Raha za Peponi (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Makala ya kwanza kati ya sehemu mbili zinazofafanua tofauti za kimsingi kati ya Pepo na maisha ya dunia hii. Sehemu ya 1: Kutokuwepo kwa vile vitu vinavyosababisha huzuni, maumivu na mateso katika maisha haya.

  • Na M. Abdulsalam (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 29 Nov 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 15 May 2023
  • Ilichapishwa: 9
  • Imetazamwa: 5,176 (wastani wa kila siku: 6)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Pleasures_of_Paradise_(part_1_of_2)_001.jpgUkweli wa Pepo ni kitu ambacho watu hawataweza kukielewa mpaka waingie humo, lakini Mwenyezi Mungu ametuonyesha mambo machache ndani ya Kurani. Ameelezea kuwa ni sehemu ambayo kimsingi ni tofauti na maisha ya dunia hii, katika asili na madhumuni ya maisha, pamoja na aina za starehe ambazo watu watafurahia humo. Kurani inawaambia watu kuhusu Pepo, ambayo Mwenyezi Mungu anawapa, inaelezea baraka zake kuu, na inatangaza uzuri wake kwa kila mtu. Inafahamisha watu kwamba Pepo ni mojawapo ya njia mbili za maisha zilizo tayarishwa kwa ajili yao huko akhera, na kwamba kila jambo jema litakuwa lao Peponi kwa kiwango kinachopita uwezo wetu wa sasa wa kufikiria. Inaonyesha pia kwamba Pepo ni mahali ambapo baraka zote zimeumbwa kikamilifu na ambapo watu watapewa kila kitu ambacho nafsi na mioyo yao itatamani, na kwamba watu watakuwa mbali na uhitaji na mahitaji, wasiwasi au huzuni, uchungu na majuto. Kila aina ya uzuri na baraka zipo Peponi na zitafunuliwa kwa ukamilifu ambao haujawahi kuonekana au kujulikana hapo awali. Mungu ametayarisha baraka kama hizo hapo kama zawadi, na hizi zitatolewa kwa watu ambao Yeye amependezwa nao.

Lakini ni nini asili ya furaha hizo peponi , na zitakuwaje tofauti na furaha za ulimwengu huu? Tutajaribu kuangazia baadhi ya tofauti hizi.

Furaha safi bila maumivu na mateso

Ingawa watu katika ulimwengu huu wanapata furaha fulani, kadhalika wanakabiliwa na taabu na mateso mengi. Ikiwa mtu angetathmini maisha wanayoishi, watajua kiwango cha magumu wanayokabiliana nayo yanazidi wepesi na starehe. Maisha ya Akhera hayatakuwa na dhiki wala taabu ndani yake, na watu wataishi humo kwa fahari na furaha tupu. Sababu zote za huzuni, maumivu na mateso wanayopata watu katika maisha haya yatakosekana huko Akhera. Hebu tuangalie baadhi ya sababu hizi.

Utajiri

Mtu anapofikiria mafanikio katika maisha haya, kwa kawaida, hupata taaswira ya nyumba kubwa, vito vya thamani na mavazi, na magari ya gharama kubwa; utulivu wa kifedha unaonekana kuwa ufunguo wa maisha ya furaha. Kwa watu wengi, mafanikio yanahusiana sana na utajiri, ingawa hii ipo mbali zaidi na ukweli. Ni mara ngapi tumewaona matajiri wakubwa wakiishi maisha duni kiasi kwamba wakati mwingine huwapelekea hata kujiua! Utajiri ni kitu ambacho wanadamu kwa asili yao wanatamani kwa gharama yoyote ile, na tamaa hii imeundwa kwa kusudi kubwa na la busara. Wakati tamaa hii haijatimizwa, husababisha kiasi fulani cha huzuni ndani ya mtu. Kwa ajili hiyo, Mwenyezi Mungu amewaahidi wakazi wa Peponi kwamba watapata kila walichokuwa wakikidhania kuhusu mali, kwa wale waliokuwa masikini wa kupindukia, hata walikumbwa na njaa na kiu, kwa wale walio na mali nzuri ambao walitamani hata zaidi. Mungu anatupa maono ya hili anaposema:

“... na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia …” (Kurani 43:71)

“Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita!” (Kurani 69:24)

“… Humo watapambwa kwa mavazi ya mikononi ya dhahabu, na watavaa nguo za kijani za hariri na at'ilasi, huku wakiegemea humo juu ya makochi. Ni malipo bora hayo! Na matandiko mazuri mno ya kupumzikia!” (Kurani 18:31)

Ugonjwa na Kifo

Sababu nyingine ya maumivu na mateso katika maisha haya ni kifo cha mpendwa au ugonjwa, ambayo yote hayapo Peponi. Hakuna atakayehisi ugonjwa au maumivu Peponi. Amesema Mtume Muhammad kuhusu watu wa Peponi rehema na amani ziwe juu yake:

Hawataugua kamwe, kupiga chafya au kutema mate. (Saheeh Al-Bukhari)

Hakuna atakayekufa Peponi. Wote wataishi milele wakifurahia starehe zilizomo. Mtume Muhammad alisema kuwa muitaji ataita watu peponi watakapoingia humo:

"Hakika uwe na afya njema na usiwe mgonjwa tena, uishi na usife tena, uwe mchanga na usiwe dhaifu tena, ufurahie, na usihisi huzuni na majuto tena." (Saheeh Muslim)

Mahusiano ya Kijamii

Kuhusu majuto yanayopatikana kwa sababu ya mpasuko katika mahusiano ya binafsi, watu hawatasikia kamwe uovu wowote au maoni au maneno yenye kuumiza katika Pepo. Watasikia tu maneno mazuri na maneno ya amani. Mungu anasema:

“Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi, Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama!” (Kurani 56:25-26)

Hakutakuwa na uadui baina ya watu wala chuki:

“Na tutaondoa chuki vifuani mwao, na mbele yao iwe inapita mito.…” (Kurani 7:43)

Mtume alisema:

“Hakutakuwa na chuki wala hasira baina yao, nyoyo zao zitakuwa moja, na watamtukuza Mwenyezi Mungu asubuhi na jioni.” (Saheeh Al-Bukhari)

Watu watakuwa na maswahaba bora katika Akhera, ambao pia walikuwa watu bora zaidi duniani:

“Na wenye kumt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume – hao wa pamoja na wale alio waneemesha Mwenyezi Mungu – miongoni mwa Manabii, na Masiddiqi, na Mashahidi, na Watu wema. Na uzuri ulioje kuwa pamoja na watu hao!” (Kurani 4:69)

Nyoyo za watu wa Peponi zitakuwa safi, maneno yao yatakuwa mazuri, na matendo yao ni mema. Hakutakuwa na mazungumzo ya kuumiza, kuudhi, kukera au kuchochea, kwani Pepo haina maneno na vitendo vyote visivyofaa. Kama tungejadili sababu zote za uchungu katika maisha haya, bila shaka tungeona kutokuwepo kwake au kinyume chake kuwa ni kweli Peponi.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.