Mitume wa Quran: Utangulizi (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kuamini manabii wa Mungu ni sehemu muhimu ya imani ya Kiislamu. Sehemu ya 1 itawataja manabii wote kabla ya Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, waliotajwa katika maandiko ya Kiislamu kuanzia Adamu mpaka Ibrahimu na wanawe wawili.

  • Na Imam Mufti (© 2013 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,470
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

ProphetsOfTheQuran1.jpgKurani inataja manabii ishirini na watano, ambao wengi wao walitajwa katika Biblia pia. Manabii hawa walikuwa ni akina nani, waliishi wapi, walitumwa kwa nani, majina yao ni nini katika Qurani na Biblia, na baadhi ya miujiza walizofanya ni ipi? Tutajibu maswali haya rahisi.

Kabla hatujaanza, ni lazima tuelewe mambo mawili:

a.Kwa Kiarabu maneno mawili tofauti hutumiwa, Nabi na Rasool. Nabi ni nabii na Rasool ni mjumbe au mtume. Maneno haya mawili yanakaribiana kimaana kwa lengo letu.

b.Kuna watu wanne wanaotajwa katika Qurani ambao wanazuoni Waislamu hawana uhakika kama walikuwa manabii au la: Dhul-Qarnain (18:83), Luqman (Sura ya 31), Uzair (9:30), and Tubba (44:37, 50:14).

1.Aadam au Adamu ni nabii wa kwanza katika Uislamu. Pia ndiye mwanadamu wa kwanza kulingana na imani ya Kiislamu. Adamu anatajwa kwa aya 25 na mara 25 katika Qurani. Mungu alimuumba Adamu kwa mikono yake na kumuumba mkewe, Hawwa au Hawa kutokana na ubavu wa Adamu. Aliishi Peponi na akafukuzwa huko na kuletwa ardhini kwa sababu ya kutotii kwake. Hadithi ya wanawe wawili imetajwa mara moja katika Sura ya 5 (Al-Maidah).

2.Idrees au Henoki anatajwa mara mbili katika Qurani. Zaidi ya hiyo hakuna mengi yanayojulikana kuhusu maisha yake. Inasemekana aliishi Babeli, Iraki na kuhamia Misri na kwamba ndiye wa kwanza kuandika kwa kalamu.

3.Nooh au Nuhu anatajwa mara 43 katika Qurani. Inasemekana alikuwa mwenyeji wa Kirk, Iraki. Ushirikina (shirk) ulionekana kwa mara ya kwanza kati ya watu wake walioishi karibu na mji wa leo wa Kufa, kusini mwa Iraki. Mke wake alikuwa mkafiri kama ilivyoelezwa katika Sura ya 66 (At-Tahrim). Mwanawe pia alichagua kutoamini na alikufa majini. Hadithi yake inapatikana katika Sura ya 11 (Hud).

Mojawapo ya miujiza yake mikubwa ilikuwa Safina ambayo aliijenga kulingana na amri ya Mungu. Ilikaa juu ya Mlima Judi ambao unasemekana upo kati ya mpaka wa Syria na Kituruki leo karibu na mji wa Ayn Diwar.

4.Hud inasemekana ndiye Heberi kwa kiingereza. Anatajwa mara 7 katika Qurani. Hud ndiye mtu wa kwanza kuongea Kiarabu na alikuwa nabii Mwarabu wa kwanza. Alitumwa kwa watu wa Aad katika eneo linalojulikana kama Al-Ahqaf ambalo ni eneo karibu na Hadramaut nchini Yemen na Ar-Rub al-Khali (Robo Tupu). Mungu aliwaangamiza kwa upepo mkali uliovuma kwa siku 8 na usiku saba.

5.Salih anatajwa mara 9 katika Qurani. Alikuwa nabii Mwarabu aliyetumwa kwa watu wa Thamud walioishi katika eneo linalojulikana kama Al-Hijr kati ya Hijaz na Tabuk. Al-Hijr lilikuwa ni jina la kale. Leo, eneo hilo linajulikana kamaMadain Salih” huko Saudi Arabia na limeorodheshwa na UNESCO kuwa kati ya Maeneno yanayopaswa kuhifadhiwa duniani. Ni majengo makubwa sana yaliyochongwa ndani ya milima. Watu walidai atoe ngamia wa kike kutoka kwa milima ili kuthibitisha madai yake ya kuwa nabii. Akafanya, na akawaonya wasimdhuru ngamia huyo, ila wakamuua licha ya maonyo ya Salih. Ukelele mkubwa - saihah - uliwaua wote.

6.Ibrahim or Ibrahimu anatajwa mara 69 katika sura 25 za Qurani. Jina la baba yake lilikuwa Aazar. Waliishi katika mji wa Ur katika ufalme wa Wakaldayo. Alitoroka Ur kwenda Harran, kaskazini mwa bara Arabu, katika nchi ya Syria, wakati Nimrodi, mfalme, alijaribu kumchoma akiwa hai. Kutoka Harran alikwenda Palestina pamoja na mkewe Sara na mwana wa kaka yake, Lutu (Loot kwa Kiarabu) na mkewe. Kutokana na ukame, walilazimika kuhamia Misri.

Baadaye alirudi pamoja na Luti kwa upande wa kusini wa Palestina. Ibrahimu akakaa Bir Saba'a na Lutu akakaa karibu na Bahari ya Chumvi.

Ibrahimu kisha akahamisha mke wake wa pili, Hagari, kwenda Makka pamoja na mwanawe Ishmaeli na akawaacha huko kwa amri ya Mungu. Makka ilikuwa jangwa na kisima cha Zamzam kilitolewa na Mungu kwa ajili ya kuishi kwao. Kabila la kale la Jurhum liliweka makazi yao karibu na zamzam. Abrahamu inasemekana alizikwa huko Hebroni, Palestina.

7, 8. Ibrahimu alikuwa na wana wawili: Ishaq au Isaka na Ismael au Ishmaeli. Isaka anatajwa mara 16 katika Qurani ilhali Ishmaeli anatajwa mara 12. Isaka aliishi na baba yake Ibrahimu, na akafa huko Hebroni, Palestina. Mungu alimuamuru Ibrahimu amtoe Ishmaeli kama dhabihu. Alikwenda Makka pamoja na wazazi wake na akaachwa huko pamoja na mama yake. Ibrahimu alimtembelea Ishmaeli mara kadhaa huko Makka, na wakati mmoja kati ya nyakati hizo, Mungu aliwaamuru Ibrahimu na Ishmaeli wajenge Ka'bah (Nyumba Takatifu). Ismaili alikufa huko Makka na kuzikwa huko. Isaka ni baba wa Wayahudi na Ismaili ni baba wa Waarabu.

Mbaya Nzuri zaidi

Mitume wa Quran: Utangulizi (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kuwaamini manabii wa Mungu ni sehemu muhimi ya imani ya Kiislamu. Sehemu ya 2 itataja manabii wote waliokuja kabla ya Mtume Muhammad, amani iwe juu yake, waliotajwa katika maandiko ya Kiislamu kuanzia Lutu hadi Yesu.

  • Na Imam Mufti (© 2013 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,303
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

9. ProphetsOfTheQuran2.jpgLuti au Loot ametajwa mara 17 katika Qurani. Yeye ni mpwa wa Ibrahimu, mwana wa nduguye Ibrahimu. Luti aliishi kwa ncha ya kusini ya Bahari ya Chumvi. Watu wake walikuwa wa Sodoma na Gomora. Luti alimwamini Ibrahimu na baada ya kurudi kutoka Misri, wakaishi kwa maeneo tofauti. Watu wa Sodoma walikuwa wa kwanza kufanya ushoga. Ndiyo sababu mashoga wakati mwingine huitwa wasodoma. Mke wake hakuwa Muumini. Yeye hakufanya dhambi hiyo, lakini aliikubali. Mawe yalinyesha kama mvua juu ya watu wa Sodoma na Gomora na yaliwaangamiza.

10. Yaqub au Yakobo, mwana wa Isaka na mjukuu wa Ibrahimu anatajwa mara 16 katika Qurani. Jina jingine la Yakobo lilikuwa Israeli. “Bani Israel,” Wana wa Israeli, au Waisraeli walipewa jina hilo kwa sababu yake. Manabii wote wa Kiebrania walitoka kwake, na wa mwisho kati yao alikuwa Eesa au Yesu. Yakobo ni baba wa makabila kumi na mawili yaliyojulikana kama Al-Asbaat (7:160) katika Qurani. Inasemekana alisafiri kuenda kaskazini mwa Iraki, akarudi Palestina na kisha kukaa Misri na kufa hapo. Alizikwa Hebroni, Palestina, pamoja na baba yake kulingana na usia wake wa mwisho. Biblia inataja kuwa Isaka alimwoa Rebeka na mwanawe Yakobo alimwoa Raheli (Rahil kwa Kiarabu).

11. Yusuf au Yosefu, mwana wa Yakobo au Israeli anatajwa mara 17 kwa Qurani. Aliachwa katika kisima huko Yerusalemu na ndugu zake, halafu akapelekwa Misri ambapo alipata cheo cha juu kwa serikali. Baadaye, baba yake, Yakobo, na ndugu zake walikaa Misri.

12. Shuaib au Yethro, aliyetajwa mara 11 katika Qurani, alitumwa kwa watu wa Madyan, na alikuwa mmoja kati ya wana wa Ibrahimu. Shuaib aliishi kati ya wakati wa Lutu na Musa na alikuwa nabii Mwarabu. Watu wake waliabudu mti uitwao Al-Ayka (15:78, 26:176, 38:13, 50:14). Walikuwa wakiwapora watu barabarani, na kuwalaghai katika shughuli za biashara. Basi zikawashukia adhabu kadhaa: Kilio cha kutisha kilichokuwa na tetemeko la ardhi kiliwaangamiza.

