Mambo 10 Tunayojifunza Kutoka kwa Yesu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kutokana na masomo mengi ambayo tunaweza kujifunza kutoka kwa maisha yenye uchaji Mungu ya Yesu, makala hii inataja baadhi yao.

  • Na Raiiq Ridwan (understandquran.com) [edited byIslamReligion.com]
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,268 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

10-Lessons-from-Jesus.jpgYesu (amani iwe juu yake) alikuwa kati ya mitume watano wakuu waliotumwa kwa wanadamu—wanaoitwa kwa pamoja Ulul'Azm.[1]. Alikuwa Mtume wa mwisho kabla ya Mtume wetu Muhammad, rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake. Kulingana na Imamu as-Suyuti, anahesabiwa pia kama Sahaba bora kati ya maswahaba (marafiki na wafuasi wa Mtume Muhammad). Hii ni kwa sababu aliinuliwa akiwa hai.

Basi, Mtume Muhammad alipokutana naye usiku wa Mi'raj (kupaa mbinguni kwa Mtume Muhammad), alikuwa bado hajafa. Anayekutana na Mtume Muhammad, anamwamini na kufa kwa imani hiyo anahesabiwa kuwa Sahaba. Kwa hivyo ni masomo gani tunaweza kujifunza kutoka kwa Yesu? Kusema kweli ni mamia! Tutazungumzia machache tu katika makala hii na kutaja 10!

Wakati watu walimuaibisha Maria (amani iwe juu yake) kwa kuwa na mtoto nje ya ndoa (hawakujua kwamba ilikuwa ni miujiza), Mungu alimpa Yesu muujiza na akazungumza kwenye malezi.

" Akasema [Yesu], 'Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu, amenipa Kitabu na amenifanya Nabii. Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo. Na ameniusia Sala na Zaka maadamu ni hai. Na nimtendee wema mama yangu. Wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu. Na amani iko juu yangu siku niliyo zaliwa, na siku nitakayo kufa, na siku nitakayo fufuliwa kuwa hai. Huyo ndiye Isa mwana wa Maryamu." (Quran 19:30-34)

1. Utumwa ndio heshima Kubwa kabisa

Kutokana na jinsi historia ya wanadamu imekwenda, neno utumwa linachukuliwa vibaya na ndivyo ilivyo hasa. Uislamu ulikuja kuwachukua watu wasiwe watumwa kwa watu wengine bali wawe watumwa kwa Mungu. Na heshima kubwa zaidi kwa mwanadamu yeyote ni kujitoa na kuwa mtumwa kwa Mungu kwa hiari yake. Mungu ndiye Bwana Mkuu, Anaamua, na tunasikia na kutii. Huo ndio mkataba, na Mwenyezi Mungu ndiye Mwingi wa Rehema kwa wale wanaoonyesha rehema. Yeye ndiye anayetoa na kutoa na kuitisha kidogo sana kutoka kwa watumwa wake. Manabii waliheshimiwa kwa sababu walikuwa bora kwa utumwa wao kwa Mungu. Na huo ndio utambulisho wetu muhimu zaidi—sisi ni watumwa wa Mungu.

2. Maandiko na unabii yanasababisha baraka

Yesu anataja kwamba amepewa Maandiko na kwamba amefanywa nabii na kwamba amebarikiwa popote alipo. Hii ni dalili kwetu kwamba kadiri tulivyo karibu na Maandiko ambayo Mungu ametuma (Qur'ani) na njia za manabii wetu, ndivyo tutakapokuwa na baraka zaidi popote tulipo. Ufunguo wa kupata baraka kutoka kwa Mungu na kuwa na maisha yenye baraka ni uhusiano wetu na Kitabu na njia ya manabii.

3. Maarifa huleta matendo

Yesu alikuwa mwanadamu bora wakati wake. Alijua Maandiko na alikuwa nabii. Hata hivyo, hapo hapo alitaja kwamba ameamrishwa kuomba na kusali na kupeana sadaka. Elimu husababisha hatua kuchukuliwa. Huu ndio Uislamu kama dini ambayo inatufundisha kutenda na sio tu kufanya.

