Sara Bokker, Mwigizaji wa Zamani na Mwanamitindo, Marekani

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi gani, Sara Bokker, mwigizaji wa zamani, mwanamitindo, mwalimu wa mazoezi ya mwili na mwanaharakati aliacha maisha ya kupendeza ya Miami kwaajili ya Uislamu na kupata ukombozi wa kweli katika Uislamu na kanuni za mavazi ya wanawake wa Kiislamu.

  • Na Sara Bokker (edited by IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,464 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Mimi ni mwanamke wa Kimarekani aliyezaliwa katikati ya "Heartland" ya Marekani. Nilikua, kama msichana mwingine yeyote, nikiwa nimevutiwa na uzuri wa maisha ya "jiji kubwa". Hatimaye, nilihamia Florida na kuelekea South Beach ya Miami, mahali penye watu wengi wanaotafuta "maisha ya kupendeza". Kwa kawaida, nilifanya kile ambacho wasichana wengi wa kawaida wa Magharibi hufanya. Niliwekea mkazo sura yangu na mvuto wangu, nikiiweka thamani yangu kwa jinsi nilivyojaliwa na wengine. Nilifanya kazi kwa bidii na kuwa mwalimu wa kibinafsi, nikapata makazi ya hali ya juu mbele ya maji, nikawa mtu wa "kwenye maonyesho" wa kwenda ufukweni, na niliweza kupata aina ya maisha ya "kuishi kwa mtindo".

Miaka ilipita, niligundua kwamba kiwango changu cha kujikamilisha na furaha kilishuka kadiri nilivyoendelea katika "mvuto wangu wa kike". Nilikuwa mtumwa wa mitindo. Nilikuwa mateka wa sura yangu.

Kadiri pengo lilivyozidi kuongezeka hatua kwa hatua kati ya ukamilifu wangu wa kibinafsi na mtindo wa maisha, nilitafuta kimbilio la kutoroka kutoka kwenye pombe na sherehe hadi kutafakari, harakati, na dini mbadala, na pengo hilo dogo kupanuka hadi lililoonekana kama bonde. Hatimaye niligundua kuwa yote yalikuwa tu ya kuua maumivu badala ya kuwa tiba madhubuti.

Kama mtetezi wa uhuru wa wanawake, na mwanaharakati ambaye alikuwa akitafuta ulimwengu ulio bora kwa wote, njia yangu ilikutana na mwanaharakati mwingine ambaye tayari alikuwa akiongoza bila kubagua kuendeleza mageuzi na haki kwa wote. Nilijiunga na kampeni zinazoendelea za mshauri wangu mpya ambazo zilijumuisha, wakati huo, mageuzi ya uchaguzi na haki za kiraia, miongoni mwa mengine. Uanaharakati wangu mpya sasa ulikuwa tofauti kabisa. Badala ya "kuchagua" kutetea haki kwa baadhi tu, nilijifunza kuwa maadili kama vile haki, uhuru, na heshima yanakusudiwa kuwa ya kimsingi kwa ulimwengu wote, na kwamba wema wao na wema wote haupingani. Kwa mara ya kwanza, nilijua maana ya “watu wote wameumbwa sawa” ilimaanisha nini. Lakini muhimu zaidi, nilijifunza kuwa inahitaji imani tu kuona ulimwengu kuwa kitu kimoja na kuona umoja katika uumbaji.

Siku moja nilikutana na kitabu ambacho kina itikadi mbaya katika nchi za Magharibi - Quran Tukufu. Hadi kufikia wakati huo, nilichokuwa nimejihusisha na Uislamu ni wanawake walifunikwa kwenye “hema”, wapigaji wake, nyumba za wanawake, na ulimwengu wa ugaidi. Nilivutiwa kwanza na mtindo na mkabala wa Quran kisha nikavutiwa na mtazamo wake juu ya kuwepo, maisha, uumbaji, na uhusiano kati ya Muumba na viumbe. Niliona Quran kuwa ni hotuba yenye utambuzi sana kwa moyo na nafsi bila ya haja ya mkalimani au mchungaji.

Hatimaye, nilifikia wakati wa ukweli: harakati zangu mpya za kujitimiza hazikuwa chochote zaidi ya kukumbatia tu imani inayoitwa Uislamu ambapo ningeweza kuishi kwa amani kama Muislamu "mtendaji".

