Diane Charles Breslin, Mkatoliki wa Zamani, Marekani (sehemu ya 2 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kusoma Uislamu kunamfanya Diane awapende tena Yesu na Maria, lakini upendo wa kweli kwa nuru mpya.

  • Na Diane Charles Breslin
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,285 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Wengine

Ilikuwa katika maandalizi yangu kwa shahada ya uzamili ndipo nilisikia mara ya kwanza kuhusu Qur'ani. Hadi wakati huo, kama Wamarekani wengi, niliwajua tu “Waarabu” kama waadui wa siri, waliokuja kuteka nyara ustaarabu wetu. Uislamu haukutajwa kamwe — yaliyotajwa ni Waarabu wachafu tu, na ngamia na mahema yao jangwani. Kama mtoto katika darasa la dini, mara nyingi nilijiuliza watu wengine hao walikuwa kina nani? Yesu alitembea huko Kaana na Galilaya na Nazareti, lakini alikuwa na macho ya rangi ya samawati, watu wengine hao walikuwa nani? Nilikuwa na hisia kwamba kulikuwa na kiunganishi kilichopotea mahali fulani. Mwaka wa 1967 wakati wa vita vya Kiarabu na Israeli, tulipata mtazamo wetu wa kwanza wa watu hao wengine, na walitazamwa wazi na wengi kama maadui. Lakini kwangu mimi, niliwapenda, bila ya sababu dhahiri. Siwezi kueleza kwa nini hadi leo, isipokuwa sasa natambua kuwa walikuwa ndugu zangu Waislamu.

Nilikuwa na miaka 35 niliposoma ukurasa wangu wa kwanza wa Quran. Niliifungua kwa nia ya kuipitia tu kikawaida ili nijue dini ya wenyeji wa eneo ambalo nilikuwa nikilitafiti kwa ajili ya Shahada yangu ya uzamili. Mwenyezi Mungu amesababisha Kitabu kifunguke kwa Surat al-mu'minun aya 52-54:

“Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi. Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo. Basi waache katika ghafla yao kwa muda.” (Quran 23:52-54)

Kutoka mara yangu ya kwanza kuisoma, nilijua kwamba huu ulikuwa ukweli usiokuwa na shaka- wazi na imara, ukifunua kiini cha ubinadamu wote na kuthibitisha yote niliyojifunza kama mwanafunzi wa Historia. Kukataa ukweli, ushindani wao usio na mwisho wa kuwa bora na kukataa kwao kwa lengo la kuwepo kwao, yote yalikuwa yamewekwa kwa maneno machache. Mataifa, utaifa, tamaduni, lugha — wote wakihisi ubora wao, huku vitambulisho vyote hivi vinaficha ukweli pekee ambao tunapaswa kufurahia katika kuishiriki- yaani kumtumikia Mungu mmoja, MLEZI MMOJA Aliyeumba kila kitu na Anayemiliki kila kitu.

Bado Nawapenda Yesu na Maria

Nikiwa mdogo nilikuwa napenda kusema maneno haya “Mtakatifu Maria, Mama wa Mungu, tuombee sisi wenye dhambi, kwa sasa na wakati wa kifo chetu, Ameni,” yanayopatikana katika sala ya “Maria Mtakatifu”. Sasa naona ni kiasi gani Maria amekosewa kwa kusifiwa kama mama wa mungu. Ni sifa ya kutosha kumsifu kama mwanamke aliyechaguliwa juu ya wanawake wote ili abebe nabii mkuu Yesu na kumzaa kibikira. Mama yangu mara nyingi alitetea maombi yake ya mara kwa mara ya kuomba msaada kutoka kwa Maria kwa kueleza kwamba yeye pia alikuwa mama na kwamba alielewa huzuni ya mama. Ingekuwa ni muhimu zaidi kwa mama yangu na wengine wote kutafakari jinsi Maria alivyotukanwa na Wayahudi wa wakati wake na kutuhumiwa kufanya dhambi chafu zaidi, ile ya uzinifu. Maria alistahimili yote haya, akijua kwamba angetetewa na Mwenyezi Mungu, na kwamba angepewa nguvu ya kukabili masaibu yote hayo.

Utambuzi huu wa imani ya Maria na tumaini lake katika huruma ya Mungu itamwezesha mtu kutambua nafasi yake kubwa zaidi miongoni mwa wanawake, na wakati huo huo kuondoa kashfa ya kumwita mama wa Mungu, ambayo ni tuhuma kubwa zaidi kuliko ile ya Wayahudi wa wakati wake. Kama Muislamu unaweza kumpenda Maria na Yesu, lakini kumpenda Mungu zaidi kutakupa Paradiso, kwani Yeye ndiye yule ambaye sheria zake lazima uzitii. Atakuhukumu siku ambayo hakuna mtu mwingine anayeweza kukusaidia. Yeye ndiye aliyekuumba, wewe na Yesu na mama yake Maria, kama alivyo muumba Muhammad. Wote walikufa au watakufa - Mungu kamwe hafi.

Yesu (`Isa kwa kiarabu) kamwe hakudai kuwa yeye ndiye Mungu. Badala yake, yeye alisisitiza mara nyingi kuwa yeye ni mtume aliyetumwa. Ninapoangalia nyuma na kutafakari kuhusu tashwishi niliokuwa nao wakati wa ujana wangu, naamini kwamba mizizi yake ilikuwa katika madai ya kanisa kwamba Yesu alikuwa zaidi ya yale ambayo alijiita yeye mwenyewe. Wakuu wa kanisa walitengeneza mafundisho ya kuunda dhana ya Utatu. Ni utoaji huu uliochanganyikiwa wa Torati na Injili za awali (maandiko waliyopewa Musa na Yesu) ambao ni msingi wa suala la Utatu.

Kwa kweli, inatosha kusema tu kwamba Yesu alikuwa nabii, ndiyo, mjumbe aliyekuja na neno la Yule aliyemtuma. Tukimwona Yesu, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, kwa nuru hii sahihi, basi ni rahisi kumkubali Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, kama ndugu yake mdogo ambaye alikuja na ujumbe huo huo — kuwaita wote kwa ibada ya Mwenyezi Mungu MMOJA, ambaye aliumba kila kitu na ambaye sisi wote tutarudi kwake. Hakuna maana yoyote katika kujadili sifa zao za kimwili. Mwarabu, Myahudi, Mzungu, macho ya samawati au kahawia, nywele ndefu au fupi - zote hazina maana kabisa kwa umuhimu wao kama wabebaji wa ujumbe huo. Kila ninapomfikiria Yesu sasa, baada ya kujua kuhusu Uislamu, ninahisi uhusiano ambao mtu anahisi katika familia yenye furaha - familia ya waumini. Yesu alikuwa “Muislamu”, ambaye anamtumikia Mungu wake aliye juu.

Amri ya kwanza kati ya “Amri Kumi” inasema:

1. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, Usiwe na miungu mingine ila mimi.

2. Usilitaje bure jina langu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.

Mtu yeyote ambaye anajua maana sahihi ya “la ilaha ill-Allah” (hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu) atatambua mara moja mfanano katika ushuhuda huu. Kisha tunaweza kwa hakika kuanza kuleta pamoja hadithi halisi ya manabii wote na kukomesha upotovu.

“Na wao ati husema kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana! Hakika mmeleta jambo la kuchusha mno! Zinakaribia mbingu kutatuka kwa hilo, na ardhi kupasuka, na milima kuanguka vipande vipande.” (Quran 19:88-90)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.