Ni Kitu Gani Kinachowachochea Watu Kusilimu? (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Changamoto ya Kurani kwa wenye akili.

  • Na Based on an article at iqrasense.com
  • Iliyochapishwa mnamo 22 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,793 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

What_Drives_People_to_Convert_to_Islam_(part_2_of_2)_001.jpgKurani inawapa changamoto wanadamu wote kufikiria na kuzingatia kuhusu mambo yao katika hali mbali mbali. Haya ni baadhi ya yale ambayo Kurani inayaelezea:

·Namna hivi tunazipambanua ishara zetu kwa watu wanaofikiri. (Yona, Kurani 10:24)

·Je, hawajifikirii nafsi zao? Mwenyezi Mungu hakuumba mbingu na ardhi na viliomo ndani yake ila kwa Haki na kwa muda maalumu. Na hakika watu wengi bila ya shaka ni wenye kukataa kuwa watakutana na Mola wao Mlezi. (Warumi, Kurani 30:8)

·Yeye ndiye aliyekujaalieni usiku mpate kutulia humo, na mchana wa kuonea. Hakika katika haya zipo ishara kwa watu wanaosikia. (Yona, Kurani 10:67)

·Ati anadhani binadamu kuwa ataachwa bure? (Ufufuo, Kurani 75:36)

·Je, mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa? (Waaminio, Kurani 23:115)

·Au wewe unadhani kwamba wengi wao wanasikia au wanaelewa? Hao hawakuwa ila ni kama nyama hoa tu, bali wao wamepotea zaidi njia. (Kigezo, Kurani 25:44)

·Je, hawafikiri? Huyu mwenzao hana wazimu. Hakuwa yeye ila ni mwonyaji aliye dhahiri. (Urefu, Kurani 7:184)

·Lau kuwa tumeiteremsha hii Kurani juu ya mlima, basi bila ya shaka ungeliuona ukinyenyekea, ukipasuka kwa khofu ya Mwenyezi Mungu. Na hiyo mifano tunawapigia watu ili wafikiri. (Mkusanyiko Mkubwa, Kurani 59:21)

Tunapochunguza visa vingi vya Waislamu wageni waliosilimu, tunaona kwamba wakijishughulisha na kufikiri kwa kina na hoja za kimantiki ni sababu yao kubadili imani zao zisizo za Kiislamu - imani zile zile ambazo hapo awali zingedhaniwa kuhamisha milima, lakini zilishindwa na sauti ya akili inayosikika kwa urahisi katika mizizi ya Uislamu. Mchakato tu wa kufikiri na kutafakari hudhihirisha mengi waziwazi ambayo yangebaki kufunikwa na pingamizi na nguvu za wachambuzi wanaochukia Uislamu. Wale ambao wamedhamiria kuona mabaya tu wanashindwa kuona nuru ya ukweli. Badala yake, wanajihusisha na uchanganuzi wa kijuujuu usioisha ili kuthibitisha bila mafanikio falsafa zao potofu.

Kuna takwimu nyingi kwenye vyombo vya habari zinazoangazia kasi ya ajabu ambayo watu husilimu. Ingawa, usahihi wa vyanzo hivi vyote haujathibitishwa, kwa madhumuni ya makala hii baadhi yao ni pamoja na yafuatayo:

·Kulingana na "The Almanac Book of Facts", idadi ya watu iliongezeka 137% katika mwongo mmoja uliopita, Ukristo uliongezeka 46%, wakati Uislamu uliongezeka 235%.

·Watu 100,000 kwa mwaka huko Amerika pekee, wanaingia katika Uislamu. Kwa kila mwanamume 1 aliyesilimu, wanawake 4 hujiunga katika Uislamu.

·Ripoti ya TV: Wajerumani 4,000 HUSILIMU Kila Mwaka.

·Karibu watu 25,000 husilimu kila mwaka nchini Uingereza pekee.

·…mifano mingi zaidi ipo.

Vipi kuhusu Waislamu?

Iwapo sauti za kutumia akili zinazopatikana ndani ya mafundisho ya Uislamu husababisha wasio Waislamu kurejea katika Uislamu kwa wingi, basi kwa nini Waislamu wengi waliozaliwa katika dini hii kawaida hushindwa kufuata kikamilifu, na kwa hivyo kufurahia, mafundisho ya dini? Ukweli ni kwamba inaweza kuwa Waislamu wengine wamekosa kutumia fikira kwa kina na mazingatio, hali inayolazimisha ulimwengu wa Kiislamu kuonekana kuwa na maisha duni kwa ujumla. Uislamu na mafundisho yake unaahidi kutimiza maisha ya kuridhisha na yenye amani kwa wote. Walakini Waislamu wanaendelea kupuuza mambo ya kimsingi na kujitatiza katika masuala ya kijamii na maadili yanayosababisha maumivu yasiyofaa na mateso kwao na familia zao. Ukweli ni kwamba ikiwa wangefikiria na kutafakari juu ya mafundisho ya dini yao wenyewe, wangeweza kuepuka matatizo mengi na changamoto zinazowakabili.

Ujumbe

Kwa wasio Waislamu ambao wameutafuta Uislamu na kuujua kijuujuu na wanaweza kukengeushwa na viongozi wale wapotofu wa dini hii pamoja na sauti za upendeleo kwenye vyombo vya habari, ujumbe kwao ni rahisi - jaribu kutazama mafundisho ya Uislamu kwa umanikinifu. Inawezekana kwamba utaweza kupata sababu zaidi kuliko vile ambavyo hapo awali ungefikiria hazikuwepo. Kwa Waislamu, ujumbe ni kwamba wakati mwingine hatuthamini mafundisho ya dini yetu wenyewe kwa sababu hatufikirii na kukua zaidi ya matendo machache ya kidini katika kuendesha maisha yetu. Juhudi makini za kujifunza, kufikiri na kutafakari zaidi zitatusaidia kukaribia mafundisho ya kidini kwa njia ambazo zinaweza kuboresha maisha yetu kwa kiasi kikubwa.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.