Статьи / видео вы запросили еще не существует.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Статьи / видео вы запросили еще не существует.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Malaika ni viumbe walioumbwa na Mungu, kutokana na nuru. Hawana uwezo wa kutokumtii Mungu na hutekeleza majukumu waliyoamriwa bila shaka au kusita. Waislamu hupata uwelewa wa malaika kutoka kwenye Kurani na mila zilizothibitishwa za Mtume Muhammad. Katika sehemu ya kwanza tuligundua kuwa malaika ni viumbe wazuri wenye mabawa, ambao huwa kulingana na ukubwa mbali mbali na kwa idhini ya Mungu, wanaweza kubadilisha maumbo yao. Malaika wana majina na majukumu wanayotakiwa kutekelezwa.
Jina linalojulikana zaidi kwa Waislamu na wasio Waislamu ni Jibrili. Malaika Jibrili anatajwa katika jamii zote za Kiyahudi na Kikristo kama malaika mkuu na mjumbe wa Mungu, na yeye[1] anashikilia hadhi kubwa katika dini zote tatu zinazoamini mungu mmoja.
“ Kwamba hakika hii ni kauli (ya Kurani imeletwa na) Mjumbe Mtukufu,(Gabriel), kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa Mtume Muhammad. Mwenye nguvu na cheo kwa (Mungu) Mwenye Enzi,. Anayetiiwa (na malaika), na muaminifu. ” (Kurani 81:19-21)
Jibrili ameleta maneno ya Mungu – Kurani – kwa Mtume Muhammad.
“... Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Kurani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini. ”. (Kurani 2:97)
Michael (Mikaeel) ndiye malaika anayehusika na mvua na Israfeel ndiye malaika ambaye atapiga tarumbeta Siku ya hukumu. Malaika hawa watatu wapo katika safu ya malaika wakubwa kwa sababu ya umuhimu mkubwa wa majukumu yao. Kila moja ya majukumu yao hushughulika na hali ya maisha. Malaika Gabrieli alileta Kurani kutoka kwa Mungu kwenda kwa Nabii Muhammad, na Kurani inalisha moyo na roho. Malaika Michael anahusika na mvua, na inalisha dunia na pia kusafisha miili yetu, Malaika Israfeel anahusika na kupiga tarumbeta na inaashiria mwanzo wa maisha ya milele, iwe Peponi au Jehanamu.
Pindi Mtume Muhammad alipoamka usiku kuomba angeanza maombi yake kwa maneno, “Ee Mungu, Mola wa Jibreeli, Mikaeel na Israfeel, Muumba wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa mambo ya yaliyojificha na yanayoonekana. Wewe ndiye Jaji wa mambo ambayo watumwa wako wanatofautiana. Niongoze kwa hoja za Ukweli kwa idhini Yako, kwa maana Wewe humwongoza yule Umtakaye kwenye Njia Iliyo Nyooka.”[2]
Tunajua pia majina ya malaika wengine kadhaa. "Malik, ndiye malaika anayejulikana kama mlinzi wa lango la motoni. "Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako!’. . .” (Kurani 43:77) Munkar na Nakeer ni malaika wanaohusika na kuhoji watu katika makaburi yao. Tunajua majina haya na tunaelewa kuwa tutaulizwa na malaika kaburini kama inavyotajwa katika mila ya Mtume Muhammad.
“Wakati marehemu anazikwa, wanakuja malaika wawili wenye rangi ya bluu-nyeusi, mmoja wao anaitwa Munkar na mwingine Nakeer. Wanamuuliza, "Ulikuwa unasema nini juu ya mtu huyu?" Na anasema kile alichokuwa akisema: "Yeye ni mtumwa na Mjumbe wa Mungu. Nashuhudia kwamba hakuna mungu ila Mungu na kwamba Muhammad ndiye mtumwa na Mjumbe wa Mungu. Wanasema, ‘Tulijua kabla ya hapo kuwa ulikuwa ukisema haya.’ Kisha kaburi lake litapanuliwa kwake kwa ukubwa wa dhiraa sabini na dhiraa sabini na atamulikwa. Halafu wanamwambia, ‘Lala.’ Anasema, ‘Rudi kwa familia yangu uwaambie.’ Wanamwambia, ‘Lala kama bwana harusi ambaye hakuna mtu atakayemuamsha isipokuwa mpendwa wake,’ mpaka Mungu atakapo mwinua....”[3]
Katika Kurani tunapata hadithi ya malaika wawili walioitwa Haroot na Maroot, ambao walitumwa Babeli kuwafundisha watu uchawi. Matumizi ya uchawi hayaruhusiwi katika Uislamu lakini malaika hawa walitumwa kama mtihani kwa watu. Kabla ya kufunua au kufundisha uchawi Haroot na Maroot waliwaonya wazi wakazi wa Babeli kwamba walitumwa kama jaribio, na kwamba wanunuzi wa uchawi hawatakuwa na sehemu yoyote katika maisha ya baadaye, yaani wataenda kuzimu.(Kurani 2:102)
Ingawa wakati mwingine hufikiriwa kuwa Malaika wa Kifo anaitwa Azraeel, hakuna chochote katika Kurani au mila halisi ya Nabii Muhammad inayoonyesha hili. Hatujui jina la Malaika wa Kifo lakini tunajua wajibu wake na kwamba ana wasaidizi.
