Wasomi wa Kikristo Wanajua Ukinzani katika Biblia (sehemu ya 6 kati ya 7): Kuendelea Kuchezea Maandiko ya Biblia

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mifano zaidi ya kuchezea Biblia

  • Na Misha’al ibn Abdullah (taken from the Book: What Did Jesus Really Say?)
  • Iliyochapishwa mnamo 19 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 6,307 (wastani wa kila siku: 8)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Dkt. Lobegott Friedrich Konstantin Von Tischendorf alikuwa mmoja wa Wasomi mashuhuri wa Kibiblia katika karne ya kumi na tisa. Alikuwa pia mmoja wa watetezi wakubwa, wenye msimamo mkali wa "Utatu" ambao historia tunayoijua. Mojawapo ya mafanikio makubwa maishani mwake ni kupatikana kwa Maandiko ya zamani kabisa ya Kibiblia yanayojulikana kwa wanadamu, "Codex Sinaiticus," Kuanzia Monasteri ya Mtakatifu Catherine huko Mlima Sinai. Moja ya uvumbuzi mbaya zaidi uliofanywa kutoka kwenye kusoma maandiko haya ya karne ya nne ilikuwa kwamba Injili ya Marko mwanzoni iliishia kwenye mistari ya 16: 8 na sio kwenye aya ya 16:20 kama inavyofanywa leo. Kwa maneno mengine, aya 12 za mwisho (Marko 16: 9 hadi Marko 16:20) "ziliingizwa" na kanisa ndani ya Biblia wakati fulani baada ya karne ya 4. Clement wa Alexandria na Origen hakuwahi kunukuu mistari hii. Baadaye, iligundulika pia aya 12 zilizosemwa, ambazo kuna hadithi ya "ufufuo wa Yesu," hazimo katika kodeki za Syriacus, Vaticanus, na Bobiensis. Hapo awali, "Injili ya Marko" haikutaja juu ya "ufufuo wa Yesu" (Marko 16: 9-20). Angalau miaka mia nne (ikiwa sio zaidi) baada ya kuondoka kwa Yesu, Kanisa lilipokea "mwongozo" wa kimungu kuongeza hadithi ya ufufuo hadi mwisho wa Injili hii.

Mwandishi wa "Codex Sinaiticus" hakuwa na shaka kuwa Injili ya Marko ilimalizika kwenye Marko 16: 8, ili kusisitiza jambo hili tunaona kwamba mara tu baada ya kufuatia aya hii anaimaliza maandishi kwa sanaa yake kwa maneno "Injili kulingana na Marko." Tischendorf alikuwa Mkristo mwenye msimamo mkali na kwa hivyo aliweza kupuuza tofauti hii kwasababu kwa kadirio lake ukweli kwamba Marko hakuwa Mtume, wala shahidi wa macho katika utawala wa Yesu, alikuwa wa pili kwa wale wa Mitume kama Mathayo na Yohana. Ila, kama inavyoonekana mahali pengine katika Kitabu hiki, wasomi wengi wa Kikristo leo wanatambua maandishi ya Paulo kuwa maandishi ya zamani zaidi ya Biblia.Hii inafuatana kwa karibu na "Injili ya Marko" na "Injili za Mathayo na Luka" zinatambuliwa kote ulimwenguni kuwa zilitegemea "Injili ya Marko." Ugunduzi huu ulikuwa ni matokeo ya karne nyingi za masomo ya kina na umakini kwa wasomi wa Kikristo na maelezo hayawezi kurudiwa hapa. Inatosha kusema kwamba wasomi wengi Wakristo wanaojulikana leo wanatambua hili kama ukweli wa msingi usiopingika.

Leo, watafsiri na wachapishaji wa Bibilia zetu za kisasa wameanza kuwa wa wazi zaidi na waaminifu kwa wasomaji wao. Ingawa hawawezi kukubali wazi wazi kwamba aya hizi kumi na mbili zilikuwa za kughushi kwa Kanisa na sio neno la Mungu, bado, angalau zinaanza kuvuta umakini wa wasomaji kwa ukweli kwamba kuna "matoleo" mawili ya "Injili ya Marko ”na kisha mwache msomaji aamue afanye nini juu ya "matoleo" haya mawili.

