Kumtambulisha "Mwenyezi Mungu"

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Utangulizi kwa Mwenyezi Mungu, Mungu, na kwa baadhi ya sifa Zake tukufu.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 08 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,150 (wastani wa kila siku: 1)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Introducing-Allah.jpgMungu, kwa Kiarabu "Allah" ni Mmoja. Yeye ni wa pekee, hakuna kitu kama Yeye (Yeye si mwanadamu kama watu wengine wanavyoweza kufikiria kimakosa), Yeye ni Muumba na Mola wa kila kitu (kila, mwanadamu, mnyama, mimea, kiumbe, nyota, galaksi; kwa kweli ni ulimwengu mzima), na kila kitu kingine isipokuwa Yeye ni Uumbaji wake. Kila kitu katika ulimwengu ni chake.

Mungu ndiye wa Kwanza na wa Mwisho. Wanakosmolojia na wanasayansi ambao bado wanashangaa jinsi ulimwengu huu wote ulivyoanza wanaweza kuelezwa kwa ufupi kwamba Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema, "Kwanza kabisa, hakuna chochote isipokuwa Mungu (kisha akaumba kiti chake cha enzi). Kiti chake cha enzi kilikuwa juu ya maji, na Yeye .... aliumba mbingu na ardhi."[1]

Nadharia ya Mshindo Mkubwa (Big Bang) kuhusu jinsi ulimwengu ulivyotokea inalingana na maelezo ya uumbaji wa ulimwengu katika Quran.[2]Mwenyezi Mungu ndiye wa Kwanza na hakuna chochote kilichokuwa mbele yake na ni wa Mwisho na hakuna kitakachokuja baada yake. Mungu aliumba anga, maada, wakati, nuru na giza; vyote vipo chini ya mpango Wake.

Mungu ni juu ya yote. Mwenyezi Mungu yu kimwili juu ya ulimwengu ulioinuliwa juu ya Kiti Chake cha Enzi kwa njia inayolingana na Ukuu Wake. Yeye yuko juu ya yote. Kila kitu kiko chini Yake. Hakuna mwanadamu anayeweza kufikiria au kufahamu jinsi Mungu anavyofanana; ni nje ya uwezo wetu kufanya hivyo. Hakuna mwanadamu ambaye amewahi kumuona Mungu na ni Peponi pekee ndipo waumini watapewa neema kubwa zaidi ambayo ni pale Mwenyezi Mungu Mtukufu atakapodhihirisha Uso Wake na waumini wataweza kumuona.

Mungu halali, hapumziki wala kula. Tofauti na wanadamu Mwenyezi anasifiwa kutokua na udhaifu wowote au kutokamilika, kama vile hitaji la kulala, kupumzika au kula. Badala yake, Yeye hutoa baraka za usingizi na kuwalisha wanadamu kwa matumaini kwamba watakuwa na shukrani na kutambua hitaji lao Kwake.

Mungu anajua, anaona na kusikia kila kitu. Fikiria jinsi mwanadamu yeyote anaweza kuona kwa macho yake kwa wakati fulani; na sasa zingatia (Mungu asifiwe) kwamba Mwenyezi Mungu huona yote ambayo watu bilioni 7 wanaweza kuona; na Anaona, Anasikia na Anajua kila tukio kubwa na dogo linalotokea katika ulimwengu. Zaidi ya hayo, ni Mungu, na Mungu pekee ndiye anayejua, wakati ujao. Je, kuna yeyote kama Mungu? Je, kuna anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye?

Mungu ni Mwenye Nguvu, Mwenye Nguvu na Ana uwezo wa kila kitu. Nabii Musa alipomuuliza Mungu kwamba anataka kumuona Mwenyezi, Mungu alimwambia Musa atazame mlima na mlima ukikaa mahali pake atamuona; na Mwenyezi Mungu alipojidhihirisha kwenye mlima ulitoweka kabisa na Musa akaangushwa na kupoteza fahamu.

Matukio ya asili kama vile vimbunga, volkano, matetemeko ya ardhi, nyota katika anga ya juu ni ishara za jinsi Mungu alivyo na nguvu, ushubavu na utukufu. Ukweli wa kuvutia ni kwamba ulimwengu unaojulikana (kwa mwanadamu) una kipenyo cha miaka ya nuru takriban bilioni 93, yaani ni umbali wa maili bilioni 550. Ambayo ina maana chombo cha anga, kinachosafiri kwa kasi ya 20,000 kwa saa, kingechukua takriban miaka trilioni 3139 kusafiri kipenyo cha ulimwengu "unaojulikana".