“Sema: Atakufisheni Malaika wa mauti aliye wakilishwa juu yenu; kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu Mlezi.” (Kurani 32:11)
mpaka mmoja wenu yakimjia mauti wajumbe wetu humfisha, nao hawafanyi taksiri.Kisha watarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, Mola wao wa Haki. ” (Kurani 6:61-62)
Kuna kundi la Malaika wanaosafiri ulimwenguni kote, wakitafuta watu wanaomkumbuka Mungu. Kutoka kwenye mila ya Mtume Muhammad tunajua kuwa, “Mungu ana malaika ambao hutembea katika barabara kuu kutafuta watu wa ukumbusho. Wanapopata watu wanaomkumbuka Mungu, wanaitatana , "Njoo kwa kile unachokuwa na njaa nacho na kuwafunika kwa mabawa yao, wakinyoosha hata mbingu ya chini kabisa. Basi Mola wao akauliza, na anajua zaidi yao, "Je! Watumwa wangu wanasema nini?" Wanasema: "Wanakutukuza, wanakutukuza, wanakuhimidi na kukusifu." Anauliza, "Je! Wameniona mimi?" Wanasema, "Hapana, na Mungu, hawajakuona." Anauliza, "Je! Ingekuwaje wakiniona?" Wanasema, "Wangekuwa wenye bidii zaidi na kujitolea katika sifa na ibada yao." Anauliza, "Wananiomba nini?" Wanasema, "Wanakuomba Pepo." Anauliza, "Na wameiona?" Wanasema, "Hapana, Mungu, Ee Mola, hawajaiona." Anauliza, "Na itakuwaje ikiwa wangeiona?" Wanasema: "Wangekuwa na hamu kubwa zaidi na wangekuomba kwa bidii zaidi." Anauliza, "Na wanaomba ulinzi Wangu kutokana na nini?" Wanasema, "Kutoka kwa Moto wa Jehanamu." Anauliza, "Je! Wameiona?" Wanasema, "Hapana, na Mungu, hawajaiona." Anauliza, "Na itakuwaje ikiwa wangeiona?" Wanasema: "Wangeogopa zaidi na wanahangaika kuukimbia." Mungu anasema: "Ninyi ni mashahidi Wangu kwamba nimewasamehe." Mmoja wa malaika anasema: "flani na flani siyo mmoja wao; alikuja (kwenye mkutano huo) kwa sababu zingine. ” Mwenyezi Mungu anasema, "Wote waliokuwa kwenye mkusanyiko huo, na mmoja wao hataondolewa (kwenye msamaha).”[4]
Waislamu wanaamini kuwa malaika wana majukumu maalum ya kufanya yanayowahusu wanadamu. Wanawalinda na kuwahifadhi, na malaika wawili wanaandika matendo mema na mabaya. Wanashuhudia sala na moja inawajibika hata kwa watoto waliomo ndani ya tumbo. Katika sehemu ya tatu tutaingia kwa undani zaidi na kuelezea ushirika kati ya malaika na wanadamu.
[1] Matumizi ya neno yeye ni kwasababu ya urahisi wa kisarufi na haimaanishi kuwa malaika ni wanaume.
[2] Saheeh Muslim
[3] Sunan kwenye Tirmidhi. Abu Isa amesema:ni ghareeb hasan hadeeth. imehukumiwa na hasan ndani ya Saheeh al-Jaami’, nambari. 724.
[4] Saheeh Al-Bukhari
Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.
Orodha yako ya historia ipo tupu.
Kwa nini kujiandikisha? Tovuti hii ina miundo kadhaa uliyoundwa mahsusi kwa ajili yako, kama vile: vipendwa vyako, historia yako, kutia alama makala ambazo umezitazama awali, kuorodhesha makala zilizochapishwa tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho, kubadilisha ukubwa wa herufi, na zaidi. Vipengele hivi vinatokana na vidakuzi na vitafanya kazi ipasavyo tu unapotumia kompyuta ile ile. Ili kuwezesha vipengele hivi kutoka kwa kompyuta yoyote, unapaswa kuingia wakati katika tovuti hii.
Tafadhali ingiza Jina lako la mtumiaji na anwani ya barua pepe kisha ubofye kitufe cha Tuma neno la siri. Utapokea neno la siri jipya hivi karibuni. Tumia neno la siri hili jipya kufikia tovuti.
Ongeza maoni