Wanasema nini kuhusu Muhammad (sehemu ya 2 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kauli za wasomi wasio Waislamu ambao wamejifunza Uislamu kuhusu Mtume. Sehemu ya 2: Kauli zao.

  • Na iiie.net (edited by IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 01 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,656 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Lamartine, Histoire de la Turquie, Paris 1854, Vol II, uk. 276-77:

“Ikiwa ukubwa wa kusudi, uduni wa njia, na matokeo ya kushangaza ni vigezo vitatu vya fikra kubwa za binadamu, ni nani angeweza kuthubutu kumlinganisha mtu yeyote mashuhuri katika historia ya kisasa na Muhammad? Wanaume mashuhuri zaidi waliunda silaha, sheria na utawala tu. Walianzisha, kama kuna kitu chochote, sio nguvu za kinyenzo ambazo mara nyingi zilibomoka mbele ya macho yao. Mtu huyu alihamisha sio tu majeshi, sheria, milki, watu na tawala, lakini hata mamilioni ya wanadamu katika theluthi moja ya ulimwengu uliokuwa na watu kaika kipindi hicho; na zaidi ya hayo, alihamisha madhabahu, miungu, dini, maoni, imani na roho ... uvumilivu katika ushindi, tamaa yake, ambayo ilikuwa imejitolea kabisa kwa wazo moja na bila kutoweka tamaa ya ufalme; sala zake zisizo na mwisho, mazungumzo yake ya kipekee na Mungu, kifo chake na ushindi wake baada ya kifo; kwa hakika haya yote siyo ya uongo bali ni usadikisho thabiti ambao ulimpa nguvu ya kurejesha fundishoya imani. Mafundisho haya yalikuwa mawili, Ummoja wa Mungu na kutokuonekana kwa Mungu; la kwanzalikieleza Mungu ni nini, la pili likielezea ambacho Mungu sio; yule anayewapindua miungu kwa njia ya upanga, na huyo mwengine akianza wazo kwa kutumia maneno.”

“Mwanafalsafa, msemaji, mtume, mtunga sheria, shujaa, mshindi wa maoni, mrudishaji wa mafundisho yenye busara, ibada isiyo na picha; mwanzilishi wa milki ishirini za kidunia na ya himaya moja ya kiroho, huyo ni Muhammad. Kwa viwango vyote ambavyo ukubwa wa kibinadamu unaweza kupimwa, tunaweza kuuliza, je! Kuna mtu yeyote mkubwa kuliko yeye? ”

Edward Gibbon na Simon Ocklay, Historia ya Dola ya Saracen, London, 1870, uk. 54:

“Sio uenezaji lakini kudumu kwa dini yake ambako kunastahili mshangao wetu, maoni yale yale safi na kamili ambayo aliandika huko Makka na Madina yamehifadhiwa, baada ya mapinduzi ya karne kumi na mbili ya Wahindi, Waafrika na Waturuki kuifuata Kurani...Wanahometan[1] wamefanikiwa kuhimili jaribu la kupunguza imani yao na kujitolea kwa kiwango cha hisia na mawazo ya mwanadamu. 'Ninaamini katika Mungu Mmoja na Muhammad Mtume wa Mungu', ni ujuzi rahisi na usiyoweza kubadilika wa Uislamu. Picha ya kiakili ya Uungu haijawahi kudhalilishwa na sanamu yoyote inayoonekana; heshima za Mtume hazijawahi kukiuka kipimo cha uwezo wa kibinadamu, na kanuni yake ya uzima imethibiti shukrani za wanafunzi wake katika mipaka ya sababu na dini.”

Bosworth Smith, Mohammed and Mohammadanism, London 1874, uk. 92:

“Alikuwa Kaisari na Papa katika umoja; lakini alikuwa Papa bila mamlaka ya Papa, Kaisari bila majeshi ya Kaisari: bila jeshi lililosimama, bila mlinzi, bila ikulu, bila mapato ya kudumu; ikiwa kuna mtu yeyote alikuwa na haki ya kusema kwamba anatawala kwa mungu sahihi, alikuwa Mohammed, kwani alikuwa na nguvu zote bila vyombo vyake na bila msaada wake. ”

Annie Besant, The Life and Teachings of Muhammad, Madras 1932, uk. 4:

