Hadithi ya Ibrahimu (sehemu ya 2 kati ya 7): Wito kwa Watu Wake

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Ibrahimu anawaalika baba yake Azar (Terah au Terakh katika Biblia) na umma kwenye Haki iliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake Mlezi.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 28 Jan 2022
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,198 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Ibrahimu na Baba yake

Kama wale walio mzunguka, baba yake Ibrahimu Azar (Terah au Teraki katika Biblia), alikuwa mwabudu sanamu. Mapokeo ya Kibiblia[1] yanasimulia juu yake kuwa ni mchongaji wao,[2] hivyo wito wa kwanza wa Ibrahimu ulielekezwa kwake. Alizungumza naye kwa mantiki na akili ya wazi, iliyoeleweka na kijana kama yeye pamoja na mwenye busara.

"Na mtaje katika Kitabu Ibrahim. Hakika yeye alikuwa mkweli, Nabii. Alipo mwambia baba yake: Ewe baba yangu! Kwa nini unaabudu visivyo sikia, na visivyo ona, na visivyo kufaa chochote? Ewe baba yangu! Kwa yakini imenifikia ilimu isiyo kufikia wewe. Basi nifuate mimi, nami nitakuongoza Njia Iliyo Sawa." (Quran 19:41-43)

Jibu kutoka kwa baba yake lilikuwa kukataliwa, jibu la wazi kwa mtu yeyote aliyepingwa na mtu mwingine mdogo kuliko yeye, changamoto iliyofanywa dhidi ya miaka ya mila na desturi.

"(Baba) akasema: ‘Unaichukia miungu yangu, ewe Ibrahim? Kama huachi, basi lazima nitakupiga mawe. Na niondokelee mbali kwa muda!’" (Quran 19:46)

Ibrahim na Watu Wake

Baada ya majaribio yasiyokoma ya kumuita baba yake aache ibada ya sanamu za uongo, Abrahamu aliwageukia watu wake akitaka kuwaonya wengine, akiwahutubia kwa mantiki ile ile rahisi.

"Na wasomee khabari za Ibrahim. Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?" Wakasema: "Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea." He said: "Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita? Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?" Wakasema: "Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo." Je! Mmewaona hawa mnao waabudu, Nyinyi na baba zenu wa zamani? Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote; Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa; Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha. Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha; Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha." (Quran 26:69-81)

Katika kuendeleza wito wake kwamba mungu pekee anayestahili kuabudiwa ni Mungu, Mwenyezi, alitoa mfano mwingine kwa watu wake kutafakari. Mapokeo ya Kiyahudi-Kikristo yanasimulia hadithi inayofanana, lakini inaionyesha katika muktadha wa Ibrahimu mwenyewe kuja kwenye utambuzi kama Mungu kupitia ibada ya viumbe hawa[3], si kwa yeye kuitumia kama mfano kwa watu wake. Katika Quran, hakuna Mitume yeyote anayesemekana kuwa alishirikisha wengine isipokuwa Mwenyezi Mungu, hata kama walikuwa hawajafahamishwa njia sahihi kabla ya kutumwa kuwa manabii. Quran inatuambia kuhusu Ibrahimu:

"Na ulipo muingilia usiku akiona nyota, akasema: 'Huyu ni Mola Mlezi wangu. Ilipo tua akasema: Siwapendi wanao tua.’" (Quran 6:76)

Ibrahimu aliwatolea kielelezo cha nyota, uumbaji usioweza kueleweka kabisa kwa wanadamu wakati huo, ulioonekana kuwa kitu kikubwa zaidi kuliko ubinadamu, na mara nyingi ukiwa na nguvu mbalimbali zinazohusishwa nazo. Lakini katika mazingira ya nyota Ibrahimu aliona kutokua na uwezo wa kuonekana kama walivyo tamani, bali usiku tu.

Kisha akatoa mfano wa kitu kikubwa zaidi, mwili wa mbinguni mzuri zaidi, mkubwa zaidi, na ambao ungeweza kuonekana wakati wa mchana pia!

