Uislam, katika Jamii ya Kisasa (sehemu 1 kati ya 2): Utangulizi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kauli za wasomi mbalimbali za wasiokuwa Waislamu juu ya ukuu wa dini ya Uislamu kama Jamii. Sehemu ya 1: Utangulizi.

  • Na iiie.net
  • Iliyochapishwa mnamo 02 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 19 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,370 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Islam__a_Profound_Civilization_(part_1_of_2)_001.jpgUislamu ambao ulifunuliwa kwa Muhammad, Mungu ampandishe, ni mwendelezo na hitimisho la dini zote zilizoteremshwa hapo awali, na kwa hivyo ni ya zama zote na watu wote. Hadhi hii ya Uislamu inadumishwa na ukweli dhahiri. Kwanza, hakuna kitabu kingine chochote kati ya vile vilivyofunuliwa ambacho kipo katika muundo na maudhui kama yale yaliyofunuliwa. Pili, hakuna dini nyingine iliyofunuliwa yenye madai yoyote ya kusadikisha yenye kutoa mwongozo katika nyanja zote za maisha ya mwanadamu kwa zama zote. Lakini Uislamu unashughulikia ubinadamu kwa ujumla na hutoa mwongozo unaohusu shida zote za wanadamu. Kwa kuongezea, imehimili mtihani wa miaka elfu moja na mia nne na ina uwezo wote wa kuanzisha jamii bora kama ilivyokuwa chini ya uongozi wa Mtume wa mwisho Muhammad.

Ilikuwa ni muujiza kwa Nabii Muhammad kuweza kuwaleta hata maadui zake wakubwa kwenye kundi la Uislamu bila kuwa na rasilimali za kutosha. Waabudu sanamu, wafuasi vipofu wa kufuata njia za mababu zao, waendelezaji wa uhasama wa kikabila, na wanyanyasaji wa utu na damu za watu wakawa taifa lenye nidhamu zaidi chini ya uongozi wa Uislamu na Mtume wake. Uislamu ulifungulia mtazamo wa ukubwa wa kiroho na hadhi ya kibinadamu kwa kutangaza haki kama kigezo pekee cha sifa na heshima. Uislamu ulirekebisha maisha yao ya kijamii, kitamaduni, kimaadili na kibiashara kwa sheria na kanuni za msingi ambazo zinaambatana na maumbile ya mwanadamu hivyo kuweza kutumika zama zote kwa kuwa maumbile ya mwanadamu hayabadiliki.

Kwa bahati mbaya Wakristo wa Magharibi badala ya kujaribu kwa dhati kuyaelewa mafanikio mazuri ya Uislamu wakati wa mwanzo, wao waliiona kama dini pinzani. Wakati wa karne za Vita vya Msalaba, mwelekeo huu ulipata nguvu nyingi na msukumo na idadi kubwa ya machapisho yalitolewa ili kuichafua taswira ya Uislamu. Lakini Uislamu umeanza kufunua ukweli wake kwa wasomi wa kisasa ambao uchunguzi wao wa kijasiri na madhubuti juu ya Uislamu kwa kujibu madai yote yaliyowekwa dhidi ya Uislamu na wale wanaojiita wataalamu wa kimashariki wasioegemea upande wowote.

Hapa tunaona maoni juu ya Uislamu kutoka kwa wanazuoni wasio Waislamu wa wakati wa sasa. Ukweli hauitaji utetezi wa kuuombea kwa niaba yake, lakini propaganda mbaya ya muda mrefu dhidi ya Uislamu imesababisha mkanganyiko mkubwa hata katika akili za wanafikra na waoni huru.

Tunatumai ya kwamba uchunguzi ufuatao utachangia katika kuanzisha tathmini yenye lengo ya Uislam.

Canon Taylor, Karatasi iliyosomwa mbele ya Bunge la Kanisa la huko Walverhamton, Oktoba 7, 1887, Imenukuliwa na Arnond katika kitabu cha The Preaching of Islam, uk. 71-72:

“Ni (Uislamu) ulibadilisha unyani na ubinadamu. Ilitoa tumaini kwa mtumwa, udugu kwa wanadamu, na kutambua ukweli wa kimsingi wa asili ya mwanadamu.”

Sarojini Naidu, Mahubuiri juu ya “The Ideals of Islam”, angalia Hotuba na Machapisho ya Sarojini Naidu, Madras, 1918, p. 167:

“Hisia ya haki ni moja wapo ya maoni mazuri ya Uislam, kwa sababu nikiwa nasoma Kurani nilipata kanuni hizo za maisha, sio za mafumbo lakini maadili ya vitendo katika maisha ya kila siku yanayofaa ulimwenguni kote.”

De Lacy O'Leary, Islam at the Crossroads, London, 1923, uk. 8:

“Historia inaweka wazi, kuwa simulizi ya Waislamu shupavu wanaotapakaa ulimwenguni na kuulazimisha Uislamu kwa njia ya upanga kwenye jamii zilizoshindwa ni moja wapo ya simulizi za ajabu sana ambazo wanahistoria wamewahi kuzirudia.”

H.A.R. Gibb, Whither Islam, London, 1932, p. 379:

“Ila Uislamu bado una kazi zaidi ya kujitoa kwa sababu ya wanadamu. Inasimama karibu kabisa na Mashariki kuliko Ulaya, na ina mila nzuri ya uelewa na ushirikiano wa kikabila. Hakuna jamii nyingine iliyo na rekodi kama hiyo ya mafanikio katika kuungana katika usawa wa hadhi, nafasi, na jitihada nyingi na asili mbalimbali za wanadamu ... Uislamu bado una nguvu ya kupatanisha mambo ambayo hayafanani ya asili na tamaduni. Ikiwa upinzani wa jamii kubwa za Mashariki na Magharibi utabadilishwa na ushirikiano, upatanishi wa Uislamu utakuwa wa lazima. Katika mikono yake lipo suluhisho la shida ambayo Ulaya inakabiliwa nayo katika uhusiano wake na Mashariki. Ikiwa wataungana, matumaini ya kuimarika kwa amani hautapimika. Ila ikiwa Ulaya,itakataa ushirikiano huu wa Uislamu, inaitupa mikononi mwa wapinzani wake, suala hilo linaweza kuwa baya kwa wote wawili.”

G.B. Shaw, The Genuine Islam, Juzuu. 1, Nambari. 81936:

“Nimekuwa nikiishikilia dini ya Muhammad kwa makadirio ya juu kwa sababu ya uhai wake mzuri. Ni dini pekee inayoonekana kwangu kumiliki uwezo huo wa kuingiza mabadiliko ya maisha ambayo inaweza kujiweka katika kila kizazi. Nimemsoma - mtu mzuri na kwa maoni yangu yupo mbali na kuwa mpinga Kristo, lazima aitwe Mwokozi wa Wanadamu. Ninaamini kuwa ikiwa mtu kama yeye angeuchukua udikteta wa ulimwengu wa sasa, angefanikiwa kutatua shida zake kwa njia ambayo italeta amani na furaha inayohitajika sana: Nimetabiri juu ya imani ya Muhammad kuwa itakubalika na Ulaya ya kesho kwani inaanza kukubalika na Ulaya ya leo.”

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.