Nilinunua gauni zuri refu na kifuniko cha kichwa kilichofanana na kanuni ya mavazi ya mwanamke wa Kiislamu na nilitembea kwenye mitaa na vitongoji vile vile ambavyo siku chache kabla nilikuwa nimetembea na kaptura yangu, bikini, au mavazi ya biashara "ya kifahari" ya magharibi. Ingawa watu, nyuso, na maduka yote yalikuwa sawa, jambo moja lilikuwa tofauti kabisa: amani ya kuwa mwanamke niliipata kwa mara ya kwanza. Nilihisi kana kwamba minyororo ilikuwa imekatika na hatimaye nilikuwa huru. Nilifurahishwa na sura mpya ya kustaajabisha kwenye nyuso za watu badala ya sura ya mwindaji anayetazama windo lake kama nilivyowahi kufikiria. Ghafla mzigo ulikuwa umetolewa kutoka kwenye mabega yangu. Sikutumia tena muda wangu wote kwa ununuzi, vipodozi, kutengeneza nywele zangu, na kufanya mazoezi. Hatimaye, nilikuwa huru.

Kati ya maeneo yote, niliupata Uislamu wangu katika kiini cha kile ambacho wengine wanakiita “mahali pa kashfa zaidi duniani”, ambapo hufanya kuwa kinachopendwa na cha pekee zaidi.

Muda mchache baadaye, habari zilianza kusikika kuhusu wanasiasa, makasisi wa Vatikani, wapenda uhuru, na wale waliojiita wanaharakati wa haki za binadamu na uhuru wakishutumu Hijabu (hijabu) kuwa ya kikandamizi kwa wanawake, kikwazo cha ushirikiano kwa kijamii, na hivi karibuni zaidi, kama afisa wa Misri alivyoita. - "ishara ya kurudi nyuma."

Ninaona kuwa ni unafiki wa wazi pale baadhi ya watu na wale wanaojiita mashirika ya haki za binadamu yanapokimbilia kutetea haki za wanawake wakati baadhi ya serikali zinaweka sheria fulani ya mavazi kwa wanawake, lakini “wapigania uhuru” hao wanaangalia sehemu nyingine wakati wanawake wananyimwa haki zao. haki, kazi, na elimu kwa sababu tu wamechagua kutumia haki yao ya kuvaa Hijabu.

Leo mimi bado ni mtetezi wa haki za wanawake, lakini ni mtetezi wa haki za wanawake wa Kiislamu, ambaye ninatoa wito kwa wanawake wa Kiislamu kubeba majukumu yao ya kutoa msaada wowote wanaouweza kwa waume zao ili wawe Waislamu wema. Kuwalea watoto wao kama Waislamu madhubuti ili wawe vinara wa nuru kwa wanadamu wote kwa mara nyingine tena. Kuamrisha mema - mema wowote - na kukataza maovu -maovu yoyote. Kuisema haki na kuyasema maofu dhidi ya maovu yote. Kupigania haki yetu ya kuvaa Hijabu na kumpendeza Muumba wetu kwa njia yoyote tuliyochagua. Lakini ni muhimu pia kubeba uzoefu wetu wa Hijabu kwa wanawake wenzetu ambao huenda hawakuwahi kupata nafasi ya kuelewa kwa nini kuvaa Hijab kuna maana kwetu na kwa nini tunavaa, kwa dhati, tunaikubali.

Kwa kupenda au kutopenda, wanawake wametingwa na mitindo ya "kuvaa-kidogo-hadi-bila kitu" inayoonekana katika kila njia ya mawasiliano mahali popote ulimwenguni. Kama mtu wa zamani asiyekuwa Muislamu, nasisitiza juu ya haki ya wanawake ya kujua kwa usawa kuhusu Hijabu, fadhila zake, na amani na furaha inayoleta katika maisha ya mwanamke kama ilivyokuwa kwangu. Jana, bikini ilikuwa ishara ya uhuru wangu, wakati kiukweli ilinikomboa tu kutoka kwenye hali yangu ya kiroho na thamani ya kweli kama mwanadamu anayeheshimika.

Sikuweza kuwa na furaha zaidi ya kuikataa bikini yangu ufukwe wa South Beach na mtindo wa maisha “wenye kupendeza” wa Magharibi ili kuishi kwa amani pamoja na Muumba wangu na kufurahia kuishi vizuri na wanadamu wenzangu nikiwa mtu mwenye thamani.

Leo, Hijabu ni ishara mpya ya ukombozi wa mwanamke katika kujitafuta yeye ni nani, kusudi lake ni nini, na aina ya uhusiano anaochagua kuwa nao na Muumba wake.

Kwa wanawake wanaojisalimisha kwa dhana mbaya dhidi ya staha ya Kiislamu ya Hijabu, ninasema: Hamjui mnakosa nini.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.