Uislamu ni nini? (sehemu ya 4 kati ya 4): Ibada ya Uislamu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kutazama baadhi ya vitendo muhimu vya Uislam, na maelezo mafupi ya Waislamu ni akina nani.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 12
  • Imetazamwa: 6,718 (wastani wa kila siku: 8)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kuna mazingatio matano rahisi ila muhimu ambayo Waislamu wanayakubali na kuyafata. Hizi ni “Nguzo za Uislamu” zinazowakilisha misingi ambayo inawaunganisha Waislamu wote.

1) ‘Tamko la Imani’

Muislamu ni yule anayetoa ushuhuda kwamba “hakuna anayestahili kuabudiwa ila Allah, na Muhammad ni mjumbe wa Allah.” Tamko hili linajulikana kama “shahada” (ushahidi, ushuhuda). Allah ni neno la Kiarabu la Mungu, kama vile Yahweh kwa Kiebrania jina la Mungu. Kwa kutamka neno hili rahisi mtu anakuwa Muislamu. Tamko linathibitisha Uislamu katika umoja wa Mungu, Haki yake ya kuabudiwa, na fundisho linalohusu kuhusisha kitu chochote na Mungu ni moja ya dhambi isiyo sameheka kama tulivyosoma kwenye Koran:

“ Hakika Mwenyezi Mungu hasamehe kushirikishwa, na husamehe yaliyo duni ya hilo kwa amtakaye. Na anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu basi hakika amezua dhambi kubwa. ” (Kurani 4:48)

Sehemu ya pili ya ushuhuda wa imani inaeleza kuwa Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, ni mtume wa Mungu kama Ibrahim, Musa na Yesu kabla yake. Muhammad ameleta ufunuo wa mwisho. Kwa kumuamini Muhammad kama “muhuri wa manabii,” Waislamu wanaamini kuwa utabili wake unathibitisha na kukamilisha ufunuo wa jumbe zote, kuanzia Adam. Cha nyongeza, Muhammad hutumika kama mfano katika maisha yake ya mfano. Jitihada za walioamini kufuata mfano wa Muhammad unaakisi mkazo wa Uislamu katika vitendo na matendo.

2) Kuswali (Salah)

Waislamu wanaswali mara tano kwa siku: alfajiri, mchana, alasili, jioni, na usiku. Inafanya Walio amini kumkumbuka Mungu katika mfadhaiko wa kazi na familia. Inauelekeza umakini wa kiroho, inaimarisha tegemeo kamili la Mungu, na huweka wasiwasi wa kilimwengu katika mtazamo wa hukumu ya mwisho na maisha ya baadaye. Sala hizo zinajumuisha kusimama, kuinama, kupiga magoti, kuweka paji la uso chini, na kukaa. Ibada ni njia ambayo inaweka mahusiano kati ya Mungu na uumbaji wake ili uweze kudumishwa. Inajumuisha kusoma Kurani, sifa za Mungu, maombi ya msamaha na dua zingine mbali mbali. Maombi ni kuonyesha kujisalimisha, unyenyekevu, na kumuabudu Mungu. Maombi yanaweza kufanywa katika sehemu yoyote iliyo safi, pekee au kwa pamoja, msikitini au nyumbani, kazini au barabarani, ndani ya nyumba au nje. Inapendeza kuswali na watu wengine kama mwili mmoja ulioungana katika ibada ya Mungu, kuonyesha nidhamu, udugu, usawa, na mshikamano. Wanaposali, Waislamu wanaangalia Makka, jiji takatifu lililoizunguka Kaaba - nyumba ya Mungu iliyojengwa na Ibrahim na mwanawe Ismaili.

