Hadithi ya Ibrahimu (sehemu ya 3 kati ya 7): Mvunja Masanamu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Ibrahimu anaharibu masanamu ya watu wake ili kuwathibitishia ubatili wa ibada yao.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 4
  • Imetazamwa: 4,310 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kisha wakati ukafika ambapo mahubiri ilibidi yaambatane na matendo halisi. Ibrahimu alipanga pigo la ujasiri na la maamuzi katika ibada ya sanamu. Maelezo ya Quran ni tofauti kidogo na yale yanayotajwa katika mila za Kiyahudi-Kikristo, kama yanavyosema kwa Ibrahimu kuharibu sanamu binafsi za baba yake.[1] Quran inasema kwamba aliharibu masanamu ya watu wake, yaliyowekwa kwenye madhabahu ya kidini. Ibrahimu alikuwa amedokeza mpango unaohusisha masanamu:

"Na Wallahi! Nitayafanyia vitimbi masanamu yenu haya baada ya mkisha geuka kwenda zenu." (Quran 21:57)

Ulikuwa ni wakati wa sikukuu ya kidini, labda iliwekwa kwa ajili ya Sin, ambao walitoka nje ya mji. Ibrahimu alialikwa kuhudhuria sikukuu hiyo, lakini akaomba radhi,

""Na akatazama kwenye nyota. Kisha akasema: 'Hakika! Najisikia mgonjwa!'’"

Kwa hiyo, wakati wenzake waliondoka bila yeye, ikawa fursa yake. Hekalu lilipoachwa, Ibrahimu alienda huko na kukaribia sanamu za mbao zilizopakwa dhahabu, ambazo zilikuwa na vyakula vingi viliyoachwa mbele yao na makuhani. Ibrahimu akawakejeli kwa ukafiri.

"Kisha akaigeukia miungu yao na kusema: 'Je, hautokula? Una shida gani hata husemi?’”

Kwani, ni nini kingeweza kumdanganya mwanadamu kuabudu miungu ya vinyago vyake mwenyewe?

"Kisha akavishambulia, akiwapiga kwa mkono wake wa kulia."

Quran inatuambia:

"Basi akayavunja vipande vipande, ila kubwa lao."

Makuhani wa hekalu waliporudi, walishtuka kuona kufuru, uharibifu wa hekalu. Walikuwa wanashangaa ni nani angeweza kufanya hivi kwa sanamu zao wakati mtu alitaja jina la Ibrahimu, akieleza kwamba alikuwa akiwasema vibaya. Walipomwita mbele yao, ilikuwa ni kwa Ibrahimu kuwaonyesha upumbavu wao:

"Akasema: ‘Muabuduni mnachokichonga wakati Mwenyezi Mungu amekuumbeni nyie na icho mnacho kitengeneza?'"

Hasira yao ilikuwa inaongezeka; bila kuhubiriwa, walifika moja kwa moja kwenye jambo hilo:

"Wakasema: Je! Wewe umeifanyia haya miungu yetu, ewe Ibrahim?"

Lakini Ibrahimu alikuwa ameacha sanamu kubwa bila kuguswa kwa sababu:

"Akasema: Bali amefanya hayo huyu mkubwa wao. Basi waulizeni ikiwa wanaweza kutamka!’"

Ibrahimu alipowapinga hivyo, waliingiwa na mkanganyiko. Wakalaumiana wao kwa wao kwa kutoyalinda masanamu na wakakataa kukutana na macho yake, wakasema:

"Kweli unajua vizuri hawa hawasemi!"

Kwa hiyo Ibrahimu akasisitiza kesi yake.

"Akasema: Basi nyinyi mnawaabudu asiye kuwa Mwenyezi Mungu wasio kufaini kitu wala kukudhuruni? Aibu yenu nyinyi na hivyo mnavyo viabudu badala ya Mwenyezi Mungu! Basi nyinyi hamtii akilini?’"

Washtaki wakawa washtakiwa. Walishutumiwa kwa kutofautiana kimantiki, na hivyo hawakuwa na jibu kwa Ibrahimu. Kwa sababu mawazo ya Ibrahimu hayakuwa na majibu, jibu lao lilikuwa hasira na ghadhabu, na walimhukumu Ibrahamu kuchomwa moto akiwa hai,

"Mjengee jengo na umtupe kwenye moto mwekundu."

Watu wa mjini walisaidia kukusanya kuni kwa ajili ya moto huo, hadi ukawa moto mkubwa zaidi kuwahi kutokea. Kijana Ibrahimu alinyenyekea kwenye majaaliwa aliyochaguliwa na Mola Mlezi wa walimwengu wote. Hakupoteza imani, bali jaribio hilo lilimfanya awe na nguvu zaidi. Ibrahimu hakukurupuka mbele ya kifo cha moto hata katika umri huu mdogo; badala yake maneno yake ya mwisho kabla ya kuingia humo yalikuwa,

"Mwenyezi Mungu ananitosheleza, na Yeye ndiye bora wa kusimamia mambo." (Saheeh Al-Bukhari)

Hapa tena kuna mfano wa Ibrahimu aliyethibitika kuwa mwaminifu kwa majaribu aliyoyakabili. Imani yake katika Mungu wa Kweli ilijaribiwa hapa, na alithibitisha kwamba alikuwa tayari hata kusitisha uwepo wake kwa wito wa Mungu. Imani yake ilithibitishwa na kitendo chake.

Mungu hakutaka kwamba hii iwe hatima ya Ibrahimu, kwa kuwa alikuwa na utume mkubwa mbele yake. Alipaswa kuwa baba wa baadhi ya manabii wakuu wanaojulikana kwa wanadamu. Mungu alimuokoa Ibrahimu kama ishara kwake na kwa watu wake pia.

“Sisi tukasema: 'Ewe moto! Kuwa baridi na salama kwa Ibrahim!’ Na wakataka kumtegea mtego, lakini tukawafanya wao kuwa wenye hasara zaidi.

Hivyo Ibrahimu aliuepuka moto, bila kudhurika. Walijaribu kulipiza kisasi kwa ajili ya miungu yao, lakini wao na sanamu zao mwishowe walidhalilishwa.



Rejeleo ya Maelezo:

[1] Maandiko: Uteuzi, H. Polano. (http://www.sacred-texts.com/jud/pol/index.htm).

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.