Mariamu katika Uislamu (sehemu ya 3 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mwisho wa makala yenye sehemu tatu inayozungumzia dhana ya Kiislamu ya Mariamu: Sehemu ya 3: Kuzaliwa kwa Yesu, na umuhimu na heshima Uislamu unampa Mariamu, mama yake Yesu.

  • Na M. Abdulsalam (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,112 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kuzaliwa Kwa Yesu

Alipoanza kujifungua, alikuwa na maumivu makali kiakili na kimwili. Mwanamke mcha Mungu na mtukufu hivyo angewezaje kuzaa mtoto nje ya ndoa? Tunapaswa kutaja hapa kwamba Mariamu alikuwa na mimba ya kawaida ambayo haikuwa tofauti na wanawake wengine, na akamzaa mtoto wake kama wengine wanavyofanya. Katika imani ya Kikristo, Mariamu hakupata uchungu wa kuzaa, kwa kuwa Ukristo na Uyahudi huona hedhi na leba kuwa laana kwa wanawake kwa ajili ya dhambi ya Hawa[1]. Uislamu hauidhinishi imani hii, wala nadharia ya ‘Dhambi ya Asili’, bali unasisitiza kwa nguvu kwamba hakuna atakayebebesha dhambi za wengine:

“…Na kila nafsi haichumii (dhambi) ila nafsi yake. Na habebi mwenye kubeba mzigo wa mwenziwe....” (Kurani 6:164)

Si hivyo tu, bali sio Kurani wala Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, haijataja kuwa ni Hawa aliyekula tunda na kumshawishi Adam. Bali Kurani inamlaumu Adam peke yake, au wote wawili.

“Basi Shet'ani aliwatia wasiwasi …Basi akawateka kwa khadaa. Walipo uonja ule mti, tupu zao zilifichuka na wakaingia kujibandika majani ya Bustanini.” (Kurani 7:20-22)

Mariamu, kutokana na maumivu na uchungu alitamani kwamba asingeumbwa kamwe, na akasema:

“Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende; akasema: Laiti ningelikufa kabla ya haya, na nikawa niliye sahaulika kabisa!” (Kurani 19:23)

Baada ya kujifungua mtoto, na pale maumivu yake yalivyopungua ukali, mtoto mchanga aliyezaliwa, Yesu, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alilia kimuujiza kutoka chini yake, akimtuliza na kumhakikishia kwamba Mungu atamlinda:

Pakatangazwa kutoka chini yake: Usihuzunike! Hakika Mola wako Mlezi amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji! Na litikise kwako hilo shina la mtende, utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu. Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako. Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema: ‘Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga; kwa hivyo leo sitasema na mtu.’” (Kurani 19:24-26)

Mariamu alihisi kufarijiwa. Huu ulikuwa muujiza wa kwanza kufanywa na Yesu. Alizungumza kwa kumtuliza mama yake alipozaliwa, na kwa mara nyingine tena watu walipomwona akiwa amembeba mtoto wake mchanga. Walipomwona, walimshtaki kwa kusema:

“Ewe Maryamu! Hakika umeleta kitu cha ajabu!...” (Kurani 19:27)

Alielekeza tu kwa Yesu, naye akazungumza kimuujiza, kama vile Mungu alivyokuwa amemwahidi baada ya kutangazwa.

“Naye atazungumza na watu katika utoto wake na katika utuuzima wake, na atakuwa katika watu wema.” (Kurani 3:46)

Yesu aliwaambia watu:

“Akasema: Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu, amenipa Kitabu na amenifanya Nabii, na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo. Na ameniusia Swala na Zaka maadamu ni hai na nimtendee wema mama yangu. Wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu. Na amani iko juu yangu siku niliyozaliwa, na siku nitakayo kufa, na siku nitakayo fufuliwa kuwa hai.” (Kurani 19:30-33)

Kuanzia hapa huanza kipindi cha Yesu, pambano lake la maisha yote kuwaita watu kwenye ibada ya Mungu, akikwepa njama na mipango ya wale Wayahudi ambao wangejitahidi kumuua.

