Статьи / видео вы запросили еще не существует.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
您所请求的文章/视频尚不存在。
The article/video you have requested doesn't exist yet.
あなたが要求した記事/ビデオはまだ存在していません。
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Статьи / видео вы запросили еще не существует.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
您所请求的文章/视频尚不存在。
The article/video you have requested doesn't exist yet.
あなたが要求した記事/ビデオはまだ存在していません。
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Kurani inataja majina mawili ya Mungu ambayo yanahusiana sana ki lugha. La kwanza ni al-Hakeem (Mwenye hekima) na la pili ni al-Haakim (Hakimu). Mungu anatajwa katika Kurani kama "Mwenye hekima" mara 93 na "Hakimu" mara sita.
Kwa mfano, Mungu anasema:
"Hakika Wewe ndiye Mjuzi Mwenye hikima." (Kurani 2:32) na "…Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima." (Kurani 2:129).
"Na ndiye Mwenye hikima na Mwenye khabari zote." (Kurani 6:18)
"Mwenyezi Mungu ni Mkunjufu Mwenye hikima. (Kurani 4:130)
Mungu anajitambua yeye kama Hakimu anaposema: "Je, nimtafute hakimu ghairi ya Mwenyezi Mungu, naye ndiye aliye kuteremshieni Kitabu kilicho elezwa waziwazi?" (Kurani 6:114)
Na: "Naye ndiye Mbora wa wenye kuhukumu." (Kurani 7:87)
Na pale Anaposema: "Na Nuhu alimwomba Mola wake Mlezi: ‘Ee Mola Mlezi wangu! Hakika mwanangu ni katika ahali zangu, na hakika ahadi yako ni haki. Na Wewe ni Mwenye haki kuliko mahakimu wote!’" (Kurani 11:45)
Na: "Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?" (Kurani 95:8)
Kuwa na hekima kuna maanisha kujua mambo jinsi yalivyo, kuyatendea ipasavyo, na kumudu kila kitu mahali pake na kazi yake ipasavyo. Mungu anasema kuhusu uumbaji wake: "Na unaiona milima unaidhunia imetulia; nayo inakwenda kama mwendo wa mawingu. Huo ndio ufundi wa Mwenyezi Mungu aliye tengeneza vilivyo kila kitu." (Kurani 27:88)
Hekima ya Mungu inaweza kushuhudiwa katika uumbaji Wake, na hasa katika uumbaji wa mwanadamu, pamoja na akili na nafsi yake. Mungu anatuambia kwamba alimuumba mwanadamu katika umbo bora kabisa:
"Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa. Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini, Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha. Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo? Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?" (Kurani 95:4-8)
Mwenyezi Mungu ni Mwenye hekima ambaye huwapa hikima wale anao wapenda miongoni mwa waja wake. Mungu anasema: "Yeye humpa hikima amtakaye; na aliye pewa hikima bila ya shaka amepewa kheri nyingi. Na hawakumbuki ila wenye akili." (Kurani 2:269)
Mungu huwapa watu fulani uwezo wa pekee wa kuchunguza matatizo na kupata masuluhisho yanayoweza kutekelezeka, ambao wanapokabiliwa na matatizo au ugumu wanaweza kupima kila jambo kwa njia ifaayo na yenye usawa. Hawa ni watu ambao wengine hushauriana nao na kuwategemea katika nyanja mbalimbali za maisha yao. Watu wengine wana hekima kuhusu masuala ya kijamii. Wengine wana hekima linapokuja suala la mahusiano baina ya watu. Wapo wenye busara linapokuja suala la uchumi.
Nyanja ya ushauri ni muhimu sana kwa sasa. Washauri wengi waliofanikiwa ni watu ambao Mungu amewabariki hekima katika nyanja zao ili kutimiza maarifa, ufahamu, na uzoefu wao.
