Lengo la maisha (sehemu ya 1 kati ya 3): Sababu na Ufunuo

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Je, “Mantiki” ni chanzo cha kutosha katika kutafuta madhumuni ya maisha?

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,062
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Utangulizi

The_Purpose_of_Life_(part_1_of_3)_001.jpg'Ni nini maana na lengo la maisha? ' Hili labda ni swali muhimu zaidi ambalo limewahi kuulizwa. Katika miaka yote, wanafalsafa wameona kuwa ni swali la msingi zaidi. Wanasayansi, wanahistoria, wanafalsafa, waandishi, wanasaikolojia na watu wa kawaida wote hupambana na swali hilo wakati fulani katika maisha yao.

Je, Mantiki ni Mwongozo wa Kutosha?

“Kwa nini tunakula?” “Kwa nini tunalala?” 'Kwa nini tunafanya kazi? ' Majibu tunayopata ya maswali haya yatakuwa yale yale. “Nala ili niishi.” “Nalala ili nipumzike.” 'Nafanya kazi ili nijisaidie na nisaidie familia yangu. ' Lakini linapokuja kwa suala la maana ya maisha, watu wanachanganyikiwa. Tunaona tahayuri wao katika aina ya majibu tunayopokea. Vijana wanaweza kusema, “Ninaishi kwa ajili ya pombe na usherati.” Mtaalamu mwenye umri wa kati anaweza kusema, “Ninaishi kuchanga ya kutosha ili kustaafu vizuri.” Mtu mzee anaweza kusema, “Maisha yangu yote, nimekuwa nikijiuliza kwa nini niko hapa. Ikiwa kuna lengo, sijali tena.” Na labda jibu la watu wengi litakuwa, “Kwa hakika Sijui!”

Je, basi, utagunduaje lengo la maisha? Tuna hiari mbili. Ya kwanza ni kuwacha 'mantiki ya mwanadamu'- mafanikio yaliyoadhimishwa ya enzi ya Elimu ya Kisayansi- kutuongoza. Baada ya yote,enzi hiyo ilitupatia sayansi ya kisasa kulingana na uchunguzi wa makini wa ulimwengu wa kiasili. Lakini wanafalsafa waliokuja baada ya enzi hiyo walielewa lengo hilo? Camus alielezea maisha kama “upuuzi”; Sartre alizungumzia “uchungu, kutelekezwa na kukata tamaa.” Kulingana na hao, maisha hayana maana. Wadarwini walidhani maana ya maisha ni kuzaana. Will Durant, kupambana na msiba wa mtu wa kisasa, aliandika, “Imani na matumaini yametoweka; shaka na kukata tamaa yamekuwa ada ya kila siku... si nyumba zetu na hazina zetu ndizo tupu, ni 'mioyo yetu.” Linapokuja kwa lengo la maisha, hata wanafalsafa wenye hekima wanakisia tu. Will Durant, mwanafalsafa aliyejulikana zaidi karne iliyopita, na Dk. Hugh Moorhead, profesa wa falsafa katika Chuo Kikuu cha Illinois Kaskazini, wote waliandika vitabu tofauti vilivyoitwa 'Maana ya Maisha.'[1] Waliandika kwa wanafalsafa maarufu, wanasayansi, waandishi, wanasiasa, na wasomi wa wakati wao duniani, wakiwauliza “Ni nini maana ya maisha?” Kisha walichapisha majibu yao. Wengine walitoa dhana zao , wengine walikiri kwamba walijitungia wenyewe lengo la maisha, na wengine walikuwa waaminifu kwa kusema kuwa hawakuwa na mwelekeo. Isitoshe, idadi kadhaa kati ya wasomi maarufu waliwauliza waandishi wawaandikie na kuwaambia kama lengo la maisha limegunduliwa!

