muislamu. Kuamini tawheed kiuhakika ndio kunahakikisha wokovu.

“Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee, Allah-us-Samad ( Mwenyezi Mungu Mkusudiwa (kwa haja zote), Hakuzaa wala hakuzaliwa;Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.” (Kurani 112)

“Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi...” (Kurani 20:14)

“Yeye ndiye Muumbaji wa mbingu na ardhi bila ya ruwaza. Itakuwaje awe na mwana naye hakuwa na mke? Naye ndiye aliye umba kila kitu. Naye ni Mwenye kujua kila kitu. La ilaha illa Huwa (hakuna aliye na haki ya kuabudiwa isipokuwa Yeye),Huyo ndiye Allah, Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu, hapana mungu ila Yeye, Muumba wa kila kitu. Basi muabuduni Yeye tu. Naye ni Mtegemewa wa kila kitu. Huyo ndiye Allah, Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu, hapana mungu ila Yeye, Muumba wa kila kitu. Basi muabuduni Yeye tu. Naye ni Mtegemewa wa kila kitu. ”” (Kurani 6:101-103)

Waislamu humwabudu Mungu peke yake bila waombezi wowote, Yeye hana washirika, jamaa, mwana, binti, au msaidizi. Ibada inaelekezwa kwa Mungu tu, kwa kuwa Yeye ndiye pekee anayestahili kuabudiwa. Hakuna kitu kikubwa kuliko Mungu.

Imani ya Kikristo ya kuwa Yesu ni mwana wa Mungu au Mungu mwenyewe ni kinyume kabisa na tawheed. Dhana ya Utatu, Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu pia imekataliwa kabisa na Uislamu. Wazo la kuwa Yesu alihukumiwa (au kuokoa roho zetu) kwa kufa ni wazo linalokinzana kabisa na imani ya Kiisilamu.

“Enyi Watu wa Kitabu! Msipite kiasi katika dini yenu, wala msimseme Mwenyezi Mungu ila kwa lilio kweli. Hakika Masihi Isa mwana wa Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na neno lake tu alilo mpelekea Maryamu, na ni roho iliyo toka kwake. Basi Muaminini Mwenyezi Mungu na Mitume wake. Wala msiseme: Utatu. Komeni! Itakuwa kheri kwenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mungu mmoja tu. Ametukuka Yeye na kuwa na mwana. Ni vyake Yeye vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu ni Mtegemewa wa kutosha.” (Kurani 4:171)

Wazo la Yesu kufa msalabani ni kiini cha imani ya Kikristo. Inawakilisha kusadiki kwamba Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi za wanadamu. Kwa maneno mengine dhambi za mtu ‘zimelipiwa’ na Yesu, na mtu yuko huru kufanya apendavyo, kwani mwisho atapata wokovu kwa kumwamini Yesu. Hii imekataliwa kabisa katika Uislamu.

Hakuna haja ya Mungu, au hata Mtume wa Mungu kujitoa muhanga kwa ajili ya dhambi za wanadamu ili anunue msamaha. Uislamu unakataa maoni haya kabisa. Msingi wa Uislamu unategemea kujua kwa hakika kwamba hakuna kitu kinachopaswa kuabudiwa isipokuwa Mungu peke yake. Msamaha unatoka kwa Mungu Pekee na wa Kweli; kwa hivyo, wakati mtu anatafuta msamaha, lazima aelekee kwa Mungu kwa unyenyekevu na majuto ya kweli na aombe msamaha, akiahidi kutorudia dhambi hiyo. Hapo ndipo tu dhambi zitasamehewa na Mungu Mwenyezi.

Uislamu unafundisha kwamba Yesu hakuja kuhukumiwa kwaajili ya dhambi za wanadamu; badala yake, kusudi lake lilikuwa kuthibitisha ujumbe wa Manabii waliopita kabla yake.

“.. hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu tu, na hakika Mwenyezi Mungu…” (Kurani 3:62)

Imani ya Kiislamu juu ya kusulubiwa na kifo cha Yesu iko wazi. Hakufa kufidia dhambi za wanadamu. Kulikuwa na njama ya kumsulubisha Yesu lakini haikufanikiwa; hakufa bali alipaa mbinguni. Katika siku za mwisho zinazoelekea Siku ya Hukumu, Yesu atarudi ulimwenguni na ataendelea kueneza imani ya Umoja wa Mungu. Quran inatuambia kwamba Siku ya hukumu Yesu atakanusha kuwaomba watu wamuabudu yeye badala ya, au pamoja na Mungu.

“Na pale Mwenyezi Mungu atakapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Ati wewe uliwaambia watu: Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu? (Na Isa) atasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hainifalii mimi kusema ambayo si haki yangu. Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwisha yajua. Wewe unayajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi yako. Hakika Wewe ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyo fichikana.Sikuwaambia lolote ila uliyo niamrisha, nayo ni: Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Na mimi nilikuwa shahidi juu yao nilipo kuwa nao. Na ulipo nifisha ukawa Wewe ndiye Muangalizi juu yao. Na Wewe ni shahidi juu ya kila kitu. ” (Kurani 5:116-117)

Mungu anatuambia katika Kurani kwamba kuna dhambi moja tu isiyosameheka, na hiyo ni ikiwa mtu atakufa akiwa amemshirikisha Mungu na hakutubu kabla ya kifo chake.

“Hakika Mwenyezi Mungu hasamehe kushirikishwa, na husamehe yaliyo duni ya hilo kwa amtakaye. Na anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu basi hakika amezua dhambi kubwa.” (Kurani 4:48)

Katika mila yake Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alitutaarifu kuwa Mungu alisema, “Mimi ni wa Kujitosheleza, sihitaji kuwa na mshirika. Kwa hivyo yeye anayefanya kitendo kwa ajili ya mwingine, na vile vile mimi, nitakataa kitendo hicho Kwangu kwa aliyenishirikisha na Mimi ”.[1]

Ila, hata dhambi kubwa ya kumshirikisha Mungu inaweza kusamehewa ikiwa mtu atamgeukia Mungu kwa dhati na kwa toba kamili.

“Na hakika Mimi ni Mwingi wa Kusamehe kwa anaye tubia, na akaamini, na akatenda mema, tena akaongoka. (mpaka kufa kwake). ” (Kurani 20:82)

“Waambie wale walio kufuru: Wakikoma watasamehewa yaliyo kwisha pita. Na wakiyarudia basi imekwisha pita mifano ya wa zamani.” (Kurani 8:38)

Kila mwanadamu anaweza kupata wokovu kwa kumuabudu Mungu Mmoja. Kukaa katika uhusiano na Mungu na kutubu makosa na dhambi ndio njia ya wokovu. Katika nakala inayofuata, tutazungumza juu ya kanuni ya toba.



Rejeleo la maelezo:

[1] Saheeh Muslim

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.