13. Ayyub au Ayubu ametajwa mara 4 katika Qurani. Inasemekana aliishi karibu na Bahari ya Chumvi au Dameski. Alikuwa nabii mwenye utajiri aliyetahiniwa na Mungu kwa ufukara na ugonjwa, lakini alikuwa na subira na alisaidiwa na mke wake mwaminifu ambaye alikaa naye kwa kila shida. Hatimaye, Mwenyezi Mungu anawalipa vizuri kwa uvumilivu wao.

14. Yunus au Yona, pia anajulikana kama “Dhun-Noon,” anatajwa mara 4 katika Qurani. Aliishi Ninawi, karibu na Mosul, nchini Iraki. Aliwaacha watu wake kabla Mungu hajampa ruhusa, akaeleka nchi ambayo kwa sasa inajulikana kama Tunisia, lakini aliishia Yafa. Alimezwa na nyangumi, kisha akamtubia Mungu na kurudi kwa watu wake huko Iraki ambapo wote, wakiwa na idadi ya 100,000 walitubu na kumwamini.

15. Dhul-Kifl ametajwa mara mbili katika Qur'ani. Baadhi ya wasomi wanasema alikuwa mwana wa Ayubu, wengine wanasema yeye ndiye Ezekieli wa Biblia.

16. Muusa au Musa ndiye nabii aliyetajwa mara nyingi katika Qurani, akitajwa mara 136. Kabla ya Musa, Yosefu alikuwa ameanza kueneza ujumbe wa umoja wa Mungu (tawhid: ibada ya Mungu Mmoja, Mungu wa kweli) miongoni mwa watu wa Misri. Ujumbe wake uliimarishwa wakati baba yake, Yakobo, na ndugu zake pia walikuja kukaa Misri, wakiwabadilisha polepole watu wa Misri nzima. Baada ya Yusuf, Wamisri waligeuka tena kwa ushirikina (shirk) na watoto wa Yakobo, Waisraeli, wakaongezeka na kupata umaarufu kwa jamii. Musa alikuwa nabii wa kwanza aliyetumwa kwa Waisraeli wakati Farao wa Misri alikuwa akiwafanya watumwa wake. Musa alikimbilia Madyan ili kuepukana na mateso. Mungu alimfanya nabii huko Mlima Toor, ulio katika Sinai na alipewa miujiza tisa kubwa.

17. Haroon au Haruni ni ndugu wa Musa na anatajwa mara 20 katika Qurani.

18,19. Ilyas au Eliya na Yas'a wanatajwa wote mara mbili katika Qurani. Wote wawili waliishi Baalbek.

20,21. Dawud au Daudi anatajwa katika Qurani mara 16. Aliwaongoza Waisraeli kwenye vita na kushinda, na alikuwa na miujiza mingi. Mwanawe, Suleiman au Sulemani anatajwa mara 17 na pia alikuwa mfalme mwenye miujiza mikubwa. Wote wamezikwa Yerusalemu.

22. Zakariyyah au Zekaria anatajwa mara 7. Alikuwa seremala. Alimlea Maria, mama yake Yesu.

23. Yahya au Yohana ni mwana wa Zekaria na anatajwa mara 5. Aliuawa Yerusalemu, na kichwa chake kikapelekwa Dameski.

24. Jina la Eesa au Yesu limetajwa mara 25, Masihi mara 11, na 'mwana wa Maryamu' mara 23. Alizaliwa Bethlehemu, Palestina. Inasemekana alitembelea Misri akiwa na mama yake. Yeye ndiye nabii wa mwisho miongoni mwa Wana wa Israeli.

Manabii watano walikuwa Waarabu: Hud, Salih, Shuaib, Ismail, na Muhammad, amani iwe juu yao. Wanne kati yao walitumwa kwa Waarabu, na Muhammad alitumwa kwa wanadamu wote.

Kwa kumalizia, manabii, wa biblia na wasio wa Biblia, ni watu wenye umuhimu mkubwa katika maandiko ya Kiislamu. Waislamu wanajiona kama warithi wa kweli wa utume wa manabii waliotumwa na Mungu kwa ubinadamu: ibada ya Mungu Mmoja wa Kweli na utiifu Kwake.

Marejeleo yaliyochaguliwa:

1.Ibn Kathir. Qasas ul-Ambiya. Cairo: Dar at-Taba’a wa-Nashr al-Islamiyya, 1997.

2.Ibn Hajr al-Asqalani. Tuhfa ul-Nubala’ min Qasas il-Ambiya lil Imam al-Hafid Ibn Kathir. Jedda: Maktaba as-Sahaba, 1998.

3.Mahmud al-Masri. Qasas ul-Ambiya lil-Atfaal. Cairo: Maktaba as-Safa, 2009.

4.Dr. Shawqi Abu Khalil. Atlas al-Quran. Damascus: Dar-ul-Fikr, 2003.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.