Hadithi ya Ibrahimu (sehemu ya 1 kati ya 7): Utangulizi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Utangulizi wa nafsi ya Ibrahimu na nafasi ya juu aliyonayo katika Uyahudi, Ukristo, na Uislamu vile vile.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 30 Jul 2023
  • Ilichapishwa: 6
  • Imetazamwa: 7,382
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Story_of_Abraham_(part_1_of_7)_001.jpgMmoja wa manabii wanaopewa kipaumbele zaidi katika Quran ni nabii Ibrahimu. Quran inaeleza juu yake na imani yake isiyo na shaka juu ya Mwenyezi Mungu, kwanza ikimuita kuwakataa watu wake na ibada yao ya masanamu, na baadae kuthibitisha kuwa ni mkweli kwa mitihani mbalimbali ambayo Mungu huweka mbele yake.

Katika Uislamu, Ibrahimu anaonekana kama muamini Mungu mmoja madhubuti ambaye anawaita watu wake kwenye ibada ya Mungu pekee. Kwa imani hii, anavumilia matatizo makubwa, hata kujitenga na familia yake na watu kwa njia ya kuhamia nchi mbalimbali. Yeye ni yule anayezitimiza amri mbalimbali za Mungu ingawa yeye alijaribiwa, akithibitisha kila moja kuwa kweli.

Kutokana na nguvu hii ya imani, Quran inaitaja dini moja ya kweli kuwa ni "Njia ya Ibrahimu", ingawa manabii wa kabla yake, kama vile Nuhu, waliitwa kwenye imani hiyo hiyo. Kwa sababu ya kitendo chake cha utiifu bila kuchoka kwa Mwenyezi Mungu, alimpa cheo maalum cha “Khaleel”, au mtumishi mpendwa, ambacho hakupewa Nabii mwingine yeyote hapo kabla. Kwa ubora wa Ibrahimu, Mwenyezi Mungu akawafanya Manabii kutoka kwenye kizazi chake, kutoka kwao Ismaili Isaka, Yakobo(Izraili) na Musa, wanaowaongoza watu kwenye haki.

Hadhi ya juu ya Ibrahimu inashirikiwa kwa usawa na Uyahudi, Ukristo na Uislamu. Wayahudi wanamwona kuwa ni mfano wa wema alipotimiza amri zote ingawa kabla hazijafunuliwa, na alikuwa wa kwanza kufika kwenye utambuzi wa Mungu Mmoja wa Kweli. Anaonekana kama baba wa kizazi teule, baba wa manabii kutokana na kwamba Mungu alianzisha mfululizo wake wa mafunuo. Katika Ukristo, anaonekana kama baba wa waamini wote (Warumi 4:11) na imani yake kwa Mungu na sadaka inachukuliwa kama kielelezo kwa watakatifu wa baadaye (Waebrania 11).

Kwa vile Ibrahimu anapewa umuhimu huo, inafaa mtu asome maisha yake na kuchunguza yale mambo ambayo yalimuinua hadi kufikia kiwango ambacho Mungu alimpa.

Ingawa Quran na Sunnah hazitoi maelezo ya maisha yote ya Ibrahimu, zinataja mambo fulani yenye kustahiki kuzingatiwa. Kama ilivyo kwa watu wengine wa Qurani na wa Biblia, Quran na Sunnah zinaeleza kwa undani vipengele vya maisha yao kama ufafanuzi wa baadhi ya imani potofu za dini zilizoteremshwa hapo awali, au vipengele vile ambavyo vina kauli mbiu na maadili yanayostahili kuzingatiwa na kusisitizwa.

Jina lake

Katika Quran, jina pekee alilopewa Ibrahimu ni "Ibraheem" na "Ibrahaam", zote zikishiriki mzizi asili, b-r-h-m. Ingawa katika Biblia Ibrahimu anajulikana kama Abramu mwanzoni, na kisha inasemekana Mungu alibadili jina lake na kuwa Ibrahimu, Quran imekaa kimya juu ya suala hili, bila kuthibitisha au kupinga. Wasomi wa kisasa wa Kiyahudi-Kikristo wana shaka, hata hivyo, katika hadithi ya mabadiliko ya majina yake na maana zao, wakiita "mchezo maarufu wa ulimwengu". Wanaasuria wanapendekeza kwamba herufi ya Kiebrania Hê (h) katika lahaja ya Minnean imeandikwa badala ya neno refu ‘a’ (ā), na kwamba tofauti kati ya Abrahamu na Abramu ni lahaja tu.[1] Vile vile inaweza kusemwa kwa majina ya Sarai na Sara, kwa kuwa maana zake pia zinafanana.[2]

Nchi Yake

Ibrahimu anakadiriwa kuwa alizaliwa miaka 2,166 kabla ya Yesu katika au karibu na Mesopotamia[3] jiji la Uru[4], maili 200 kusini mashariki mwa Baghdad ya sasa[5]. Baba yake alikuwa ‘Aazar’, ‘Terah’ au ‘Terakh’ katika Biblia, mwabudu sanamu, ambaye alitokana na uzao wa Shemu, mwana wa Nuhu. Baadhi ya wasomi wa ufafanuzi wanapendekeza kwamba huenda aliitwa Azar kutokana na sanamu alilokuwa amejitolea kwake.[6] Yaelekea alikuwa Mkadiani, watu wa Kisemiti kutoka Rasi ya Arabia walioishi Mesopotamia wakati fulani katika milenia ya tatu KK.

