Kwa nini Mungu aliwaumba wanadamu? (sehemu ya 4 kati ya 4): Kupingana na Kusudi la Uumbaji

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kusudi la uumbaji wa wanadamu ni ibada. Sehemu ya 4: Kupinga kusudi la uumbaji wa binadamu basi ni dhambi kubwa zaidi ambao mwanadamu anaweza kufanya.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,733 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Dhambi Kubwa Zaidi

Kupingana na kusudi la uumbaji wa mtu basi ni uovu mkubwa zaidi ambao mwanadamu anaweza kufanya. Abdullaah aliripoti kwamba alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (rehma iwe juu yake) kwamba ni ipi dhambi kubwa zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu na akajibu,

“Kuwashirikisha wengine na Mwenyezi Mungu ijapo kuwa amekuumba.” (Saheeh Al-Bukhari)

Kuwaabudu wengine badala ya Mwenyezi Mungu, inayoitwa shirk kwa Kiarabu, ni dhambi isiyo ya kusamehewa. Na mwanaadamu akifa bila kutubu dhambi zake, basi huenda Mwenyezi Mungu akamsamehe dhambi zake zote isipokuwa shirk. Katika suala hili, Mungu alisema:

“Hakika Mwenyezi Mungu hasamehi kushirikishwa na kitu lakini yeye husameheyasiyokuwa hayo kwa amtakaye.” (Kurani 4:116)

Kuabudu wengine badala ya Mungu kimsingi kunahusisha kutoa sifa za Muumba kwa uumbaji Wake. Kila madhehebu au dini hufanya hivyo kwa namna yao wenyewe. Kikundi kidogo cha watu wenye mijadala sana kimekanusha kuwepo kwa Mungu kuanzia zama za kale. Katika kujitetea kwao, walidai kwamba ulimwengu huu hauna mwanzo. Madai yao hayana mantiki kwa sababu sehemu zote zinazoonekana za ulimwengu zina mwanzo kwa wakati, kwa hivyo lazima sehemu za ulimwengu pia ziwe na mwanzo. Pia ni mantiki tu kudhani kwamba chochote kilicholeta ulimwengu hakingekuwa ndani ya ulimwengu huo wala kiwe na mwanzo kama ulimwengu. Madai ya wakanaji Mungu ya kwamba ulimwengu hauna mwanzo ina maana kwamba vipengelea vilivyounda ulimwengu ni vya milele. Hii ni kauli ya shirk, ambapo sifa ya Mungu ya kutokuwa na mwanzo imepewa maumbile yake. Idadi ya wakanaji Mungu katika kihistoria daima ilikuwa ndogo kabisa kwa sababu, licha ya madai yao, wao kiasili hujua kwamba Mungu yupo. Hiyo ni, licha ya miongo kadhaa ya ufundishaji wa kikomunisti, wengi wa Warusi na Wachina waliendelea kumwamini Mungu. Muumba Mwenyezi alizungumzia jambo hili, akisema:

“Na walizikanusha kwa dhulma na kujivuna, na hali ya kuwa nafsi zao zina yakini nazo.” (Quran 27:14)

Kwa wasiokiri kuwepo kwa Mungu na wapenda mapambo ya dunia, maisha hayana kusudi zaidi ya kutimiza tamaa zao. Kwa hivyo, matamanio yao yanakuwa mungu wanaye mtii badala ya Mungu Mmoja wa Haki. Katika Qurani, Mungu alisema:

“Je! Umemwona aliyefanya matamanio kuwa ndiyo mungu wake?” (Quran 25:43, 45:23)

Wakristo walimpa Nabii Isa (Yesu Kristo) sifa za Muumba kwa kumfanya kwanza awe na ushirika wa milele na Mungu, halafu kwa kumfanya awe na dhati ya Mungu ambaye walimwita “Mungu Mwana.” Wahindu, kwa upande mwingine, wanaamini kwamba Mungu amekuwa mwanadamu kwa miaka mingi, kwa njia ya mwilisho inayoitwa avatari, na kisha kugawanya sifa za Mungu kati ya miungu mitatu, Brahma Muumba, Vishnu mwokozi na Shiva Mwangamizi.

