Wokovu katika Uislamu (sehemu ya 1 kati ya 3): Wokovu ni nini?

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Fikia wokovu kupitia ibada ya kweli

  • Na Aisha Stacey (© 2010 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,069 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: 1.9 kati ya 5
  • Imekadiriwa na: 53
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Salvation_in_Islam_(part_1_of_3)._001.jpgUislamu unatufundisha kuwa wokovu unapatikana kupitia kumwabudu Mungu peke yake. Mtu lazima amwamini Mungu na afuate amri Zake. Huu ni ujumbe ule ule uliofundishwa na Manabii wote wakiwemo Musa na Yesu. Kuna Mmoja tu anayestahili kuabudiwa. Mungu mmoja, peke yake bila washirika, wana, au mabinti. Wokovu na kwa hivyo furaha ya milele inaweza kupatikana kwa ibada ya kweli.

Kwa kuongezea Uislamu unatufundisha kuwa wanadamu huzaliwa bila dhambi na kiasili wana mwelekeo wa kumwabudu Mungu peke yake (bila waombezi wowote). Ili kudumisha hali hii ya kutokuwa na dhambi mwanadamu lazima afuate tu amri za Mungu na ajitahidi kuishi katika maisha ya haki. Ikiwa mtu ataangukia kwenye dhambi, kinachotakiwa ni toba ya kweli ikifuatiwa na kutafuta msamaha wa Mungu. Mtu anapotenda dhambi yeye hujisukuma mbali na huruma ya Mungu, hata hivyo toba ya kweli inamrudisha mtu kwa Mungu.

Wokovu ni neno lenye nguvu ambalo kamusi hufafanua kama kitendo cha uhifadhi au ukombozi kutoka kwa uharibifu, shida, au uovu. Kitheolojia ni uokoaji wa kiroho kutokana na dhambi na matokeo yake. Mahususi zaidi, kwenyeUkristo inahusishwa na ukombozi na upatanisho wa Yesu. Wokovu katika Uislamu ni dhana tofauti sana. Ingawa inatoa ukombozi kutokana na moto wa kuzimu, inakataa pia kanuni zingine za kimsingi za Ukristo na inasema wazi kwamba wokovu unapatikana tu kwa kujitiisha kwa Mungu aliye mwingi wa rehema.

“Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa Mbingu na Ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika! Basi tukinge na adhabu ya Moto. ” (Kurani 3:191)

Kulingana na mafundisho ya Kikristo, wanadamu wanachukuliwa kuwa wapotovu na wenye dhambi. Mafundisho ya dhambi ya asili inasema kwamba wanadamu wamezaliwa tayari wamechafuliwa na dhambi ya Adamu na kwa hivyo wamejitenga na Mungu, na wanahitaji mkombozi. Uislamu kwa upande mwingine hukataa kwa haki dhana ya Kikristo ya dhambi ya asili na wazo ya kuwa wanadamu wamezaliwa wakiwa wenye dhambi.

Kwa Wazo la kuwa watoto wachanga wasio na hatia au watoto wana dhambi wazo hili ni la kipumbavu kwa muumini ambaye anajua Uislamu linahusisha msamaha wa asili sio dhambi ya asili. Binadamu, kulingana na Uislamu huzaliwa katika hali ya usafi, bila dhambi na kwa kawaida wamewekewa kumwabudu na kumsifu Mungu. Ila, wanadamu pia hupewa hiari na kwa hivyo wana uwezo wa kufanya makosa na kutenda dhambi; wana uwezo hata wa kutenda uovu mkubwa.

Muda wowote mtu anapotenda dhambi, yeye peke yake ndiye huwajibika kwa dhambi hiyo. Kila mtu anajibika kwa matendo yake mwenyewe. Kwa hivyo, hakuna mwanadamu aliyewahi kuishi anayehusika na makosa yaliyofanywa na Adamu na Hawa. Mungu anasema katika Quran:

“Na mbebaji habebi mzigo wa mwingine. ” (Kurani 35:18)

Adamu na Hawa walifanya makosa, walitubu kwa dhati, na Mungu kwa hekima yake isiyo na kipimo aliwasamehe. Wanadamu hawajahukumiwa kuadhibiwa, kizazi baada ya kizazi. Dhambi za baba hazitembelewi juu ya wana.

