Mariamu katika Uislamu (sehemu ya 1 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Makala ya kwanza kati ya sehemu tatu zinazozungumzia dhana ya Kiislamu ya Mariamu: Sehemu ya 1: Kipindi cha Utoto wake.

  • Na M. Abdulsalam (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 01 Aug 2022
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,309 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Mary_in_Islam_(part_1_of_3)_001.jpgMariamu, Mama wa Yesu, ana nafasi ya pekee sana katika Uislamu, na Mungu anamtangaza kuwa mwanamke bora zaidi kati ya wanadamu wote, ambaye alimchagua juu ya wanawake wengine wote kutokana na ucha mungu na kujitolea kwake.

“Na angalia pale Malaika walipo sema: ‘Ewe Maryamu! Kwa hakika Mwenyezi Mungu amekuteuwa, na akakutakasa, na akakutukuza kuliko wanawake wote.Ewe Maryamu! Mnyenyekee Mola Mlezi wako na usujudu na uiname pamoja na wainamao.’” (Kurani 3:42-43)

Pia alifanywa na Mungu kuwa mfano wa kufuata, kama alivyosema:

“Na Mariamu binti wa Imrani (Mwenyezi Mungu amepiga mfano kwa walio amini), aliye linda ubikira wake, na tukampulizia humo kutoka roho yetu, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi na Vitabu vyake, na alikuwa miongoni mwa wat'iifu.” (Kurani 66:12)

Hakika alikuwa mwanamke ambaye alifaa kuleta muujiza kama ule wa Yesu, ambaye alizaliwa bila baba. Alijulikana kwa uchamungu wake na usafi wake wa kimwili, na kama ingekuwa tofauti, basi hakuna ambaye angeamini madai yake ya kuzaa huku akiwa amebakia katika hali ya ubikira, imani na ukweli ambao Uislamu unashikilia kuwa ni wa kweli. Asili yake maalumu ilikuwa ule ambao miujiza mingi ilithibitisha kutoka utotoni mwake. Hebu tukumbuke kile ambacho Mungu alifunua kuhusiana na hadithi nzuri ya Mariamu.

Kipindi cha Utoto wa Mariamu

“Hakika Mwenyezi Mungu alimteuwa Adam na Nuhu na ukoo wa Ibrahim na ukoo wa Imran juu ya walimwengu wote. Ni wazao wao kwa wao; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kujua. Alipo sema mke wa Imran: Mola wangu Mlezi! Nimekuwekea nadhiri kilichomo tumboni mwangu kuwa wakfu; basi nikubalie. Hakika Wewe ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua.” (Kurani 3:33-35)

Mariamu alizaliwa kwa Imrani na mkewe Hannah ambaye alikuwa wa ukoo wa Daudi, hivyo alitoka katika familia ya Manabii, kuanzia Ibrahimu, Nuhu, hadi Adam, Amani na Baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote. Kama ilivyotajwa katika mstari huo, alizaliwa kwa familia iliyochaguliwa ya Imrani, ambaye alizaliwa katika familia iliyochaguliwa ya Ibrahimu, ambaye pia alizaliwa katika familia iliyochaguliwa. Hannah alikuwa mwanamke tasa ambaye alitamani kupata mtoto, na aliweka nadhiri kwa Mungu kwamba, ikiwa angempa mtoto, atamweka wakfu kwa huduma yake Hekaluni. Mungu akajibu maombi yake, naye akapata mimba ya mtoto. Alipojifungua, alihuzunika, kwani mtoto wake alikuwa wa kike, na kwa kawaida wanaume walikuwa wakipewa huduma kwa Bait-ul-Maqdis.

“Basi alipo mzaa alisema: ‘Mola wangu Mlezi! Nimemzaa mwanamke... Na mwanamume si sawa na mwanamke.”