"Alipo uona mwezi unachomoza alisema: 'Huyu ndiye Mola Mlezi wangu. Ulipotua akasema: Kama Mola Mlezi wangu hakuniongoa, nitakuwa katika kaumu walio potea.’" (Quran 6:77)

Kisha kama kielelezo chake cha mwisho, alitoa mfano wa kitu kikubwa zaidi, moja wapo ya viumbe vyenye nguvu zaidi, ambacho bila icho uhai wenyewe ulikuwa hauwezekani.

"Na alipo liona jua linachomoza akasema: 'Huyu ndiye Mola Mlezi wangu. Huyu mkubwa kuliko wote.' Lilipo tua, alisema: 'Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayo fanyia ushirikina. Hakika mimi nimeuelekeza uso wangu sawa sawa kwa aliye ziumba mbingu na ardhi, wala mimi si miongoni mwa washirikina.'" (Quran 6:78-79)

Ibrahimu aliwathibitishia kwamba Mola Mlezi wa walimwengu hatakiwi kuwa katika uumbaji ambao masanamu yao yaliwakilisha, bali alikuwa, badala yake, ni yule aliyewaumba na kila kitu walichokiona na kukitambua; kwamba Bwana hahitaji kuonekana ili kuabudiwa. Yeye ni Mola Mweza wa Yote, asiyefungwa na mipaka kama vile uumbaji unaopatikana katika ulimwengu huu ulivyo. Ujumbe wake ulikuwa rahisi:

"Na Ibrahim pale alipo waambia watu wake: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na mcheni Yeye. Hiyo ndiyo kheri yenu, ikiwa nyinyi mnajua. Hakika nyinyi mnaabudu masanamu badala ya Mwenyezi Mungu, na mnazua uzushi. Hakika hao mnao waabudu badala ya Mwenyezi Mungu hawakumilikiini riziki yoyote. Takeni riziki kwa Mwenyezi Mungu, na mumuabudu Yeye, na mumshukuru Yeye. Kwake Yeye ndio mtarudishwa." (Quran 29:16-17)

Alihoji waziwazi kushikamana kwao na mapokeo ya mababu zao.

"“Alisema: ‘Hakika nyinyi na baba zenu mlikuwa katika upotofu ulio dhaahiri.’"

Njia ya Ibrahimu ilijaa uchungu, shida, majaribu, upinzani, na maumivu ya moyo. Baba yake na watu walikataa ujumbe wake. Wito wake ulianguka kwenye masikio ya viziwi; wasingetoa sababu. Badala yake, alipingwa na kudhihakiwa,

"Wakasema: 'Lete kwetu ukweli, au wewe ni mcheshi?"

Katika hatua hii ya maisha yake, Ibrahimu, kijana mwenye wakati ujao unaotazamiwa, anaipinga familia na taifa lake mwenyewe ili kueneza ujumbe wa imani ya kweli ya Mungu Mmoja, imani katika Mungu Mmoja wa Kweli, na kukataa miungu mingine yote ya uongo, iwe kuwa ni nyota na viumbe vingine vya mbinguni au duniani, au picha za miungu kwa namna ya sanamu. Alikataliwa, kutengwa na kuadhibiwa kwa ajili ya imani hii, lakini alisimama kidete dhidi ya maovu yote, tayari kukabiliana hata zaidi katika siku zijazo.

"Na Mola wake Mlezi alipo mjaribu Ibrahim kwa kumpa amri fulani, naye akazitimiza..." (Quran 2:124)



Rejeleo la maelezo:

[1] Gen r. xxxviii, Tanna debe Eliyahu. Ii. 25.

[2] Abraham. Charles J. Mendelsohn, Kaufmann Kohler, Richard Gottheil, Crawford Howell Toy. Kitabu cha Kiyahudi. (http://www.jewishencyclopedia.com/view.jsp?artid=360&letter=A#881)

[3] Maandiko: Uteuzi, H. Polano. (http://www.sacred-texts.com/jud/pol/index.htm).

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.