Upendo wa Mungu

Shirk pia hutokea wakati binadamu wanapenda, kuamini au kuogopa viumbe zaidi ya Mungu. Katika ufunuo wa mwisho, Mungu alisema:

“Na miongoni mwa watu wapo wanao chukua waungu wasiokuwa Mwenyezi Mungu. Wanawapenda kama kumpenda Mwenyezi Mungu. Lakini walioamini wanampenda Mwenyezi Mungu zaidi sana.” (Quran 2:165)

Wakati hisia hizi na nyingine zinazofanana zinaelekezwa zaidi kwenye viumbe, zinasababisha binadamu kutomtii Mungu kwa jitihada za kumpendeza binadamu. Hata hivyo, Mungu pekee ndiye anayestahili uazimiaji kamili wa kihisia ya kibinadamu, kwani ni Yeye pekee ambaye anapaswa kupendwa na kuogopwa juu ya viumbe vyote. Anas ibn Maalik alisimulia kwamba Nabii (rehma iwe juu yake) alisema:

“Na aliye na sifa hizi tatu basi ameonja utamu wa Imani: anaye mpenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake kuliko vyote, na anaye penda mwanadamu mwingine kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake, na anaye chukia kurudi kufuru baada ya Mwenyezi Mungu kumwokoa anavyochukia kutupwa motoni.” (As-Suyooti)

Sababu zote ambazo binadamu hupenda wanadamu wengine au kupenda viumbe vingine vilivyoumbwa ndizo sababu za kumpenda Mungu zaidi ya uumbaji wake. Binadamu hupenda maisha na mafanikio, na huchukia kifo na kutofaulu. Kwa kuwa Mungu ndiye chanzo cha maisha na mafanikio, Anastahili upendo kamili na ibada kutoka kwa wanadamu. Binadamu pia huwapenda wale wanaowafaidisha na kuwasaidia wanapokuwa na haja. Kwa kuwa faida zote (7:188) na msaada (3:126) hutoka kwa Mungu, anapaswa kupendwa kuliko wengine.

“Ikiwa mtajaribu kuzihesabu baraka za Mwenyezi Mungu, humwezi kuzidhibiti.” (Quran 16:18)

Hata hivyo, upendo mkuu ambao wanadamu wanapaswa kuhisi kwa Mungu haupaswi kupunguzwa hadi kwa kiwango cha mapenzi yao kwa viumbe. Kama vile upendo wa wanadamu kwa wanyama haupaswi kuwa sawa na mapenzi yao kwa binadamu wengine, upendo wa Mungu unapaswa kuvuka mapenzi ya wanadamu kwa wenzao. Upendo wa kibinadamu wa Mungu unapaswa kuwa, kimsingi, upendo unaoonekana katika utii kamili kwa sheria za Mungu:

“Na ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi (Mtume wa Mungu) na Mwenyezi Mungu atawapenda.” (Quran 3:31)

Hii sio kudhania tu, kwa sababu upendo wa binadamu kwa wanadamu wengine pia unamaanisha utiifu. Hiyo ni ikiwa mpendwa anaomba kitu kifanyike, wanadamu watajitahidi kufanya hivyo kulingana na kiwango cha upendo wao kwa mtu huyo.

Upendo wa Mungu pia unapaswa kuonyeshwa katika upendo wa wale ambao Mungu anawapenda. Haiwezekani kwamba mtu anayempenda Mungu kuwachukia wale ambao Mungu anawapenda na kuwapenda wale anaowachukia. Nabii (rehma ziwe juu yake) alinukuliwa na Aboo Umaamah akisema:

“Anayependa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na akachukia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na hupeana kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na hunyima kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, [na anaoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu] ameikamilisha imani yake.” (As-Suyooti)

Kwa hivyo, wale ambao imani yao ni sahihi watawapenda wote wampendao Mungu. Katika Sura ya Maryamu, Mungu anaonyesha kwamba anaweka upendo ndani ya mioyo ya Waumini kwa walewaaminio.

“Hakika Mwenyezi Mungu atawajalia mapenzi ( katika mioyo ya waumini kwa) waloamini na wakatenda mema.” (Kurani 19:96)

Aboo Hurayrah pia alisimulia kwamba Mtume wa Mungu (rehma ziwe juu yake) alisema yafuatayo katika suala hili:

“Kama Mungu anampenda mja Anamwambia malaika Jibrili kwamba anampenda fulani na fulani na anamwambia ampende, hivyo Jibril anampenda. Kisha Jibril akawaita wenyeji wa mbinguni: Mwenyezi Mungu anampenda fulani, basi mpendeni. Basi wenyeji wa mbinguni wanampenda. Kisha anapewa upendo wa watu wa dunia. ” (Saheeh Muslim)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.