4. Matendo kwa ajili ya watu na matendo kwa ajili ya Mungu

Jambo jingine kati ya mambo mazuri ya Uislamu ni jinsi inavyochanganya masuala ya kiroho na vitendo. Mungu alimuamuru Yesu asali, kwa manufaa yake mwenyewe ya kiroho na ili kuwa na uhusiano na Mungu; na kutoa sadaka kwa watu, pia kwa manufaa ya kiroho na ili kuwa na uhusiano na Mungu na watu pia. Uislamu ni dini ya ubinadamu sana na inachanganya masuala ya kiroho na vitendo.

5. Tabia njema ni suala kuu katika Uislamu

Yesu anasema kwamba yeye si mwenye kiburi na si muovu. Mtume Muhammad alisema: "Siku ya Kiyama hakuna kitu nzito katika mizani ya mema kuliko tabia njema."[2]Miongoni mwa matendo makubwa tunayoweza kufanya ni kuwa na tabia njema. Pia ni muhimu hasa hapa kwa sababu ingawa watu walisema mambo mabaya sana kuhusu mama yake, alijibu vizuri na kupeana jibu imara bila kumdhalilisha mtu yeyote. Hakujibu moto kwa moto. Alijibu maneno mabaya kwa maneno mazuri .

6. Mama, mama, mama

Katikati ya majadiliano haya magumu, Yesu alipata muda wa kutaja kwamba ameamrishwa awe mwema kwa mama yake. Hakuna mtu mwingine muhimu zaidi katika maisha yetu kuliko mama yetu. Hakuna uhusiano mwingine ulio takatifu zaidi. Hakuna mtu mwingine anayestahili upendo wetu na utiifu wetu. Wao ni njia yetu rahisi ya kufikia Pepo. Wao ni msafara utakao kuwa na nafasi kwa ajili yetu kila mara. Kisima kitakachotupatia maji safi daima.

"Kwa hivyo mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi na ni Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka." (Quran 3:51)

7. Taqwa ndio kipimo cha mafanikio yetu

Kati ya vigezo vingi ambavyo Mungu angeweza kuchagua kutuhukumu navyo, Alichagua kimoja ambacho hakuna hata mmoja wetu anayeweza kukiona—taqwa (uchaji wa Mungu). Mtume alisema, "Taqwa ipo hapa" huku akiashiria kifua chake. Hiyo ndio amri kutoka kwa Yesu pia. Mkumbuke Mwenyezi Mungu. Tunawezaje kuwa na taqwa? Njia bora na rahisi kwetu ni kumkumbuka Mungu katika shughuli zetu za kila siku na tujiulize kabla ya kuchukua hatua yoyote, “Je, Mungu atakuwa radhi nami kwa hili?”

8. Njia iliyo nyooka ni rahisi

Hatuna haja ya kutatiza mambo. Njia Iliyo Nyooka ni rahisi—Mungu ndiye Mola wetu Mlezi, na sisi tunamtii. Sisi ni watumwa wake na tunafanya anavyotaka tufanye. Hiyo ndiyo Njia Iliyo Nyooka.

9. Idadi ya wafuasi sio kipimo cha mafanikio

Inajulikana kuwa si watu wengi waliitikia wito wa Yesu. Hii haimaanishi kuwa hakufanikiwa. Mioyo ya watu imo mikononi mwa Mungu. Sisi tumeamrishwa kufikisha tu. Na ndiyo sababu licha ya idadi ndogo ya wanafunzi wake wa karibu, amekuwa mmoja kati ya manabii watano wakuu katika historia.

10. Kuwa na Ukweli hata kama watu ni wachache

Hata kama watu ni wachache wanaofuata Uislamu, tunapaswa kuendelea kuifuata. Hata kama wafuasi ni wachache, haimaanishi kuwa si kweli. Msingi wa ukweli ni dhana na fikira, si idadi ya wafuasi.



Rejeleo la maelezo:

[1] Inajumuisha Mtume Nuhu, Ibrahimu, Musa, Isa na Muhammad (amani iwe juu yao wote).

[2] Imepokelewa na at-Tirmidhi.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.