Kwa nini Mungu aliwaumba wanadamu? (sehemu ya 2 kati ya 4): Haja ya kumkumbuka Mungu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Lengo la uumbaji wa wanadamu ni ibada. Sehemu ya 2: Jinsi dini ya Uislamu imeagiza njia za kumkumbuka Mungu.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,150 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kumkumbuka Mungu

Matendo yote ya ibada yaliyomo katika sheria za kimungu yameundwa ili kuwasaidia binadamu kumkumbuka Mungu. Ni kawaida kwa binadamu wakati mwingine kusahau hata mambo muhimu kabisa. Mara nyingi wanadamu hushughulika sana na shughuli za kutimiza mahitaji yao ya kimwili na kusahau kabisa mahitaji yao ya kiroho. Sala za kawaida zimewekwa ili kupanga siku ya mwumini katika kumkumbuka Mungu. Inashirikisha mahitaji ya kiroho pamoja na mahitaji ya kimwili kila siku. Mahitaji ya kila siku ya kula, kufanya kazi na kulala yanahusishwa na haja ya kila siku ya kusasisha uhusiano wa mwanadamu na Mungu. Kuhusu sala ya kawaida, Mungu anasema katika ufunuo wa mwisho,

“Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu, hakuna mungu ila Mimi tu. Basi mniabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili kunikumbuka Mimi.” (Kurani 20:14)

Na kuhusu swaumu, Mwenyezi Mungu alisema katika Kurani,

“Enyi mlio amini! Mmeandikiwa kufunga kama walivyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kumjua Mwenyezi Mungu.” (Kurani 2:183)

Waumini wanahimizwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu mara nyingi iwezekanavyo. Ingawa wastani katika nyanja zote za maisha, ikiwa ni za kimwili au kiroho, kwa ujumla huhimizwa katika sheria tukufu, ila ukumbusho wa Mungu ni tofauti. Haiwezekani mtu avuke mpaka katika kumkumbuka Mungu zaidi, Kwa hivyo, katika ufunuo wa mwisho, Mungu anawahimiza Waumini kumkumbuka mara nyingi iwezekanavyo:

“Enyi mlio amini! Na mkumbukeni Mwenyezi Mungu mara nyingi.” (Kurani 33:41)

Ukumbusho wa Mungu unasisitizwa kwa sababu dhambi kwa ujumla hufanywa wakati Mungu anasahauliwa. Nguvu za uovu hufanya kazi kwa uhuru zaidi wakati ufahamu na ukumbusho wa Mungu unapotea. Kwa hivyo, majeshi ya kishetani yanajaribu kushughulisha akili za watu na mawazo yasiyo na maana na tamaa za kuwafanya wamsahau Mungu. Pindi Mungu anaposahauliwa tu, watu hufanya madhambi kwa hiari yao. Ufunuo wa mwisho unashughulikia jambo hili kwa yafuatayo:

“Na Shet'ani amewatawala na akawasahaulisha kumkumbuka mwenyezi mungu. Hao ndio kundi la shetani. Hakika kundi la shetani ndilo lenye kukhasirika.” (Quran 58:19)

Mungu, kupitia sheria zake, amekataza ulevi na kamari hasa kwa sababu vinamfanya mwanadamu amsahau Mungu. Akili ya binadamu na mwili wake kwa urahisi huwa na uraibu wa madawa za kulevya na michezo ya kubahatisha. Mara baada ya kuwa waraibu, hamu ya wanadamu ya kuendelea kulewa inawaongoza katika kufanya aina zote za uharibifu na vurugu kati yao wenyewe. Mungu anasema katika Qur'ani:

“Hakika Shet'ani anakusudia kuwachochea uadui na chuki miongoni mwenu kwa ulevi na kamari, na kuwazuia kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kuswali. Basi je! mmeacha?” (Quran 5:91)

Kwa hivyo, wanadamu wanahitaji kumkumbuka Mungu kwa ajili ya wokovu wao wenyewe na ukuaji wao. Binadamu wote wana nyakati za udhaifu ambapo wanafanya dhambi. Na ikiwa hawana njia ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu, basi wao huzama katika ufisadi kwa kila dhambi. Hata hivyo, wale wanaofuata sheria za kimungu watakumbushwa Mungu daima, na hilo huwapa nafasi ya kutubu na kujisahihisha wenyewe. Ufunuo wa mwisho unaelezea kwa usahihi taratibu hizi:

“Wale ambao wamefanya kitu cha aibu au wamejidhulumu nafsi zao, humkumbuka Mwenyezi Mungu na wakaomba msamaha kwa dhambi zao mara moja...” (Quran 3:135)

Dini ya Uislamu

Mfumo kamili wa ibada unaopatikana kwa wanadamu leo ni mfumo unaopatikana katika dini ya Uislamu. Jina lenyewe la “Uislamu” lina maana ya 'kujisalimisha kwa Mungu.' Ingawa kwa kawaida hujulikana kama 'dini ya tatu kati ya madini ya kiabrahamu,' si dini mpya kamwe. Ni dini iliyoletwa na manabii wote wa Mungu kwa wanadamu. Uislamu ulikuwa dini ya Adamu, Abrahamu, Musa na Yesu. Mungu anazungumzia suala hili katika Qurani kuhusu Nabii Ibrahimu, akisema:

“Ibrahimu hakuwa Myahudi wala Mkristo, bali alikuwa Muislamu mnyofu ambaye hakuwaabudu wengine badala ya Mwenyezi Mungu.” (Quran 3:67)

Kwa kuwa kuna Mungu Mmoja tu, na wanadamu ni wa aina moja, dini ambayo Mungu ameiweka kwa wanadamu ni moja. Hakuagiza dini moja kwa Wayahudi, nyingine kwa Wahindi na nyingine kwa Wazungu, nk. Mahitaji ya kiroho na kijamii ni sare, na asili ya binadamu haijabadilika tangu mwanamume na mwanamke wa kwanza kuumbwa. Kwa hivyo, hakuna dini nyingine inayokubalika kwa Mwenyezi Mungu isipokuwa Uislamu, kama Anavyoeleza wazi katika ufunuo wa mwisho:

“Hakika Dini ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu...” (Quran 3:19)

“Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasiri.” (Kurani 3:85)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa