Diane Charles Breslin, Mkatoliki wa Zamani, Marekani (sehemu ya 3 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Diane anaeleza kukubali kwake kwa Uislamu, maisha yake mapya, na maombi kwa ajili ya Amerika.

  • Na Diane Charles Breslin
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,564 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Safari Yangu ya Kuelekea Uislamu

Ilichukua miaka mitatu kamili ya kutafiti na kusoma Qurani kabla sijakuwa tayari kutangaza kwamba nilitaka kuwa Muislamu. Bila shaka niliogopa mabadiliko katika nguo na tabia, kama vile kuwa na uhusiano na wanaume na kulewa ambayo nilikuwa nimeyazoea. Muziki na densi zilikuwa sehemu kubwa ya maisha yangu, na bikini na sketi fupi zilikuwa vyanzo vyangu vya umaarufu. Wakati wote huu sikuwa na nafasi ya kukutana na Waislamu wowote, kwani hawakuwa kwa sehemu yoyote katika eneo langu isipokuwa wahamiaji wachache ambao hawakuweza kuongea Kiingereza vizuri walioishi masafa ya umbali wa saa moja kwa gari kwenye msikiti pekee katika jimbo letu wakati huo. Kila nilipotaka kwenda Sala ya Ijumaa ili kujaribu kuangalia dini hii niliyoizingatia, ningeangaliwa kwa macho ya kudadisi kwani nilishukiwa nilikuwa mpelelezi kama ilivyokuwa, na bado iko, katika mikusanyiko mingi ya Kiislamu. Hakukuwa na Mmarekani mmoja Muislamu aliyepatikana wa kunisaidia na, kama nilivyosema, ilikuwa nadra sana kwa wakazi wote wahamiaji kuwakaribisha watu.

Katikati ya awamu hii ya maisha yangu, baba yangu alikufa kutokana na saratani. Nilikuwa naye wakati wa kifo chake na nilishuhudia kwa uhakika malaika wa kifo akiondoa roho yake. Alishikwa na hofu huku machozi yakitiririka juu ya mashavu yake. Maisha ya anasa, maboti ya raha, vilabu, magari ghali... kwa yeye na mamangu, yote yakiwa matokeo ya mapato ya riba, na sasa yamekwisha.

Nilihisi hamu ya ghafla ya kuingia kwenye Uislamu kwa haraka, huku nikiwa na wakati bado, na kubadili njia zangu na kutoendelea kutafuta kwa upofu kile nilicholelewa nikiamini kuwa ni maisha mazuri. Muda mfupi baada ya hapo nilikuja Misri, na kushiriki safari ndefu ya polepole kupitia muujiza wa lugha ya Kiarabu na kugundua ukweli ulio wazi - Mungu ni Mmoja, ni wa Milele na Daima; Ambaye kamwe hakuzaliwa wala hakuzaa na hakuna kitu kama Yeye.

Pia ni usawa kati ya wanadamu ulionivuta sana kwa dini hiyo. Nabii Muhammad, Rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema kuwa watu ni kama meno ya kichanuo, wote ni sawa na bora zaidi ni anayemcha Mungu. Katika Qur'ani tunaambiwa kuwa walio bora zaidi ni wachamngu. Ucha Mungu unahusisha upendo na kumcha Mungu peke yake. Hata hivyo kabla hujaweza kuwa mcha Mungu, lazima ujifunze Mungu ni nani. Na kumjua ni kumpenda. Nilianza kujifunza Kiarabu ili kusoma neno la Mwenyezi Mungu kwa lugha ya Kiarabu kama ilivyofunuliwa.

Kujifunza Qurani kumebadilisha kila nyanja ya maisha yangu. Sitaki tena kuwa na anasa zozote za kidunia; si magari si nguo si safari, vyote haviwezi kunivuta kwa mtandao ule wa tamaa zisizo na maana, uliokuwa umeniteka nyara mbeleni. Ninaishi maisha mazuri ya muumini; lakini kama wanavyosema... hayajaingizwa tena moyoni... yamo mikononi tu. Siogopi kuwapoteza marafiki zangu wa zamani au jamaa zangu - Mungu akiamua kuwaleta karibu, basi iwe hivyo, lakini najua kwamba Mungu ananipa hasa kile ninachohitaji, si zaidi, si chache. Sijisikii tena kuwa na wasiwasi wala huzuni, wala sina wasiwasi na yaliyonipita, kwa sababu niko salama katika utunzaji wa Mungu - MLEZI MMOJA Niliyemjua siku zote lakini sikujua jina lake.

Maombi kwa Marekani

Ninamwomba Mwenyezi Mungu amruhusu kila Mwamerika nafasi ya kupokea ujumbe wa Umoja wa Mungu kwa njia rahisi, moja kwa moja... Wamarekani, kwa sehemu kubwa, hawajui habari kuhusu theolojia sahihi ya Kiislamu. Lengo kila mara lipo kwa siasa, ambayo inalenga matendo ya wanadamu. Ni wakati muafaka kwa sisi kulenga na kushughulika na matendo ya manabii ambao wote walikuja kutuongoza kutoka kwa giza na kutupeleka kwa mwangaza. Hakuna shaka kwamba giza lipo katika msukosuko unaoathiri Amerika sasa. Nuru ya kweli itatuhusisha sisi sote, na ikiwa mtu atachagua kufuata au kukataa njia ya Kiislamu, hakuna shaka kwamba kuizuia au kuzuia wengine kuifuata kwa hakika kutasababisha taabu zaidi. Ninajali sana masilahi ya nchi yangu, na nina hakika kwamba kujifunza zaidi kuhusu Uislamu kutaongeza uwezekano wa matumaini yangu kutimia.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.