Hebu Tuache mbingu “Ziseme”

Ikiwa mwanafalsafa hana jibu la uhakika, labda jibu linaweza kupatikana ndani ya moyo na akili ambayo sisi wenyewe tunamiliki. Je! Umewahi kutazama angani usiku ukiwa wazi? Utaona idadi isiyo hesabika ya nyota. Tazama darubini na utaona thurea ya nyota, nebula nzuri ambapo nyota mpya zinaundwa, mabaki ya mlipuko ya kale wa supanova yaliyoundwa katika mlipuko wa mwisho wa nyota, miviringo maridadi ya Zohali na miezi ya Mshtarii. Je, inawezekana mtu akose kuathirika na kuona nyota hizi nyingi katika anga ya usiku ikiangaza kama vumbi la almasi kwenye tandiko la mahameli nyeusi? Makundi ya nyota, yanayoendelea mpaka nyuma; yanayokuwa nzito sana kiasi kwamba yanaonekana yakiungana katika visima maridadi. Uadhama huu hutunyenyekeza, hutufurahisha, huhamasisha tamaa ya uchunguzi, na hutufanya tutafakuri. Ni jinsi gani ilikuja kuwa? Tunahusianaje na hilo, na tuna nafasi gani ndani yake? Je, tunaweza kusikia mbingu “zikizungumza” nasi?

”Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili. Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa mbingu na ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika!” (Qur'an 3:190 -191)

Tunaposoma kitabu, tunakubali kwamba kuna mwandishi. Tunapoona nyumba, tunakubali kuwa wajenzi wapo. Mambo hayo yote yalifanywa kwa kusudi na wale walioyafanya. Ubunifu, utaratibu, na utata wa ulimwengu pamoja na ulimwengu unaotuzunguka ni ushahidi wa kuwepo kwa akili kuu, mtengenezaji kamili. Sehemu zote za mbinguni zinadhibitiwa na sheria thabiti za fizikia. Je, kuna sheria bila mwanasheria? Mwanasayansi wa roketi Dr. von Braun alisema: “Sheria za kiasili za ulimwengu ni sahihi na thabiti sana kiasi kwamba hatuna shida ya kutengeneza roketi ya kupaa hadi kwa mwezi na tunaweza kuirusha na kuhesabu mwendo wake kwa kila sekunde. Lazima sheria hizi zimewekwa na mtu.” Paul Davies, profesa wa fizikia, anahitimisha kwamba kuwepo kwa mwanadamu sio tu jambo la kibahati lisilotarajiwa. Anasema: “Hakika tuliwekwa hapa.” Na anasema kuhusu ulimwengu: “Kupitia kazi zangu ya kisayansi, nimekuja kuamini zaidi na zaidi kwamba ulimwengu wa dhahiri umewekwa pamoja na ujuzi wa kushangaza sana kiasi kwamba siwezi kukubali tu kama ukweli usiopingika. Lazima, inaonekana kwangu, kuwa kuna kiwango cha kina cha maelezo.” Ulimwengu, ardhi, na vitu vilivyo hai duniani vyote vinatoa ushuhuda kwa ukimya kwa Muumba mwenye hekima, mwenye nguvu.

The_Purpose_of_Life_(part_1_of_3)_002.jpg

Kielelezo 2 Kanda ya Kati ya Nebula iliyochukuliwa na darubini ya Gemini kwenye Mauna Kea kwenye Kisiwa Kikubwa cha Hawaii, Juni 5, 2002. Iko katika kundi la Mshale, na ni nebula nzuri yenye wingu kubwa, yenye nguvu ya gesi na vumbi ambako nyota zinazaliwa. Moja ya nyota kubwa kwenye katikati ya nebula ilizaliwa takriban miaka 100,000 iliyopita. Umbali wa nebula kutoka mfumo wa Jua kwa ujumla umekubaliwa kuwa takriban kati ya miaka ya nuru 2,200 hadi 9,000.

Picha kwa hisani ya picha wa Uchunguzi Wa Gemini /Tume ya GMOS

Ikiwa tuliumbwa na Muumba, basi hakika Muumba lazima awe na sababu, kusudi, katika kutuumba. Hivyo, ni muhimu kwamba tutafute kujua kusudi la Mungu kwa kuwepo kwetu. Baada ya kufikia lengo hili, tunaweza kuchagua kama tunataka kuishi kulingana na hilo. Lakini inawezekana tujue nini kingetokea iwapo tungeachwa pekee yatu bila mawasiliano yoyote kutoka kwa Muumba? Ni kawaida kwamba Mungu mwenyewe atatujulisha kuhusu kusudi hili, hasa kama tunatarajiwa kuitimiza.

