Ishara za Mungu (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kurani ni muujiza mkubwa wa Mwenyezi Mungu na ilitumwa kwa Mtume Muhammad ambaye ndiye Mtume wa mwisho kwa wanadamu wote. Sehemu ya 2: Asili - Ishara nyingine kubwa ya Mungu iliyotajwa sana katika Kurani.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 08 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,804 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

4)Asili

Signs-of-God02.jpgKile kilichopo duniani katika umbo la misitu, mito, milima, maporomoko ya maji, bahari, na aina mbalimbali za mimea na wanyama kwa kweli ni jambo la kustaajabisha. Sio pomboo anayejizatiti kwa mfumo wa hali ya juu zaidi na mzuri zaidi wa kusikia duniani, wala si ndege tai nor is it the eagle that equips itself with eyesight four or five times stronger than that of humans – they both are the works of the Creator Who perfected everything He made. uwezo wa kuona mara nne au tano zaidi ya wanadamu - wote ni kazi za Muumba Aliyekamilisha kila kitu alichotengeneza. Kwa kuangalia uumbaji Wake ni njia mojawapo ya kujua jinsi Muumba alivyo wa ajabu na Mwenye uwezo.

Mungu anatuonyesha ishara katika wanyama aliowaumba ili watutumikie. Farasi, nyumbu, na punda wapo kwa ajili ya wanadamu kuwatumia kwenda sehemu za mbali ambazo zingechukua muda mrefu kufika kwa miguu. Ng'ombe, kondoo na mbuzi hutoa maziwa, na ngozi zao na sufu tunazitumia kama nguo, na tunazichinja kuwa chakula; huku kuku hutaga mamilioni ya mayai kila siku - yote haya ni ishara ili tuweze kukiri baraka za Mungu juu yetu na kumshukuru. "Na hakika katika nyama hoa nyinyi mna mazingatio. Tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, vikatoka baina ya mavi na damu, maziwa safi mazuri kwa wanywao. Na kutokana na matunda ya mitende na mizabibu mnatengeneza ulevi na riziki nzuri. Hakika katika hayo ipo Ishara kwa wanao tumia akili." (Kurani 16:66-67)

Tukitazama juu angani; anga la dunia lilitengenezwa kwa safu ya kipekee ya ulinzi. Jua hutupatia mwanga unaowezesha uhai, mhimili wake ulioinama hutupatia misimu minne ili tufurahie hali tofauti za hewa. Nyota, vimondo, na kila kitu tunachoweza kuona angani ni vya kuvitazama, kuvutiwa na uzuri wao, kukiri kwamba Mungu aliumba ulimwengu, na kukubali kwamba bila shaka uliumbwa kwa kusudi fulani. Ukweli ni kua, kila kitu katika ulimwengu kilitengenezwa kwa ajili yetu. "Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, na kukhitalifiana usiku na mchana, na marikebu ambazo hupita baharini kwa viwafaavyo watu, na maji anayo yateremsha Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni, na kwa hayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake, na akaeneza humo kila aina ya wanyama; na katika mabadiliko ya pepo, na mawingu yanayo amrishwa kupita baina ya mbingu na ardhi, bila shaka zimo Ishara kwa watu wanao zingatia." (Kurani 2:164)

Pia tofauti za wanadamu, jinsia tofauti, na kila kitu kizuri maishani ni ishara zote za uwezo wa Mungu wa kufanya chochote na wema Wake. "Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri.Na katika Ishara zake ni kuumba mbingu na ardhi, na kutafautiana ndimi zenu na rangi zenu. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa wajuzi." (Kurani 30:21-22)

Sio tu kwamba mvua ni baraka na maji ni chanzo cha maisha yote, lakini kutajwa mara kwa mara kwa mvua katika Kurani ni kwa madhumuni makubwa zaidi. "Na Yeye ndiye anaye peleka pepo (za kuvuma) kuwa ni bishara kabla ya kufika rehema yake. Hata hizo pepo zinapo beba mawingu mazito tunayachunga mpaka kwenye nchi iliyo kufa. Kisha tunateremsha kwayo maji, ndio kama hivyo tukatolesha kila aina ya matunda. Basi hali kadhaalika tunavyo wafufua wafu, ili mpate kukumbuka" (Kurani 7:57) "Na katika Ishara zake ni kwamba unaiona ardhi nyonge, lakini tunapo iteremshia maji mara unaiona inataharaki na kuumuka. Bila ya shaka aliye ihuisha ardhi ndiye atakaye huisha wafu. Hakika Yeye ni Muweza wa kila kitu." (Kurani 41:39)Baada ya mvua kunyesha mtu anapaswa kukumbuka kwamba Mungu (kupitia michakato ya kibiolojia na kemikali inayojulikana ) hugeuza mbegu iliyokufa kuwa mimea hai. Hili linapaswa kumfanya mtu akiri kwamba ni kwa jinsi Mungu anavyoifanya mbegu iliyokufa kuwa hai, Siku ya Kiyama atawarudisha na kuwafufua wanadamu wote kwa ajili ya hukumu. Kujua hilo kunapaswa kumfanya mtu kujitayarisha kwa ajili ya Siku hiyo isiyo na kifani kwa kufanya yale yanayompendeza Mungu na kuepuka yale yanayomkasirisha.

Kwa hiyo Mwenyezi Mungu huwaonyesha wanadamu ishara ambazo zikifuatwa huelekeza kwenye mwongozo wa kweli Kwake; mwongozo ulio mkali kuliko jua. Mwongozo huu ni Uislamu. "Na pindi wakikuhoji, basi sema: Mimi nimeusalimisha uso wangu kumwelekea Mwenyezi Mungu, na kadhaalika walio nifuata. Na waambie walio pewa Kitabu na wasio na kisomo: Je! Mmesilimu? Wakisilimu basi wameongoka. Na wakikengeuka basi juu yako ni kufikisha ujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake." (Kurani 3:20) "Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini." (Kurani 5:3) Kwa kuwa watu wanaozikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu, basi ni dalili zitakazotumika juu yao Siku ya Kiyama. Yeyote anayeziitikia Ishara za Mwenyezi Mungu na akaifuata njia yake, atalipwa raha ya milele, Peponi, na anayezikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu ataadhibiwa kwa adhabu ya moto wa milele.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.