Mariamu katika Uislamu (sehemu ya 2 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Makala ya pili kati ya sehemu tatu zinazozungumzia dhana ya Kiislamu ya Mariamu: Sehemu ya 2: Matamshi yake.

  • Na M. Abdulsalam (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,881 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Matamshi Yake

Mungu anatufahamisha kuhusu mfano ambao malaika walimpa Mariamu habari njema ya mtoto, atakuja kua na hadhi kubwa duniani hivi karibuni, na baadhi ya miujiza atakayofanya:

“Na pale Malaika walipo sema: ‘Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu). Naye atazungumza na watu katika utoto wake na katika utuuzima wake, na atakuwa katika watu wema.’ Maryamu akasema: ‘Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa mwanaadamu?’ Mwenyezi Mungu akasema: ‘Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba apendacho. Anapo hukumu jambo, huliambia: Kuwa! Likawa.’ Na atamfunza kuandika na Hikima na Taurati na Injili. ” (Kurani 3:45-48)

Hii inaonekana kama maneno yaliyotajwa katika Biblia:

“Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Na tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yesu."

Kwa mshangao, alijibu:

"Hili linawezaje kuwa, kwani sijui mwanaume?" ( Luka 1:26-38 )

Mfano huu ulikuwa jaribu kubwa kwake, kwa kuwa uchamungu wake mkuu na kujitolea kulijulikana kwa kila mtu. Aliona yajayo kwamba watu wangemshtaki kuwa mchafu.

Katika aya nyingine za Kurani, Mungu anasimulia maelezo zaidi ya matamshi ya Jibrili kwamba angemzaa Mtume.

“Na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea Roho wetu, akajifananisha kwake sawa na mtu. (Maryam) akasema: ‘Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe, ukiwa ni mchamngu.’ (Malaika) akasema: Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako Mlezi ili nikubashirie tunu ya mwana aliye takasika.’” (Kurani 19:17-19)

Wakati, Mariamu alipotoka msikitini ili kuona mahitaji yake, malaika Jibrili alimjia katika umbo la mwanaume. Aliogopa kwa sababu ya ukaribu wa mtu huyo, na akatafuta kimbilio kutoka kwa Mungu. Kisha Jibrili akamwambia kwamba yeye hakuwa mtu wa kawaida, bali ni malaika aliyetumwa na Mungu kutangaza kwake kwamba angezaa mtoto safi kabisa. Kwa mshangao, alisema

“Akasema: Nitampataje mwana hali mwanaadamu yeyote hajanigusa, wala mimi si kahaba?!’” (Kurani 19:20)

Malaika alieleza kwamba ilikuwa ni amri ya Mwenyezi Mungu ambayo tayari imeshawekwa, na kwamba hakika ni jambo jepesi kwa Mwenyezi Mungu. Mungu alisema kuzaliwa kwa Yesu, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, kutakuwa ishara ya uweza wake, na kwamba, kama vile ilivyo muumba Adamu bila baba wala mama, alimuumba Yesu bila baba.

“(Malaika) akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: ‘Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu, na Rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo lilio kwisha hukumiwa.’” (Kurani 19:21)

Mungu akapuliza roho ya Yesu kupitia malaika Jibrili ndani ya Mariamu, na Yesu akatungwa ndani ya tumbo lake, kama Mungu alivyosema katika sura nyingine:

“Na Mariamu binti wa Imrani, aliye linda ubikira wake, na tukampulizia humo kutoka roho yetu, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi na Vitabu vyake, na alikuwa miongoni mwa wat'iifu (Jibrili).” (Kurani 66:12)

Dalili za ujauzito zilipodhihirika, Mary alizidi kuwa na wasiwasi kuhusu watu wangesema nini kumhusu. Habari zake zilienea kila mahali na, isingeweza kuepukika, wengine walianza kumshutumu kuwa mchafu. Tofauti na imani ya Kikristo kwamba Mariamu alichumbiwa na Yusufu, Uislamu unashikilia kwamba hakuwa ameposwa, wala kuchumbiwa au kuolewa, na hilo ndilo lililomsababishia uchungu huo. Alijua kwamba watu wangefanya hitimisho pekee la kimantiki kuhusu hali yake ya ujauzito, kwamba hakuwa ameolewa. Mariamu alijitenga na watu na kwenda nchi tofauti. Mungu anasema:

“Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali. Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende; akasema: Laiti ningeli kufa kabla ya haya, na nikawa niliye sahaulika kabisa!” (Kurani 19:22-23)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.