Mbadala Wa Uvumi: Muulize Mungu

Hii inatuleta kwenye chaguo la pili: mbadala wa uvumi kuhusu maana na madhumuni ya maisha ni ufunuo. Njia rahisi zaidi ya kugundua madhumuni ya uvumbuzi ni kuuliza mvumbuzi. Ili kugundua lengo la maisha yako, muulize Mungu.



Vielezi-chini:

[1] “Kuhusu Maana ya Maisha” na Will Durant. chapa: Ray Long & Richard R. Smith, Inc New York 1932 na “Maana ya Maisha” na Hugh S. Moorhead (ed.). chapa: Chicago Tathmini Press, 1988.

Mbaya Nzuri zaidi

Lengo la Maisha (sehemu ya 2 kati ya 3): Maoni ya Kiislamu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Ufafanuzi wa Uislamu kuhusiana na lengo la maisha, na mjadala mfupi juu ya maana ya ibada.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,951
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Je, Ukristo Unaweza Kujibu Swali?

Katika Ukristo, maana na lengo la maisha linategemea imani katika injili ya Yesu Kristo, katika kumkubali Yesu kama Mwokozi. “Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” Hata hivyo, pendekezo hili halikosi matatizo makubwa. Kwanza, kama hii ndiyo kusudi la uumbaji na sharti la uzima wa milele, kwa nini haikufundishwa na manabii kwa mataifa yote ya ulimwengu? Pili, Mungu angegeuka kuwa mwanadamu wakati wa Adamu wanadamu wote wangekuwa na nafasi sawa ya uzima wa milele, ila wale waliokuja kabla ya wakati wa Yesu walikuwa na lengo lingine la kuwepo kwao! Tatu, jinsi gani watu wa leo ambao hawajasikia habari za Yesu watatimiza kusudi la Kikristo la uumbaji? Kwa kawaida, kusudi na lengo hilo ni jembamba sana na linakwenda kinyume na haki ya Mungu.

Jibu

Uislamu ndio jibu la binadamu katika utafutaji wake wa maana na lengo. Kusudi la uumbaji kwa wanaume na wanawake wote kwa nyakati zote limekuwa moja: kumjua na kumwabudu Mungu.

Qurani inatufundisha kwamba kila mwanadamu amezaliwa akimfahamu Mungu,

"Na pale Mola wako Mlezi alipo waleta katika wanaadamu kutoka migongoni mwao kizazi chao, na akawashuhudisha juu ya nafsi zao, akawaambia: Je, Mimi si Mola Mlezi wenu? Wakasema: Kwani! Tumeshuhudia. Msije mkasema Siku ya Kiyama sisi tulikuwa tumeghafilika na hayo. Au mkasema: Hakika baba zetu ndio walio shirikisha kabla yetu, na sisi ni dhuriya zao tu baada yao. Basi utatuangamiza kwa sababu ya waliyo yafanya wapotovu?’"(Quran 7:172-173)

Nabii wa Uislamu anatufundisha kwamba Mungu aliumba haja hii ya kimsingi katika asili ya binadamu wakati Adamu alipoumbwa. Mwenyezi Mungu alichukua agano kutoka kwa Adamu alipo muumba. Mungu aliwaondoa wazao wote wa Adamu ambao bado hawajazaliwa, kizazi baada ya kizazi, akawatandaza, akachukua agano kutoka kwao. Akaziambia nafsi zao moja kwa moja, akiwashuhudia kwamba Yeye ndiye Mola wao Mlezi. Kwa kuwa Mungu aliwafanya wanadamu wote kuapa kwa Ubwana wake alipomuumba Adamu, kiapo hiki kinachapishwa kwenye nafsi ya binadamu hata kabla ya kuingia kwa mtoto tumboni, na hivyo mtoto anazaliwa na imani ya kiasili katika Umoja wa Mungu. Imani hii ya kiasili inaitwa fitra kwa Kiarabu. Kwa hivyo, kila mtu hubeba mbegu ya imani katika Umoja wa Mungu ambayo iko kwa undani na imezikwa chini ya matabaka ya kutoshughulikiwa na kudhoofishwa na hali ya kijamii. Ikiwa mtoto huyo angeachwa peke yake, angekua kwa ufahamu wa Mungu - Muumba mmoja - lakini watoto wote wanaathiriwa na mazingira yao. Nabii wa Mungu alisema,