Sasa soma kile Mungu anasema, "Na wala hawakumhishimu Mwenyezi Mungu kama anavyo stahiki kadiri yake. Na Siku ya Kiyama ardhi yote itakuwa mkononi mwake, na mbingu zitakunjwa katika mkono wake wa kuume. Subhanahu wa Taa'la Ametakasika na Ametukuka na hayo wanayo mshirikisha nayo." (Quran 39:67)Siku ya Hukumu ulimwengu wote utashikwa katika Mkono wa Kuume wa Mwenyezi Mungu. Je, kuna yeyote kama Mungu? Je, kuna anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye?

Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kurehemu. Mwingi wa Rehema ni Miongoni mwa Majina ya Mwenyezi Mungu. Baadhi ya Majina Yake mengine ni Mwingi wa Huruma, Muumba, Mmoja wa Pekee, Nuru, Mkuu, Mkarimu, Mtukufu, Mtakatifu Zaidi, Mlinzi, Mwenye Enzi, Chanzo cha Amani, Mpaji wa Uhai. Mpokeaji wa Uzima, Mwenye Upendo, Mwenye kusamehe, Mwenye Kukubali toba daima, Mwenye Hekima, Mwenye Haki, na Mkombozi. Ni faida kubwa sana unapomwomba Mungu chochote kwa kumwita kwa Majina yake Mazuri. Wakati wa kuomba mali mtu anaweza kusema "Ee Mungu, Mkarimu" na wakati wa kuomba msamaha mtu anaweza kusema "Ee Mungu, Mwenye kusamehe, Mwenye kupokea toba".

Kutoka kwa rehema za Bwana ni kwamba, "Na amezishika mbingu zisianguke juu ya ardhi ila kwa idhini yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye huruma kwa watu, Mwenye kurehemu." (Quran 22:65) Mtume Muhammad, rehema na baraka ziwe juu yake, siku moja alimuona mama mlezi akimtafuta mtoto wake mchanga aliyepotea, na alipompata mtoto wake Mtume akasema, “Unadhani mwanamke huyu anaweza kumtupa mtoto wake kwenye moto?" Tukajibu: "Hapana, ikiwa ana uwezo wa kutomtupa (motoni)." Kisha Mtume akasema: “Mwenyezi Mungu ni mwingi wa rehema kwa waja wake kuliko mwanamke huyu kwa mwanawe.[3]

Mungu Ndiye Aliye Hai Milele, Yule Anayeishi Mwenyewe. Haya ni Majina mengine mawili Mazuri ya Mungu. Kila kilichopo kinamhitaji Mungu kwa ajili ya kuishi na Mungu hahitaji mtu. Kila binadamu ataangamia, na Mola Mlezi wa utukufu (pia ni miongoni mwa Majina yake Mazuri) yu hai. asiyoweza kufa.

"Hakika Mola Mlezi wenu ni Mwenyezi Mungu aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akatawala juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zinazo tumika kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba na amri ni zake. Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote." (Quran 7:54) Kila kitu kinachotokea katika ulimwengu huu si kwa yenyewe au kwa bahati mbaya, lakini ni Mwenyezi ndiye anayedhibiti kila kitu. Mchana na usiku, majira ya joto na baridi, mvua na ukame, kila seli kazi katika mwili (ambayo kuna matrilioni), kuota kwa mbegu katika mimea, seli kujizalisha kutengeneza kiinitete kisha mtoto, na watu kufa; yote yanatokea kwa amri ya Mungu. Je, kuna yeyote kama Mungu? Je, kuna anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye?



Rejeleo la maelezo:

[1] Al-Bukhari 414.

[2] Sherif, Juni 2008. Quran juu ya Ulimwengu Unaoenea na Nadharia ya Mshindo Mkubwa. Imetolewa kutoka https://www.islamreligion.com/articles/1560/quran-on-expanding-universe-and-big-bang-theory/

[3] Al-Bukhari 73 # 28.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.