Kwa nini Mungu aliumba wanadamu? (sehemu ya 1 kati ya 4): Ibada ya Mungu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kusudi la uumbaji wa wanadamu ni ibada. Sehemu ya 1: Haja ya binadamu ya ibada.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 1
  • Imetazamwa: 5,385
  • Ukadiriaji: 1.7 kati ya 5
  • Imekadiriwa na: 49
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Why_Did_God_Create_Mankind_(part_1_of_4)_001.jpgKutokana na mtazamo wa wanadamu, swali la “Kwa nini Mungu aliumba mwanadamu?” linamaanisha “Kwa sababu gani mwanadamu aliumbwa?” Katika ufunuo wa mwisho (Qur'ani) swali hili linajibiwa bila ya utata wowote. Kwanza wanadamu wanaambiwa na Mungu kwamba kila mwanadamu anazaliwa na ufahamu wa kiasili wa Mungu. Katika qurani Mungu anasema:

"Na pale Mola wako Mlezi alipo waleta katika wanaadamu kutoka migongoni mwao kizazi chao, na akawashuhudisha juu ya nafsi zao, akawaambia: Je, Mimi si Mola Mlezi wenu? Wakasema: Kwani! Tumeshuhudia. Msije mkasema Siku ya Kiyama sisi tulikuwa tumeghafilika na hayo. Au mkasema: Hakika baba zetu ndio walio shirikisha kabla yetu, na sisi ni dhuriya zao tu baada yao. Basi utatuangamiza kwa sababu ya waliyo yafanya wapotovu?" (Qurani 7:172)

Nabii, rehma na baraka za Mungu ziwe juu yake, alieleza kwamba Mungu alipomuumba Adamu, alichukua kutoka kwake agano katika mahali paitwapo Na'maan siku ya 9 ya mwezi wa 12. Kisha akawaondoa kutoka kwa Adamu wazao wake wote ambao wangezaliwa mpaka mwisho wa dunia, kizazi baada ya kizazi, na kuwatandaza mbele yake ili kuchukua agano kutoka kwao pia. Akawaambia uso kwa uso, akiwashuhudisha kwamba yeye ndiye Mola wao Mlezi. Kwa hivyo, kila mwanadamu anawajibika kuwa na imani katika Mungu, ambayo imechapishwa kwa kila nafsi. Ni kutokana na imani hii ya kuzaliwa nao ndio Mungu alifafanua kusudi la uumbaji wa wanadamu katika Qur'ani:

"Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi." (Qurani 51:56)

Hivyo basi, lengo muhimu ambalo wanadamu waliumbiwa ni ibada ya Mungu. Hata hivyo, Mwenyezi hana haja na ibada ya wanadamu. Hakumuumba binadamu kutokana na haja kwa upande Wake. Kama hakungekuwa na mwanadamu hata mmoja wa kumwabudu Mungu, haingepunguza utukufu Wake kwa njia yoyote, na kama wanadamu wote wangemwabudu, haingeongeza kwa utukufu Wake kwa njia yoyote. Na Mwenyezi Mungu ni mkamilifu. Yeye peke yake yupo bila mahitaji yoyote. Viumbe vyote vilivyoumbwa vina mahitaji. Kwa hivyo, ni mwanadamu anayehitaji kumwabudu Mungu.

Maana ya Ibada

Ili kuelewa ni kwa nini binadamu wanahitaji kumwabudu Mungu, ni lazima mtu aelewe kwanza maana ya neno 'ibada.' Neno la Kiingereza la 'ibada' limetoka kwa neno la Kingereza cha Kale (weorthscipe) linalomaanisha 'heshima.' Kwa hivyo, ibada katika lugha ya Kiingereza hufafanuliwa kama 'utendaji wa vitendo vya ibada kama heshima kwa Mungu.' Kwa maana hii, mwanadamu anaagizwa kuonyesha shukrani kwa Mungu kwa kumtukuza. Katika Qurani, Mungu anasema:

"Mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi..." (Kurani 15:98)

Katika kumtukuza Mungu, mwanadamu anachagua kuwa sawa na viumbe vyote ambavyo kwa kawaida humtukuza Muumba. Mungu anazungumzia jambo hili katika sura nyingi za Qurani. Kwa mfano, katika Qurani, Mungu anasema:

"Zinamtakasa zote mbingu saba na ardhi na vyote viliomo ndani yake. Na hapana kitu ila kinamtakasa kwa sifa zake." (Qurani 17:44)

Hata hivyo, kwa Kiarabu, ambayo ni lugha ya ufunuo wa mwisho, ibada inaitwa 'ibaadah, ambalo linahusiana kwa karibu na nomino 'abd, inayomaanisha 'mtumwa. ' Mtumwa ni yule anayetarajiwa kufanya chochote anachotaka bwana Wake. Kwa hivyo, ibada, kulingana na ufunuo wa mwisho, inamaanisha “ utiifu kwa Mungu.” Hii ilikuwa kiini cha ujumbe wa manabii wote waliotumwa na Mungu kwa wanadamu. Kwa mfano, ufahamu huu wa ibada ulionyeshwa kinagaubaga na Nabii Yesu (Masihi au Yesu Kristo),

“Si kila mtu anayesema, ‘Bwana, Bwana,’ ambaye ataingia katika Ufalme wa mbinguni ila ni wale wanaofanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”

Ikumbukwe kwamba 'mapenzi' katika nukuu hii inamaanisha 'kile Mungu anataka mwanadamu kufanya' na si 'kile ambacho Mungu anaruhusu wanadamu kufanya, 'kwa sababu hakuna kinachotokea katika uumbaji bila ya majaliwa (idhini) ya Mungu. “Mapenzi ya Mungu' yamepatikana katika sheria zilizofunuliwa na Mungu ambazo manabii waliwafundisha wafuasi wao. Kwa hivyo, utii wa sheria ya Mungu ni msingi wa ibada. Kwa maana hiyo utukufu unakuwa pia ibada wakati binadamu wanapochagua kutii maagizo ya Mungu kuhusu utukufu Wake.

Haja ya kuabudu

Kwa nini binadamu wanahitaji kumwabudu na kumtukuza Mungu kwa kutii sheria zilizofunuliwa na Mungu? Kwa sababu utii wa sheria ya Mungu ni ufunguo wa kufanikiwa katika maisha haya na ya pili. Wanadamu wa kwanza, Adamu na Hawa, waliumbwa katika paradiso na baadaye kufukuzwa kutoka huko kwa kuasi sheria tukufu. Njia pekee ya binadamu kurudi peponi ni kwa utiifu wa sheria. Nabii Yesu, aliripotiwa katika Injili kulingana ya Matayo kuwa amesema utii wa sheria za Mungu ndio ufunguo wa paradiso.

“Mwalimu mwema, nifanye jambo jema gani ili nipate uzima wa milele?” Basi akamwambia, “Kwa nini unaniita mwema? Hapana aliye mwema ila ni mmoja tu, Mwenyezi Mungu. Lakini mkitaka kuingia katika uzima, shika amri.”

Pia Nabii Yesu aliripotiwa kuwa amesisitiza juu ya utii mkali wa amri, akisema:

“Basi, yeyote atakayevunja hata amri moja ndogo kuliko zote, na kuwafundisha wengine wafanye hivyo, huyo atakuwa mdogo kabisa katika Ufalme wa mbiguni. Lakini yule atakayezishika na kuwafundisha wengine, huyo atakuwa mkubwa katika Ufalme wa mbinguni.”

Sheria za Kimungu zinawakilisha mwongozo kwa wanadamu katika nyanja zote za maisha. Zinawafafanulia sahihi na batili na kuwapa wanadamu mfumo kamili unaoongoza mambo yao yote. Muumba peke yake anajua zaidi yaliyo na manufaa kwa uumbaji Wake na yasiyokuwa na manufaa. Sheria za kimungu zinaamuru na kuzuia vitendo na vitu mbalimbali ili kulinda roho ya binadamu, mwili wa binadamu na jamii ya binadamu kutokana na madhara. Ili binadamu waweze kutimiza uwezo wao kwa kuishi maisha ya uchamungu, wanahitaji kumwabudu Mungu kwa njia ya utiifu wa amri Zake.