"Kila mtoto amezaliwa katika hali ya 'fitra', lakini wazazi wake humfanya Myahudi au Mkristo. Ni kama vile mnyama anavyozaa watoto wa kawaida. Je! Umemwona mtoto aliyezaliwa akiwa ameshakatwa kabla hujamkata?"[1]

The_Purpose_of_Life_(part_2_of_3)_001.jpg

Kielelezo 1 Ajabu ya maisha. Mtoto aliye tumboni akinyonya kidole chake.

Kwa hivyo, kama mwili wa mtoto unavyojisalimisha kwa sheria za kimaumbile, zilizowekwa na Mungu ardhini, nafsi yake pia inajisalimisha kwa kawaida kwa ukweli kwamba Mungu ndiye Bwana na Muumba wake. Hata hivyo, wazazi wake wanamfanya afuate njia yao wenyewe, na mtoto hana uwezo wa akili wa kuipinga. Dini ambayo mtoto huifuata katika hatua hii ni ya mila na malezi, na Mwenyezi Mungu hatamuuliza kuhusu dini hii. Mtoto anapokua na kuwa mtu mzima, lazima sasa afuate dini ya elimu na sababu. Kama watu wazima, watu lazima sasa wapigane kati ya asili yao ya kumuelekea Mungu na tamaa zao ili kupata njia sahihi. Wito wa Uislamu unaelekezwa kwa hali hii ya kwanza, tabia ya kiasili, alama ya Mwenyezi Mungu juu ya nafsi, fitra, ambayo imesababisha nafsi za kila hai kukubali kuwa Yeye aliyewaumba ni Mola wao Mlezi, hata kabla ya kuundwa kwa mbingu na ardhi,

"Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi." (Quran 51:56)

Kulingana na Uislamu, kumekuwa na ujumbe wa msingi ambao Mungu ametufunulia kupitia manabii wote, tangu wakati wa Adamu hadi mwisho wa manabii, Muhammad, amani iwe juu yao. Manabii wote waliotumwa na Mungu walikuja na ujumbe huo muhimu:

"Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani...’" (Quran 16:36)

Manabii walileta jibu hilo hilo kwa swali la kutisha zaidi kwa wanadamu, jibu linalozungumzia hamu ya nafsi kwa Mungu.

Ibada ni Nini?

‘Uislamu' maana yake ni 'kujisalimisha', na kuabudu, katika Uislamu, maana yake ni 'utii kwa Mungu.’

Kila kitu kilichoumbwa 'kinajisalimisha' kwa Muumba kwa kufuata sheria za kimaumbile zilizoundwa na Mungu,

"Na vyake Yeye vilivyo mbinguni na katika ardhi. Vyote vinamt'ii Yeye." (Quran 30:26)

Wao, hata hivyo, hawapewi thawabu wala kuadhibiwa kwa 'kujisalimisha' kwao, kwa maana haihusishi hiari. Malipo na adhabu ni kwa wanao muabudu Mwenyezi Mungu, wanaokubali sheria ya kimaadili na kidini ya Mwenyezi Mungu kwa hiari yao. Ibada hiyo ndiyo kiini cha ujumbe wa manabii wote waliotumwa na Mungu kwa wanadamu. Kwa mfano, ufahamu huu wa ibada ulionyeshwa kinagaubaga na Yesu Kristo,

"Si kila mtu anayesema, ‘Bwana, Bwana,’ ambaye ataingia katika Ufalme wa mbinguni ila ni wale wanaofanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni."