Inaonekana kana kwamba Azar alihama pamoja na baadhi ya jamaa zake hadi mji wa Harani katika utoto wa mapema wa Ibrahimu kabla ya kutofautiana na watu wake, ingawa baadhi ya mapokeo ya Kiyahudi-Kikristo[7] yanasema kuwa ni baadaye katika maisha yake baada ya yeye kukataliwa katika mji wake wa asili. Katika Biblia, Harani, mmoja wa ndugu za Ibrahimu inasemekana alikufa huko Uru, “katika nchi aliyozaliwa” (Mwanzo 11:28), lakini alikuwa mkubwa zaidi kuliko Ibrahimu, kama vile ndugu yake mwingine Nahori alimchukua binti wa Harani kama mke (Mwanzo 11:29). Biblia pia haitaji kuhama kwa Ibrahimu kwenda Harani, bali amri ya kwanza ya kuhama ni ile ya kutoka Harani, kana kwamba walikuwa wamekaa huko hapo awali (Mwanzo 12: 1-5). Ikiwa tutachukua amri ya kwanza kumaanisha kuhama kutoka Uru hadi Kanaani, inaonekana hakuna sababu yoyote kwa Ibrahimu kukaa na familia yake huko Harani, na kumwacha baba yake huko na kwenda Kanaani baadaye, bila kutaja kutowezekana kwake kwa kijiografia [Angalia ramani].

Quran inataja kuhama kwa Ibrahimu, lakini inafanya hivyo baada ya Ibrahimu kujitenga na baba yake na watu wa kabila lake kutokana na ukafiri wao. Ikiwa angekuwa Uru wakati huo, inaonekana kwamba baba yake asingeenda pamoja naye hadi Harani baada ya kutoamini na kumtesa pamoja na watu wa mji wake. Kuhusu ni kwa nini walichagua kuhama, ushahidi wa kiakiolojia unapendekeza kwamba Uru ulikuwa mji mkuu ambao ulishuhudia kuinuka na kuanguka katika maisha ya Ibrahimu[8], hivyo wanaweza kuwa walilazimika kuondoka kutokana na ugumu wa mazingira. Huenda waliichagua Harani kwa sababu ya kua na dini sawa na Uru[9].

The_Story_of_Abraham_(part_1_of_7)_002.jpg

Dini ya Mesopotamia

Uvumbuzi wa kiakiolojia wa wakati wa Ibrahimu unatoa picha wazi ya maisha ya kidini ya Mesopotamia. Wakazi wake walikuwa washirikina walioamini katika miungu, ambapo kila mungu alikuwa na nyanja ya ushawishi. Hekalu kubwa liliwekwa kwa Akkadian[10] mungu wa mwezi, Sin, ilikuwa kituo kikuu cha Uru. Harani pia ilikuwa na mwezi kama mungu mkuu. Hekalu hili liliaminika kuwa nyumba ya kimwili ya Mungu. Mungu mkuu wa hekalu alikuwa sanamu ya mbao yenye sanamu zingine, au ‘miungu’, ili kumtumikia.

The_Story_of_Abraham_(part_1_of_7)_003.jpg

Ziggurati Mkuu wa Uru, hekalu la mungu wa mwezi Nanna, anayejulikana pia kama Sin. Ilipigwa mwaka 2004, picha hiyo ni kwa hisani ya Lasse Jensen.

Maarifa ya Mungu

Ingawa wanazuoni wa Kiyahudi-Kikristo wametofautiana kuhusu lini Ibrahimu alikuja kumjua Mungu, akiwa na umri wa miaka mitatu, kumi, au arobaini na nane[11], Quran iko kimya katika kutaja umri kamili ambao Ibrahimu alipokea ufunuo wake wa kwanza. Inaonekana, ilikuwa, hata hivyo, alipokuwa mdogo katika umri, kwa vile Quran inamuita kijana wakati watu wake wanajaribu kumuua kwa kukataa masanamu yao, na Ibrahimu mwenyewe alisema kuwa hakuwa na ufahamu kwa baba yake wakati alipomuita kumwabudu Mungu peke yake kabla wito wake haujaenea kwa watu wake (19:43). Quran iko wazi, hata hivyo, kwa kusema kwamba alikuwa ni mmoja wa Mitume waliofunuliwa Kitabu:

"Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo, Vitabu vya Ibrahimu na Musa." (Quran 87:18-19)



Rejeleo la maelezo:

[1] Ibrahimu. Kitabu cha Kikatoliki, Juzuu ya I. Hakimiliki © 1907 kwa Kampuni ya Robert Appleton. Toleo la Mtandaoni Hakimiliki © 2003 kwa K. Knight Nihil Obstat, Machi 1, 1907. Remy Lafort, S.T.D., Censor. Imprimatur. +John Cardinal Farley, Askofu Mkuu wa New York. (http://www.newadvent.org/cathen/01051a.htm)

[2] Sarah. Kitabu cha Kikatoliki, Juzuu ya I. Hakimiliki © 1907 kwa Kampuni ya Robert Appleton. Toleo la Mtandaoni Hakimiliki © 2003 kwa K. Knight Nihil Obstat, Machi 1, 1907. Remy Lafort, S.T.D., Censor. Imprimatur. +John Cardinal Farley, Askofu Mkuu wa New York. (Abraham. Charles J. Mendelsohn, Kaufmann Kohler, Richard Gottheil, Crawford Howell Toy. Kitabu cha Kiyahudi.)