Sasa swali linakuwa "ikiwa Kanisa limevuruga Injili ya Marko, je waliachia hapo, au kuna hadithi zaidi ya hii?. Kama inavyotokea, Tischendorf pia aligundua kwamba "Injili ya Yohana" imebadilishwa sana na Kanisa kwa miaka mingi. Kwa mfano,

1.Ilibainika kuwa aya zinazoanzia Yohana 7:53 hadi 8:11 (hadithi ya mwanamke aliyechukuliwa katika uzinzi) hazipatikani katika nakala za zamani zaidi za Biblia kama zinavyo patikana kwenye Ukristo leo, hususani, kodeki za Sinaiticus au Vaticanus .

2.Ilibainika pia Yohana 21:25 ilikuwa imeingizwa , na kuwa aya kutoka kwenye injili ya Luka (24:12) ambayo inazungumza juu ya Petro kugundua kaburi tupu la Yesu haipatikani katika maandiko ya zamani.

(Kwa habari zaidi juu ya mada hii tafadhali soma ‘Secrets of Mount Sinai’ na James Bentley, Doubleday, NY, 1985).

Ugunduzi mwingi wa Dkt Tischendorf kuhusu kuendelea na kuchezewa kwa maandishi ya Bibilia kwa miaka yote kumethibitishwa na sayansi ya karne ya ishirini. Kwa mfano, uchunguzi wa Codex Sinaiticus chini ya mwangaza wa ultraviolet umegundua kuwa "Injili ya Yohana" mwanzoni iliishia kwenye aya ya 21:24 na ikifuatiwa na kipande kidogo na kisha maneno "Injili kulingana na Yohana." Ila, muda mwingine, mtu tofauti "aliyeongozwa" alichukua kalamu mkononi, akafuta maandishi yaliyofuata ya mstari wa 24, na kisha akaongeza katika maandishi "yaliyoongozwa" ya Yohana 21:25 ambayo tunayapata katika Biblia zetu za leo.

Ushahidi wa kuchezea hunaendelea na kuendelea. Kwa mfano, katika Codex Sinaiticus, "sala ya bwana" ya Luka 11: 2-4 inatofautiana kwa kiasi kikubwa na toleo ambalo limetufikia kupitia wakala wa karne ya marekebisho "yaliyoongozwa". Luka 11: 2-4 katika maandiko haya ya zamani zaidi ya maandiko yote ya Kikristo inasoma:

“Baba, uliyetakaswa kwa jina lako, Ufalme wako ufike. Mapenzi yako yatimizwe, kama mbinguni, vivyo hivyo duniani. Utupe kila siku mkate wetu wa kila siku. Utusamehe dhambi zetu, kama sisi pia tunavyowasamehe watu waliotukosea. Wala usitutie majaribuni.”

Pia, “Codex Vaticanus,” ni andiko lingine la zamani lililoshikiliwa na wasomi wa Ukristo katika msimamo uleule wa heshima kama Codex Sinaiticus. maandiko haya mawili ya karne ya nne yamehesabiwa kuwa nakala za zamani zaidi za Biblia zinazopatikana leo. Katika codex Vaticanus, tunaweza kupata toleo la Luka 11: 2-4 tenafupi kuliko lile la Codex Sinaiticus. Katika toleo hili hata maneno "Mapenzi yako yatimizwe, kama mbinguni, vivyo hivyo duniani." hayapatikani.

Sasa, nini msimamo rasmi wa Kanisa kuhusu "tofauti" hizi? Je! Kanisa liliamuaje kushughulikia hali hii? Je! Waliwaita wasomi wote wa kwanza wa fasihi ya Kikristo kuja kwa pamoja katika mkutano wa misa ili kusoma kwa pamoja maandiko ya zamani zaidi ya Kikristo yanayopatikana kanisani na kufikia makubaliano ya pamoja juu ya neno la kweli la asili la Mungu ni lipi? Hapana!

Sasa basi, je! waliweka juhudi zote kutengeneza nakala nyingi za maandishi ya asili na kuyapeleka kwenye ulimwengu wa Kikristo ili waweze kufanya maamuzi yao wenyewe juu ya neno la Mungu la awali ambalo halijabadilika? Kwa mara nyingine tena, Hapana!

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.