‘Anachotaka Mungu' inamaanisha 'kile Mungu anataka wanadamu wafanye. 'Anavyovitaka Mungu' vinapatikana katika sheria zilizofunuliwa na Mungu ambazo manabii waliwafundisha wafuasi wao. Kwa hivyo, utii wa sheria ya Mungu ni msingi wa ibada. Ni wakati tu binadamu anapomwabudu Mungu wake kwa kujisalimisha kwa sheria Yake ya kidini ndipo anaweza kuwa na amani na maelewano katika maisha yake na matumaini ya kuingia peponi, kama vile ulimwengu unavyoendana kwa umoja kwa kujisalimisha kwa sheria za kimaumbile zilizowekwa na Mola Mlezi. Unapoondoa tumaini la kuingia mbinguni, unaondoa thamani na madhumuni ya maisha. Vinginevyo, kuna tofauti gani muhimu kama tunaishi maisha mema au mabaya? Hatima ya kila mtu itakuwa ni moja tu..



Vielezi-chini:

[1] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim. Waarabu wangekata masikio ya ngamia na wanyama wengine kama ibada kwa miungu yao katika nyakati za kabla ya Uislamu.

Mbaya Nzuri zaidi

Lengo la Maisha (Sehemu ya 3 ya 3): Miungu ya Uongo ya Kisasa

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jamii ya kisasa imeunda miungu ya uongo ambayo huitumikia, na hivyo kutupa ulimwengu katika hali ya sintofahamu.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,796
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Nani Anahitaji Ibada?

Mungu hana haja na ibada yetu, ni wanadamu wanaohitaji kumwabudu Mungu. Kama hakungekuwa na mtu anayemwabudu Mungu, haingeondoa kwa utukufu Wake kwa njia yoyote, na kama wanadamu wote wangemwabudu Yeye, haingeongeza kwa utukufu Wake. Ni sisi tulio na haja na Mungu:

"Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti." (Quran 51:57-58)

"…Na Mwenyezi Mungu si mhitaji, na nyinyi ndio wahitaji...." (Quran 47:38)

Jinsi ya Kumwabudu Mungu: Na Kwa Nini

Mungu anaabudiwa kwa kutii sheria alizozifunua kupitia manabii. Kwa mfano, katika Biblia, Nabii Yesu alifanya utiifu kwa sheria za Mungu kuwa ufunguo wa paradiso:

"kama unataka kuingia uzimani, tii amri." (Matayo 19:17).

Pia Nabii Yesu anaripotiwa katika Biblia kuwa amesisitiza juu ya utiifu mkali kwa amri, akisema:

"Basi, yeyote atakayevunja hata amri moja ndogo kuliko zote, na kuwafundisha wengine wafanye hivyo, huyo atakuwa mdogo kabisa katika Ufalme wa mbiguni. Lakini yule atakayezishika na kuwafundisha wengine, huyo atakuwa mkubwa katika Ufalme wa mbinguni." (Matthew 5:19)

Kwa nini binadamu wanahitaji kumwabudu Mungu kwa kutii sheria zilizofunuliwa na Mungu? Jibu ni rahisi. Utiifu kwa sheria tukufu huleta amani katika maisha haya na wokovu katika maisha ijayo.

Sheria za Kimungu huwapa wanadamu kanuni wazi ya kuongoza kila nyanja ya maisha ya binadamu na mwingiliano wao. Kwa kuwa Muumba peke yake anajua zaidi yaliyo bora kwa uumbaji Wake, Sheria Zake zinalinda nafsi ya binadamu, mwili, na jamii kutokana na madhara. Ili binadamu watimize kusudi lao la uumbaji, ni lazima wamwabudu Mungu kwa kutii amri Zake.

Miungu ya Uongo ya Kisasa

Mwenyezi Mungu ndiye anayeyapa maana na mwelekeo kwa maisha. Kwa upande mwingine, maisha ya kisasa hayana kituo kimoja, mwelekeo mmoja, lengo moja, kusudi moja. Hayana kanuni moja au mwongozo..

Kwa kuwa Uislamu unaamini Mungu huabudiwa kutokana na upendo, heshima ya kina, na kutarajia thawabu, mtu anaweza kusema kwamba dunia ya kisasa hutumikia miungu mingi. Miungu ya kisasa huyapa maana na mazingira kwa maisha ya mtu wa kisasa.