[3] Mesopotamia: "(Mes·o·po·ta·mi·a) Eneo la kale la kusini-magharibi mwa Asia kati ya mito ya Tigri na Eufrate katika Iraq ya sasa. Huenda eneo hilo liliwekwa makazi kabla ya mwaka wa 5000 KK, eneo hilo lilikuwa makao ya watu wa mjini wa mapema wakiwemo Sumer, Akkadi, Babeli na Ashuru." (Kamusi ya Lugha ya Kiingereza ya American Heritage® , Toleo la Nne Hakimiliki © 2000 kwa Kampuni ya Houghton Mifflin.)

[4] Mhenga wa watu wa Kiebrania, Abramu, alikuwa, tunaambiwa, alizaliwa katika "Uru ya Wakaldayo." "Wakaldayo" ni tafsiri isiyo sahihi ya Kiebrania Kasdim, Kasdim ni jina la Agano la Kale la Wababeli, wakati Wakaldayo walikuwa kabila lililoishi kwenye mwambao wa Ghuba ya Uajemi, na hawakuwa sehemu ya wakazi wa Babeli hadi wakati wa Hezekia. Uru ilikuwa mojawapo ya majiji ya kale na mashuhuri zaidi ya Babeli. Mahali pake sasa hivi panaitwa Mugheir, au Mugayyar, kwenye ukingo wa magharibi wa Euphrates, Kusini mwa Babilonia. (Kamusi ya Biblia ya Easton ya 1897). Baadhi ya wasomi wa Kiyahudi-Kikristo wanasema kwamba "Uru-Kasdim" iliyotajwa katika Biblia sio Uru, lakini kwa kweli ni jiji la Uru-Keshi, lililoko kaskazini mwa Mesopotamia na karibu na Harani (Kutoka kwa Ibrahimu hadi Yusufu - Ukweli wa kihistoria ya enzi za mfumo Dume. Claus Fentz Krogh (http://www.genesispatriarchs.dk/patriarchs/abraham/abraham_eng.htm).

[5] Ibn Asakir, mwanazuoni maarufu wa Kiislamu na mwanahistoria, pia alithibitisha maoni haya na kusema kwamba alizaliwa Babeli. Tazama "Qisas al-Anbiyaa" ibn Katheer.

[6] Hadithi za Mitume, ibn Kathir. Machapisho ya Darussalam.

[7] Kwa kuwa kuna maelezo machache kuhusu maisha ya Ibrahimu katika Biblia, mengi ya yale ambayo kwa kawaida yanaaminika kuhusu Ibrahimu yanaundwa kupitia mapokeo mbalimbali ya Kiyahudi-Kikristo, yaliyokusanywa katika kitabu na maandishi mengine ya marabi. Mengi ya yale yaliyotajwa katika Biblia pamoja na mapokeo mengine yanachukuliwa miongoni mwa wasomi wa Kiyahudi-Kikristo kuwa wakongwe, ambazo nyingi haziwezi kuthibitishwa. (Abraham. Kitabu cha Kikatoliki, Juzuu ya I. Hakimiliki © 1907 kwa Kampuni ya Robert Appleton. Toleo la Mtandaoni Hakimiliki © 2003 kwa K. Knight Nihil Obstat, Machi 1, 1907. Remy Lafort, STD, Censor. Imprimatur. +John Cardinal Farley, Askofu Mkuu ya New York.) (Abraham. Charles J. Mendelsohn, Kaufmann Kohler, Richard Gottheil, Crawford Howell Toy. Kitabu cha Kiyahudi. (http://www.jewishencyclopedia.com/view.jsp?artid=360&letter=A#881)

[8] (http://www.myfortress.org/archaeology.html)

[9] (http://www.myfortress.org/archaeology.html)

[10] Akkad: "(Ak·kad) Eneo la kale la Mesopotamia linalomiliki sehemu ya kaskazini ya Babeli." (Kamusi ya Lugha ya Kiingereza ya American Heritage®, Toleo la Nne Hakimiliki © 2000 kwa Kampuni ya Houghton Mifflin.)

[11] Gen R. xxx. Ibrahimu. Charles J. Mendelsohn, Kaufmann Kohler, Richard Gottheil, Crawford Howell Toy. Kitabu cha Kiyahudi. (http://www.jewishencyclopedia.com/view.jsp?artid=360&letter=A#881).

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa