Jason Cruz, Kasisi wa Zamani, Marekani

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Akitangatanga katika dini, kasisi wa Marekani anaukubali Uislamu.

  • Na Jason Cruz
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,435 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Alhumdulillah (Asante Mungu), nimebarikiwa na Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya Uislamu tangu mwaka 2006. Nilipoombwa niandike kuhusu njia niliyoipitia na jinsi Mwenyezi Mungu alivyonibariki, nilisitasita. Nimeona wengine wakinaswa na umaarufu wa kibinafsi kwa kusimulia jinsi walivyokuja kwenye Uislamu na nilijua kuwa sikutaka kuwa na changamoto kama hiyo.

Ninakuomba uichukulie hadithi hii kuwa ni kazi ya Allah na uzingatie rehema na ukuu wake badala ya kuwa hadithi yangu tu, insha Allah. Hakuna anayekuja kwenye Uislamu bila ya rehema ya Mwenyezi Mungu na ni kazi yake sio ya urejeo ndiyo yenye umuhimu.

Nilizaliwa katika familia iliyojiita kuwa ni ya Kikaoliki ya roma huko Kaskazini mwa New York. Nilikuwa na mama Mkatoliki na baba Mpresbiteri ambaye aliingia Ukatoliki ili aowe.

Tulihudhuria kanisani siku za Jumapili na nilipitia katekisimu, komuniyo ya kwanza, na hatimaye kipaimara ndani ya Kanisa Katoliki la Roma. Nilipokuwa mdogo nilianza kuhisi wito kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Wito huu niliufasiri kama wito kwa ukuhani wa Kikatoliki wa Roma na nikamwambia mama yangu hivyo. Alifurahishwa na jambo hilo, alinipeleka kukutana na kasisi katika parokia yetu.

Kwa bahati nzuri au mbaya, kasisi huyu hakufurahishwa na wito wake na akanishauri nijiepushe na ukuhani. Hili lilinikasirisha na hata leo, sijui jinsi gani mambo yangekuwa tofauti ikiwa majibu yake yangekuwa mazuri zaidi.

Kutokana na ule mswada wa awali wa wito wa Mwenyezi Mungu, na kutokana na upumbavu wangu mwenyewe na katika miaka yangu ya ujana, nilienda njia nyingine. Familia yangu ilisambaratika nikiwa na umri mdogo wa miaka saba na niliteseka kwa kumkosa baba baada ya talaka.

Kuanzia umri mdogo wa miaka 15, nilianza kupendezwa zaidi na vilabu vya usiku na pati kuliko Mola wa Ulimwengu. Nilikuwa na ndoto ya kuwa wakili, kisha mwanasiasa mwenye jumba la kifahari huko Manhattan ili niweze kushiriki katika mtindo wa maisha ya kimtindo.

Baada ya kuhitimu kwa heshima, kutoka shule yangu ya upili, nilienda chuo kikuu kwa muda mfupi. Lakini mtazamo wangu binafsi uliopotoka ulinipelekea kuacha chuo kikuu na kuhamia Arizona (ambako ninaendelea kuishi hadi sasa) badala ya kupata digrii yangu.

Hili ni jambo ambalo najutia hadi leo. Wakati flani huko Arizona, hali yangu ilizidi kuwa mbaya zaidi. Nilikutana na umati mbaya zaidi kuliko niliokuwa nao nyumbani na nikaanza kutumia dawa za kulevya. Kwa sababu ya kukosa elimu, nilifanya kazi za hali ya chini na niliendelea kutumia wakati wangu katika dawa za kulevya, uasherati, na vilabu vya usiku.

Katika kipindi hiki, nilikutana kwa mara ya kwanza na Muislam. Alikuwa mwanamume ambaye alikuwa akisoma chuo cha ndani akiwa mwanafunzi wa kigeni. Alikuwa akichumbiana na rafiki yangu mmoja na mara nyingi aliandamana nasi kwenye vilabu vya usiku na karamu nyinginezo tulizohudhuria. Sikujadili Uislamu naye bali nilimhoji kuhusu utamaduni wake ambao aliuonyesha kwa uhuru. Uislamu haukuja. Tena nashangaa mambo yangekuwa tofauti kama angekuwa Muislamu wa vitendo.

Mtindo wangu mbaya wa maisha uliendelea kwa miaka kadhaa na sitaueleza kiundani sana. Nilikuwa na majeraha mengi, watu ambao niliwajua walikufa, nilichomwa visu na kujeruhiwa kwa njia nyingine lakini hii sio hadithi ya hatari ya dawa za kulevya.

Naitaja tu kueleza kuwa popote ulipo, Mwenyezi Mungu anaweza kukurudisha kutoka humo inshaa Allah. Nitaipeleka mbele hadi nilipokuwa msafi kutoka kwenye dawa za kulevya. Sehemu ya mchakato wa kuondokana na madawa ya kulevya ni kuanzisha uhusiano na "nguvu ya juu".

Kwa wengi, huyu ni Mungu na au misemo mengine ya uungu. Kwa muda mrefu nilikuwa nimepoteza uhusiano wangu na Mwenyezi Mungu hivyo nikaenda kutafuta uwezo wangu wa juu zaidi. Kwa kusikitisha, sikupata ukweli mwanzoni. Badala yake, nilienda kwenye Dini ya Uhindu, ambayo ilinivutia kwa sababu ya maelezo hayo ya kwa nini mateso yalikuwa yamenipata.

Niliingia ndani kabisa, hata nikabadilisha jina langu kuwa la Kihindu. Ilitosha kuniweka mbali na dawa za kulevya na kuyapeleka maisha yangu katika mwelekeo mzuri zaidi, ambao ninashukuru. Hatimaye, ingawa nilianza tena kuhisi mvutano kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Hilo lilianza kunionyesha kwamba kwangu, Uhindu haukuwa njia ya kweli.

Mwenyezi Mungu aliendelea kunidunga sindano hadi nilipoacha Uhindu na nikaanza kurudi kwenye Ukristo. Nililifata Kanisa Katoliki la Roma ili niwe kasisi, kwa kuwa hilo ndilo nililohisi Mwenyezi Mungu alikuwa akiniita, nao wakanipa elimu na wadhifa katika nyumba ya watawa huko New Mexico. Kufikia wakati huu familia yangu (mama, kaka, na dada) ilikuwa imehamia Arizona na nilikuwa na uhusiano wa karibu na marafiki wengi.

Bila kusema, sikuwa tayari. Badala yake, nilipata kanisa katoliki linalojitegemea ambalo ningeweza kusoma kupitia programu yao ya seminari kutoka nyumbani na kutawazwa na kupangiwa sehemu nilipokuwa nikiishi. Kanisa hili la Kikatoliki linalojitegemea pia lilinivutia mawazo yangu ya kiliberali ambayo nilikuwa ninayo katika miaka yangu mabaya. Nilihudhuria programu yao ya seminari na mwaka 2005 nikapewa ukasisi.

Huduma yangu ya kwanza katika jukumu langu jipya ilikuwa mahusiano ya dini mbalimbali. Kazi yangu ilikuwa kutembelea na kujifunza kuhusu mila tofauti za imani katika eneo la Phoenix Metro na kushirikiana nao ujumbe wa imani na maelewano kutoka kwenye kanisa langu.

Tamaduni nyingi za Kikristo nilikuwa tayari nimezisoma na kuzijua. Niliendelea kwenye uyahudi na dini nyinginezo za Mashariki ya Mbali. Nilikuwa yule anayejulikana kama kasisi mfanyakazi, ambayo ina maana kwamba nilikuwa na kazi wakati huo huo nilipokuwa nikifanya huduma yangu. Nilikuwa nimebadilika kutoka kufanya kazi katika shirika la Marekani hadi kufanya kazi katika wakala wa afya ya kitabia.

Kazi yangu ilikuwa chini ya barabara kutoka Masjid. Nilifikiria kuwa hii ilikuwa nafasi yangu ya kujifunza kuhusu Uislamu kwa ajili ya mahusiano yangu na dini mbalimbali. Nilienda msikitini na kukutana na ndugu wengine wazuri sana ambao walinielekeza kwenye msikiti, Arizona.

Pia nilianza kusoma kuhusu Uislamu kwa kujitegemea na nilishtushwa na jinsi nilivyoguswa na nilichokuwa nikisoma. Mwenyezi Mungu alikuwa na mimi sasa lakini nilikuwa bado sijajua. Nilikwenda kwenye msikiti wa Tempe na nilikutana na mwalimu mzuri katika umbo la Ahmad Al Akoum.

Kk. Al Akoum, ambaye ni mkurugenzi wa eneo wa Jumuiya ya Waislamu wa Marekani, alikuwa na utangulizi wa darasa la Uislamu lililofunguliwa kwa watu wa dini zote ambapo nilianza kuhudhuria. Nilipokuwa nikihudhuria darasa hili, nilianza kuona kwamba Uislamu ndio ukweli. Ilikuwa ni muda mfupi tu baadaye nilipotoa Shahadah kwenye msikiti wa Tempe pamoja na Sheikh Ahmed Shqeirat. Wote wawili Kk. Al Akoum na Sheikh Shqeirat ni watu wakubwa na bila wao, nisingekuwa na raha ya kuja katika Uislamu. Nililiacha kanisa na nimekuwa Muislamu tangu muda huo, Alhumdulillah.

Maisha yangu yamebadilika sana na kuwa bora tangu nisilimu. Mwanzoni, familia yangu ilihuzunika kuwa niliacha ukuhani na sikuelewa, hata kuogopa, Uislamu. Lakini kwa vile njia yangu ya kuingiliana nao, kulingana na kuongezeka kwa furaha yangu na kujitahidi kwangu kushikamana na Quran na Sunnah, imebadilika, wameona kwamba ni jambo zuri.

Kk. Al Akoum alijua kuwa mwaka wa kwanza ndio mgumu zaidi kwa waliosilimu. Ili kupunguza mawazo yake, alihakikisha kwamba nilijumuishwa katika shughuli nyingi za jumuiya na kukutana na ndugu wengi wazuri. Ni kwa kuwasiliana tu na Waislamu wengine ndipo kutamfanikisha anayesilimu.

Akiachwa peke yake, kunaweza kuwa kubaya na imani yao inaweza kuteleza, kwa hivyo ikiwa unawajua waliosilimu, tafadhali watembelee angalau mara moja kila baada ya siku tatu. Nimesonga mbele zaidi katika kazi yangu kwa sababu ya msingi wangu mpya kama Muislamu. Nikawa meneja wa programu inayolenga kuzuia matumizi mabaya ya pombe na dawa za kulevya, VVU, na Homa ya Ini kwa watu walio katika hatari.

Nimekuwa mtu wa kujitolea sio tu katika Jumuiya ya Waislamu wa Marekani lakini pia Kituo cha Vijana cha Waislamu cha Arizona na sehemu zingine za Waislamu. Hivi majuzi nimeteuliwa kwenye bodi ya msikiti wa Tempe ambapo niliitamka shahadah kwa mara ya kwanza. Alhumdulillah pia imebainisha nani ni marafiki zangu wa kweli dhidi ya wale wasiokuwa.

Nina marafiki wachache wasio Waislamu sasa kwa vile siwezi kushirikiana nao katika shughuli wanazochagua kufanya kwa ajili ya kujifurahisha lakini nimekuza urafiki wa thamani na ndugu Waislamu ambao ni bora kuliko kitu chochote nilichokuwa nacho hapo awali. Inshaallah kama Allah akinipenda, natamani kwenda kusoma Fiqh ili kuendeleza uislamu na kuunufaisha Ummah niupendao. Yote haya yalikuwa kwa neema ya Mwenyezi Mungu na makosa tu ni yangu.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.