Mbaya Nzuri zaidi

Kwa nini Mungu aliwaumba wanadamu? (sehemu ya 2 kati ya 4): Haja ya kumkumbuka Mungu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Lengo la uumbaji wa wanadamu ni ibada. Sehemu ya 2: Jinsi dini ya Uislamu imeagiza njia za kumkumbuka Mungu.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,000
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kumkumbuka Mungu

Matendo yote ya ibada yaliyomo katika sheria za kimungu yameundwa ili kuwasaidia binadamu kumkumbuka Mungu. Ni kawaida kwa binadamu wakati mwingine kusahau hata mambo muhimu kabisa. Mara nyingi wanadamu hushughulika sana na shughuli za kutimiza mahitaji yao ya kimwili na kusahau kabisa mahitaji yao ya kiroho. Sala za kawaida zimewekwa ili kupanga siku ya mwumini katika kumkumbuka Mungu. Inashirikisha mahitaji ya kiroho pamoja na mahitaji ya kimwili kila siku. Mahitaji ya kila siku ya kula, kufanya kazi na kulala yanahusishwa na haja ya kila siku ya kusasisha uhusiano wa mwanadamu na Mungu. Kuhusu sala ya kawaida, Mungu anasema katika ufunuo wa mwisho,

“Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu, hakuna mungu ila Mimi tu. Basi mniabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili kunikumbuka Mimi.” (Kurani 20:14)

Na kuhusu swaumu, Mwenyezi Mungu alisema katika Kurani,

“Enyi mlio amini! Mmeandikiwa kufunga kama walivyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kumjua Mwenyezi Mungu.” (Kurani 2:183)

Waumini wanahimizwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu mara nyingi iwezekanavyo. Ingawa wastani katika nyanja zote za maisha, ikiwa ni za kimwili au kiroho, kwa ujumla huhimizwa katika sheria tukufu, ila ukumbusho wa Mungu ni tofauti. Haiwezekani mtu avuke mpaka katika kumkumbuka Mungu zaidi, Kwa hivyo, katika ufunuo wa mwisho, Mungu anawahimiza Waumini kumkumbuka mara nyingi iwezekanavyo:

“Enyi mlio amini! Na mkumbukeni Mwenyezi Mungu mara nyingi.” (Kurani 33:41)

Ukumbusho wa Mungu unasisitizwa kwa sababu dhambi kwa ujumla hufanywa wakati Mungu anasahauliwa. Nguvu za uovu hufanya kazi kwa uhuru zaidi wakati ufahamu na ukumbusho wa Mungu unapotea. Kwa hivyo, majeshi ya kishetani yanajaribu kushughulisha akili za watu na mawazo yasiyo na maana na tamaa za kuwafanya wamsahau Mungu. Pindi Mungu anaposahauliwa tu, watu hufanya madhambi kwa hiari yao. Ufunuo wa mwisho unashughulikia jambo hili kwa yafuatayo:

“Na Shet'ani amewatawala na akawasahaulisha kumkumbuka mwenyezi mungu. Hao ndio kundi la shetani. Hakika kundi la shetani ndilo lenye kukhasirika.” (Quran 58:19)

Mungu, kupitia sheria zake, amekataza ulevi na kamari hasa kwa sababu vinamfanya mwanadamu amsahau Mungu. Akili ya binadamu na mwili wake kwa urahisi huwa na uraibu wa madawa za kulevya na michezo ya kubahatisha. Mara baada ya kuwa waraibu, hamu ya wanadamu ya kuendelea kulewa inawaongoza katika kufanya aina zote za uharibifu na vurugu kati yao wenyewe. Mungu anasema katika Qur'ani:

“Hakika Shet'ani anakusudia kuwachochea uadui na chuki miongoni mwenu kwa ulevi na kamari, na kuwazuia kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kuswali. Basi je! mmeacha?” (Quran 5:91)

Kwa hivyo, wanadamu wanahitaji kumkumbuka Mungu kwa ajili ya wokovu wao wenyewe na ukuaji wao. Binadamu wote wana nyakati za udhaifu ambapo wanafanya dhambi. Na ikiwa hawana njia ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu, basi wao huzama katika ufisadi kwa kila dhambi. Hata hivyo, wale wanaofuata sheria za kimungu watakumbushwa Mungu daima, na hilo huwapa nafasi ya kutubu na kujisahihisha wenyewe. Ufunuo wa mwisho unaelezea kwa usahihi taratibu hizi:

“Wale ambao wamefanya kitu cha aibu au wamejidhulumu nafsi zao, humkumbuka Mwenyezi Mungu na wakaomba msamaha kwa dhambi zao mara moja...” (Quran 3:135)

Dini ya Uislamu

Mfumo kamili wa ibada unaopatikana kwa wanadamu leo ni mfumo unaopatikana katika dini ya Uislamu. Jina lenyewe la “Uislamu” lina maana ya 'kujisalimisha kwa Mungu.' Ingawa kwa kawaida hujulikana kama 'dini ya tatu kati ya madini ya kiabrahamu,' si dini mpya kamwe. Ni dini iliyoletwa na manabii wote wa Mungu kwa wanadamu. Uislamu ulikuwa dini ya Adamu, Abrahamu, Musa na Yesu. Mungu anazungumzia suala hili katika Qurani kuhusu Nabii Ibrahimu, akisema:

“Ibrahimu hakuwa Myahudi wala Mkristo, bali alikuwa Muislamu mnyofu ambaye hakuwaabudu wengine badala ya Mwenyezi Mungu.” (Quran 3:67)

Kwa kuwa kuna Mungu Mmoja tu, na wanadamu ni wa aina moja, dini ambayo Mungu ameiweka kwa wanadamu ni moja. Hakuagiza dini moja kwa Wayahudi, nyingine kwa Wahindi na nyingine kwa Wazungu, nk. Mahitaji ya kiroho na kijamii ni sare, na asili ya binadamu haijabadilika tangu mwanamume na mwanamke wa kwanza kuumbwa. Kwa hivyo, hakuna dini nyingine inayokubalika kwa Mwenyezi Mungu isipokuwa Uislamu, kama Anavyoeleza wazi katika ufunuo wa mwisho:

“Hakika Dini ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu...” (Quran 3:19)

“Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasiri.” (Kurani 3:85)

Mbaya Nzuri zaidi

Kwa nini Mungu aliwaumba wanadamu? (sehemu ya 3 kati ya 4): Maisha kama Ibada

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kusudi la uumbaji wa wanadamu ni ibada. Sehemu ya 3: Katika mfumo wa Kiislamu, kila kitendo cha binadamu kinaweza kubadilishwa kuwa kitendo cha ibada.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,749
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kila Tendo ni Ibada

Katika mfumo wa Kiislamu, kila kitendo cha binadamu kinaweza kubadilishwa kuwa kitendo cha ibada. Hakika Mwenyezi Mungu anawaamrisha Waumini wajitolee maisha yao yote kwake. Katika Qurani, Mungu anasema:

“Sema: Hakika Sala yangu, na dhabihu yangu, na uhai wangu, na kufa kwangu, ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote’” (Kurani 6:162)

Hata hivyo, kujitolea huku, ili kukubalika kwa Mungu, kila kitendo lazima kitimize masharti mawili ya kimsingi:

1. Kwanza, tendo hilo lazima lifanyike kwa dhati kwa ajili ya radhi ya Mungu na si kwa kutambuliwa na kusifiwa kwa wanadamu. Na muumini pia amjue Mwenyezi Mungu anapo fanya tendo ili kuhakikisha kwamba haijaharamishwa na Mwenyezi Mungu wala Mtume wa mwisho, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Ili kuwezesha mabadiliko hayo ya matendo ya kawaida kuwa ibada, Mungu alimuagiza Mtume wa mwisho, afundishe dua fupi za kusemwa kabla ya kufanya hata vitendo rahisi zaidi. Maombi mafupi ambayo inaweza kutumika kwa hali yoyote ni: Bismillaah (Kwa jina la Mungu). Hata hivyo kuna maombi mengine mengi yaliyowekwa kwa vipindi maalum. Kwa mfano, kila wakati ambao kipande kipya cha nguo huvaliwa, Mtume aliwafundisha masahaba wake kusema:

“Ewe Mwenyezi Mungu! Shukrani na sifa njema ni zako, kwani ni Wewe ndiye uliyenivisha. nakuomba manufaa yake na manufaa ya kila uliotengenezewa , na kujikinga kwako kutokana na uovu wake na uovu ulio uliotengenezewa.” (An-Nasa’i)

2. Sharti ya pili ni kwamba tendo lazima lifanyike kulingana na njia ya mtume, inayoitwa kwa Kiarabu Sunnah. Manabii wote waliwaagiza wafuasi wao wafuate njia yao kwa sababu waliongozwa na Mungu. Yale waliyofundisha yalikuwa ukweli kutoka kwa Mungu, na ni wale tu waliofuata njia yao na kukubali ukweli ndio wangerithi uzima wa milele katika paradiso. Ni katika muktadha huu ambapo Nabii Yesu, amani na baraka za Mungu ziwe juu yake, iliripotiwa kuwa alisema katika Injili kulingana na Yohana 14:6, akisema:

“Mimi ndiye njia na kweli na uzima, hakuna mtu ajaye kwa Baba ila kwa njia yangu.”

Vilevile, Abdullaah ibn Mas'ood alinukuli kwamba…

“Siku moja Mtume Muhammad alichora mstari kwenye mchanga na akasema: Hii ndiyo Njia ya Mwenyezi Mungu. Kisha akachora mistari kadhaa kuelekea kulia na kushoto, na akasema: Hizi ni njia ambazo Shet'ani anawaita watu kuzifuata. Kisha akasoma Aya: Na kwa hakika hii ndiyo Njia yangu Iliyo Nyooka. Basi ifuateni, wala msifuate njia nyingine, zikakutengeni na Njia yake. Haya amekuusieni ili mpate kuchamngu.’” (Ahmed)

Kwa hivyo, njia pekee inayokubalika ya kumwabudu Mungu ni kulingana na njia ya manabii. Kwa hivyo, uvumbuzi katika mambo ya dini utachukuliwa na Mungu kuwa kati ya madhambi mbaya zaidi. Mtume Muhammad, iliripotiwa kuwa alisema,

“Mambo mabaya zaidi ni uvumbuzi katika dini, kwa maana kila uvumbuzi katika dini ulilaaniwa, unaopotosha na unaongoza kwenye moto wa Jahannamu.” (An-Nasa’i)

Uvumbuzi katika dini ni haramu na haikubaliki kwa Mungu. Mke wa mtume, Aa'ishah, aliripoti kuwa Mtume alisema:

“Atakaye ongeza kitu katika dini yetu, ambacho si cha dini, basi kitakataliwa.” (Saheeh Al-Bukhari)

Kimsingi, ni kutokana na ubunifu ndipo ujumbe wa manabii wa awali ulipotoshwa na dini nyingi za uongo zilizoko leo zimeibuka. Kanuni ya jumla ya kufuata ili kuepukana na uvumbuzi katika dini ni kwamba aina zote za ibada ni marufuku, isipokuwa zile ambazo zimeagizwa hasa na Mungu na kuletewa kwa binadamu na mitume wa kweli wa Mungu.

Viumbe Bora Zaidi

Wale wanao mwamini Mungu Mmoja wa pekee, bila washiriki wala watoto, na wakatenda mema [kulingana na masharti yaliyotajwa hapo juu] huwa taji ya viumbe. Yaani, ingawa binadamu si kiumbe mkubwa zaidi kati ya viumbe wa Mungu, ana uwezo wa kuwa bora wa uumbaji Wake. Katika ufunuo wa mwisho, Mungu anasema ukweli huu kama ifuatavyo:

“Hakika walio amini na wakatenda mema ni bora wa uumbaji.” (Kurani 98:7)

Mbaya Nzuri zaidi

Kwa nini Mungu aliwaumba wanadamu? (sehemu ya 4 kati ya 4): Kupingana na Kusudi la Uumbaji

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kusudi la uumbaji wa wanadamu ni ibada. Sehemu ya 4: Kupinga kusudi la uumbaji wa binadamu basi ni dhambi kubwa zaidi ambao mwanadamu anaweza kufanya.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,583
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Dhambi Kubwa Zaidi