Ni lazima tutambue kwamba hekima inaweza kuwa maalumu. Mtu anaweza kuwa na hekima nyingi katika sehemu moja au zaidi ya maisha, bila kuwa na hekima katika kila njia. Mtu anaweza kuwa na hekima katika mambo ya kidunia bila ya kuwa na hekima katika mambo ya imani, hakika bila hata ya kuwa muumini.
Mungu ana ukuu juu ya mambo yote katika uumbaji. Hili linawasilishwa kwa jina al-Hakam, ambalo linaonekana katika aya ifuatayo: "Je, nimtafute hakimu ghairi ya Mwenyezi Mungu, naye ndiye aliye kuteremshieni Kitabu kilicho elezwa waziwazi?" (Kurani 6:114)
Zaidi ya hayo, hakuna kinachotokea katika uumbaji isipokuwa kwa mamlaka na amri Yake. Mungu anasema: "Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo." (Kurani 55:29)
Vivyo hivyo, amri Yake inaweza kuwa ya asili kisheria. Mungu huhalalisha baadhi ya matendo na matendo mengine kuwa dhambi. Anatuamuru kufanya mambo fulani na kutukataza kufanya mengine. Amri yake haiwezi kubadilishwa au kupinduliwa na mtu yeyote. Mungu anasema: "Fahamuni! Kuumba na amri ni zake." (Kurani 7:54)
Kurani inamtaja Mungu kama "Mbora wa Mahakimu." Huu ni uthibitisho wa haki yake kamilifu na rehema kubwa. Kamwe Mungu hamdhulumu mtu yeyote na hadhulumu. Sheria anazowawekea waja wake si mzigo wala haiwi isiyo na haki. Bali mafundisho ya kweli ya Uislamu yanasimamia haki za watu wote bila ya upendeleo: mtawala na mtawaliwa, mwenye nguvu na dhaifu, mwanaume na mwanamke, mwadilifu na mtenda dhambi, muumini na kafiri. Inasimamia haki zao wakati wa amani na wakati wa vita, na katika hali zote bila ubaguzi.
Ndio maana Waislamu warejee Kurani na Sunna (mafundisho) ya Mtume, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kwa ajili ya mwongozo katika mambo yote. Wanapaswa kufanya hivyo kama watu binafsi ili kuwaongoza katika maisha yao binafsi, na wanapaswa kufanya hivyo kama jumuiya, jamii, na mataifa kwa mwongozo katika masuala yao ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.
Mwenyezi Mungu ni Mwenye hekima na ndiye Hakimu mwadilifu. Katika imani za Kiislamu, hakuna mtu anayeeleweka kubeba dhambi ya mwingine. Hakuna anayekosewa na Mungu. Hakuna mtenda dhambi anayeadhibiwa zaidi ya ukubwa wa dhambi iliyotendwa na hakuna jambo jema linalopita bila malipo.
Mungu anasema: "Hakika wale walio amini na wakatenda mema - hakika Sisi hatupotezi ujira wa anaye tenda mema." (Kurani 18:30)
Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.
Orodha yako ya historia ipo tupu.
Kwa nini kujiandikisha? Tovuti hii ina miundo kadhaa uliyoundwa mahsusi kwa ajili yako, kama vile: vipendwa vyako, historia yako, kutia alama makala ambazo umezitazama awali, kuorodhesha makala zilizochapishwa tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho, kubadilisha ukubwa wa herufi, na zaidi. Vipengele hivi vinatokana na vidakuzi na vitafanya kazi ipasavyo tu unapotumia kompyuta ile ile. Ili kuwezesha vipengele hivi kutoka kwa kompyuta yoyote, unapaswa kuingia wakati katika tovuti hii.
Tafadhali ingiza Jina lako la mtumiaji na anwani ya barua pepe kisha ubofye kitufe cha Tuma neno la siri. Utapokea neno la siri jipya hivi karibuni. Tumia neno la siri hili jipya kufikia tovuti.
Ongeza maoni