Alipoonyesha huzuni yake, Mungu alimkemea akisema:

“…Na Mwenyezi Mungu anajua sana aliye mzaa …” (Kurani 3:36)

…kwani Mungu alimchagua binti yake, Mariamu, kuwa mama wa moja ya miujiza mikuu ya uumbaji: kuzaliwa kwa Yesu na bikira, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake. Hannah akamuita mtoto wake Mariamu (Maryam kwa Kiarabu) na akamwomba Mungu amlinde yeye na mtoto wake kutoka kwa Shetani:

“…Na mimi nimemwita Maryamu. Nami namkinga kwako, yeye na uzao wake, uwalinde na Shet'ani aliye laaniwa.” (Kurani 3:36)

Hakika Mungu aliikubali dua yake hii, na akampa Mariamu na mtoto wake atakayekuja hivi karibuni, Yesu, sifa maalumu - ambayo hakupewa yeyote kabla wala baada yake; hakuna hata mmoja wao aliyepatwa na mguso wa Shetani wakati wa kuzaliwa. Amesema Mtume Muhammad rehema na amani ziwe juu yake:

“Hakuna azaliwaye ambaye Shetani huwagusa katika kuzaliwa kwao, na hutoka huku akipiga kelele, isipo kuwa Maryamu na mwanawe (Yesu). (Ahmed)

Hapa, tunaweza kuona mara moja mfanano kati ya simulizi hii na nadharia ya Kikristo ya “Mimba Imara” ya Mariamu na Yesu, ingawa kuna tofauti kubwa kati ya hizo mbili. Uislamu hauenezi nadharia ya ‘dhambi ya asili’, na kwa hiyo haukubaliani na tafsiri hii ya jinsi walivyokuwa huru kutokana na mguso wa Shetani, bali kwamba hii ilikuwa ni neema iliyotolewa na Mungu kwa Mariamu na mwanawe Yesu. Akiwa kama manabii wengine, Yesu alilindwa asitende dhambi nzito. Ama Maryamu, hata tukichukua msimamo kuwa hakuwa nabii wa kike, lakini alipata ulinzi na mwongozo wa Mwenyezi Mungu ambao huwapa waumini wema.

“Tena Mola wake Mlezi akampokea kwa mapokeo mema na akamkuza makuzo mema, na akamfanya Zakariya awe mlezi wake.” (Kurani 3:37)

Baada ya kuzaliwa kwa Maryamu, mama yake Hannah alimpeleka Bait-ul-Maqdis na akamtoa kwa wale waliokuwa msikitini ili akue chini ya malezi yao. Wakijua fahari na uchamungu wa familia yao, waligombana ni nani angekuwa na heshima ya kumlea. Walikubaliana kupiga kura, na hakuwa mwingine ila nabii Zakaria aliyechaguliwa. Ilikuwa chini ya uangalizi wake na malezi ambayo alilelewa.

Miujiza katika Uwepo Wake na Kutembelewa na Malaika

Mariamu alipoanza kukua, hata nabii Zakaria aliona sifa maalumu za Mariamu, kutokana na miujiza mbalimbali iliyotokea mbele yake. Mary alipokuwa akikua, alipewa chumba cha faragha ndani ya msikiti ambapo angeweza kujitolea kwa ajili ya ibada ya Mungu. Wakati wowote Zakaria alipoingia chumbani ili kuona mahitaji yake, alikuta matunda mengi mbele yake, na sio kipindi cha msimu wake.

“Kila mara Zakariya alipo ingia chumbani kwake alimkuta na vyakula. Basi alimwambia: Ewe Maryamu! Unavipata wapi hivi? Naye akasema: Hivi vinatoka kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu.” (Kurani 3:37)

Alitembelewa na malaika zaidi ya tukio moja. Mungu anatuambia kwamba malaika walimtembelea na kumjulisha juu ya hadhi yake ya na sifa kati ya wanadamu:

“Na angalia pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Kwa hakika Mwenyezi Mungu amekuteuwa, na akakutakasa (kutokana na ibada yako), na akakutukuza kuliko wanawake wote (kwa kukufanya kuwa mama wa nabii Yesu). ‘Ewe Maryamu! Mnyenyekee Mola Mlezi wako na usujudu na uiname pamoja na wainamao.’” (Kurani 3:42-43)

Kwa sababu ya kutembelewa na malaika na kuchaguliwa kwake juu ya wanawake wengine, wengine wameshikilia kuwa Mariamu alikuwa nabii wa kike. Hata kama hakuwa hivyo, ambalo ni suala la mjadala, Uislamu bado unamwona kuwa na hadhi ya juu kabisa miongoni mwa wanawake wote kutokana na ucha mungu na kujitolea kwake, na kutokana na kuchaguliwa kwake kwa ajili ya kuzaliwa kwa Yesu kwa kimiujiza.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.