Kupingana na kusudi la uumbaji wa mtu basi ni uovu mkubwa zaidi ambao mwanadamu anaweza kufanya. Abdullaah aliripoti kwamba alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (rehma iwe juu yake) kwamba ni ipi dhambi kubwa zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu na akajibu,

“Kuwashirikisha wengine na Mwenyezi Mungu ijapo kuwa amekuumba.” (Saheeh Al-Bukhari)

Kuwaabudu wengine badala ya Mwenyezi Mungu, inayoitwa shirk kwa Kiarabu, ni dhambi isiyo ya kusamehewa. Na mwanaadamu akifa bila kutubu dhambi zake, basi huenda Mwenyezi Mungu akamsamehe dhambi zake zote isipokuwa shirk. Katika suala hili, Mungu alisema:

“Hakika Mwenyezi Mungu hasamehi kushirikishwa na kitu lakini yeye husameheyasiyokuwa hayo kwa amtakaye.” (Kurani 4:116)

Kuabudu wengine badala ya Mungu kimsingi kunahusisha kutoa sifa za Muumba kwa uumbaji Wake. Kila madhehebu au dini hufanya hivyo kwa namna yao wenyewe. Kikundi kidogo cha watu wenye mijadala sana kimekanusha kuwepo kwa Mungu kuanzia zama za kale. Katika kujitetea kwao, walidai kwamba ulimwengu huu hauna mwanzo. Madai yao hayana mantiki kwa sababu sehemu zote zinazoonekana za ulimwengu zina mwanzo kwa wakati, kwa hivyo lazima sehemu za ulimwengu pia ziwe na mwanzo. Pia ni mantiki tu kudhani kwamba chochote kilicholeta ulimwengu hakingekuwa ndani ya ulimwengu huo wala kiwe na mwanzo kama ulimwengu. Madai ya wakanaji Mungu ya kwamba ulimwengu hauna mwanzo ina maana kwamba vipengelea vilivyounda ulimwengu ni vya milele. Hii ni kauli ya shirk, ambapo sifa ya Mungu ya kutokuwa na mwanzo imepewa maumbile yake. Idadi ya wakanaji Mungu katika kihistoria daima ilikuwa ndogo kabisa kwa sababu, licha ya madai yao, wao kiasili hujua kwamba Mungu yupo. Hiyo ni, licha ya miongo kadhaa ya ufundishaji wa kikomunisti, wengi wa Warusi na Wachina waliendelea kumwamini Mungu. Muumba Mwenyezi alizungumzia jambo hili, akisema:

“Na walizikanusha kwa dhulma na kujivuna, na hali ya kuwa nafsi zao zina yakini nazo.” (Quran 27:14)

Kwa wasiokiri kuwepo kwa Mungu na wapenda mapambo ya dunia, maisha hayana kusudi zaidi ya kutimiza tamaa zao. Kwa hivyo, matamanio yao yanakuwa mungu wanaye mtii badala ya Mungu Mmoja wa Haki. Katika Qurani, Mungu alisema:

“Je! Umemwona aliyefanya matamanio kuwa ndiyo mungu wake?” (Quran 25:43, 45:23)

Wakristo walimpa Nabii Isa (Yesu Kristo) sifa za Muumba kwa kumfanya kwanza awe na ushirika wa milele na Mungu, halafu kwa kumfanya awe na dhati ya Mungu ambaye walimwita “Mungu Mwana.” Wahindu, kwa upande mwingine, wanaamini kwamba Mungu amekuwa mwanadamu kwa miaka mingi, kwa njia ya mwilisho inayoitwa avatari, na kisha kugawanya sifa za Mungu kati ya miungu mitatu, Brahma Muumba, Vishnu mwokozi na Shiva Mwangamizi.