Mariamu katika Uislamu

Tumeshajadili hadhi kubwa ambayo Uislamu unampa Mariamu. Uislamu unampa hadhi ya kuwa mwanamke mkamilifu zaidi aliyeumbwa. Katika Kurani, hakuna mwanamke aliyepewa mazingatio zaidi kuliko Mariamu ingawa Mitume wote, isipokuwa Adam, walikuwa na mama. Kati ya sura 114 za Kurani, yeye ni miongoni mwa watu nane ambao wana sura inayoitwa kwa majina yao, sura ya kumi na tisa "Mariamu", ambayo ni Maryamu kwa Kiarabu. Sura ya tatu katika Kurani imepewa jina la baba yake Imran (Heli). Sura za Maryamu na Imran ni miongoni mwa sura nzuri sana katika Kurani. Kwa kuongezea, Mariamu ndiye mwanamke pekee aliyetajwa katika Kurani. Mtume Muhammad amesema:

“Wanawake bora duniani ni wanne: Mariamu binti Ali, Aasiyah mke wa Firauni, Khadiyjah binti Khuwaylid (Mke wa Mtume Muhammad), na Fatimah, binti wa Muhammad, Mtume wa Mwenyezi Mungu.” (Al-Tirmidhi)

Pamoja na sifa zote hizi tulizozitaja, Mariamu na mwanawe Yesu walikuwa ni binadamu tu, na hawakuwa na sifa zozote ambazo zilikuwa nje ya eneo la ubinadamu. Wote wawili walikuwa viumbe walioumbwa na ‘waliozaliwa’ katika ulimwengu huu. Ingawa walikuwa chini ya uangalizi maalumu wa Mwenyezi Mungu ili kutokufanya madhambi makubwa (ulinzi kamili - kama manabii wengine - katika jambo la Yesu, na ulinzi kama wa watu wengine wema katika jambo la Mariamu, ikiwa tutachukua msimamo kwamba hakuwa nabii wa kike), bado walikuwa na mwelekeo wa kufanya makosa. Tofauti na Ukristo, ambao unashikilia Mariamu kuwa hana dosari[2], hakuna yeyote anayepewa sifa hii ya ukamilifu isipokuwa Mungu Pekee Yake.

Uislamu unaamuru imani na utekelezaji wa tauhidi kali; kwamba hakuna yeyote mwenye nguvu zisizo za kawaida isipokuwa Mwenyezi Mungu, na kwamba Yeye pekee ndiye anayestahiki kuabudiwa na ibada. Ingawa miujiza inaweza kuwa ilitokea mikononi mwa manabii na watu wema wakati wa maisha yao, hawana uwezo wa kujisaidia wenyewe, achilia wengine, baada ya kifo chao. Wanadamu wote ni watumwa wa Mungu na wanahitaji msaada na rehema zake.

Ndivyo ilivyo kwa Mariamu. Ingawa miujiza mingi ilitokea mbele yake, yote haya yalikoma baada ya kifo chake. Madai yoyote ambayo watu wametoa kwamba waliona mzimu wa Bikira, au kwamba watu waliokolewa kwenye madhara baada ya kumwomba, kama yale yaliyotajwa katika maandiko ya apokrifa kama vile "Transitus Mariae", ni maonyesho tu yaliyofanywa na Shetani ili kuwaelekeza watu mbali na ibada na kujitolea kwa Mungu Mmoja wa Kweli. Ibada kama vile 'Salamu Maria' inayosifiwa juu ya rozari na matendo mengine ya ukuu, kama vile ibada ya makanisa na maelezo ya sikukuu kwa Mariamu, yote huwaongoza watu kuwatukuza na kuadhimisha wengine badala ya Mungu. Kutokana na sababu hizo, Uislamu umeharamisha vikali uzushi wa aina yoyote ile, pamoja na kujenga nyumba za ibada juu ya makaburi, yote hayo ili kuhifadhi asili ya dini zote zilizotumwa na Mwenyezi Mungu, ujumbe safi wa kumwabudu Yeye pekee na kuacha ibada potofu nyingine zote isipokuwa Yeye.

Mariamu alikuwa mjakazi wa Mungu, na alikuwa mwanamke safi kuliko wanawake wote, aliyechaguliwa hasa kuzaa Yesu kimuujiza, mmoja wa manabii mkuu zaidi wa wote. Alijulikana kwa uchamungu wake na usafi wake wa kimwili, na ataendelea kushikiliwa katika suala hili kuu katika enzi zote zijazo. Hadithi yake imesimuliwa ndani ya Kurani Tukufu tangu kuja kwa Mtume Muhammad, na itaendelea kuwa hivyo, bila kubadilika katika umbile lake safi, hadi Siku ya Hukumu.



Rejeleo la maelezo:

[1]Tazama Mwanzo (3:16)

[2] Mtakatifu Augustino: “De nat. et gratis”, 36.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.