3) Sadaka ya Lazima (Zakah)

Kwenye Uislamu, mmiliki wa kweli ni Mungu, siyo mwanadamu. Watu wanapewa utajiri kama amana kutoka kwa Mungu. Zakah ni ibada na zawadi kwa Mungu kwa kuwasaidia masikini, na kwa hilo mtu anasafishwa. inahitajika mchango wa kila mwaka wa asilimia 2.5 ya utajiri wa mtu binafsi na mali. Kwa hiyo, Zakah siyo “Msaada”, ni wajibu kwa wale ambao wamepata utajiri kutoka kwa Mungu kukidhi mahitaji ya wanajamii wasio na baraka hiyo. Zakah inatumika kuwasaidia masikini na wanaohitaji, msaada wale wenye deni, na, kipindi cha zamani, kuwaachia watumwa.

4) Kufunga Ramadan (Sawm)

Ramadhani ni mwezi wa tisa wa kalenda ya mwezi wa Kiislamu ambayo hutumika katika kufunga. Waislamu wenye afya hujinyima chakula, vinywaji, na tendo la ndoa alfajiri hadi machweo. Kufunga kunaongeza imani, kumtegemea Mungu, na kuleta utambulisho kwa wale wasio na bahati. Sala maalumu ya usiku pia ufanyika msikitini ambapo usomaji wa Kurani unasikika. Familia zinaamka kabla ya asubuhi kupata chakula cha kwanza cha siku ili kuweza kuhimili hadi jioni. Mwezi wa Ramadhani unaisha kwa sherehe kuu mbili za Kiislamu, Siku kuu ya Kuvunja Saumu, inaitwa Eid al-Fitr, ambayo inapambwa kwa furaha, familia kutembeleana, na kubadilishana zawadi.

5) Nguzo ya tano ni Hajj kwenda Makka

Angalau mara moja katika maisha, Muislamu mtu mzima ambaye anauwezo wa kiakili na kipesa anahitajika kuutoa kafara muda, mali, cheo, na maisha mazuri ya kila siku kufanya safari ya Hajj, kujiweka katika huduma ya Mungu. Kila mwaka zaidi ya walio amini milioni mbili kutoka tamaduni mbali mbali na lugha husafiri kutoka ulimwenguni kote kwenda katika mji mtakatifu wa Makka[1] Kuitikia wito wa Mungu.

Waislamu ni Akina nani?

Neno la Kiarabu la “Muislamu” linamaanisha “mtu ambaye yupo kwenye hali ya Uislamu (kujisalimisha katika mapenzi na sheria ya Mungu)”. Ujumbe wa Uislamu ulikusudiwa kwa walimwengu wote, na mtu yoyote atakaye ukubali ujumbe huu atakuwa Muislamu. Kuna Waislamu zaidi ya bilioni duniani. Waislamu wanawakilisha idadi kubwa ya watu katika nchi hamsini na sita. Watu wengi wanashangaa kujua kuwa Waislamu wengi siyo Waarabu. Japokuwa Waarabu wengi ni Waislamu, kuna Waarabu ambao ni Wakristo, Wayahudi na Wasiokuwa na dini. Asilimia 20 tu ya Waislamu bilioni 1.2 duniani wanatoka nchi za Kiarabu. Kuna idadi kubwa ya Waislamu kutoka India, Uchina, Jamuhuri ya Asia ya kati, Urusi, Ulaya, na Marekani. Iwapo mtu ataangalia watu mablimbali wanoishi Ulimwengu waUislamu - kuanzia Nigeria hadi Bosnia na kuanzia Morocco hadi Indonesia - ni rahisi kuona kuwa Waislamu wanatoka katika asili, makabila, tamaduni na mataifa tofauti tofauti. Uislamu mara zote umekuwa ujumbe wa ulimwengu kwa watu wote. Uislamu ni dini kubwa ya pili katika ulimwengu na karibuni itakuwa dini ya pili kwa ukubwa ndani ya Marekani. Huku ni , watu wachache wanajua Uislamu ni nini.



Rejeleo la maelezo:

[1] Makka ni mji Uliopo Saudi Arabia.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.