Upendo wa Mungu

Shirk pia hutokea wakati binadamu wanapenda, kuamini au kuogopa viumbe zaidi ya Mungu. Katika ufunuo wa mwisho, Mungu alisema:

“Na miongoni mwa watu wapo wanao chukua waungu wasiokuwa Mwenyezi Mungu. Wanawapenda kama kumpenda Mwenyezi Mungu. Lakini walioamini wanampenda Mwenyezi Mungu zaidi sana.” (Quran 2:165)

Wakati hisia hizi na nyingine zinazofanana zinaelekezwa zaidi kwenye viumbe, zinasababisha binadamu kutomtii Mungu kwa jitihada za kumpendeza binadamu. Hata hivyo, Mungu pekee ndiye anayestahili uazimiaji kamili wa kihisia ya kibinadamu, kwani ni Yeye pekee ambaye anapaswa kupendwa na kuogopwa juu ya viumbe vyote. Anas ibn Maalik alisimulia kwamba Nabii (rehma iwe juu yake) alisema:

“Na aliye na sifa hizi tatu basi ameonja utamu wa Imani: anaye mpenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake kuliko vyote, na anaye penda mwanadamu mwingine kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake, na anaye chukia kurudi kufuru baada ya Mwenyezi Mungu kumwokoa anavyochukia kutupwa motoni.” (As-Suyooti)

Sababu zote ambazo binadamu hupenda wanadamu wengine au kupenda viumbe vingine vilivyoumbwa ndizo sababu za kumpenda Mungu zaidi ya uumbaji wake. Binadamu hupenda maisha na mafanikio, na huchukia kifo na kutofaulu. Kwa kuwa Mungu ndiye chanzo cha maisha na mafanikio, Anastahili upendo kamili na ibada kutoka kwa wanadamu. Binadamu pia huwapenda wale wanaowafaidisha na kuwasaidia wanapokuwa na haja. Kwa kuwa faida zote (7:188) na msaada (3:126) hutoka kwa Mungu, anapaswa kupendwa kuliko wengine.

“Ikiwa mtajaribu kuzihesabu baraka za Mwenyezi Mungu, humwezi kuzidhibiti.” (Quran 16:18)

Hata hivyo, upendo mkuu ambao wanadamu wanapaswa kuhisi kwa Mungu haupaswi kupunguzwa hadi kwa kiwango cha mapenzi yao kwa viumbe. Kama vile upendo wa wanadamu kwa wanyama haupaswi kuwa sawa na mapenzi yao kwa binadamu wengine, upendo wa Mungu unapaswa kuvuka mapenzi ya wanadamu kwa wenzao. Upendo wa kibinadamu wa Mungu unapaswa kuwa, kimsingi, upendo unaoonekana katika utii kamili kwa sheria za Mungu:

“Na ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi (Mtume wa Mungu) na Mwenyezi Mungu atawapenda.” (Quran 3:31)

Hii sio kudhania tu, kwa sababu upendo wa binadamu kwa wanadamu wengine pia unamaanisha utiifu. Hiyo ni ikiwa mpendwa anaomba kitu kifanyike, wanadamu watajitahidi kufanya hivyo kulingana na kiwango cha upendo wao kwa mtu huyo.

Upendo wa Mungu pia unapaswa kuonyeshwa katika upendo wa wale ambao Mungu anawapenda. Haiwezekani kwamba mtu anayempenda Mungu kuwachukia wale ambao Mungu anawapenda na kuwapenda wale anaowachukia. Nabii (rehma ziwe juu yake) alinukuliwa na Aboo Umaamah akisema:

“Anayependa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na akachukia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na hupeana kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na hunyima kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, [na anaoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu] ameikamilisha imani yake.” (As-Suyooti)

Kwa hivyo, wale ambao imani yao ni sahihi watawapenda wote wampendao Mungu. Katika Sura ya Maryamu, Mungu anaonyesha kwamba anaweka upendo ndani ya mioyo ya Waumini kwa walewaaminio.

“Hakika Mwenyezi Mungu atawajalia mapenzi ( katika mioyo ya waumini kwa) waloamini na wakatenda mema.” (Kurani 19:96)

Aboo Hurayrah pia alisimulia kwamba Mtume wa Mungu (rehma ziwe juu yake) alisema yafuatayo katika suala hili:

“Kama Mungu anampenda mja Anamwambia malaika Jibrili kwamba anampenda fulani na fulani na anamwambia ampende, hivyo Jibril anampenda. Kisha Jibril akawaita wenyeji wa mbinguni: Mwenyezi Mungu anampenda fulani, basi mpendeni. Basi wenyeji wa mbinguni wanampenda. Kisha anapewa upendo wa watu wa dunia. ” (Saheeh Muslim)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.