El artículo / video que has solicitado no existe todavía.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
El artículo / video que has solicitado no existe todavía.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Kisha wakati ukafika ambapo mahubiri ilibidi yaambatane na matendo halisi. Ibrahimu alipanga pigo la ujasiri na la maamuzi katika ibada ya sanamu. Maelezo ya Quran ni tofauti kidogo na yale yanayotajwa katika mila za Kiyahudi-Kikristo, kama yanavyosema kwa Ibrahimu kuharibu sanamu binafsi za baba yake.[1] Quran inasema kwamba aliharibu masanamu ya watu wake, yaliyowekwa kwenye madhabahu ya kidini. Ibrahimu alikuwa amedokeza mpango unaohusisha masanamu:
"Na Wallahi! Nitayafanyia vitimbi masanamu yenu haya baada ya mkisha geuka kwenda zenu." (Quran 21:57)
Ulikuwa ni wakati wa sikukuu ya kidini, labda iliwekwa kwa ajili ya Sin, ambao walitoka nje ya mji. Ibrahimu alialikwa kuhudhuria sikukuu hiyo, lakini akaomba radhi,
""Na akatazama kwenye nyota. Kisha akasema: 'Hakika! Najisikia mgonjwa!'’"
Kwa hiyo, wakati wenzake waliondoka bila yeye, ikawa fursa yake. Hekalu lilipoachwa, Ibrahimu alienda huko na kukaribia sanamu za mbao zilizopakwa dhahabu, ambazo zilikuwa na vyakula vingi viliyoachwa mbele yao na makuhani. Ibrahimu akawakejeli kwa ukafiri.
"Kisha akaigeukia miungu yao na kusema: 'Je, hautokula? Una shida gani hata husemi?’”
Kwani, ni nini kingeweza kumdanganya mwanadamu kuabudu miungu ya vinyago vyake mwenyewe?
"Kisha akavishambulia, akiwapiga kwa mkono wake wa kulia."
Quran inatuambia:
"Basi akayavunja vipande vipande, ila kubwa lao."
Makuhani wa hekalu waliporudi, walishtuka kuona kufuru, uharibifu wa hekalu. Walikuwa wanashangaa ni nani angeweza kufanya hivi kwa sanamu zao wakati mtu alitaja jina la Ibrahimu, akieleza kwamba alikuwa akiwasema vibaya. Walipomwita mbele yao, ilikuwa ni kwa Ibrahimu kuwaonyesha upumbavu wao:
"Akasema: ‘Muabuduni mnachokichonga wakati Mwenyezi Mungu amekuumbeni nyie na icho mnacho kitengeneza?'"
Hasira yao ilikuwa inaongezeka; bila kuhubiriwa, walifika moja kwa moja kwenye jambo hilo:
"Wakasema: Je! Wewe umeifanyia haya miungu yetu, ewe Ibrahim?"
Lakini Ibrahimu alikuwa ameacha sanamu kubwa bila kuguswa kwa sababu:
"Akasema: Bali amefanya hayo huyu mkubwa wao. Basi waulizeni ikiwa wanaweza kutamka!’"
Ibrahimu alipowapinga hivyo, waliingiwa na mkanganyiko. Wakalaumiana wao kwa wao kwa kutoyalinda masanamu na wakakataa kukutana na macho yake, wakasema:
"Kweli unajua vizuri hawa hawasemi!"
Kwa hiyo Ibrahimu akasisitiza kesi yake.
"Akasema: Basi nyinyi mnawaabudu asiye kuwa Mwenyezi Mungu wasio kufaini kitu wala kukudhuruni? Aibu yenu nyinyi na hivyo mnavyo viabudu badala ya Mwenyezi Mungu! Basi nyinyi hamtii akilini?’"
Washtaki wakawa washtakiwa. Walishutumiwa kwa kutofautiana kimantiki, na hivyo hawakuwa na jibu kwa Ibrahimu. Kwa sababu mawazo ya Ibrahimu hayakuwa na majibu, jibu lao lilikuwa hasira na ghadhabu, na walimhukumu Ibrahamu kuchomwa moto akiwa hai,
"Mjengee jengo na umtupe kwenye moto mwekundu."
Watu wa mjini walisaidia kukusanya kuni kwa ajili ya moto huo, hadi ukawa moto mkubwa zaidi kuwahi kutokea. Kijana Ibrahimu alinyenyekea kwenye majaaliwa aliyochaguliwa na Mola Mlezi wa walimwengu wote. Hakupoteza imani, bali jaribio hilo lilimfanya awe na nguvu zaidi. Ibrahimu hakukurupuka mbele ya kifo cha moto hata katika umri huu mdogo; badala yake maneno yake ya mwisho kabla ya kuingia humo yalikuwa,
"Mwenyezi Mungu ananitosheleza, na Yeye ndiye bora wa kusimamia mambo." (Saheeh Al-Bukhari)
Hapa tena kuna mfano wa Ibrahimu aliyethibitika kuwa mwaminifu kwa majaribu aliyoyakabili. Imani yake katika Mungu wa Kweli ilijaribiwa hapa, na alithibitisha kwamba alikuwa tayari hata kusitisha uwepo wake kwa wito wa Mungu. Imani yake ilithibitishwa na kitendo chake.
Mungu hakutaka kwamba hii iwe hatima ya Ibrahimu, kwa kuwa alikuwa na utume mkubwa mbele yake. Alipaswa kuwa baba wa baadhi ya manabii wakuu wanaojulikana kwa wanadamu. Mungu alimuokoa Ibrahimu kama ishara kwake na kwa watu wake pia.
“Sisi tukasema: 'Ewe moto! Kuwa baridi na salama kwa Ibrahim!’ Na wakataka kumtegea mtego, lakini tukawafanya wao kuwa wenye hasara zaidi.
Hivyo Ibrahimu aliuepuka moto, bila kudhurika. Walijaribu kulipiza kisasi kwa ajili ya miungu yao, lakini wao na sanamu zao mwishowe walidhalilishwa.
[1] Maandiko: Uteuzi, H. Polano. (http://www.sacred-texts.com/jud/pol/index.htm).
Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.
Orodha yako ya historia ipo tupu.
Kwa nini kujiandikisha? Tovuti hii ina miundo kadhaa uliyoundwa mahsusi kwa ajili yako, kama vile: vipendwa vyako, historia yako, kutia alama makala ambazo umezitazama awali, kuorodhesha makala zilizochapishwa tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho, kubadilisha ukubwa wa herufi, na zaidi. Vipengele hivi vinatokana na vidakuzi na vitafanya kazi ipasavyo tu unapotumia kompyuta ile ile. Ili kuwezesha vipengele hivi kutoka kwa kompyuta yoyote, unapaswa kuingia wakati katika tovuti hii.
Tafadhali ingiza Jina lako la mtumiaji na anwani ya barua pepe kisha ubofye kitufe cha Tuma neno la siri. Utapokea neno la siri jipya hivi karibuni. Tumia neno la siri hili jipya kufikia tovuti.
Ongeza maoni