Tunaishi katika nyumba ya lugha, na maneno yetu ni madirisha ambayo tunaangalia ulimwengu kupitia kwayo. Mageuzi, utaifa, uke, ujamaa, Umaksi, na, kulingana na jinsi wanavyoajiriwa, demokrasia, uhuru, na usawa zinaweza kuorodheshwa kati ya itikadi zisizoweza kuelezwa za nyakati za kisasa. “Maneno ya plastiki,” kwa kukopa maneno ya Uwe Poerksen, mwanaisimu Mjerumani, yametumika kunyakua nguvu na mamlaka ya Mungu ili kuunda na kufafanua lengo la jamii, au hata la ubinadamu wenyewe. Maneno haya yanaleta ufahamu na hisia ya 'kujisikia vizuri'. Maneno yasiyotambulika yanakuwa na ubora usio na kikomo. Kwa kufanya ubora wao usiwe na kikomo, mahitaji yasiyoisha yanaamshwa, na mahitaji hayo yanapofufuliwa, yanaonekana kuwa 'dhahiri.'

Kwa kuwa ni rahisi kuanguka katika tabia ya kuabudu miungu ya uongo, watu hawana ulinzi dhidi ya wingi wa miungu ambayo njia za kisasa za kufikiri zinahitaji kutumikiwa. “Maneno ya plastiki” huwapa nguvu kubwa wale 'manabii' wanaoyazungumzia, kwa sababu wanasema kwa jina la ukweli 'dhahiri', hivyo watu wengine wananyamaza. Lazima tufuate mamlaka yao; wataalamu wa udhahiri wanaoweka sheria kwa ajili ya afya yetu, ustawi, na elimu.

Dirisha la kisasa ambalo kwa kulipitia tunaona ukweli leo limevunjika na lina uchafu na sehemu zisizoonekana, na vichujio. Linaziba ukweli. Na ukweli ni kwamba watu hawana haja ya kimsingi isipokuwa kwa Mungu. Lakini siku hizi, hizi 'sanamu' tupu zimekuwa vitu vya ibada kwa watu, kama vile Qurani inasema:

" Je! Umemwona aliye fanya matamanio yake kuwa ndiye mungu wake?..."(Quran 45:23)

Kila moja ya “maneno ya plastiki” haya hufanya maneno mengine kuonekana kuwa ya kale. 'Waumini' wa sanamu za kisasa wanajivunia kuabudu miungu hii; marafiki na wenzao wanawaona kuwa wataalamu kwa kufanya hivyo. Wale ambao bado wanasisitiza kushikilia Mungu “wa kale” wanaweza kuficha aibu ya kufanya hivyo kwa kuabudu miungu ya kisasa pamoja naye. Kwa hakika, watu wengi ambao wanadai kuabudu Mungu “wa zamani” watapotosha mafundisho yake katika tukio hili, ili Yeye pia anaonekana anatuambia tuyatumikie “maneno haya ya plastiki.”

Ibada ya miungu ya uongo inahusisha uharibifu sio tu wa watu binafsi na jamii, bali pia wa maumbile ya ulimwengu. Watu wanapokataa kumtumikia na kumwabudu Mungu kama alivyowaagiza wamtumikie, hawawezi kutimiza wajibu aliowaumbia. Matokeo yake ni kwamba ulimwengu wetu unakuwa na machafuko zaidi, kama vile Qurani inatuambia:

" Ufisadi umedhihiri bara na baharini kwa iliyo yafanya mikono ya watu." (Quran 30:41)

Jibu la Uislamu kwa lengo na kusudi la maisha linatimiza mahitaji ya kimsingi ya binadamu: kurudi kwa Mungu. Hata hivyo, kila mtu anarudi kwa Mungu kiholela, hivyo swali sio kurudi tu, lakini jinsi mtu anavyorudi. Je! Itakuwa katika minyororo yenye fedheha na adhabu, au kwa unyenyekevu wa kushukuru kwa aliyo ahidi Mwenyezi Mungu? Ikiwa unangojea ya pili, basi kwa njia ya Qur'ani na mafundisho ya Mtume Muhammad, Mwenyezi Mungu huwaongoza watu kurudi kwake kwa namna ambayo itahakikisha furaha yao ya milele.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.