“Haiwezekani kwa mtu yeyote anayesoma maisha na tabia ya Mtume mkubwa wa Uarabuni, ambaye anajua jinsi alivyofundisha na jinsi alivyoishi, hatahisi chochote isipokuwa heshima kwa Mtume huyo hodari, mmoja wa wajumbe wakuu wa Mkuu. Na ingawa katika kile ninachoweka kwako nitasema vitu vingi ambavyo vinaweza kufahamika na wengi, lakini mimi mwenyewe ninajisikia kila ninapo rudia kusoma tena, njia mpya ya kupendeza, hisia mpya ya heshima kwa mwalimu huyo hodari wa Uarabuni. ”

W. Montgomery, Mohammad at Mecca, Oxford 1953, uk. 52:

"Utayari wake wa kusumbuka kwasababu ya imani yake, tabia ya juu ya maadili ya wanadamu ambao walimwamini na kumtazama kama kiongozi, na ukubwa wa mafanikio yake ya mwisho - yote yanasisitiza msingi wa uadilifu wake. Kudhani Muhammad ni muongo kunaleta shida nyingi kuliko utatuzi. Cha kuongezea, hakuna mtu yeyote mashuhuri wa historia anayethaminiwa sana Magharibi kama Muhammad. ”

James A. Michener, ‘Islam: The Misunderstood Religion’ in Reader’s Digest (American Edition), May 1955, uk. 68-70:

“Muhammad, mtu anayeangaliwa aliyeanzisha Uislamu, alizaliwa mnamo 570 B.K katika kabila la Kiarabu ambalo liliabudu masanamu. Alikuwa yatima, kila wakati alikuwa akiwaangalia sana masikini na anayehitaji, mjane na yatima, mtumwa na mnyonge. Katika umri wa miaka ishirini alikuwa tayari mfanyabiashara aliyefanikiwa, na baadaye kuwa kiongozi wa misafara ya ngamia kwa mjane tajiri. Alipofikia umri wa miaka ishirini na tano, mwajiri wake, kwa kutambua sifa yake, alipendekeza ndoa kwa ruhusa yake. Ingawa alikuwa mkubwa kwake kwa umri wa miaka kumi na tano, alimuoa, na katika maisha yake , alibaki kuwa mume bora.

"Kama ilivyo kwa kila mtume mkubwa kabla yake, Muhammad alipigania kwa aibu ya kufanya huduma ya kuwa mpeleka neno la Mungu, akihisi mapungufu yake mwenyewe. Ila malaika alimuamuru 'Soma'. Kama tunavyojua, Muhammad hakuweza kusoma au kuandika, lakini alianza kuyasema maneno hayo ya kuvutia ambayo baadae yalibadilisha sehemu kubwa ya dunia: "Kuna Mungu mmoja."

“Katika mambo yote Muhammad alikuwa akifanya kwa vitendo. Pindi mtoto wake mpendwa Ibrahim alipokufa, kulitokea kupatwa kwa jua, na rambirambi ya Mungu ilitokea haraka. Ambapo inasemekana Muhammad alisema, 'Kupatwa kwa jua ni jambo la asili. Ni upumbavu kuhusisha vitu kama hivyo kutokana na kifo au kuzaliwa kwa mwanadamu. ’

"Wakati wa kifo cha Muhammad jaribio lilifanywa la kumfanya kuwa mungu, lakini mtu ambaye angekuwa mrithi wake wa utawala aliua mawazo hayo kwenye moja ya hotuba nzuri zaidi katika historia ya dini: 'Iwpoa kuna yeyote kati yenu aliyemuabudu Muhammad, basi ajuwe amekufa. Lakini ikiwa ni Mungu ndiye unayemuabudu, basi Yeye anaishi milele. ’”

Michael H. Hart, The 100: A Ranking of the Most Influential Persons in History, New York: Kampuni ya Uchapishaji ya Hart, Inc. 1978, uk. 33:

"Chaguo langu la Muhammad kuongoza orodha ya watu wenye ushawishi mkubwa ulimwenguni linaweza kuwashangaza wasomaji wengine na linaweza kuulizwa na wengine, lakini alikuwa mtu pekee katika historia ambaye alikuwa amefanikiwa sana katika ngazi ya dini na ya kidunia."



Rejeleo la maelezo:

[1] Neno Mahometans na Mohammedanism ni jina lisilo la kawaida linalowasilishwa na wataalamu wa mashariki kwa sababu ya ukosefu wao wa kuelewa Uislamu, kwa kufananisha Kristo na Ukristo.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.