“Basi wakaula wote wawili, na uchi wao ukawadhihirikia na wakaanza kujibandika majani ya Bustani. Na Adam akamuasi Mola wake Mlezi, na akapotea njia. Kisha Mola wake Mlezi akamteuwa, naye akamkubalia toba yake, naye akamwongoa. ” (Kurani 20:121-122)

Zaidi ya yote Uislamu unatufundisha kwamba Mungu ni msamehevu zaidi, na ataendelea kusamehe, kila wakati. Sehemu ya kuwa mwanadamu ni wa kufanya makosa. Wakati mwingine makosa hufanywa bila kufikiri au nia mbaya, lakini wakati mwingine tunatenda dhambi na kujua kwa makusudi na kuwatendea wengine vibaya. Kwa hivyo kama wanadamu, tunahitaji msamaha kila wakati.

Maisha ya ulimwengu huu yamejaa majaribu na dhiki, hata hivyo Mungu hakuwaacha wanadamu kwenye mitihani hii. Mungu aliwapatia wanadamu akili na uwezo wa kufanya uchaguzi na maamuzi. Mungu pia alitupa maneno ya mwongozo. Kama muumba wetu, Yeye anajua vizuri asili yetu na anatamani kutuongoza kwenye njia iliyonyooka ambayo inatuongoza kwenye raha ya milele.

Quran ni ufunuo wa mwisho wa Mungu na inatumika na wanadamu wote; watu wote, sehemu zote, nyakati zote. Katika Quran Mungu hutuhitaji kila mara tugeuke kwake kwa toba na kumwomba msamaha. Hii ndio njia ya wokovu. Huu ndio ukombozi wetu kutokana na uharibifu.

“Na anaye tenda uovu au akajidhulumu nafsi yake, kisha akaomba maghfira kwa Mwenyezi Mungu, atamkuta Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghfira, Mwenye kurehemu.” (Kurani 4:110)

“Na enyi watu wangu! Muombeni msamaha Mola wenu Mlezi, kisha mtubie kwake. Atakuleteeni mbingu zenye kunyesha mvua ya kumiminika, na atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu. Wala msigeuke mkawa wakosefu. ” (Kurani 11:52)

“Sema: Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu. ’” (Kurani 39:53)

Quran sio tu kitabu cha mwongozo, ni kitabu cha matumaini. Ndani yake upendo wa Mungu, rehema, na msamaha ni dhahiri na kwa hivyo wanadamu wanakumbushwa kutokata tamaa. Haijalishi ni dhambi gani ambayo mtu anaweza kuwa ameitenda ikiwa atarudi kwa Mungu, na kutafuta msamaha wokovu wake umehakikishwa.

Mtume Muhammad alielezea dhambi kama madoa meusi yanayofunika moyo. Alisema, “ Hakika ikiwa muumini atatenda dhambi, doa jeusi litafunika moyo wake. Ikiwa atatubu, na kuacha dhambi, na kutafuta msamaha kwa ajili yake, moyo wake unakuwa safi tena. Ikiwa ataendelea (badala ya kutubu), doa huongezeka hadi kufunika moyo wake…”[1]

Wokovu katika Uislamu hauhitajiki kwa sababu ya doa la dhambi ya asili. Wokovu unahitajika kwa sababu wanadamu hawajakamilika na wanahitaji msamaha wa Mungu na upendo. Ili kuelewa dhana ya wokovu kwa usahihi lazima tuelewe mada zingine zilizowekwa ndani ya wokovu. Hizi ni, kuelewa umuhimu wa tawheed, au Umoja wa Mungu, na kujua jinsi ya kutubu kwa kweli. Tutazungumzia mada hizi katika makala mbili zifuatazo.



Rejeleo la maelezo:

[1] Ibn Majah.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.